Ajali yaua 2 mtoto wa Mbunge na dereva

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,474
39,987
TAARIFA KWA UMMA
__________

YAH. AJALI YA GARI ILIYOTOKEA LEO 18.7.2008 ASUBUHI
ENEO LA GAIRO

Kutokana na ajali mbaya ambayo imetokea leo Ijumaa 18.7.2008 majira ya asubuhi eneo la Gairo Mkoani Morogoro na kusababisha vifo vya watu wawili ambao ni mtoto wa Mheshimiwa Mbunge Saverina Mwijage ambaye anaitwa Stella Silvanus mwenye umri wa miaka 18 pamoja na dereva wa gari hilo ambaye ni Ndugu Anderson Kaindoa mwenye umri wa miaka 40.

Pamoja na waliopata ajali pia wapo watoto wengine wa Mheshimiwa Mbunge ambao ni Gervas Silvanus, Silli Silvanus na Irene Silvanus mwenye miaka 3, pamoja na Imelda Mussa ambaye ni mtoto wa Mheshimiwa Mercy Emmanuel Mbunge.

Wote hawa walikuwa wanatokea mjini Dodoma kuelekea
Dar es salaam baada ya likizo ya shule kumalizika tayari kwa ajili ya kuendelea na masomo yao.

Kwa simanzi kubwa Kambi ya Upinzani inapenda kutoa pole kwa Mheshimiwa Saverina Mwijage kwa kupotelewa na mwanaye kipenzi pamoja na ndugu na jamaa wa dereva aliyepoteza maisha yake.


Tunapenda kutoa shukrani za dhati kwa wale wote waliohusika katika juhudi za kuokoa maisha ya vijana hawa, na shukrani za kipekee zimwendee Mheshimiwa Mohamed Shabiby Mbunge wa Gairo ambaye alikuwa wa kwanza pamoja na wananchi wake kufika eneo la tukio na kuhakikisha kuwa marehemu, majeruhi na mali zao zote ziko salama pamoja na kuwafikisha wahusika Hospitali.

Pia tunapenda kuwashukuru sana waheshimiwa wabunge wafuatao kwa kuweza kufika eneo la tukio kwa niaba ya Bunge kwa ajili ya kwenda kusaidia kuokoa maisha ya watoto wetu nao ni waheshimiwa Abbas Jecha (Mb), Mkiwa Adam Kimwanga (Mb), Martha Mlata (Mb) na Felister Bura (Mb). Hiyo ndio timu iliowakilisha Bunge katika kuwafikisha marehemu na majeruhi hapa Dodoma.

Pia tunapenda kutoa shukrani za dhati kwa madaktari wakiongozwa na Daktari mkuu wa Hospitali ya Gairo Dr. Mkoba, Dr. Abdalla wa Kituo cha Afya Berege pamoja na Nesi wa Hospitali kuu ya Dodoma Mery Shadrack kwa juhudi zao za kuokoa maisha ya vijana hawa. Afande Revocatus ambaye ni Trafiki kwa huduma nzuri ya kiusalama.

Mwisho lakini kwa umuhimu mkubwa tunapenda kumshukuru Mama Kippa, Mkurugenzi Msaidizi Huduma kwa Wabunge, kwa kazi kubwa aliyofanya baada ya kupata taarifa za tukio hili la kusikitisha.


Imetolewa na:




Hamad Rashid Mohamed (Mb)
KIONGOZI WA UPINZANI BUNGENI
18.7.2008
 
Last edited by a moderator:
Mungu na ampe nguvu mama mzazi wa mtoto huyu kwani kama waliagana asubuhi kwa ajili ya kwenda shule na ghafla analetewa msiba inauma sana.

Huyu naambiwa kuwa ndio mwanaye wa kwanza.
 
Wafiwa poleni sana, wagonjwa ugueni pole.

-Gari limegonga mti, limepinduka, limeacha njia, au limetumbukia mtoni?

-Aliyefiwa ni Mbunge wa wapi?

-Wabunge waliosafiri kwenda “kujaribu kuokoa maisha ya watoto” waliambiwa njooni kuna victims wanaghala ghala barabarani, au? Waliwakuta? Wabunge walienda kusaidia kuokoa maisha vipi, kwa kupitisha muswada wa kufunga njia eneo la tukio ?

-Halafu your biggest priority unapoenda eneo la tukio sio “kuhakikisha kuwa marehemu, majeruhi na mali zao zote ziko salama…” Marehemu na majeruhi hawawezi kuwa salama. Wameshaathirika. Na marehemu na majeruhi huwa hawaibwi!

Mbunge wa Upinzani ameandika kitu kimekaa kama kikolela holela hivi. Ovyo ovyo tu!
 
Kuhani.. I have noticed a certain tendency with you...

well.. nawapa familia waliofiwa na wahanga wote nawaombea unafuu.

Mungu ailaze roho ya Marehemu mahala pema peponi.

Amina.
 
Wafiwa poleni sana, wagonjwa ugueni pole.

-Gari limegonga mti, limepinduka, limeacha njia, au limetumbukia mtoni?

-Aliyefiwa ni Mbunge wa wapi?

-Wabunge waliosafiri kwenda “kujaribu kuokoa maisha ya watoto” waliambiwa njooni kuna victims wanaghala ghala barabarani, au? Waliwakuta? Wabunge walienda kusaidia kuokoa maisha vipi, kwa kupitisha muswada wa kufunga njia eneo la tukio ?

-Halafu your biggest priority unapoenda eneo la tukio sio “kuhakikisha kuwa marehemu, majeruhi na mali zao zote ziko salama…” Marehemu na majeruhi hawawezi kuwa salama. Wameshaathirika. Na marehemu na majeruhi huwa hawaibwi!

Mbunge wa Upinzani ameandika kitu kimekaa kama kikolela holela hivi. Ovyo ovyo tu!


POLITICS mpaka msibani? jua watu wanasimanzi na wamefiwa na pia jua huenda wako bize sana na kazi za huko dodoma.
 
POLITICS mpaka msibani? jua watu wanasimanzi na wamefiwa na pia jua huenda wako bize sana na kazi za huko dodoma.

Sio politics. Ila ni taarifa za msiba zilizoandikwa kama anaandikia illiterate society.

Sasa Mbunge aliyefiwa ni Mbunge wa wapi?

Gari limeua watu, nini kilitokea. Lilipigwa na radi? Matairi yalichomoka? Au daraja lilibomoka?

Literal advancement na mawasiliano ni muhimu katika maendeleo ya jamii.

Tukiwa na maendeleo, maajali ya kila leo kama haya yatapungua.

Nilichokisema kina relevance hapa, ila kwa literal level ya jamii yetu unaweza ukadhani niko nitpicking au political kwenye misiba.

La hasha.

Ni taarifa tu naomba.

Mbunge aliyefiwa ni Mbunge wa wapi?

Gari lililoua, ni nini kilitokea?
 
Namwomba Mwenyezi Mungu Aweke Pahali Pema Peponi Roho Za Marehemu. Amen.

Nawapa Pole Ndugu Na Marafiki Wote.


SteveD.
 
Innalillahi Wa Innalillahi Raaj'un!

Mola aziweke pema roho za marehemu na awajalie subra wafiwa wote.

Amin.

./Mwana wa Haki
 
Sio politics.... Ila ni taarifa za msiba zilizoandikwa kama anaandikia illiterate society.....


Nilichokisema kina relevance hapa, ila kwa literal level ya jamii yetu unaweza ukadhani niko nitpicking au political kwenye misiba.

na hiki ndicho ulichosema mwanzo:

Wafiwa poleni sana, wagonjwa ugueni pole.

-Gari limegonga mti, limepinduka, limeacha njia, au limetumbukia mtoni?

-Aliyefiwa ni Mbunge wa wapi?

-Wabunge waliosafiri kwenda “kujaribu kuokoa maisha ya watoto” waliambiwa njooni kuna victims wanaghala ghala barabarani, au? Waliwakuta? Wabunge walienda kusaidia kuokoa maisha vipi, kwa kupitisha muswada wa kufunga njia eneo la tukio ?

-Halafu your biggest priority unapoenda eneo la tukio sio “kuhakikisha kuwa marehemu, majeruhi na mali zao zote ziko salama…” Marehemu na majeruhi hawawezi kuwa salama. Wameshaathirika. Na marehemu na majeruhi huwa hawaibwi!

Mbunge wa Upinzani ameandika kitu kimekaa kama kikolela holela hivi. Ovyo ovyo tu!

Sasa,

Hekima si kusema kitu sahihi tu na kupatia, lakini pia kukipima kitu hicho unapokisema, wakati na mandhari ya unachokisema. Yawezekana ukosoaji wake wa lugha na fasihi ni sawa kabisa, lakini je ni wakati muafaka? Kati ya yote uliyoyasoma humo, kilichokushtua ni lugha?

Wakati wengine ambao yawezekana "literal (literacy??) level ya jamii" yetu ni ndogo tunaweza kufikiri kuwa mwenzetu unajali zaidi maneno kuliko roho za watu.

Tutoe pole kwanza msibani, mengine tunazungumza pembeni au baadaye. Hiyo ndiyo hekima.
 
Back
Top Bottom