Charles Mkubya
JF-Expert Member
- Aug 27, 2009
- 206
- 159
Kuna ajali imetokea usiku karibu na mataa ya Chang'ombe ukitokea Karume ikihusisha Treni na Magari mawili ya abiria, moja ikiwa ni ya Mbagala na nyingine ya Tandika. Majeruhi ni wengi japo sijashuhudia maiti lakini uwezekano wa kuwapo watu waliopoteza maisha upo. Atakaekuwa na taarifa zaidi asisite kutupasha ila nawapa pole wote walipatwa na tatizo hili kwa namna moja au nyingine