Ajali ya Mto Wami: Dereva aliekuwa anaendesha lori la mbele ashitakiwe kwa kusababisha ajali

Mimi nilipata ajali hapo nikiwa naenda kilimanjaro october 1996 tukiwa ndani ya SAWAYA basi yetu ilifeli break lkn derva alimudu kuongoza kwenye zile kona, wakati tunaanza tu kuingia kwenye daraja tayari upande wa pili TAYASARI ikitokea tanga ilikuwa imefika katikati ya daraja. yule dereva kule alikuwa mtu mzima sana alichoamua ni kufunga break na kusimama maana ilishakuwa too late hata kurudi nyuma.

Ile collision ilitokea pale asikuambie mtu ni kama tulikuwa tumebeba stool tumekalia, tuliokuwa nyuma tuliondoka na viti hadi mbele ingawa wakati huo kule mbele yalikuwa mabati yameshikana na kiasi hata cha milango yote kubanwa na tuliokuwa na afadhali tulitokea madirishani.

Mambo ni mengi ila niseme tu kama tayasari isingesimama tungetumbukia wote mtoni maana ile ndio ilikuwa kama kinga yetu. RIP kwa madereva wote wawili pamoja na abiria maana pale pale palikuwa na death kama 20 kwa ujumla wao na wengine walienda kufariki baadae tumbi na muhimbili.

Wakati ule hakukuwa na msaada wa haraka maana ajali ilitokea saa nne na majeruhi walianza kuchukuliwa saa kumi na gari ya jeshi. yani mtu anapoteza damu hadi anafariki.

Duh...! Ilikuchukua muda gani kusahau tukio??duh inatosha Sana...hukuachwa na majeraha makubwa?pole sana
 
Nashukuru kwa kunikosoa, next time nitajirekebisha.
Ni hivi: Yule dereva wa lori la mbele alikuwa tayari kwenye daraja alipoona lile lori la nyuma linakuja kwa kasi. Na anasema alijua kuwa litakuwa limekataa breki hivyo akaamua kusimama na kuvuta hand break. Alifanya hivyo kwa sababu Lori la nyuma lilikuwa linakuja kwa kasi sana na yeye asingeweza kumaliza kuvuka lile daraja kabla lile lori la nyuma halijamfikia. Na aliogopa litakampomfikia wakati akiwa kwenye motion, lori lake lingesombwa na kutupwa ndani ya maji. Sasa hapa tunaweza kujiuliza: je, kama lori la mbele lingekuwa limeendelea na mwendo hali ingeweza kuwaje? (kumbuka hata kama angeendelea na mwendo na hata ajaribu kuongeza bado tu lori la nyuma lingemgonga kwa sababu sehemu ile magari, hasa malori, hupunguza mwendo kabisa). Jibu litakuwa ni la kukisia tu lakini kwangu mimi naona wangeweza kuingia kwenye maji wote. Na nadhani alisiposimama alifikiri kuwa anamsaidia dereva wa nyuma ili gari yake imgonge na kusimama.
 
Duh...! Ilikuchukua muda gani kusahau tukio??duh inatosha Sana...hukuachwa na majeraha makubwa?pole sana

Asante sana....

Nilipata majeraha kichwani ila baada ya xray muhimbili wakasema nipo vizuri ni vidonda tu, wakati huo hamna ct scan wala mri.

Changamoto ni kuwa nilikuwa boarding school sasa baada ya kupona lazima nirudi shule hapo sasa ndio nilikuwa natamani kuwe na njia nyingine tofauti na wami maana nikishafika pale ni kama naona ndio mwisho wangu.
 
Asante sana....

Nilipata majeraha kichwani ila baada ya xray muhimbili wakasema nipo vizuri ni vidonda tu, wakati huo hamna ct scan wala mri.

Changamoto ni kuwa nilikuwa boarding school sasa baada ya kupona lazima nirudi shule hapo sasa ndio nilikuwa natamani kuwe na njia nyingine tofauti na wami maana nikishafika pale ni kama naona ndio mwisho wangu.


Duh pole Sana! Inatisha..uwi
 
Mimi nilipata ajali hapo nikiwa naenda kilimanjaro october 1996 tukiwa ndani ya SAWAYA basi yetu ilifeli break lkn derva alimudu kuongoza kwenye zile kona, wakati tunaanza tu kuingia kwenye daraja tayari upande wa pili TAYASARI ikitokea tanga ilikuwa imefika katikati ya daraja. yule dereva kule alikuwa mtu mzima sana alichoamua ni kufunga break na kusimama maana ilishakuwa too late hata kurudi nyuma.

Ile collision ilitokea pale asikuambie mtu ni kama tulikuwa tumebeba stool tumekalia, tuliokuwa nyuma tuliondoka na viti hadi mbele ingawa wakati huo kule mbele yalikuwa mabati yameshikana na kiasi hata cha milango yote kubanwa na tuliokuwa na afadhali tulitokea madirishani.

Mambo ni mengi ila niseme tu kama tayasari isingesimama tungetumbukia wote mtoni maana ile ndio ilikuwa kama kinga yetu. RIP kwa madereva wote wawili pamoja na abiria maana pale pale palikuwa na death kama 20 kwa ujumla wao na wengine walienda kufariki baadae tumbi na muhimbili.

Wakati ule hakukuwa na msaada wa haraka maana ajali ilitokea saa nne na majeruhi walianza kuchukuliwa saa kumi na gari ya jeshi. yani mtu anapoteza damu hadi anafariki.
Dah pole sana mkuu, so sad!!!
 
Asante sana....

Nilipata majeraha kichwani ila baada ya xray muhimbili wakasema nipo vizuri ni vidonda tu, wakati huo hamna ct scan wala mri.

Changamoto ni kuwa nilikuwa boarding school sasa baada ya kupona lazima nirudi shule hapo sasa ndio nilikuwa natamani kuwe na njia nyingine tofauti na wami maana nikishafika pale ni kama naona ndio mwisho wangu.

Aise pole sana, wanadamu tunapitia mengi sana
 
Kutatua tatizo ni kujenga daraja la kisasa, magari mawili yapishane na kila upande uwe na road service in case ..

Kale ka daraja kamejengwa miaka ya 90's ni kembamba mno kataua wengi..

Hata hivyo bracking system ya gari haiwezi ku fail ghafla kama imefanyiwa service yote inayotakiwa...so uzembe na uchakavu wa chombo pia ni chanzo kingine cha ajali nyingi.

Kuna daraja jipya pale wanalijenga waChina ambalo litakua juu zaidi na sehem ya mbali kidogo kulinganisha na hili lala sasa. Pia kwenye kibao cha cotractor wameeka litakua na njia Nne
 
Jamaa amekoea sana.Hivi angekuwa na vits kwa mfano, angethuhutu kweli kusimamia na kusubiri jamaa aje kumgonga kwa nyuma?
 
Mtu anaetakiwa kushtakiwa katika tukio lile ni dereva wa lori lililokuwa mbele ya hili lililotumbukia.

Ukisikia anavyosimulia anasema kwamba, alivyoona roli la nyuma linakuja kwa kasi, akajua ya kwamba tayari limefeli breki hivyo akaamua na yeye kusimama kwa ghafra na kuvuta hand brake ili kuepusha mazingira ya wote wawili kutumbukia mtoni iwapo roli la nyuma lingekuja kuwagonga wakiwa kwenye motion.

Okay, tukubaliane na maelezo yake, lakini, what if kama huyu dereva(marehemu) labda angeweza kulimudu roli lake lililofeli break mpaka likafika usawa wa mwinuko hivyo likashindwa kuendelea kwa kasi ile ile na mwishowe likasimama? Nadhani angeokoa maisha yake na leo kusingekua na mada kama hii.

Kwa nini dereva wa gari ya mbele hakuchukua uamuzi wa kuongeza mwendo(wataalamu mtanifafanulia hapa)kwa kasi ya haraka na kuamua kuvuta hand breki? Kwa mtazamo wangu haya yalikua mauaji yasiyo ya kukusudia, hivyo kwa uelewa wangu nafikiri dereva wa gari iliyokua mbele ya gari ya marehemu ASHITAKIWE KWA KUSABABISHA AJALI NA KUUA BILA KUKUSUDIA.

Mtakao nikosoa, tizameni kwanza video na kisha mje mmejipanga
Mkuu uko sahihi asilimi zote atakakaye kukosoa siyo dereva, kwanza hakuna ruhusa kusimama darajani labda gari imeharibika ghafla kitendo cha yeye kusimama ndiyo kulisababisha dereva wa gari iliyopata ajali akate kushoto kuingia mtoni ili asiigonge gari iliyokuwa mbele yake lakini huyu angevuta kidogo maskini kijana wa watu alikuwa amekaribia kumaliza daraja na asingekufa wala ajali isingetokea gari ingepoa pale milimani. KWA HIYO MIMI NASEMA ASHITAKIWE TU AFANDE MSILIMU SAIDIA HAKI ITENDEKE
 
Mnyenz,

Naona wewe si dereva wa magari.

Malori hasa principle ya uendeshaji wake si sawa na gari dogo.

Hata kwa sehemu tambarare lori haliwezi kuongeza spidi kwa kasi hata ukikamua acclerator yote.
Gari dogo unaweza faulu lakini si lori.
KWA KIFUPI SANA ANGEENDELEA KUTEMBEA GARI ISINGEMKUTA PALE NA DEREVA YULE ASIKATA KUSHOTO KUMKWEPA NA YEYE KUTUMBUKIA DARAJI
 
Mtu anaetakiwa kushtakiwa katika tukio lile ni dereva wa lori lililokuwa mbele ya hili lililotumbukia.

Ukisikia anavyosimulia anasema kwamba, alivyoona roli la nyuma linakuja kwa kasi, akajua ya kwamba tayari limefeli breki hivyo akaamua na yeye kusimama kwa ghafra na kuvuta hand brake ili kuepusha mazingira ya wote wawili kutumbukia mtoni iwapo roli la nyuma lingekuja kuwagonga wakiwa kwenye motion.

Okay, tukubaliane na maelezo yake, lakini, what if kama huyu dereva(marehemu) labda angeweza kulimudu roli lake lililofeli break mpaka likafika usawa wa mwinuko hivyo likashindwa kuendelea kwa kasi ile ile na mwishowe likasimama? Nadhani angeokoa maisha yake na leo kusingekua na mada kama hii.

Kwa nini dereva wa gari ya mbele hakuchukua uamuzi wa kuongeza mwendo(wataalamu mtanifafanulia hapa)kwa kasi ya haraka na kuamua kuvuta hand breki? Kwa mtazamo wangu haya yalikua mauaji yasiyo ya kukusudia, hivyo kwa uelewa wangu nafikiri dereva wa gari iliyokua mbele ya gari ya marehemu ASHITAKIWE KWA KUSABABISHA AJALI NA KUUA BILA KUKUSUDIA.

Mtakao nikosoa, tizameni kwanza video na kisha mje mmejipanga
Video inaonesha yote hayo usemayo?
 
Nilipoiona video nilijiuliza kwa nini dereva aliyetumbukia mtoni asingelivaa kwa nyumba lile la mbele, sikujua ya kuwa wa mbele alisimama. Sioni kosa la wa mbele, ila wa nyuma sijui alifikiri anakwepa nini wakati anajua anaingia mtoni.
 
Nilipoiona video nilijiuliza kwa nini dereva aliyetumbukia mtoni asingelivaa kwa nyumba lile la mbele, sikujua ya kuwa wa mbele alisimama. Sioni kosa la wa mbele, ila wa nyuma sijui alifikiri anakwepa nini wakati anajua anaingia mtoni.
Mkuu dereva alikuwa anakwepa Lori la mbele yake na alizingatia sheria kuwa ukigonga kwa nyuma umevunja sheria hivyo aliamua kutii sheria bila shuruti akatumbukia mtoni hata hivyo naona kama alikuwa sahihi kwa sababu speed aliyokuwa nayo angeigonga ile gari labda wangekufa wote kwa sababu impact ingekuwa kubwa kwao na si kwenye gari ya mbele.
 
Mnyenz,

Hili nililiona tokea tu yule dereva wa mbele alivyoelezea namna ilivyokuwa, eti wangetumbukia mtoni wote! Kivipi? Yeye hata Kama angeweka free tu, inamaana angesukumwa mbele ya daraja, na hata ile impact isingekuwa kubwa kiivyo, na huenda injini iling'oka Pale pale.
Huwezi fikia hitimisho hilo eti impact isingekuwa kubwa!! Impact ingetegemea spidi ya hilo gari lililomgonga!!! Haya mambo yazungumzeni tu ukiwa umekaa!!! Gari liko kwenye mteremko lina mzigo wa tani 30,breki ifeli lije ligonge gari, kwa nyuma usema impact yake utaweza kui thibiti?!!!
 
Huwezi fikia hitimisho hilo eti impact isingekuwa kubwa!! Impact ingetegemea spidi ya hilo gari lililomgonga!!! Haya mambo yazungumzeni tu ukiwa umekaa!!! Gari liko kwenye mteremko lina mzigo wa tani 30,breki ifeli lije ligonge gari, kwa nyuma usema impact yake utaweza kui thibiti?!!!
Dereva wa mbele alijuaje kama lina mzigo wa tani 30?
 
Back
Top Bottom