Ajali ya Meli Zanzibar: Meli kama chombo na mazingira ya ajali

Alwaz

JF-Expert Member
Apr 29, 2010
6,834
10,375
Namba za mabaharia wawili wa muda mrefu wa hii meli hizi hapa.
+255773467746 na +255777899987.
Huyu wa pili ni shujaa kati ya mabaharia kwani ndiye aliyepiga simu akiwa juu ya mlingoti wa meli muda mrefu kuwajulisha ndugu na polisi.
Mara ya mwisho kulingana na mmoja ya waliopigiwa alisema...."Leo ndio tunakufa,tupo juu ya mlingoti hatuzidi watu 30 na simu yangu muda wowote itazima.
Tangu muda huo nami nimejaribu kuwapigia sijawapata.Huenda line yangu ina matatizo nawaombeni nisaidieni kuwatafuta.
 
Zipo dalili zote kwamba hii ajali ya meli iliyotokea Zanzibar haijatazamwa kama janga na pahala pa kupata mafunzo bali imefanywa ni jukwaa la kupiga siasa.
Nasema hivyo kwa kuangalia idadi zinazotangazwa za waliokufa na waliookolewa.
Sijapata kusikia meli imezama tena katikati ya safari na wengi ya abiria wakaokolewa kuliko waliokufa.
Kumbuka meli imezama na ilikuwa imejaza abiria na si mabaharia!
Jee hizi idadi si katika mambo ya kisiasa ili kuepusha kuwajibika?.
 
Awali habari zilipoanza kutoka kuhusu kuzama kwa meli ya mv Spice ilielezwa kuwa zaidi ya watu 2000 wanahofiwa kufa.

Habari zimebadilika mpaka vyombo vya habari vinatangaza watu 163 kufa na zaidi ya 500 kuokolewa.

Kwa wajuzi wa safari za meli na hali ilivyokuwa siku meli ilipoanza safari na kwamba meli yenyewe imezama tena katikati ya bahari zipo kila sababu kuamini kwamba maisha ya watu yamepuuzwa kwa faida za kisiasa.

Ukweli utabaki ni ule wa mwanzo kwamba watu 2000 wanahofiwa kufa. Binafsi nina sababu za kuamini kuwa zaidi ya 1000 watakuwa wamekufa iwapo watakaookolewa watajumlisha idadi ya 2000.
 
Best! Yani hawa mapapa yani wao wanaona kama wa2 hawaoni wala hawatambui kuona kinachoendelea ktk Nchi yao. Kwa mtazamo tu,ina maana yule aliyesema wa2 walikuwa 2000 alikuwa hana mtazamo wa kutambua?
 
Best! Yani hawa mapapa yani wao wanaona kama wa2 hawaoni wala hawatambui kuona kinachoendelea ktk Nchi yao. Kwa mtazamo tu,ina maana yule aliyesema wa2 walikuwa 2000 alikuwa hana mtazamo wa kutambua?
Mimi bwana ni mtambuzi wa meli.
Nionavyo wanasiasa wanataka kulindana ndio maana idadi ya waliokufa inafanywa ndogo na waliookolewa ndio kubwa.
Lakini meli imezama!,na wengi wa abiria ni akina mama na watoto.
 
Nilisikia mmoja wa abiria aliyeokoka akidai kulikuwa na abiria zaidi ya 3elfu..takwimu za kisiasa zinaweza kupingwa iwapo ndugu wa waliosafiri wakijitokeza wote na kuorodhesha wale waliosafiri vs waliookoka kinachobakia ni waliopoteza maisha,,
mungu awarehemu.
 
Nahodha wa hii meli nimewahi kukutana nae.Tangu juzi nampigia simpati.
Katika mazungumzo akijitetea kuhusu jambo fulani,aliashiria kurudisha malalamiko kwa mmiliki wa meli ambaye ni muwakilishi fulani katika baraza la wawakilishi Zanzibar.
 
Nahodha wa hii meli nimewahi kukutana nae.Tangu juzi nampigia simpati.<br />
Katika mazungumzo akijitetea kuhusu jambo fulani,aliashiria kurudisha malalamiko kwa mmiliki wa meli ambaye ni muwakilishi fulani katika baraza la wawakilishi Zanzibar.
<br />
<br />
Hivi hii si ilikuwa meli ya mizigo na abiria, inamaana haikuwa na mizigo kabisa? Maana yake watu elfu mbili au tatu ni wengi sana!
 
Mpk jana waliookolewa ni 750,maiti zimepatikana 263,na mudahuu wa saa3 asubuh meli yauokozi mv serengeti imeshusha maiti zaid ya 800 mm nipo hapa bandarini unguja hao maiti wameokotwa wakielea bado meli hawajaifikia iko ktk kinakirefu sana chini ya bahar,sasa kwamahesabu waliookolewa 750,mait zajana karibu 300 naleo zimepatikana maiti 800 sasa hapo ni hesabu 1850,serikali iache kudanganya watu.tunajionea kwa macho kila kitu hatudanganyiki.
 
Siasa zinaimaliza nchi hii. Je unategemea uchunguzi huru katika mazingira kama hayo? Je tume waliyoiunda itarudisha maisha ya mamia ya watu waliokufa katika hiyo ajali? Ilikuwaje mamlaka zinazohusika zikaruhusu meli iliyobeba abiria zaidi ya uwezo wake isafiri? Sumatra ya Zanzibar vipi? Na je nani atawatetea wananchi hawa ilihali hakuna chama cha upinzani huko kwenu visiwani?
 
Hii ajali itakuwa ndio kubwa kuliko zote Tanzania na pengine Afrika.
Kumbuka wengi wa abiria ni watoto waliotoka likizo.
Pale bandarini kuna jamaa aliyewahi kuponea chupuchupu kufa katika ajali nyengine ya meli.Alipoona jinsi umati ulilvyo ndani ya meli alinyerereka na kurudi nyumbani.Meli ilipozama ilitupa watu baharini kama taka.
Askari wa bandari walipokea chochote ndipo wakaruhusu meli kuondoka huku tayari ilikuwa inavuja ndani.Au hakuna utaratibu wa kukagua ndani mpaka kwenye injini kabla meli kuondoka!.
 
...ni UZEMBE tu,yaliyotokea Mv Bukoba wengi bado tunayakumbuka,Mpaka leo hakuna TULICHOJIFUNZA.Iweje idadi ya waliosafiri isijulikane..??Hapa ndio kuna umuhimu wa SIASA kutenganishwa na BIASHARA...Sasa na hapa WAJIVUE GAMBA kama sio NGOZI.
 
jamani mungu awatienguvu walio okolewa na aziweke roho za marehemu wote mahalipema peponi. Ameni
 
Natamani Mungu angekuwa anashuka at the moment pindi mtu hasa kiongozi mkubwa wa cnhi au idara unaudanganya umma,hivi ni kweli waliokolewa hai wanafika idadi hiyo,na je waliokufa ni idadi hiyo tu?kama ni hivyo manifesto iwekwe wazi mbona kama imepotea?na je meli ilikuwa imebeba tani ngapi za mzigo na je capacity ya meli ni kubeba tani ngapi?je Nani alisaini Meli kuondoka bandarini,nani aliifanyia ukaguzi kabla ya kuondoka?Je report za kitaaluma zinasema meli ilikuwa na tatizo gani kwa kipindi japo cha miezi mitatu ya nyuma na je ilipatiwa matengenezo?Je ilituwaamini hawa kwa siku zijazo wananchi na waathirika wote wa majanga makubwa haya tufanyaje?maana ya MV Bukoba,ya Treni pale Nsagali-karibia Dodoma na la MV Spice kutokea inamaana hakukuwa na fundisho lolote kwa matukio ya nyuma na mambo yaliendelea kufanyika kwa mazoea.Tuambie ukweli tujue watanzania wenzetu wangapi wamepoteza maisha,jamani wenzetu mlioko Zanzibar shirikianeni na walioko Pemba mjue ukweli wa ndugu waliofariki,wala msitumie JF kutoa habari zisizo rasimi semeni ukweli tutawaamini kuliko wenzetu wa Chama chetu na mwenzao B.
 
Hii ajali itakuwa ndio kubwa kuliko zote Tanzania na pengine Afrika.&lt;br /&gt;<br />
Kumbuka wengi wa abiria ni watoto waliotoka likizo.&lt;br /&gt;<br />
Pale bandarini kuna jamaa aliyewahi kuponea chupuchupu kufa katika ajali nyengine ya meli.Alipoona jinsi umati ulilvyo ndani ya meli alinyerereka na kurudi nyumbani.Meli ilipozama ilitupa watu baharini kama taka.&lt;br /&gt;<br />
Askari wa bandari walipokea chochote ndipo wakaruhusu meli kuondoka huku tayari ilikuwa inavuja ndani.Au hakuna utaratibu wa kukagua ndani mpaka kwenye injini kabla meli kuondoka!.
&lt;br /&gt;<br />
&lt;br /&gt;<br />
Ami! Yaelekea unapoteza kumbukumbu sometime,kwa sbb hii pigo la leo ni cha mtoto kwa ile ya Mv Bukoba. Ile kuwa kiboko kwani takwimu pamoja na serikali ya awamu ya tatu kukataa kutangaza lakini hakika ilikuwa zaidi ya watu 4,700 walipoteza maisha ila kumbuka kbs ya kwmb mapapa waliipotezea wakasema watu walikuwa 1500 tu. Yani bila mabadiliko ya haki hakika tutaendelea kuwapoteza ndg,jamaa na hata marafiki we2. Walale kwa Amani ya Bwana wale wote waliotutangulia mbele ya haki. Mapapa kweli ni janga kwa Taifa le2.
 
Siasa zinaimaliza nchi hii. Je unategemea uchunguzi huru katika mazingira kama hayo? Je tume waliyoiunda itarudisha maisha ya mamia ya watu waliokufa katika hiyo ajali? Ilikuwaje mamlaka zinazohusika zikaruhusu meli iliyobeba abiria zaidi ya uwezo wake isafiri? Sumatra ya Zanzibar vipi? Na je nani atawatetea wananchi hawa ilihali hakuna chama cha upinzani huko kwenu visiwani?

Tusidanganyike na hizi SUMATRA,EWURA NA TCRA hivi vyombo vyote viko kisiasa zaidi badala ya kufanya kazi yake,vyombo hivi vilitakiwa viundwe na walaji sio serikali,mfano mzuri ni chama cha wapangaji lakini serikali inakijima nguvu ya kisheria ili kifanye kazi yake vizuri.
Ndio maana hata walaji tunaonewa hovyo kwa sababu mtetezi yupo kwenye gamba la serikali,viongozi wanateuliwa na Raisi unategemea nini hapo?Watanzania tutaendelea kufa kwa kila namna,wafanya biashara wakubwa miongoni mwao ni viongozi wakubwa serikalini hivi vyombo havitafanya kitu,mfano Mafuta bei zake ni za ajabu ajabu tu,chombo ambacho tulitegemea kitusaidie ndio kina side na hao hao wafanyabiashara.
 
Waziri anayehusika na usafirishaji SMZ anasubiri nini? Na nasikia anatokea CUF. Siyo ndo wakati wa ndugu zetu CUF kuonyesha tofauti yao na CCM.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom