Ajali ya Meli: Maoni na mtazamo wa wananchi kwa yaliyojiri

GHOST RYDER

JF-Expert Member
Jun 10, 2011
1,025
475

Baada ya Tukio la MV Bukoba katika ziwa VICTORIA na kama idadi ya watu wanaohofiwa kupoteza maisha ikawa hiyo inayodhaniwa kati ya 1500 - 2000 itakuwa ni ajali ya majini kubwa kuliko zote katika historia ya Taifa hili. Huu ni msiba usioelezeka (endapo idadi itakuwa hiyo ama kuvuka)

Kwa mintarafu hiyo Uncle Lundenga na Ndugu yangu George Rwehumbiza hamna sababu yoyote ya kuwaweka Watanzania pale Mlimani City wakimkufuru Mungu huku wengine wanaomboleza. Najua mnaweza kutia pamba masikio na mkaamua kuobserve silence kwa dakika 1, lakini dhambi hii haitawatoka kamwe kama mtapuuza maono haya.

Kama kawaida yetu tutasema unajua tumekodi na kulipa gharama kubwa kwa wataalam kutoka maeneo mbalimbali ndani na Nje ya Tanzania kwa hiyo hatuwezi kupoteza fedha hizi na hakuna wa kuzilipa tena kuandaa Tamasha, Aaah nyie watu hizi fedha za nani kama si wauza vitumbua na karanga wa msata hadi mahenge ambao hawalali wakikesha kutuma meseji na kushiriki bahati nasibu wasiyoshinda hata siku moja huku shilingi zao zikiteketea kama fupa katika domo la fisi.

Ndugu zetu wapendwa wa VODACOM na LINO AGENCY INTERNATIONAL kaeni meza moja na mtafakari hili msiba huu leo ni mkubwa kwa Taifa, hatuna haja ya kusherekea kupitia matangazo ya LIVE katika Luninga kwa mabinti zetu kupita wakiwa Nusu Uchi huku mamia ya ndugu zao bado wapo majini miili yao ikiwa inasakwa na huzuni kubwa imeligubika Taifa.

Kila jambo ni mapenzi ya Mungu na kwa moyo wa Unyenyekevu kabisa natoa pole kwa familia zilizoguswa na msiba huu kwa niaba ya wana JF wenzangu.

Bwana Alitoa, Bwana Ametwaa...Jina lake lihimidiwe

Ina lilah waina ilaih rajuun

sfsf.jpg

Kaka Mkubwa amerejea katikati ya Sintofahamu Nyingi...Inakadiriwa waliopoteza maisha ni 192 kwa mujibu wa REUTERS, Zanzibar Yatangaza Maombolezo ya Siku 3, BLOG ZOTE ZASUSIA Highlight za Tamasha ambazo miaka yote hutoa dondoo za awali...MOYO WA UZALENDO (MICHUZI, Sufiani Mafoto, Full Shangwe, G Sengo na Wengine)


ADIOS
 
Nilikuwa sina taarifa hii naangalia news CNN nikaona wanabreak news about Tanzania nikaona niweke TV ya Taifa, nakutana na watoto wanaimba kwaya

Hivi hii TV ya taifa inayoendeshwa na my PAYE ina faida gani jamani ?

Poleni wafiwa, its national mourning and I hope the pageant(sp) will be postponed
 
Tumefiwa na wapendwa wetu kweli ila shughuli zingine ni lazima ziendelee. Maisha ni lazima yasonge mbele.
 
Hii kitu ukiitazama kwa juu ni kama iko pouwa tu..ila ukiitazama kwa undani ni kama unaweza kushangaa
Usiku wa jana ...huko Zanzibar au Tanzania Visiwani..wamepatwa na msiba mkubwa sana..wakupoteza watu wengi kwa ajari ya meli

Leo jumamosi..Tanzania Bara tunafanya shindano kubwa la urembo ..Vodacom Miss Tanzania..kumbuka Miss Tanzania haina mshiriki toka Zanznibar(Tanzania Visiwani)...

Je hii haiwezi kuzua mjadala...kwa wazanzibari

Ni wangu mtazamo
 
Wakuu nimestaajabishwa sana na hili hasa kwa upande wa TV stations ikiwa za nje zimeweza kuujuza ulimwengu kwanini TV stations zetu hawana updates/wamechelewa kutuletea updates zaidi ya kutuonyesha cartoons na maandishi kupita kwa chini? Au wapo busy na Miss Tanzania? Inasikitisha sana.
 
Kama wana busara wataahirisha hayo mashindano yao ya umiss..
 
Zanzibar ni wilaya ndani ya JMT.Zipo wilaya nyingi ambazo hazina uwakilishi kwenye mashindano ya Miss Tanzania Zanzibar ni mojawapo wa wilaya zilizokosa uwakilishi nini cha ajabu !.

Hii kitu ukiitazama kwa juu ni kama iko pouwa tu..ila ukiitazama kwa undani ni kama unaweza kushangaa
Usiku wa jana ...huko Zanzibar au Tanzania Visiwani..wamepatwa na msiba mkubwa sana..wakupoteza watu wengi kwa ajari ya meli

Leo jumamosi..Tanzania Bara tunafanya shindano kubwa la urembo ..Vodacom Miss Tanzania..kumbuka Miss Tanzania haina mshiriki toka Zanznibar(Tanzania Visiwani)...

Je hii haiwezi kuzua mjadala...kwa wazanzibari

Ni wangu mtazamo
 
mkuu Ngongo umeua kabisa...kwahiyo sio kesi wao kukosa mwakilishi miss tanzania...hahahahahaahaha..twende tukawape pole..
na pia Invisible atoe taarifa ya rambi rambi kwa msiba huo..kwa niaba ya wanajf wote
 
shossi ..unazungumzia hizi media zetu makanjanja?....mie natoka pale itv saa hz ndio wanapeleka mtu znz...mpk arudi Aljazeera washamaliza kila kitu katika habari...wacha tu subiri saa mbili tuliyozea
 
Wakuu nimestaajabishwa sana na hili hasa kwa upande wa TV stations ikiwa za nje zimeweza kuujuza ulimwengu kwanini TV stations zetu hawana updates/wamechelewa kutuletea updates zaidi ya kutuonyesha cartoons na maandishi kupita kwa chini? Au wapo busy na Miss Tanzania? Inasikitisha sana.
wanasubiri maelekezo wasema watu wangapi wamekufa.....
 
Hakika isipohairishwa leo kweli VODACOM japo hakuna sehemu yoyote wanafungwa kwa hilo lakini kama wanajali wanuwezo mkubwa sana kuhairishwa tamasha hilo [Event].

Ni kwa faida yao na kwa jamii kuwa wanajali na kuwa wao ni sehemu ya Watanzania kama corporate social responsibility kwao kuwa wanajuha kuwa jamii ya Watanzania leo imeondokewa na mamia ya Watanzania kwa ajali ya Meli huko Zanzanzibar.

Kwenye mikataba yao na makampuni waliyo outsource shughuri hiyo nadhani kuna vipengele vya demage caused by nature disaster.[Force M] wanaweza kutumia kuhairisha kwa muda.

Nia kwa nia njema ya kutengenezaa positive impression juu ya macho ya Watanzania na kuonyesha kuwa mnajali hata wakati wa matatizo nyie ni sehmu ya jamii.
 
Nyie watu vipi? Misiba mbona iko kila siku. Msiba unatokea kwenye familia au ukoo na wanandugu wanakuja kutoa pole kisha hao wanaendelea na shughuli zao.

Hii standard ya kusema shughuli zisitishwe kisa msiba imeanza lini?

Naunga mkono kusimama kimya dakika moja kuwakumbuka marehemu, lakini sio kusitiisha shughuli yote.
Inategemea ukubwa wa msiba au janga mkuu
Kupoteza watu zaidi ya 200(idadi kamili bado kuthibitishwa?) siyo msiba mdogo
 
Nilikuwa nasoma habari ya ajali ya kuzama meli huko Unguja na Pemba, BBC kama tulivyo watanzania wengi nao wameshindwa kuelezea ajali ilipotokea.
Habari yao inachanganya na kuibua maswali Tanzania ni nchi gani? Je Zanzibar ni Nchi au Kisiwa? Je Pemba ni sehemu ya Zanzibar? Unguja ni wapi kwenye ramani ya dunia?
Angalia hii habari na ramani iliyowekwa na BBC BBC News - Zanzibar ferry disaster: Scores die, many more missing.
nadhani tunahitaji kuweka mambo clear kutambua nchi zinazotengegeza muungano wa Tanzania.
 
sasa wakisubiri taarifa ya polisi..watakuwa wameenda kutafuta habari au kuchukua habari?...media zetu bana..uwiiiiii
 
Shossi vyombo vyetu vya habari ikifika usiku sisi tukilala navyo vinalala vinaamka saa 12 asubuhi.

Umeongea maneno ya msingi na yenye ukweli usiopingika tena wanatuona mafala wote wanatukusanya saa mbili usiku tunakuwa wajingaaa tukiahamishahamisha stations
 
sasa wakisubiri taarifa ya polisi..watakuwa wameenda kutafuta habari au kuchukua habari?...media zetu bana..uwiiiiii

Rafiki yangu yeye hakujizuia hisia yake amesema kwenye facebook
[h=6]Saleh Mahdi

kama mzanzibari sitaitazama tena TBC kwa upuuzi waliotuonesha yaani watu wako na huzuni eti wao wanaonesha katuni na kila mzanzibari mwenye uchungu na nduguzetu walopotea lazma itawagusa allah awape jannah waliokufa shahid baharini[/h]
 
8 Reactions
Reply
Back
Top Bottom