Kibaki anajali watu wake. Ingekuwa watanzania ndiyo yamewakuta huko Kenya hata balozi wetu asingehangaika achia mbali kutuma ndege. Sisi tunaitana ndugu lakini ukweli si ndugu kitu bali unafiki. Tunawacheka wakenya kwa ukabila wakati sisi tunao tena jumlisha ujimbo, udini hata uanachama. Kimsingi, Tanzania went to dogs the day mwalimu Nyerere left the state house. Tuna serikali ya kuhudumia genge dogo la walaji wasio na shukrani wala visheni isipokuwa kujihudumia na kula kwa miguu na mikono tena bila kunawa. Good Job brother Mwai wa Kibaki jamba ya Othaya. Ni wega muno (samahani kwa kutumia lugha ya Kibaki).
Toa basi mifano kuthibitisha hoja yako.Umesahau kuna mawaziri wamejiuzulu na wameshatakiwa UN kwa kufadhili mauaji ya kimbari?Kibaki huyu huyu kalazimisha ushindi matokeo yake watu zaidi ya 1,000 waliuawa mbona hakupeleka ndege sehemu za mauaji?
Unajua kua waathirika wa ajali ya juzi 90% walikua ni wakikuyu?je wangekua wajaluo angeleta ndege?