dubu
JF-Expert Member
- Oct 18, 2011
- 3,495
- 3,458
Watu 50 wamenusurika kifo baada ya basi la Mbukio Mission waliokuwa wakisafiria kugongana na lori la mafuta katika eneo la Mlima Nyoka,mkoani Mbeya.
Ajali hiyo inaelezwa kuwa imetokana na mwendokasi ambapo basi hilo lilimshinda dereva nguvu wakati akitaka kukwepa lori hilo la mafuta na hivyo kujikuta akisababisha ajali,ambapo baada ya ajali baadhi ya vijana ambao hawakufahamika majina yao mara moja walionekana kuziba maandishi ya basi hilo la abiria kusudi waandindishi waliokuwa wakipiga picha wasipige picha jina la basi hilo, bila kujua sababu ya msingi.
Hata hivyo Dereva wa lori lililokuwa na namba za Usajili T3332 Aaga Bw,Godfrey Lymo(33) yeye amejeruhiwa vibaya kufuatia ajali hiyo.
Chanzo:ITV