Ajali Tanzania: Mawazo mbadala kuhusu udhibiti wa ajali Tanzania

SMU

JF-Expert Member
Feb 14, 2008
9,616
7,862
Hivi karibuni na hata siku za nyuma tumeshuhudia malumbano kati ya wamiliki wa mabasi ya abiria kwa upande mmoja na serikali (Polisi, Sumatra) kwa upande mwingine juu ya ulazima wa kufunga vidhibiti mwendo (Speed Governor) kwenye mabasi.

Wamiliki wa mabasi wanasema speed governor hazijasaidia kupunguza ajali za barabarani. Na zaidi wanaona msisitizo wa serikali wa kufunga speed governor unamsukumo wa kibiashara zaidi kuliko kupunguza ajali.

Je ni kweli speed governor hazisaidii kupunguza ajali? Kama hazisaidii, je nini kifanyike kupunguza ajali za barabarani?
------------

ajali-jpg.322579


Ndg wanabodi Heshima kwenu..

Bila shaka vifo vingi vinavyotokea kwa kiasi kikubwa hivi sasa ni kutokana na ajali za magari barabarani hasa Mabasi..

Tunaipongeza serikali kwa hatua mbalimbali ambazo imekua ikichukua ili kukabiliana na Changamoto hii kubwa japo kwa kiasi kikubwa bado ajali ni janga kwa nchi yetu..

Kwa kua akili ni nywele na kila mtu anazake,nami pia naomba kuwashirikisha fikra nilizonazo kama ifuatavyo..

1)SERIKALI IANZISHE VYUO MAALUMU KWA AJILI YA MAFUNZO YA UDEREVA WA MAGARI YA ABIRIA PEKEE..

Serikali na sio vyuo binafsi vianzishe vyuo maalumu kwa ajili ya Madereva wa Abiria pekee...
Hii itasaidia kupunguza madereva wa Mtaani wanaopiga dayworker kisha baada ya Muda wanaendesha mabasi ya Abiria.

Nimesema vyuo maalumu na wala si VETA wala vyuo binafsi Kutokana na sababu kua sasa ,VETA na vyuo vingine binafsi vimekosa credibility yaani mtu yeyote anaweza pata leseni hata kwa magumashi ilimradi awe na pesa..

Lakini pia ili mtu A-qualify kusomea udereva wa magari ya abiria awe amesoma mpaka kidato cha nne na awe amefaulu ili kupata watu makini wanaojielewa na si kuokoteleza hadi STD VII kama ilivyo sasa.

2)KILA BASI LISAFIRI NA ASKARI WA BARABARANI ANGALAU MMOJA:

Sio lazima askari aanze mwanzo wa safari mpaka mwisho wa safari...kunaweza kua na utaratibu wa askari maalumu wa barabarani kupokezana kila wilaya ambako gari hiyo itapita..hii itasaidia kwa kiasi kikubwa kum-control driver hivyo kufata sheria zote za barabarani kama inavyopaswa.

3)MISHAHARA YA MADEREVA IBORESHWE

Hii itasaidia watu wengi kuwa motivated na kupenda kazi ya udereva ma mabasi hivyo kupata watu wengi wanaoqualify,hii inamana mtu aiendeshe gari kwa kua ameona ndo sehemu ya kutokea bali udereva uwe tamanio la mtu mwenyewe.

Wapewe pesa ya kutosha na posho juu ili kumfanya Dereva afurahie kazi yake na kupunguza msongo wa mawazo..

4)MISHAHARA YA ASKARI WA BARABARANI IBORESHWE


Hii itasaidia kwa kiasi kikubwa askari hawa kutoshawishika kuchukua pesa ndogondogo wanazopewa njiani hivyo kupelekea kufanya kazi zao kwa uaminifu na umakini wa hali ya Juu.

5)ASKARI WA BARABARANI WAPUNGUZWE

Wingi wa Askari wa barabarani waliopo hivi sasa haimanishi ni kuboresha utendaji na udhibiti wa ajali barabarani..unaweza kua na askari wachache na wakafanya kazi nzuri yenye zaidi,iwapo madereva hawataokotwa mitaani,wakalipwa pesa vizuri na askari nao wakalipwa pesa vizuri hakika makosa barabarani yatapungua kwa kiasi kikubwa..hii ina apply kwa madereva wa magari yote barabarani...

Iwapo adadi ya askari barabarani itakua ndogo itakua rahisi kuwa hudumia financially na kwa pesa nzuri zaidi.
Nashauri askari barabarani walipwe kuanzia milioni 1 kwa Mwezi.
Utitiri wa askari barabarani haimanishi ndio uimarikaji wa utendaji kazi.

6)UKAGUZI WA MABASI YA ABIRIA KABLA YA SAFARI UIMARISHWE..

Ukaguzi wa maramojamoja unaofanywa na askari wa barabarani kwa sasa unamapungufu makubwa..
Pawe na kikosi kazi maalumu ambacho kazi yake ni kukagua mabasi yote ya abiria siku moja kabla ya safari na gari hiyo iwe na alama kua imekidhi vigezo vya kusafirisha abiria kesho yake..Hii itasaidia hasa kupunguza ajali zitokazazo na uchovu wa magari yenyewe hasa yale yanayounga safari bila kupumzishwa..
ikiwa na pamoja na kumpima dereva kabla ya kuanza safari kama hatumii madawa ya kulevya wala kilevi chochote..

7)SUMATRA WASIFANYE KAZI KWA MATUKIO PEKEE
SUMTRA Wasisubiri kupaza sauti katika kuwaambia umma kua nauli zitapanda kutokana na bei za mafuta kuongezeka,na wasisubiri mpaka matatizo yatokee ndo wajitokeze kwa waandishi wa habari kama wanavyofanya hivi sasa.SUMATRA Ifanye kazi yake ipasanyo na isifanye kazi kisiasa...

Nimesema ni mawazo tu sio msaafu wala Biblia unaweza kosoa au kuboresha kwa Mtazamo chanya ili kutoa mawazo sahihi kisha yafanyiwe kazi na mamlaka husika.

Karibuni kwa Mawazo chanya pia.

Mpangawangu said:
Kwanza kabisa nikupongeze kwa kuguswa na hili na kutuletea mada yanye tija kwa kila mmoja wetu,nategemea kuwaona watu mkiweka maoni yenu hapa kuliko kushabikia siasa zinazojadili watu badala ya mijadala yenye tija kama hii.

Naungana na yote uliyoyasema isipokuwa hilo la mabasi kusafiri na Askari.

Mawazo yangu ili kudhibiti ajali ni lazima kwanza kutambua vyanzo vya ajali,

pamoja na vyanzo kuwa vingi lkn mwendo kasi na uzembe wa madereva ndio chanzo kikuu cha ajali za barabarani.

Suluhisho ni kuwapangia muda madereva kufika kwenye vituo.

Mfano mabasi yaondoke Dar saa 12.00 alfajiri na yafike morogoro saa 4:00 yafike Dodoma saa 8:00,yafike manyoni saa 9:30,Singida Saa 11:00,Misigiri saa 12.30, Igunga saa 1:50,Nzega Saa 2:30 na hatimae kahama saa 4:00.


Masaa hayo yapangwe kitaalamu na watu wa sumatra baada ya kujiridhisha umbali toka eneo moja kwenda eneo jingine,

Kila kituo kiwe na askari ambao wapo serious na kuwepo na utaratibu kama ule wa treni wa kupewa line clear,hivyo mtu atachukua kibali maalum mahala anapoanzia safari kinachoonyesha muda na atapaswa kukabidhi kibali hicho kwenye kituo cha mbele na kupewa kingine kinachomruhusu kuendelea na safari,afanye hivyo mpaka mwisho wa safari yake,.

ili kuepusha usumbufu maeneo vinapotolewa vibali pawepo na vyoo pamoja na hotel za kula chakula,lengo ni kutumia mudaa wa kuonyesha kibali huku abiria wakiruhusiwa kuchimba dawa na kupata chakula,hivyo hakutakuwa na malalamiko,

Kama hilo halitoshi tunaweza kuyatumia maeneo mizani kama check point ya muda wa kuwasili eneo husika.

tukifanya hivi italeta self control ya madereva ,adhabu yake iwe kuahirishwa safari na abiria kuwekwa katika mabasi mengine kwa kibali maalum na dereva kuwekwa ndani mwezi mmoja na gari kufungiwa kusafirisha abiria kwa muda wa mwezi mmoja.


kama tutafanya hayo hakika hakuna dereva wala mmiliki wa gari atakaefika eneo husika kabla ya wakati.

Kufanya hivyo kutawafanya madereva kutembea mwendo wa kawaida na hivyi kupunguza ajali kwa kiwango kikubwa.

Pendekezo hili ni baada ya safari yangu toka Dodoma,gari ya kwanza kufika Dodoma ilikuwa campuni ya KISBO ikiduatiwa na Leina na CITY BOY.


Hizi ni basi zilizojizolea umaarufu kwa kukimbia kupita kiasi kiasi cha kufika kahama saa 12:30 badala ya saa tatu usiku.

Tulipofika manyoni walisimama petrol station na kutueleza abiria kuwa tunasubiri muda wa kufika Singida.

ilikuwa saa 7:20 za mchana na singida tulipaswa kuingia kuanzia saa 10.30 au zaidi ya hapo.

Hivyo tulilazimika kukaa muda wa saa moja na nusu ndipo tukaendelea na safari,


Gari zoote zilizotoka Dar zilikuwa kama msafara na hakuna aliethubutu kukimbia,waliogopa faini kubwa ambayo hutozwa singida endapo Gari itafika kabla ya muda uliopangwa.

Mwisho ni kwetu wapiga kura ambao ndio wahanga wa ajali hizi,tusiwachague tena wafanyabishara kuwa wabunge wetu,maana wengi wao hutumia fursa ya vyeo vyao kuwafanya hata askari Polisii wayaogope magari yao.

Chrizant Kibogoyo, post: 21072131, member: 380599"]KUNA UHUSIANO GANI KATI YA VYETI ALIVYONAVYO DEREVA, UJUZI ALIONAO DEREVA, KIPATO HALALI APATACHO DEREVA, NA ONGEZEKO LA HIZI AJALI ZA BARABARANI?

Kwa muda mrefu kama taifa tumekuwa tukijaribu kupunguza ajali za barabarani kwa kutumia mbinu za askari wa usalama barabarani kuwabana madereva. Japo yapo mafanikio, lakini kushindwa kwa sekta/idara zingine kushiriki kupambana Na ajali barabarani husussn zinazohusisha mabasi ya abiria kuna punguza mafanikio hayo.

Katika mchezo wa soka kuna msemo maarufu kuwa "Football is a game of mistakes" Na inadaiwa karibu magoli yote yanayofungwa katika mchezo huo utokana Na kosa/makosa ya wachezaji wa timu iliyofungwa. Hivyo basi kama kila kosa lingeweza kusababisha maafa, majanga,misiba na simanzi kama makosa ya kibinadamu afanyayo dereva. Dunia/nchi vingekuwa na katika wakati mgumu sana.

Hivyo basi dereva ana nafasi ya kipekee katika Jamii. Je ni kweli Jamii zetu zinatambua hilo? Chukua mfano wa kosa/makosa ya kibinadamu aliyofanya dereva mwenzetu wa basi la wanafunzi lililopata ajali huko Karatu. Kosa/makosa take yalisababisha simanzi nchi nzima, watu 33 wakapoteza uhai Na madhara mengine mbali mbali.

Ni kwanini jitihada kubwa za kikosi cha askari wa usalama barabarani zinashindwa kupunguza kwa uendelevu tatizo hili (yaani hata zisipokuwepo tochi, pasiwepo ajali za mabasi ya abiria)?

Kwa mtazamo wangu kutokana na uzoefu nilioupata nikiwa kiongozi was madereva wa mabasi. Mchawi ni mfumo wetu wa usimamizi was sekta ya ussafirishaji unamfanya dereva was basi la abiria kuwa mtekelezaji muhimu wa ukuzaji mapato ya kampuni Na yeye binafsi.

Kutokana na upungufu huo dereva w basi kipaumbele chake cha kwanza in mapato ya kampuni ili aweze kuendelea kuwepo katika ajira hiyo kupitia kushindana kuipatia kampuni abiria zaidi. Pili ni kuongeza kipato chake binafsi kwa kuwa ujira wao ni Mdogo sana kulinganisha na majukumu yao na umuhimu wao katika Jamii. Tatu ndio hufuata kutumia ujuzi wao vyema na Nne ndio kuzingatia n kutii sheria za usalama barabarani. Mfano hai ni ajali za hivi karibuni za mabasi ya Ally's Na BM coach.

Mfumo wa uendeshaji wa BRT unamfanya dereva kipaumbele chakeiwe ni kiwe kutii na kuheshimu taa na alama za vivuko vya waenda kwa miguu n.k ili aweze kuendelea na ajira yake. Hii ni kutokana ukweli kuwa dereva was BRT sio sehemu ya utekelezaji wa mipango ya kukuza mapato ya kampuni kupitia ushindani wa kupata abiria zaidii.

Tukiondoa umachinga ktk sekta yetu ya usafiri wa umma kwa kuwepo utitiri wa kampuni za mabasi hususan kati ya mkoa mmoja hadi mwingine. Na badala yake tukawa na professional passengers operators wenye uwezo wa kuwekeza ktk yafuatayo:- a) Mabasi ya kisasa kulingana Na miundombinu yetu (b) Raslimali watu yaani madereva, makondakta, mafundi n.k wenye ujuzi Na weledi was kutosha (c) Kuwekeza ktk stahiki za watumishi ikiwemo mishahara bora, malipo mengine kama vile Masaa ya ziada, matibabu,kiinua mgongo n.k (d) Kuwekeza ktk teknoljia za kufuatilia Na kudhibiti mienendo ya watumishi kama vile Tachometer, Tachograph katika Magari yao n.k. Na hivyo kupunguza ajali za mabasi kama sio kuzimaliza kabisa Na vile vile serikali kupunguxiwa mzigo mkubwa was kuwa idadi kubwa ya askari bsrabarani kudhibiti madeteva hawa toka utitiiri wa kamouni za mabasi kutokana uwepo was kamouni za mabasi zenye mifumo ya ndani (inernal mechanisms) ya kudhibiti madereva wake Na kuwaondoa wale wasiofaa kabla yavkusababisha ajali


"Samurai, post: 28308232, member: 28531"]Tumekua na ajali za mara kwa mara ambazo haziishi lakini sidhani kama mpaka sasa vyanzo hivi muhimu vya ajali vinazungumziwa zaidi ya kuambiwa tatizo ni mwendo kasi, na Uzembe wa dereva.

Fatigue, Umasikini, Ubovu wa barabara, Elimu ndogo ya vyombo vya moto, Elimu ya msingi (std 1 to std 7), pia ni vyanzo vikubwa sana vya ajali hapa Tanzania.
Nitaelezea kwa uchache na wengine wataweka nyama.

FATIGUE (UCHOVU):
Madereva wengi wa malori, mabasi na hata gari ndogo huwa hawapumziki vya kutosha kiasi cha kufanya safari ndefu, Madereva wa mabasi na malori husafiri mamia ya km lakini huwa hawalali vya kutosha kiasi cha kuwa na nguvu ya kuanza safari siku inayofuata. Wengi wa madereva hawa wakifika kwenye vituo vyao vya kupumzika huanza kufanya starehe kwa maana ya pombe na umalaya na matokeo yake asubuhi huamka na hangover ya K**MA na POMBE, hangover ya hivi vitu viwili ni usingizi na uchovu kupitiliza siku ya pili yake. Elimu ya kujitambua na kuirasimisha hiyo ajili ndio muarobaini pekee kwenye hili, vijana wanahitaji elimu ya kutosha ya kujitambua na Serikali iifanye hiyo kama ajira rasmi kwa maana ya watu walipwe mishahara, night allowance's na wawe na mikataba inayotambulika kisheria wakatwe PAYE NA HIFADHI YA JAMII.

UMASIKINI:

Jamii nyingi sana za kitanzania ziko kwenye umasikini mkubwa na huu umasikini ni chanzo cha matatizo mengi sana Tanzania.
Jamii nyingi za kimasikini ndio zimetoa hawa madereva wengi wanaoendesha roho za watu huko barabarani, na jamii hizi za kimasikini zimekuwa tegemezi sana kwa hawa ndugu zao ambao ni madereva wetu, Shida/Umasikini huleta stress na mwisho wa siku hupunguza umakini barabarani. Dereva huyu anapenda kuwapa wanae elimu bora kama wengine maana anaona mateso anayoyapata yeye barabarani, Dereva huyu anahitaji kusomesha ndugu zake wapate elimu bora, Dereva huyu anahitaji kuwa na nyumba bora ya kuishi, Dereva huyu anahitaji kuwapa matibabu ndugu na wanae, Dereva huyu anahitaji kuwa lishe bora watoto wake, Dereva huyu anahitaji kulea wazee wake choka mbaya wanaishi kijijini huko, HAYO YOOTE MWISHO WA SIKU HULETA STRESS KWA HUYU DEREVA NA MATOKEO YAKE NI KUPUNGUZA UMAKINI AU KUTOKUWA MAKINI KABISA.

Serikali au wenye mamlaka lazima watambue umasikini ni tatizo kubwa Tanzania na tukiwatoa watanzania kwenye umasikini tutakuwa tumetatua mengi, Dereva na ndugu zake wakiwa na kipato kizuri ataishi maisha ya furaha na kazi yake ataifanya vizuri na kwa umakini maana ndio inamuweka mjini ( mfano Madereva South Africa, Botswana, Namibia,Zambia pale London, USA nk).

UBOVU WA BARABARA:

Tanroad jaribuni kuwa na road patrol za mara kwa mara kila mkoa, kila wilaya ili mjue matatizo yaliyopo kwenye barabara zebu na muamue haraka, uzibaji wenu wa viraka bado ni wakizamani na huchukua muda mrefu, barabara zinakaa na mashimo na mibonyeo kwa muda mrefu sana (hapa ni vyema kila Tanroad mkoa ikawa na fungu la emergency){naikumbuka ajali ya basi la MAJINJA PALE KATI YA IRINGA NA MBEYA NA LILE KONTENA CHANZO NI LILE SHIMO PALE).

Tanroad ni vyema mpeleke watu wenu nje wajifunze namna bora ya usimamizi na ujenzi wa barabara ili mwisho wa siku tuwe na Standard yetu ya ubora wa barabara zetu ili kila mjenzi akija tunampa specifications zetu, Kona zisizo na msingi ni nyingi kwenye barabara zetu kiasi cha kutengeneza hatari zisizotakiwa, Maeneo korofi yote yakijengwa mjaribu kuyafanya yawe mapana na ikiwezekana muweke TAA eneo husika ili usiku iwe rahisi. TANROAD NA SERIKALI acheni siasa kaeni chini mchunguze kwa wenzetu ili tupata standard yetu ya ubora wa barabara zetu na tuachane na hizi barabara zinazobonyea na kuchimbika kila siku, kona sehemu zisizohitajika (kifupi makona sio muhimu mbona Kenya hapo wanatushinda hawana kona zisizoeleweka, kule Zambia pia mbona hakuna makona kona kila mahali)

ELIMU NDOGO YA VYOMBO VYA MOTO.

Watanzania wengi wanamiliki na kuendesha vyombo vya moto lakini hawajui matumizi sahihi ya vyombo hivi kifupi wengi hawavijui hivi vyombo sio lazima uwe fundi au proffesional driver hapana hapa tunaongelea General knowledge ya kujua magari na tabia zake mfano huwezi ukawa na IST unataka kuovertake FORTUNER na mbele yako linakuja LANDCRUISER V8 na bado unajiamini utaliwahi, huwezi ukawa na gari yako inachelewa kubadili Gia na wewe huna habari, Ufanyaji wa service kwa wakati na kujua wakati sahihi hii sio kazi ya Fundi, Oil sahihi kwa matumizi ya Gari, Upepo sahihi kwa matumizi ya Gari lako, kwa wale wanaondesha manual kujua wakati gani utumie gia gani, Waendeshaji wa Magari sio lazima uwe umeajiriwa kuna umuhimu wa kulijua gari zako hata kwa kusoma broachure mbali mbali za magari, kuangalia vipindi mbalimbali vya magari, kuzungumza na wataalamu wa magari upate abcd za magari ili ubongo ujue matumizi sahihi ya magari na barabara.

ELIMU YA MSINGI (STD 1- STD 7).
Hii elimu ni nzuri na muhimu sana kwa watu kuwa na uelewa na kujitambua, Elimu ya msingi humsaidia mtu kujijua yeye ni nani na anatakiwa afanye nini, Elimu ya msini humsaidia mtu kujua kusoma na kuandika na hili litamsaidia mtu kujua na kuelewa alama mbalimbali za barabarani, Elimu ya msingi itamfanya mtu kuwa muelewa hata pale anapokosea na kuruhusu kueleweshwa na sio kuwa mbishi, Elimu hii humfanya mtu ajielewe na kuwa na utu barabarani kiasi cha kureport jambo lolote baya alionalo barabarani, Elimu hii humsaidia mtu kuwa na ubongo active kiasi cha kuwa na maamuzi sahihi barabarani.

Watanzania tuitilie mkazo sana elimu ya Tanzania ili watu wengi waweze kuipata, Serikali ni vyema ikahakikisha elimu ya msingi inakuwa bora ili watu wamalizapo shule ya msingi wawe na content sahihi kichwani itakayowawezesha kweli kupambana na mazingira yao, Elimu bora ya msingi ijikite zaidi kwa watu kupata uelewa na kujitambua na kuwafundisha watu mambo yasiyo na msingi, vitu kama alama za barabara,namna bora ya matumizi ya barabara inaweza kuwa kipindi maalumu kwa wanafunzi wa darasa la sita, tusifikirie sana watu kufanya mtihani au mitihani migumu katika level hii hapana ziwepo tu test za kupima uelewa na continuous assessment , Elimu bora ya msingi itajenga watu bora wenye msingi imara ambao mwisho wa siku watatupunguzia matatizo mengi..[/QUOTE]
 
Hazisaidii mkuu

madereva na wamiliki wa mabasi wana HOJA kwa sabau hii kitu ilikuwa introduced like 15 yrs ago, lakini ajali ndo zimezidi

hakuna aliyekuwa anafatilia mbona yale mabasi yaliyodaiwa kufungwa , bado yalikuwa yanakimbia? na ajali zikawa pale pale

mi naona kwanza serikali ijisafishe:

1. jeshi la polisi liache kutoa leseni kwa rushwa. Madereva waende shule, wapimwe, wapite mitihani, wapimwe hadi akili ndo wapewe leseni

2. Leseni zote sasa hivi zibadilishwe..tuwe na mfumo wa leseni amboa ni computerised, data za kila dereva ziwepo, na akisababisha ajali kuwe na point system apunguziwe na kosa likiwa kubwa anyang'anywe kabisa leseni

3. mabasi yote ambayo ni malori yaondolewa barabarani..kwa maana ya kwamba ni mabasi ya abiria tu yaruhusiwe kubeba abiria. chasis za malori zilizojengewa bodi zisiruhusiwe kabisa. Inasikitisha serikali inalifahamu hili lakini bado wanaendelea kuwafumbia macho.

4. mabasi yote yakagyuliwe pia kama yanakidhi viwango, mfano matairi nk. kampuni itakayoonekana kuwa na mabasi mabovu mabovu ifungiwe.

5. Sheria za usalama barabarani zifuatwe. Mwendo kasi wa juu uongezwe kutoka 80km/h hadi 120km/hr iwe ndo maximum..tuwe realistic kwenye hili. bara bara zetu zimetengenezwa kwa sasa na kama kuna madereva makini, mabasi imara, nk hakuna sababu ya ajali

6. Madereva wawe na mikataba kabisa na matajiri wao. walipwe kisheria na iwe inajulikana hata serikalini. Huu mtindo wa kulipwa posho tu unawafanya wasiwe na confidence na kazi yao, hivyo kuwaza mambo mengi ikiwemo kukimbiza magari ili wawahi kufika na hivyo kuonekana wanafaa zaidi kuliko wengine.
 
hakuna aliyekuwa anafatilia mbona yale mabasi yaliyodaiwa kufungwa , bado yalikuwa yanakimbia? na ajali zikawa pale pale

Kaizer,

Asante kwa mchango wako. Kama kina Kombe wanapitia humu:rolleyes: huenda wakapata mwazo mapya!

Pengine pia tunahitaji vigezo ili tuweze kupima kama ajali zinaongezeka ama zinapungua.

Najua kuna watu wanajenga hoja kuwa magari yameongezeka. So kama kwa mfano mwaka 2000 kulikuwa na magari ya abiria 50,000 na tukawa na ajali 5,000 kwa mwaka, then unaweza sema kwa kila magari 10 ya abiria unategemea ajali moja kwa mwaka.

Kama mwaka 2010, tuna magari ya abiria 140,000 barabarani na mwisho wa mwaka tukawa na ajali say 7,000, then 'in absolute terms', ajali zimeongezeka lakini 'in relative terms' zimepungua sana kwa sababu katika kila magari 20 inatokea ajali moja tu.

Hata hivyo kwa kutizama idadi ya vifo in absolute terms, kwa hakika tunahitaji kufanya kitu kupunguza zaidi ajali hizi.
 
OVERSPEEDING ni moja ya sababu za ajali,kama sio sababu kuu,sasa utazuiaje hili tatizo la speeding?huwezi kuweka traffic officers every mile from dar-mbeya-arusha

SPEED GOVERNOR zina work kama kukiwa na ufuatiliaji mzuri,tatizo hizi speed governor zao wanaweka kienyeji na madereva wanaweza kuzidisconnect then wana reset wakikaribia destination zao..tatizo ni madereva na traffic officers wasio waaminifu

Ukisema speed limit 120km/hr hawa wavuta bangi(baadhi ya madereva wa mabasi )utawacontrol vipi waendeshe within limit?ukiwawekea muda wanaendesha faster wanasimama wakikaribia destination hadi muda ufike.

Gari zote tunazoendesha ni ELECTRONICALLY LIMITED TO THE MAX SPEED unayoiona kwenye odometer mostly japanese cars(except those coming to europe and other western cars are limited to approx 180km/hr=110miles/hr, european models like bmw/merc ziko limited to 155mil/hr which is approx 260 km/hr

Kama serikali iko serious iweke sheria hayo mabasi huko yanakotoka yawe ELECTRONICALLY LIMITED to speed which they think is safe,otherwise hizi governor zao za vichochoroni watu wata-temper nazo kila siku.
 
Spidi Govana si suluhu hata kidogo, tabu ama shida yetu tunatafuta majibu rahisi kwenye matatizo magumu, speed 80Km/Hr inaweza kuua kama sheria za usalama barabarani haitazingatiwa ama kusimamiwa vyema, naamini Trafic hawatimizi wajibu wao hatakidogo....natutakufa tu kama hatutabadili mfumo wa udhibiti wa Kanuni na sheria zetu .
 
I n my opinion maybe we need to go back to those days where we were having the state owned transport before start discussing this one.Je is any one who can at least gives us the accident statistics of those days? Again we can now ask on this:-

1.Are our drivers have permanent employment?
2.Did they have /receive packages and services like others normal government/private workers?
Nadhani na maswali mengine of this type ,then ndio tuanze na kuona maisha yetu wanayadhamini vipi |
 
I n my opinion maybe we need to go back to those days where we were having the state owned transport before start discussing this one.Je is any one who can at least gives us the accident statistics of those days? Again we can now ask on this:-
1.Are our drivers have permanent employment?
2.Did they have /receive packages and services like others normal government/private workers?
Nadhani na maswali mengine of this type ,then ndio tuanze na kuona maisha yetu wanayadhamini vipi |
Hilo lawezakuwa Jibu kwa upande mmoja ama mwingine, lakini swala la msingi ni kutimiza sheria kwa makini, na zile legelege zipewe makali zaidi, Police wetu wa barabarani wazisimamie kwa umakini bila kujali huyu dereva ni wagari la Kikwete ama Pinda.

Dereva atakae gonga na kuua, ikithibitika ni kwa uzembe wake afugwe kifungo kirefu kuanzia miaka saba.
Faini ziwekwe kali na na zakuogopesha
 
They need to think twice! What if accidents continue after the installation of speed governor???
 
They need to think twice! What if accidents continue after the installation of speed governor???
kwani walivyoweka gavana hizo miaka 1996 nakumbuka, zilisaidia nini, ajali ziliendelea kuwepo, maana hakuna Polisi wanaotimiza wajibu wao barabara katika upande wa Usalama barabarani.

weka mabango ya mwendo unaopaswa kwenda kwenye barabara kuu zote, hata iwe 30Km/hr kisha ukimkamata dereva kazidisha, mpe adhabu itakayokuwa funzo na kwa wenzake, mwanzoni itakua ngumu ila wakizoea wataogopa nakuziheshimu sheria ipasavyo.

kama kungekua na usimamizi makini wa sheria alama ya PUNDAMILIA kwenye vivuko vya waenda kwa miguu vingetosha badala ya matuta kwenye barabara zetu kuu.

ukitaka kujua tatizo ni usimamizi duni wa sheria zetu angalia hata kazi ya kusimamia routes za daladalla zimewashinda Police wetu hadi kufikia kubinafsisha kazi hiyo...AIBU.
 
AAAAH mie nilipanda basi moja kupitia nairobi Dereva amefungasha kifurushi naulizia nini hii naambiwa mirungi ...speed tulikuwa tunaenda nadhani 150 ikipungua 130 nilikoma kupanda hayo mabasi
Hivi hiyo mirungi haina kilevi na kwa nini barabara zima dereva yeye ni kutafuna tu ..
nadhani waajiri wa hawa madereva wakiwa serious ajali zitapungua namna fulani
 
AAAAH mie nilipanda basi moja kupitia nairobi Dereva amefungasha kifurushi naulizia nini hii naambiwa mirungi ...speed tulikuwa tunaenda nadhani 150 ikipungua 130 nilikoma kupanda hayo mabasi
Hivi hiyo mirungi haina kilevi na kwa nini barabara zima dereva yeye ni kutafuna tu ..
nadhani waajiri wa hawa madereva wakiwa serious ajali zitapungua namna fulani
SASA hapo jiulize, dereva anakula mirungi kwenye safari ndefu kama hiyo, hapo bado hajachanganya baghi na bia .
kweli tunapozungumzia matatizo ya barabarani hapa Tz lazima tunayatizame kwa mapana hayo.....kuliko kung'ang'ana na spidi gavana..........Mtatufungia hizo gavana, wakati madereva wanakula unga , Mirungi plus baghi njia nzima.
 
hakuna overspeeding kuna bad driving. Kama tukiondoa hii bad driving tutakuwa na nafasi ya kuzungumza. Ni kweli kama wanataka kufunga hayo magavana yao waende huko viwandani lakini si kutumia teknolojia ya kuibana pumzi mashine kubwa iliyotengenezwa miaka 15 baada ya kutolewa teknolojia ya gavana hii ambayo tunaingangania ahh tunaing'ang'ania. Polisi wanakuwa bure kichwani bure akilini.

Hivi huu ugawaji wao wa leseni za kuendesha mabasi ya abiria si ndio wao wanaufanya kama pipi? hata wendawazimu wanatuendesha siku hizi. Akili zao bure bilesh katika kona badala ya kupunguza yeye anaongeza halafu analala kwa mwenzake upande ule ambao anakwenda... anambana anayekuja.Katika eneo ambalo ameambiwa kuna mtelezo yeye anasema hapa ndio bomba pa kuteleza anatanua pumzi anakanyaga zaidi anaitia mashine kujifukua zaidi.

Bad driving na kama tusipoondoa bad driving tutaisha tu, ovateki nyingine ni laana tupu, hakuna hesabu . Na hao matajiri nao wanawapeleka watu kilimita 600 bila kuwapumzisha nao ni wendawazimu kabisa. Ni hayo tu, pokonya watu leseni waambie jifunzeni.
 
OVERSPEEDING ni moja ya sababu za ajali,kama sio sababu kuu,sasa utazuiaje hili tatizo la speeding?huwezi kuweka traffic officers every mile from dar-mbeya-arusha...
SPEED GOVERNOR zina work kama kukiwa na ufuatiliaji mzuri,tatizo hizi speed governor zao wanaweka kienyeji na madereva wanaweza kuzidisconnect then wana reset wakikaribia destination zao..tatizo ni madereva na traffic officers wasio waaminifu
Ukisema speed limit 120km/hr hawa wavuta bangi(baadhi ya madereva wa mabasi )utawacontrol vipi waendeshe within limit?ukiwawekea muda wanaendesha faster wanasimama wakikaribia destination hadi muda ufike.
Gari zote tunazoendesha ni ELECTRONICALLY LIMITED TO THE MAX SPEED unayoiona kwenye odometer mostly japanese cars(except those coming to europe and other western cars are limited to approx 180km/hr=110miles/hr, european models like bmw/merc ziko limited to 155mil/hr which is approx 260 km/hr
Kama serikali iko serious iweke sheria hayo mabasi huko yanakotoka yawe ELECTRONICALLY LIMITED to speed which they think is safe,otherwise hizi governor zao za vichochoroni watu wata-temper nazo kila siku.

Mpwa what u've elaborate ni good sana nakukubali,

Tatizo linakuja kwa serikali yetu imejipangaaaaa kwenda kwa new technologies zinazokujaaa na hao police wanavifaaaa vya kudhibiti hii haliii?

Nadhani twahitaji kuwa tiali kwa hili janga na pasiwepo longolongo na ufisadi,
Mfano mzuri ni mabasi ya Mombasa Raha siju the owner ni yuko shinyanga au Mwanza au Dar ila nasikia tu utaratibu wao ni mzuri wan Databse system ambayo wejiunga kwa Satellite system ambayo ina tracker ya mabasi yote na mwendo kasi na kama kweli yafanya kazi vyema kwanini wengine wasijitumbukize kwa system kama izo?

Hizo speed governor zenu kwanza zilisha shindwa iweje leo tena zirudishweeee ivi serikali imeshindwa kweli kuja mawazo ya kimsingi ivi huko USA,EUROPE na kwingineko huwa mwaenda kura rahaaaaa hamchunguzi mambo wenzetu huko wanafanyaje??

 
HTML:
hakuna overspeeding kuna bad driving. Kama tukiondoa hii bad driving
tutakuwa na nafasi ya kuzungumza. Ni kweli kama wanataka kufunga hayo magavana yao waende huko viwandani lakini si kutumia teknolojia ya kuibana pumzi mashine kubwa iliyotengenezwa miaka 15 baada ya kutolewa teknolojia ya gavana hii ambayo tunaingangania ahh tunaing'ang'ania. Polisi wanakuwa bure kichwani bure akilini. Hivi huu ugawaji wao wa leseni za kuendesha mabasi ya abiria si ndio wao wanaufanya kama pipi? hata wendawazimu wanatuendesha siku hizi. Akili zao bure bilesh katika kona badala ya kupunguza yeye anaongeza halafu analala kwa mwenzake upande ule ambao anakwenda... anambana anayekuja.Katika eneo ambalo ameambiwa kuna mtelezo yeye anasema hapa ndio bomba pa kuteleza anatanua pumzi anakanyaga zaidi anaitia mashine kujifukua zaidi. Bad driving na kama tusipoondoa bad driving tutaisha tu, ovateki nyingine ni laana tupu, hakuna hesabu . Na hao matajiri nao wanawapeleka watu kilimita 600 bila kuwapumzisha nao ni wendawazimu kabisa. Ni hayo tu, pokonya watu leseni waambie jifunzeni.
Hapo umenena Mkuu, nasisitiza kuwa hakuna OVERSPEEDING kuna BAD DRIVING.
 
Shule, shule, shule,

Nilipata bahati kutembelea nchi moja nilishangazwa na utaratibu wao wa kutoa leseni.

Hebu cheki utaratibu huu halafu mfananishe na TZ.

1. Mtu unaingia darasani mwaka mzima kujifunza theories. Hapa ina maana unajifunza alama zote za barabarani na kuzielewa maana yake. Wakati huo huo unaingia barabarani Practical ukiwa na mwalimu kwenye gari maalum.

2. Baada ya mwaka mmoja, unapewa provisional licence ambayo unaruhusiwa kuendesha gari ila ukiwa na mtu mwenye senior licence pembeni. Hii nayo ni kwa mwaka mzima halafu ndo unapata full licence.

3. Ukitaka kuwa dereva wa public service vehicles (Taxi, Buses) unatakiwa kuwa na leseni yenye miaka kumi au zaidi. Huko hamna mambo ya class A, B, C, D, au E. Huko ni experience na nidhamu.

4. Ukifanya kosa pointi zinatolewa, zikifika kiasi fulani unatakiwa kuingia darasani si chini ya miezi sita. Hapo ndipo unalipia gharama za shule ambazo si mchezo.

5. Dereva wa public transport (buses) kwa mwezi analipwa si chini ya $ 1,000. Wanaheshimu kazi ya udereva.

6. Hairuhusiwi kuagiza nje ya nchi gari lenye umri wa zaidi ya miezi 12.

Sasa kwa hali kama hii, ajali bado zipo lakini si fatal kama bongo. Ajali ni chache sana ukilinganisha hata na America ingawa wapo kwenye car ownership ratio sawa.
 
Ni kweli kwamba soeed fovernors zilikuwa introduced 15 years aga ba hazikuweza kupunguza ajali kutokana na wqamiliki wa mabasi kuziwekea electronic switch ya kuzima na kuwasha. Hata sasa watafanya hivyo hivyo kinachotakiwa na ammbacho watanzania hatukufanya wakati ni kuwapeleka mahaka,ani wamiliki wa mabasi kuwadai compensation kutokana na kushindwa kutimiza masharti ya lesenu,

Sectuioin 14 ya Katiba inasema hivi "Ki8la mtu ana haki ya uhai na kupata ulinzi wa misha kutoka kwa jamii kwa mujibu wa sheria" Hibyo speed governors ni moja ya sheria zilizowekwqa kulinda maisha. Mmmiliki wa basi aspofunga kifaa na kuhakikisha kinafanya kazi sawa sawa na basi likaendeshwa kwa mwendo kasi na kuua watu au kujeruhi.

Apart from fidia ya bima ambayo huwa ni kidogo lwa iy is assimed that ajali husika lilikuwa ni tendo la bahati mbaya, ndugu wa marehemu na waliojeruhiwa wanapaswa kufungiua mashataka katika mahakama kuprove kuwa basi hilo lilikuwa mwendo kasi na ndio chanzo cha ajali iliyopoteza maisha ya ndugu zao na kiujeruhi; na hivyo kudai fidia kubwa sana ambayo itapelekea mabasi kuuzwa ndipo hawa wamiliki watajapo shika adabu.

Utaratibu huu hufanyika nchi za jiranim basi la SCANDINAVIA liliwahi kuginga punda katika bumps yenye alama ya 30 KMs anout 7 years ago. Mwenye punda alikomaa hhadi akalipwa equivalent of 900,000/= za Kitanzania wakati huo. Basi lingine likaangika na kuua mama mmoja ilibidi mabasi ya 2 ya kampuni hiyo yauzwe kutosha kumlipa pampja na matibabu yake huko Kenya,

Sio kweli kwamba ni vigogo wameagiza, ila ni sisi wanaharakati tulioingia katika sekta hii baada ya ajali za mabasi kuongezeka ndio tulividai tarehe 09 January 2010, ili wananchi waweze kupata conclusive evidence ya kuwafilisi wamil;iki wa Hazardous buses. HAYA WANANSHERIA CHANGAMKIENI TENDA HII

Naomba wanasheria watusaidie mawazo ya kufanikisha wananchi wanaopoteza ndugu zao au kujeruhiwa kutpokana na mwendo kasi watakavyoweza kuwadai wamiliki wa mabasi haya fidia kubwa kubwa
Thanks
 
Hazisaidii mkuu

madereva na wamiliki wa mabasi wana HOJA kwa sabau hii kitu ilikuwa introduced like 15 yrs ago, lakini ajali ndo zimezidi

hakuna aliyekuwa anafatilia mbona yale mabasi yaliyodaiwa kufungwa , bado yalikuwa yanakimbia? na ajali zikawa pale pale

mi naona kwanza serikali ijisafishe:

1. jeshi la polisi liache kutoa leseni kwa rushwa. Madereva waende shule, wapimwe, wapite mitihani, wapimwe hadi akili ndo wapewe leseni

2. Leseni zote sasa hivi zibadilishwe..tuwe na mfumo wa leseni amboa ni computerised, data za kila dereva ziwepo, na akisababisha ajali kuwe na point system apunguziwe na kosa likiwa kubwa anyang'anywe kabisa leseni

3. mabasi yote ambayo ni malori yaondolewa barabarani..kwa maana ya kwamba ni mabasi ya abiria tu yaruhusiwe kubeba abiria. chasis za malori zilizojengewa bodi zisiruhusiwe kabisa. Inasikitisha serikali inalifahamu hili lakini bado wanaendelea kuwafumbia macho.

4. mabasi yote yakagyuliwe pia kama yanakidhi viwango, mfano matairi nk. kampuni itakayoonekana kuwa na mabasi mabovu mabovu ifungiwe.

5. Sheria za usalama barabarani zifuatwe. Mwendo kasi wa juu uongezwe kutoka 80km/h hadi 120km/hr iwe ndo maximum..tuwe realistic kwenye hili. bara bara zetu zimetengenezwa kwa sasa na kama kuna madereva makini, mabasi imara, nk hakuna sababu ya ajali

6. Madereva wawe na mikataba kabisa na matajiri wao. walipwe kisheria na iwe inajulikana hata serikalini. Huu mtindo wa kulipwa posho tu unawafanya wasiwe na confidence na kazi yao, hivyo kuwaza mambo mengi ikiwemo kukimbiza magari ili wawahi kufika na hivyo kuonekana wanafaa zaidi kuliko wengine.

Hoja kuhusu vyanzo vya ajali hazina research suport na kwa mimi binafsi siungi mkono hata moja!

Mabasi yamejengwa juu ya chasis za malori.....
........Takwimu zilizopo zinazoonyesha kwamba hili linaweza kuwa ni tatizo?
........Na kama ni tatizo ni kwa kiwango gani?
........Je tatizo ni chasis au spidi iliyosababishwa injini kubwa?
........Je kuna tofauti ya spidi kati ya marcopolo ya brazili yenye gia nane (designed to carry passengers) na marcopolo ya kenya yenye gia 10?(Modified to carry passenger) ...vipi nissani yenye gia sita? uhusika wa aina hizi za magari ulivyo?

Madereva wawe na mikataba ya ajira........
........Kwa vile kwa sasa hawana mikataba ya ajira, wanasababisha ajali kwa makusudi! Confidence inatokana na mshahara au kuijua kazi?
........Mwalimu wa madereva ana uelewa wa kutosha (kinadharia na kivitendo)

Mabasi yakaguliwe kama yanakidhi viwango.......
........Yakaguliwe na nani (Vehicle inspector, afisa wa TBS, SUMATRA au Majembe?) na kufuata viwango vipi (TBS, JAAI vya India au Italy?)
........Vipuli feki vya magari vina mchango gani katika hili? (matairi, na vipuli vingine vinavyohusiana na breki za haya magari? Je vinahitaji ukaguzi madhubuti kabla havijafika sokoni?

Miundombinu.......
.........Barabara zimekaaje (upana wa barabara, alama za barabara, mawimbi barabarani ujenzi wa barabara usiokua wa viwango unaosababisha utelezi, n.k)

Rushwa......
.........Nafasi ya rushwa katika tatizo zima la ajali barabarani ikoje inaweza kudhibitiwa? na nani?

Spidi gavernor.......
.........Dereva anayeijua kazi yake anahitaji spidi governor? je inafanya kazi kwenye miteremiko mikali ambapo madereva hupiga kofi gia?

Tunahitaji utafiti zaidi ili kuja njia sahihi ya kupambana na ajali nchini!
 
OVERSPEEDING ni moja ya sababu za ajali,kama sio sababu kuu,sasa utazuiaje hili tatizo la speeding?huwezi kuweka traffic officers every mile from dar-mbeya-arusha...
SPEED GOVERNOR zina work kama kukiwa na ufuatiliaji mzuri,tatizo hizi speed governor zao wanaweka kienyeji na madereva wanaweza kuzidisconnect then wana reset wakikaribia destination zao..tatizo ni madereva na traffic officers wasio waaminifu
Ukisema speed limit 120km/hr hawa wavuta bangi(baadhi ya madereva wa mabasi )utawacontrol vipi waendeshe within limit?ukiwawekea muda wanaendesha faster wanasimama wakikaribia destination hadi muda ufike.
Gari zote tunazoendesha ni ELECTRONICALLY LIMITED TO THE MAX SPEED unayoiona kwenye odometer mostly japanese cars(except those coming to europe and other western cars are limited to approx 180km/hr=110miles/hr, european models like bmw/merc ziko limited to 155mil/hr which is approx 260 km/hr
Kama serikali iko serious iweke sheria hayo mabasi huko yanakotoka yawe ELECTRONICALLY LIMITED to speed which they think is safe,otherwise hizi governor zao za vichochoroni watu wata-temper nazo kila siku.


Hili nalo ni wazo zuri sana mkuu. Ila kama tu watanunua mabasi na sio chasis za malori.

kwa hiyo unaweza kuona kwamba tunatakuiwa kwanza mabasi yaliyo malori kwanza yaondoliewe kwa sababu engine capacity zao ni kubwa lakini mzigo mdogo soi yanakuwa very powerful and hence high speed. Pili yanakuwa sio mazima ki ivyo.

tungeweka standards kwamba basi lazima liwe basi kweli na liwe na speed ambayo imesetiwa electronically

halafu hizi speed governors hazina interference na mfumo mzima wa gari kweli?
 
Speed governor ni mradi tuu wa watu huo.
Ni kheri wafunge GPS ambayo ni more efficient and cheap.
Unaweza kuta CCM wanataka kusanya ela ya uchaguzi bure maana uyo Tosi amekomaa
 
Napenda kuwataarifu wasomaji na wadau wa JF kuwa mambo ya gavana yamepigwa stop kw amuda kidogo na jamaa wanarejea mezani kwa mazungumzo kuona jambo la maana la kufanya ili kupunguza ajali.Hii ni kwa mujibu wa Mssika msemaji wa POLISI.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom