Mkuu, umeandika points nzuri sana, una hoja za msingi sana, ila kuna haya
1. Limit less speed sio Tanzania pekee, zipo nchi za SADC, nimekuwa South Africa, Zambia na Uganda, ukiacha maeneo yenye vibao vya speed limit unatembea, kama sipo sahihi naomba niambie kwenye hizo nchi nilizotaja bara bara zao limit ni ipi (na bahati nzuri mtaala wa uderva wa nchi za SADC ni mmoja, unaitwa K50)
2. Ni kweli hilo la speed limit za bara bara zetu inabidi liwepo na ni jukumu la TANROADS/TARURA kuset hizo limit kulingana na viwango vya ubora wa bara bara.
3. Ni kweli Polisi na TANROADS wametengeneza mianya ya Rushwa.
Mkuu ninaandika haya kiasi kwa uchungu. Binafsi nimetembea nchi nyingi duniani. Hakuna kitu kama limitless speed na vibao barabarani vina apply kwa magari yote na si vinginevyo. Huko Africa kusini kuna haya:
"The speed limit on a road in South Africa is normally specified by a sign alongside that road.
If no sign is present, then the general speed limits are:
- 60km/h on every public road in an urban area.
- 100km/h on every public road situated outside an urban area excluding a freeway.
- 120km/h on every freeway.
Waweza yaona haya katika site hii pia:
At what speeds you will be fined and arrested for speeding in South Africa
Awapaye watanzania incentive ya kuendesha bila limit anapaswa kuchukuliwa hatua hana nia njema na maisha yetu. Hii si incentives mnatufanya kuingia mabarabarani kwa woga mkubwa.
Dunia nzima Polisi si mtunga sheria hawa wetu wanaotutungia sheria kila leo wanaanzia wapi? Kumbukeni yakiwamo yale ya taa za hazard na zebra crossing. Haya ni Tanzania tu ambako Polisi ni mtunga sheria na msimamizi wakati huo huo. Ajali haziwezi isha kwa mwendelezo huu.