Wanabodi
Kama isomavyo "tetesi", nikiwa mazingira ya butimba chuoni leo kwa usafiri wa bodaboda, nimetaarifiwa kwamba wakati wanachuo wakiwa mchaka mchaka alfajiri, baadhi yao wamegongwa na daladala.
Sijui ni mazingira ya namna gani, imetokea vipi na ni kwa namna gani wanafunzi 2 wamefariki papo hapo na majeruhi wa kutosha wamepelekwa wengine hosiptali ya mkoa, seketure kwa matibabu zaidi.
NIMEAMBIWA KWAMBA:-
" ...wakati mchaka mchaka ukiendelea alfajiri, giza likiwa nene, wanafunzi wakiwa kwenye lami, daladala ambayo haikuwa imewasha taa, ilipiga breki katikati ya umati wa wanafunzi hao ambapo 2 walifariki papo hapo, wakati dereva akitafuta namna ya kusimama, akazidi kujeruhi wengine..."
Kama ulivyo na maswali mengi, mimi pia nina maswali mengi, inakuaje kuaje yani? Nimejaribu kuwauliza wanafunzi wa sekondari butimba wanoenda shule asubuhi ya saa moja, wengi wao hawajui. Ila boda wana taarifa hii.
Naomba eidha wanafunzi wenyewe watujuze au wanaoishi viunga hivyo. Kama hili ni kweli au laa.
Narudia, tetesi hii nimepewa na bodaboda wanaopaki maeneo ya geti la butimba ttc.
Kama isomavyo "tetesi", nikiwa mazingira ya butimba chuoni leo kwa usafiri wa bodaboda, nimetaarifiwa kwamba wakati wanachuo wakiwa mchaka mchaka alfajiri, baadhi yao wamegongwa na daladala.
Sijui ni mazingira ya namna gani, imetokea vipi na ni kwa namna gani wanafunzi 2 wamefariki papo hapo na majeruhi wa kutosha wamepelekwa wengine hosiptali ya mkoa, seketure kwa matibabu zaidi.
NIMEAMBIWA KWAMBA:-
" ...wakati mchaka mchaka ukiendelea alfajiri, giza likiwa nene, wanafunzi wakiwa kwenye lami, daladala ambayo haikuwa imewasha taa, ilipiga breki katikati ya umati wa wanafunzi hao ambapo 2 walifariki papo hapo, wakati dereva akitafuta namna ya kusimama, akazidi kujeruhi wengine..."
Kama ulivyo na maswali mengi, mimi pia nina maswali mengi, inakuaje kuaje yani? Nimejaribu kuwauliza wanafunzi wa sekondari butimba wanoenda shule asubuhi ya saa moja, wengi wao hawajui. Ila boda wana taarifa hii.
Naomba eidha wanafunzi wenyewe watujuze au wanaoishi viunga hivyo. Kama hili ni kweli au laa.
Narudia, tetesi hii nimepewa na bodaboda wanaopaki maeneo ya geti la butimba ttc.