Ajali mbaya nje kidogo ya Morogoro Municipal!

Jaguar

JF-Expert Member
Mar 6, 2011
3,438
1,026
Nilikuwa ndani ya gari nikisafiri kuelekea Dumila, tulipofika maeneo ya Mkundi alfajiri ya leo hii tumeshuhudia maiti tatu zikiwa zimesambaa barabarani. Miili hii iliyoharibika vibaya kiasi cha kutotazamika na mtu asiye na ujasiri ni ya vijana watatu wanaojishughulisha na biashara ya mkaa. Vijana hao walikuwa wakisafirisha mkaa kwa kutumia piki piki zao kuelekea Morogoro mjini.Kwa dondoo za haraka haraka inasemekana ni lori ndo limepelekea umauti wa wale vijana. R.I.P.
 
Duh! siku za mwanadamu zinahesabika

Ni vema wakati wa maisha yetu yote kuwa tayari kuondoka. Sisi binadamu ni wapita njia tu, tunapaswa kutengeneza njia kwa kumpokea YESU KRISTO kuwa Bwana na mwokozi wetu ili tuweze kuokoka na kuingia Mbinguni.

Najua wengi tutabisha lakini ndio ukweli. NA NAMNA YA KUYASHINDA MAOVU NA YOTE MABAYA NI TUNAWEZA KWA KUMPOKEA ROHO WA MUNGU. ROHO WA MUNGU ANATUFANYA TUSHINDE KILA BAYA NA KUWEKA KATIKA MAISHA AMBAYO YANAYO KIBALI TOKA KWA MUNGU.

Kazi ni kweni hata kama hamtaamini, ninayo furaha ya kuwa message sent, delivered and reserved by you.

I submit
 
RIP vijana.

lakini wale vijana wa Morogoro kutokea dumila na maeneo hayo wanaofanya biashara ya mkaa kwa Pikipiki wanahatarisha maisha yao.

Kwanza wanabeba mkaa mwingi na wanapakia magunia across, kuna hatari ya kugongwa, issue ya pili ni hatari ya kukosa balance kwani wao wanalazimika kukaa juu ya tank la mafuta. nimeshashuhudia mmoja akiyumba na kupiga mweleka mwenyewe hata bila kuguswa na kitu.
 
Ni vema wakati wa maisha yetu yote kuwa tayari kuondoka. Sisi binadamu ni wapita njia tu, tunapaswa kutengeneza njia kwa kumpokea YESU KRISTO kuwa Bwana na mwokozi wetu ili tuweze kuokoka na kuingia Mbinguni.

Najua wengi tutabisha lakini ndio ukweli. NA NAMNA YA KUYASHINDA MAOVU NA YOTE MABAYA NI TUNAWEZA KWA KUMPOKEA ROHO WA MUNGU. ROHO WA MUNGU ANATUFANYA TUSHINDE KILA BAYA NA KUWEKA KATIKA MAISHA AMBAYO YANAYO KIBALI TOKA KWA MUNGU.

Kazi ni kweni hata kama hamtaamini, ninayo furaha ya kuwa message sent, delivered and reserved by you.

I submit
najua wengi mtabisha, kwanini? uwe na imani haba. injili haina mashaka ndani yake kuwa na imani muda wote ukiwa umeisimamia kweli.ktk pendo hakuna hofu, [ukiona hofu ujue si ule upendo , tuliohubiriwa]
 
R.I.P -natoa ushauri kwa waendesha pikipiki , nimefuatilia saana uendeshaji wao na kero wanazozisababisha kwa waendesha magari, ni kweli sheria wanazotumia , waendesha pikipiki na waendesha magari ndo hizo hizo, lkn nawashauri waendesha pikipiki watumie saaana side mirrow zao, kama kuna gari nyuma yake na mbele kuna uwazi yaani hakuna magari asishindane na gari lililonyuma yake , alipishe kwa kupunguza mwendo na kusogea pembeni, maana unakomaaa unamzuia halafu mkifika kwenye foleni , hukai foleni unaanza kupenya penya, hivyo unakuwa kero nashauri huo nadhani ni uendeshaji salama, mbio zisizo na maana za nini? mtu akikusifia kwa kwenda kasi sio rafiki mwema. mwisho kama barabara ina nafasi pembeni tumieni hiyo madereva wa magari wametofautiana saana kimaadili.
 
Back
Top Bottom