Jaguar
JF-Expert Member
- Mar 6, 2011
- 3,438
- 1,026
Nilikuwa ndani ya gari nikisafiri kuelekea Dumila, tulipofika maeneo ya Mkundi alfajiri ya leo hii tumeshuhudia maiti tatu zikiwa zimesambaa barabarani. Miili hii iliyoharibika vibaya kiasi cha kutotazamika na mtu asiye na ujasiri ni ya vijana watatu wanaojishughulisha na biashara ya mkaa. Vijana hao walikuwa wakisafirisha mkaa kwa kutumia piki piki zao kuelekea Morogoro mjini.Kwa dondoo za haraka haraka inasemekana ni lori ndo limepelekea umauti wa wale vijana. R.I.P.