Ajali Mbaya Chalinze: Zaidi ya 20 Wapoteza maisha papo kwa papo!

Jamani!!!! Mungu atufumbue akili tupate njia muafaka kudhibiti ajali hizi.

Leka

Mungu ni mwema tu, kuna ajali lakini nyingi tunajitakia madereva wengi hawajui sheria za barabara na kama wanazijua wanapuuza.
-Dereva anaovertake kwenye kilima au kwenye kona unatarajia nini?
-Matairi ya gari ni vipara unatarajia nini?
-Askari anaacha kumtoza faini mkosaji barabarani faini 250,000 anapozwa 5,000 anamwachia aende, wataacha makosa kweli? unatarajia nini?
-Dereva anaongea na simu gari iko mwendo unatarajia nini?
-Dereva amelewa unatazamia nini?
-Uwezo wa gari tani 3 imebeba tani 3.750 unatarajia nini?

Mungu awarehemu waliopoteza maisha na majeruhi wapone upesi. Inshaalah!
 
Hivi suluhisho la ajali hizi ni nini?

Mimi ni dreva, lakini sikubaliani na kuwa kuendesha kasi pekee ndio chanzo cha ajali hizi. Chanzo cha ajali nyingi ni uendeshaji wa kizembe (wreckless driving). Na hili hata tukiwalaumu askari wa usalama barabarani haitasaidia. Madereva wa mabasi na mafuso wanatakiwa kubadili fikra.

Ajali nyingi (not quantified) hutokana na overake isiyo zingatia usalama. Madereva wengi wa mabasi kwa kiburi au kutojua, hupuuzia na kuendesha magari kiholela; wana overtake kwenye Kona na kutegemea bahati kuponya ujinga wao. Na mara nyingi husababisha ajali mbaya!

EE mwenyezi Mungu uwajalie majeruhi wapone upesi, na uwalaze pema peponi marehemu wote. Amen.
 
poleni wafiwa wote. hivi hizi ajali za miaka nenda rudi huwa zinafanyiwa uchunguzi na vyombo husika? na je baada kufanya uchunguzi wamependekeza nini kifanyike kupunguza hizi ajali zaidi ya kutuhumu uzembe wa dereva wakati tunajua wazi kwamba barabara zetu pia zinachangia zaidi.


kama serikali wameona hawana uwezo wa kutanua barabara zetu za mikoani ni bora waweke matuta kwenye barabara za mikioni kama zitaokoa maisha yetu.nina huakika kama tuna nafasi ya kuchagua kati ya kuchelewa kufika safari zetu au ku-risk maisha yetu ni bora kuchelewa kufika.


poleni wafiwa na mungu atuepushe na ajali hizi.
 
Hivi suluhisho la ajali hizi ni nini?

Mimi ni dreva, lakini sikubaliani na kuwa kuendesha kasi pekee ndio chanzo cha ajali hizi. Chanzo cha ajali nyingi ni uendeshaji wa kizembe (wreckless driving). Na hili hata tukiwalaumu askari wa usalama barabarani haitasaidia. Madereva wa mabasi na mafuso wanatakiwa kubadili fikra.

Ajali nyingi (not quantified) hutokana na overake isiyo zingatia usalama. Madereva wengi wa mabasi kwa kiburi au kutojua, hupuuzia na kuendesha magari kiholela; wana overtake kwenye Kona na kutegemea bahati kuponya ujinga wao. Na mara nyingi husababisha ajali mbaya!
.
kuendesha kasi kubwa zaidi ya limit iliowekwa ni sababu kubwa pamoja na barabara zetu ni nyembamba mno.

kama viongozi wetu wangekuwa na malengo,basi barabara za mikoani nyingi zingekuwa zimetanuliwa kitambo sana.
 
The Following 8 Users Say Thank You to Omumura For This Useful Post: Abunwasi (Today), BelindaJacob (Today), Invisible (Today), Lekanjobe Kubinika (Today), nyani<abiziani> (Today), Pasco (Today), The Farmer (Today), Tshala (Today)
The Following 12 Users Say Thank You to Pasco For This Useful Post: Abunwasi (Today), Balantanda (Today), BelindaJacob (Today), carmel (Today), Kizimkazimkuu (Today), Lekanjobe Kubinika (Today), MwanajamiiOne (Today), nyani<abiziani> (Today), Omumura (Today), Pengo (Today), The Farmer (Today), Tshala (Today)
Hivi nyie mnaotoa 'thanks' baada ya kusoma habari za kusikitisha mnamaanisha nini? Je, mnafurahia ajali hiyo? Watu wamepoteza maisha yao nyie mnafurahia si ndiyo?
 
duu poleni sana wafiwa!nini ni chanzo cha ajali?ajali nyingi za tz zinasababishwa na uzembe!
 
Hivi nyie mnaotoa 'thanks' baada ya kusoma habari za kusikitisha mnamaanisha nini? Je, mnafurahia ajali hiyo? Watu wamepoteza maisha yao nyie mnafurahia si ndiyo?
asante wametoa kwa kupewa taarifa.bila hio taarifakuwekwa wasingejua.
 
Kuna habari kwamba mchana huu katika eneo la kitumbi Mkoani Tanga kumetokea ajali mbaya ikihusisha basi la chatco lililokuwa likitokea Dar pamoja na Fuso, vifo vipo pamoja na majeruhi,tunaendelea kufuatilia zaidi ukweli wake!!

Ajali hizi zinaweza kupunguzwa kama tutabadili system nzima ya public transport.labda nielezee experience yangu.as a former basi driver wa nchi fulani.
1.basi lazima liwe katika hali nzuri na kuna ukaguzi makini,hakuna wa kumuhonga apitishe gari bovu,dereva una haki ya kukataa kuendesha gari kama unaona lina ubovu fulani,sababu hata ukisababisha ajali kwa ubovu wa basi dereva as well as the bus owner wote mnakuwa responsible.
2.basi lina speed limit(electronically limited) ambayo ni 65mph approx 100kmh(hii pia iko kwenye malori),hakuna fundi mangungu wa kutegua hii speed limit kama mabasi ya dar-mbeya
3.basi limefungwa kitu kinaitwa TACHOGRAPH,kifaa hiki kinarekodi muda ambao dereva anaendesha,lazima usign/log in ukianza na ukimaliza,kuna mamlaka inakagua hii kuona dereva hazidishi masaa anayotakiwa kuendesha kisheria(hii pia iko kwenye malori)
4.mafunzo na upatikanaji wa leseni ni ya hali ya juu,hakuna mambo ya kuletewa leseni nyumbani,kuna point system kila kosa unalofanya linakuongezea points kwenye leseni,zikifika idadi fulani unapoteza leseni na maana yake umemwaga unga(haikwepeki ukinasa umenasa)
5.barabara nyingi za kwenda mikoani(highway)ni 6 lane i.e 3 to and 3 fro
na basi au lorry haliruhusiwi kuendesha kwenye outer lane unless overtaking an extremely slow vehicle which u cant find in these kind of roads

kuna vitu vingi sana ambavyo as a driver i went through,ila naamini tukizingatia hivi vichache tunaweza kupunguza ajali
 
Ajali hizi zinaweza kupunguzwa kama tutabadili system nzima ya public transport.labda nielezee experience yangu.as a former basi driver wa nchi fulani.
1.basi lazima liwe katika hali nzuri na kuna ukaguzi makini,hakuna wa kumuhonga apitishe gari bovu,dereva una haki ya kukataa kuendesha gari kama unaona lina ubovu fulani,sababu hata ukisababisha ajali kwa ubovu wa basi dereva as well as the bus owner wote mnakuwa responsible.
2.basi lina speed limit(electronically limited) ambayo ni 65mph approx 100kmh(hii pia iko kwenye malori),hakuna fundi mangungu wa kutegua hii speed limit kama mabasi ya dar-mbeya
3.basi limefungwa kitu kinaitwa TACHOGRAPH,kifaa hiki kinarekodi muda ambao dereva anaendesha,lazima usign/log in ukianza na ukimaliza,kuna mamlaka inakagua hii kuona dereva hazidishi masaa anayotakiwa kuendesha kisheria(hii pia iko kwenye malori)
4.mafunzo na upatikanaji wa leseni ni ya hali ya juu,hakuna mambo ya kuletewa leseni nyumbani,kuna point system kila kosa unalofanya linakuongezea points kwenye leseni,zikifika idadi fulani unapoteza leseni na maana yake umemwaga unga(haikwepeki ukinasa umenasa)
5.barabara nyingi za kwenda mikoani(highway)ni 6 lane i.e 3 to and 3 fro
na basi au lorry haliruhusiwi kuendesha kwenye outer lane unless overtaking an extremely slow vehicle which u cant find in these kind of roads

kuna vitu vingi sana ambavyo as a driver i went through,ila naamini tukizingatia hivi vichache tunaweza kupunguza ajali

Ahsante sana Bwana Mmbebabox nimekupata. Mawazo positive kama haya ndio yanayotakiwa (na sio kukimbilia kuandika "inauma sana jamani). Japo mi-jiongozi yetu haitakusikia lakini umetimiza wajibu wako...
 
sijui niwe natembea kwa miguu now days...!? lkn moshi nitatumia siku ngapi? duh!
 
sijui niwe natembea kwa miguu now days...!? lkn moshi nitatumia siku ngapi? duh!

hahaha,

usiogope kifo kiasi hicho mpendwa,

hata uking'ang'ania kubaki nyumbani kifo kikja utakufa tu, uliza haiti kama walikuwa wanasfiri wale. tumshukuru Mungu kila siku tuayomaliza tukiwa na afya njema (rejea wimbo wa Mungu anakupenda) wa kijitonyama upendo group utakueleza logic ya maisha hapa duniani.

tuliahi kusafiri na mtu kwenye ndege na aliniona nasoma habari iliyohusu ajali ya ndege iliyopoteza watu zaidi ya 100, alinizuia nisisome kwani akisikia habari za ajali za ndege naye yumo ndani ya ndoge akiwa kwenye safari ya zaidi ya masaa tisa, anakosa amani, anasikia kama hali ya pressure yake inabadilika, jibu langu kwake lilikuwa "Mungu anakupenda, ndio maana waishi hata leo hii!"

kwa hao waliokufa...........................,
"Bwana alitoa na Bwana ametwaa, jina la Bwana libarikiwe"
 
I think itabidi hawa Madereva wa Magari especially wa livery waanze kuwajibishwa kwa kufungwa maisha, na kuchapwa viboko hamsa hamsini kila mwezi mpaka kifo kitakapo wachukua. This is pathetic, kuwa na madereva wasio jali maisha ya watu.

Pili, mwenye basi, nayeye awajibishwe kwa kulipa faini kali na kama ikibainika alikuwa na madereva njaa, aswekwe jela vile vile kwa miezi mitatu, viboko ishirini anapo ingia jela na vingine ishirini akamuonyeshe mke wake anapo toka jela.

Zaidi ya hapo, viongozi wa Serikali nao vile vile lazima waonje joto ya jiwe, kwa kuruhusu kuwa na madereva njaa, kwa kushindwa kuinforce sheria za barabarani, kwa kushindwa kuweka alama husika ambazo zitawa alart madereva. Nao waswekwe jela miezi mitatu, walambe viboko ishirini wakiingia jela, na ishirini wakitoka jela waende kuwaonyesha ndugu zao.

 
Ajali hizi zinaweza kupunguzwa kama tutabadili system nzima ya public transport.labda nielezee experience yangu.as a former basi driver wa nchi fulani.
1.basi lazima liwe katika hali nzuri na kuna ukaguzi makini,hakuna wa kumuhonga apitishe gari bovu,dereva una haki ya kukataa kuendesha gari kama unaona lina ubovu fulani,sababu hata ukisababisha ajali kwa ubovu wa basi dereva as well as the bus owner wote mnakuwa responsible.

Tanzania hakuna ukaguzi makini Trafiki wapo SUMATRA imeshindwa imewakabidhi Majembe lakini nao njaa tupu Tanzania ni tofauti dereva ukikataa kuendesha eti gari bovu kesho yake unakuta kakalia mwingine

2.basi lina speed limit(electronically limited) ambayo ni 65mph approx 100kmh(hii pia iko kwenye malori),hakuna fundi mangungu wa kutegua hii speed limit kama mabasi ya dar-mbeya

Zilikuwepo sijui kama bado zinafuatiliwa maana kila gari lina speed limit(governor) lakini zimechokonolewa na mafundi njaa kiasi kwamba hazifanyi kazi wakati mwingine inakuwa ni dili la mkubwa fulani anataka kuuza speed governor zake zikiisha hakuna tena ufuatiliaji

3.basi limefungwa kitu kinaitwa TACHOGRAPH,kifaa hiki kinarekodi muda ambao dereva anaendesha,lazima usign/log in ukianza na ukimaliza,kuna mamlaka inakagua hii kuona dereva hazidishi masaa anayotakiwa kuendesha kisheria(hii pia iko kwenye malori)

ni mambo mazuri lakini kwa nchi kama Tanzania ni ya kufikirika zaidi kwanza dereva wa Tanzania hajawahi hata kuiona hiyo TACHOGRAPH sembuse matumizi yake na kama mamlaka ya kusoma yaliyorekodiwa ni hawa hawa polisi trafiki wetu hakifanyiki kitu

4.mafunzo na upatikanaji wa leseni ni ya hali ya juu,hakuna mambo ya kuletewa leseni nyumbani,kuna point system kila kosa unalofanya linakuongezea points kwenye leseni,zikifika idadi fulani unapoteza leseni na maana yake umemwaga unga(haikwepeki ukinasa umenasa)

Inawezekana kama chombo kinachotoa leseni kitakuwa si chini ya polisi trafiki nchi zingine chombo kinachotoa leseni ni tofauti kabisa na trafiki, trafiki wenyewe wanatoa viwango tu vya ufaulu, mafunzo na driving test yanafanywa na chombo kingine

5.barabara nyingi za kwenda mikoani(highway)ni 6 lane i.e 3 to and 3 fro
na basi au lorry haliruhusiwi kuendesha kwenye outer lane unless overtaking an extremely slow vehicle which u cant find in these kind of roads kuna vitu vingi sana ambavyo as a driver i went through,ila naamini tukizingatia hivi vichache tunaweza kupunguza ajali

kwa nchi kama yetu inakuwa ni mpango wa muda mrefu hizo barabara za six lane ni lini tutazifikia wakati hata hizi za single lane zinatushinda kuzikarabati

Mimi nafikiri kama ulivyosema kinachotakiwa ni ku-overhaul system nzima inayohusika na mambo ya usafiri na usafirishaji ikiwemo system nzima ya polisi trafiki haya mengine ya six lane yatakuja baadae.
 
Poleni wafiwa na majeruhi!!!

There is this triangle that is always ignored in Tz, Speed - Ulevi - Fatigue. On top of driving qualifications if the mentioned things are well monitored and observed we have got a big chance to improve.

Lakini all in all, road safety in Tanzania is almost zero, I have been in buses that overtake at bends, corners, hills u name it. Breki magumashi, pale mbele kwa driver kuna makonda kama nane wanampigisha dereva stori, Dereva huyu ambaye jana yake aliendesha Dar - Arusha, akalala saa nane usiku akiwa mbwii na jishangingi pembeni. Leo kumi na mbili asubuhi yupo route ya Dar - Mbeya akiendeshwa na nguvu ya ndumu........

An overhaul of road safety is necessary for now!
 
Tanzania Daima

ZAIDI ya watu 24 wamefariki dunia na wengine 32 kujeruhiwa vibaya, baada ya basi la Kampuni ya Chatco walilokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na basi jingine.
Ajali hiyo ambayo ni moja ya ajali kubwa mwaka huu, ilitokea jana majira ya saa saba mchana katika eneo la Kitumbi, wilayani Handeni, mkoani Tanga.
Basi hilo lenye namba za usajili T 548 ANS, lililokuwa likiendeshwa na Mambo Myami (38), lilipata ajali hiyo baada ya kugongana uso kwa uso na Fuso Mini Bus, lililokuwa likiendeshwa na Shindu Abdallah.
Vyanzo vya habari kutoka eneo la ajali vilisema kuwa basi la Kampuni ya Chatco ambalo lilikuwa katika mwendo kasi, lilikuwa likitokea mkoani Arusha kwenda Dar es Salama wakati Fuso Mini Bus, lilikuwa likitokea Dar es Salmaa kwenda Hedaru.
Baadhi ya majeruhi wa ajali hiyo walitibiwa na kuondoka na wengine wamelazwa katika Hospitali ya Magunga, Korogwe.
Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Tanga, Simon Ngawe, alithibitisha kutokea kwa ajili hiyo.
Alisema uchunguzi wa awali unaonyesha ajali hiyo imetokana na uzembe wa madereva. Kamanda Ngawe aliahidi kutoa taarifa ya majina ya waliofariki dunia na majeruhi leo, wakati maiti wamehifadhiwa katika Hospitali ya Wilaya ya Mombo.


Mola awalaze mahala pema peponi amen
 
I think itabidi hawa Madereva wa Magari especially wa livery waanze kuwajibishwa kwa kufungwa maisha, na kuchapwa viboko hamsa hamsini kila mwezi mpaka kifo kitakapo wachukua. This is pathetic, kuwa na madereva wasio jali maisha ya watu.

Pili, mwenye basi, nayeye awajibishwe kwa kulipa faini kali na kama ikibainika alikuwa na madereva njaa, aswekwe jela vile vile kwa miezi mitatu, viboko ishirini anapo ingia jela na vingine ishirini akamuonyeshe mke wake anapo toka jela.

Zaidi ya hapo, viongozi wa Serikali nao vile vile lazima waonje joto ya jiwe, kwa kuruhusu kuwa na madereva njaa, kwa kushindwa kuinforce sheria za barabarani, kwa kushindwa kuweka alama husika ambazo zitawa alart madereva. Nao waswekwe jela miezi mitatu, walambe viboko ishirini wakiingia jela, na ishirini wakitoka jela waende kuwaonyesha ndugu zao.

Baranara zetu bado ni shida sana sijui ndo umasiki au ndo kodi zetu zinaelekezwa ambako siyo hapo ndo sina uhakika sana.Kwa maoni yangu kama tutapanua barabara zetu hata kwa mita chache tu tutapunguza ajali kwa kiwango kikubwa sana.
 
Back
Top Bottom