Mwifwa
JF-Expert Member
- Apr 3, 2017
- 46,918
- 122,177
LORI linalosafirisha bidhaa za mayai na nyama ya kuku nchini Australia, limepata ajali na kubaki limening'inia kwenye daraja juu ya mithili ya lile la Mfugale, jijini Dar es Salaam, eneo la Tazara.
Taarifa za mtandao juzi jioni zinasema, bidhaa zilizokuwa zinasafirishwa na lori hilo zilimwagika na kutapakaa kwenye barabara iliyoko chini na inaelezwa dereva wa lori hilo alijeruhiwa na kukimbizwa hospitalini.
Hata hivyo, kuna taarifa dereva huyo hakujeruhiwa katika hali mbaya zaidi, ingawaje alipata ajali katika mazingira ya hatari zaidi dhidi ya maisha yake, ikilinganishwa na eneo lilikopatikana ajali hiyo.
Inaelezwa kwamba, tayari uchunguzi ulishaanza juzi hiyo jioni kubaini chanzo cha ajali, ingawaje kuna taarifa zisizo rasmi kwamba, lori hilo liligonga kizuizi pembeni mwa barabara na kupinduka.
Eneo la juu ambako gari hilo lilipata ajali, ni mithili ya darala la Mfugale katika eneo la juu inakopita barabara ya Nyerere na mizigo iliangukia mithili ya barabara ya Mandela jijini Dar es Salaam, mazingira yanayofungua somo la uangalifu kwa watumiaji wa Darala la Mfugale ambalo bado ni jipya na limezinduliwa siku chache zilizopita.
Source: IPP Media.
Taarifa za mtandao juzi jioni zinasema, bidhaa zilizokuwa zinasafirishwa na lori hilo zilimwagika na kutapakaa kwenye barabara iliyoko chini na inaelezwa dereva wa lori hilo alijeruhiwa na kukimbizwa hospitalini.
Hata hivyo, kuna taarifa dereva huyo hakujeruhiwa katika hali mbaya zaidi, ingawaje alipata ajali katika mazingira ya hatari zaidi dhidi ya maisha yake, ikilinganishwa na eneo lilikopatikana ajali hiyo.
Inaelezwa kwamba, tayari uchunguzi ulishaanza juzi hiyo jioni kubaini chanzo cha ajali, ingawaje kuna taarifa zisizo rasmi kwamba, lori hilo liligonga kizuizi pembeni mwa barabara na kupinduka.
Eneo la juu ambako gari hilo lilipata ajali, ni mithili ya darala la Mfugale katika eneo la juu inakopita barabara ya Nyerere na mizigo iliangukia mithili ya barabara ya Mandela jijini Dar es Salaam, mazingira yanayofungua somo la uangalifu kwa watumiaji wa Darala la Mfugale ambalo bado ni jipya na limezinduliwa siku chache zilizopita.
Source: IPP Media.