Ajali iliyoua watu 6 Dodoma: Wanaopaswa kukamatwa na kuwekwa ndani ni Mfugale na Meneja wa Dodoma wa TANROADS Dodoma, sio dereva wa lori

Ni shida sana, kuna barabara ya lami imejengwa goba-makongo imejazwa matuta hadi unashangaa, kila mita 100 unaruka tuta. Yaani unajenga barabara nzuri ya lami unaishia kuiharibu na matuta. Unaishia kusababisha usumbufu kwa madereva na kuwaingiza gharama za matengenezo ya shock up na gharama za mafuta. maana utaendesha hapa na hapa unapunguza mwendo kuruka tuta


Wabongo wengi wanatabia ya kuendesha magari kwa mwendo kasi kinyume na matakwa ya kisheria!

Maeneo hayo ni makazi ya watu kwanini muendeshe magari kwa mwendo kasi?

Halafu ukiona sehemu imewekwa mafuta mengi mara nyingi kunakuwa na tukio au matukio ya historia ya ajali mbaya, kwa hiyo wanaweka matuta kama tahadhari watu wapunguze mwendo!

Sheria ya usalama barabarani iko wazi mwendo wa maeneo ambayo ni makazi ya watu, mijini, n.k

Kwa hiyo uwepo wa hayo matuta ni sahihi kabisa!


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimepita pale jumatatu iliyopita, tena ilikuwa usiku, aisee hawa TANROADS watatumaliza.

Ingawa na sisi tunawachukuliaga poa, hakuna hata kesi wanaposhtakiwa kwa uzembe na kwa kutotekeleza wajibu waliopaswa kutekeleza.
Miaka 4 iliyopita basi la Majinjah liliua watu wengi huko Mbarali kwa sababu kama hii lakini si Tanroad wala mkandarasi aliyeshtakiwa. Ni vema sasa tuanze kuishtaki na serikali pia na Polisi watusaidie kuandika ukweli wa visababishi vya ajali, mbali ya mwendo kasi/uzembe wa dereva watuandikie pia ubovu wa barabara.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hata Wafanyakazi wa AZAM TV pale Kizonzo - Shelui walikufa kwa ajali ya Lorry na Coaster kwa pamoja wakikwepa mashimo katikati ya barabara,

Ajabu Tanroad hawakuguswa.
Fikiria kipande cha kuanzia kibaha- chalinze Ile lami ina mabonde ambayo huwezi kukwepa kitu cha ghafla au kuovertake
 
Sheria inamtaka dereva kuendesha gari kutokana na hali ya barabara....kwenye matope, mvua kali na utelezi napo tumlaumu nani? Mungu?

Sent using Jamii Forums mobile app

Mawazo yako mepesi, hayasaidii kwenye mada inayojadiliwa, mvua kubwa na utelezi akili ya dereva, mashimo katikati ya barabara, alama hakuna dereva anahusikaje?
 
Na wanakusanya ushuru. Fikiria hapo ni stand kubwa,trafic wapo,hao tanroads wapo. Lakin hakuna anayejali. Wagome tu kulipa ushuru hadi warekebishe.

Hawa tanroads wanachangia kwa sehem kubwa kuharibu magari ya wananchi kwa kushindwa kuzihudumia barabara.
Ukienda pale stendi ya mbezi mwisho kama unataka kutoka kuna bonge la mshimo, hili shimo limekuwa ni kero sana kwakweli na linazidi kuchimbika sasa sijui hilo shimo wanategemea pesa za msaada kutoka kwa mabeberu

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ninachotaka kuona ni kimoja tu - Magufuli atoe amri kwa Mfugale kwamba kuanzia sasa sitaki kusikia ajali imetokea kwenye barabara kuu za lami za TANROADS na chanzo eti kulikuwa na gari ikikwepa shimo dereva aliloona ghafla katikati ya barabara.
  1. Fanya ukaguzi wa kila wakati wa barabara kuu zote za lami na kuhakikisha eidha mashimo yamefukiwa permanently au kwa hatua za muda
  2. Shimo lolote lililofukiwa kwa hatua za muda sehemu hiyo iwekwe alama za tahadhali kwa madereva kuwaonya juu ya uwepo wa shimo kubwa barabarani. Kwa hiyo wakaguzi watembee na alama za onyo kuweka barabarani
  3. KIla mvua kubwa ikinyesha TANROADS wapite kufanya ukaguzi barabarani kuhakikisha hakuna vifusi vilivyuporomokea barabarani. KUna ajali ilitokea mikumi kutokana na hili
  4. KIla Mkoa wa TANROADS uwe na kikosi cha kazi cha kurekebisha barabara kwa muda na kiwe on call masaa 24 kwa siku katika siku saba za juma
  5. TANROADS wawe na call centre ya road emergency na watoe namba za simu za emergency au watumie 112 ili madereva wanapoona hali mbaya barabarani wawapigie na watatue hilo tatizo mara moja. Namba hizi zitangazwe kikamili pamoja na kuwekwa kwenye stika za insurance ili watu wazione na kuzijua
Hebu niambieni wana JF, Mfugale akitekeleza haya, ni ajali ngapi na vifo vingapi vitaepushwa? NI gharama kubwa kiasi gani itahitajika kufanya haya?

Je tumesahau ile ajali ya Mafinga iliyoua watu zaidi ya 40 palepale ilikuwa tu ni suala la uzembe kama huu ambapo upande mmoja wa barabara ulikuwa haupitiki na basi (Majinja) ikagongana na lori katika kukwepa upande wa barabara usiopitika?

Kama Mfugale hawezi haya mie niko tayari kuteuliwa na Magufuli nisimamie TANROADS. Angalau kwa miezi sita anipe nionyenye kazi hapa, hatutaki watu wanaofanya kazi kwa mazoea:)
 
Ukienda pale stendi ya mbezi mwisho kama unataka kutoka kuna bonge la mshimo, hili shimo limekuwa ni kero sana kwakweli na linazidi kuchimbika sasa sijui hilo shimo wanategemea pesa za msaada kutoka kwa mabeberu

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu hilo shimo limeshafukiwa? Kama bado tumwandikie Mfugale sasa hivi.
 
Mie sijawahi kuona sababu za msingi za Magufuli kumsifia Mfugale. Inafanya niwe tu na wasiwasi uhusiano wao wakati Magufuli ni waziri kwa kuwa tunajua wazi miradi ya barabara ina fedha nyingi na mianya mingi ya ufisadi.Na Mfugale toka asifiwe inaonekana amejisahau sana.

Ajali na vifo kutokana na uzembe wa Tanroads katika barabara za nchini haviwezi kusafishwa na kujenga fly over Dar es Salaam. Ajali zinazotokana na mashimo makubwa ya muda mrefu barabarani ni uzembe unaopaswa Mfugale sio tu atumbuliwe kwa uzembe bali pia ashitakiwe na kufikishwa mahakamani, pamoja na kosa la matumizi mabaya ya mfuko wa kurekebisha barabara tunaochangia kwa kununua mafuta. Lakini tunajua Magufuli hawezi kumtumbua na watu wataendelea kufa kwa kuwa Tanroads hawana muda wa kufikia mashimo makubwa ya ghafla kwenye hizi barabara zetu.
Once again, hii post yangu kwenye thread yangu mwenyewe imejidhihirisha ukweli wake.
 
Back
Top Bottom