Aisha Mbegu ‘Madinda’ amegeuka kuwa muhamasishaji kwa ‘mateja’ ambao bado wanatumia ‘unga’

MaxShimba

JF-Expert Member
Apr 11, 2008
35,772
4,054
BAADA ya kutumia dawa za kuondoa sumu ya madawa ya kulevya mwilini mwake, aliyekuwa Mnenguaji wa Bendi ya Extra Bongo, Aisha Mbegu ‘Madinda’ amegeuka kuwa muhamasishaji kwa ‘mateja’ ambao bado wanatumia ‘unga’.

Akizungumza na paparazi wetu jijini Dar juzi, Aisha alisema ingawa bado anaendelea kwenda Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa ajili ya kumeza dawa lakini amepata kazi ya uhamasishaji katika Shirika la Kudhibiti Madawa ya Kulevya na Ukimwi (PHRP) lililopo Kinondoni.



Aisha Mbegu ‘Madinda’
Aidha, alisema kazi hiyo ya uhamasishaji anaifanya kwa wiki mara tatu ambapo ni Jumatatu, Jumatano na Ijumaa. Alisema hutoa somo kwa waathirika wa unga wanaoishi katika kituo hicho.

Aisha aliongeza kuwa, somo analotoa linahusu umuhimu wa kuzingatia dawa na jinsi ya kusahau utumiaji wa unga kwa vile imebainika kuna wakati waathirika walioamua kuacha, hutamani kuendelea kutumia.

“Namshukuru Mungu sasa hivi kipimo cha dawa kimepungua kwa sababu nilipoanza nilikuwa nakunywa kikombe kizima, kwa sasa nakunywa nusu kutokana na afya yangu kuendelea vizuri, lakini pia nimekuwa muhamasishaji wa PHRP kwa kutoa somo kwa waathirika,” alisema.
Alimpongeza mwanamuziki wa Bongo Fleva, Rehema Chalamila ‘Ray C’ kwa uamuzi wake wa kukubali kuanza kutumia dozi ambapo sasa afya yake imerudi vizuri tofauti na siku za nyuma.
 
Dzaaaahh nimepoteza namba yako nibipu aisha ....nakumbuka mambo yetu yale kule wistaz chalet hatareeeeeee
 
Pole zenu kwa kubwia. Hongera zenu kwa kupona uteja.

Kupona uteja inahitaji kuwa na strong willpower na mara nyingi hawa jamaa hurudia tena na wakifanya hivyo basi kuacha inakuwa ngumu sana kwani kwa 'urge' ya ile kitu teja anaweza hata kuua ili apate doze
 
Back
Top Bottom