Mlolongo
JF-Expert Member
- Jul 4, 2019
- 3,269
- 5,890
Recently nimenunua gari ndogo (babywoka).
Sisemi gari gani lakin ni mojawapo kati ya haya matano (IST, VITZ, Passo, Honda Fit, Suzuki Swift)
Leo asubuhi sana kuna issue nilikua nawahi pale UDSM. Nilikua natokea Ubungo mataa, wakati nakunja pale kona ya njia panda ya Chuo (kuna kituo cha daladala na babaji nyingi wanapaki pale). Nikaona watu wengi wanapiga mkono kuomba msaada wa lift. Wengi wao walikua kinamama wanaofanya usafi na upishi katika cafeteria mbalimbali za UDSM.
Kutokana na kuwa wanafunzi wameanza likizo ndefu, daladala zinapita kwa kuotea sana pale. Kuna ile tunasema "I wish" kila mtu anakua nazo.
Mimi siku zote nimekua najisemea, "siku nikimiliki gari, nitakua nawapa lift kina mama, watoto wanafunzi wadogo wa primary na wazee hasa during rush hours au pakiwa na tabu ya usafiri". Basi mtu mzima nikaachia mafuta, nikawasha indicator ya kushoto, nikabonyeza breki pssssssssss... Nikasimama. Nikawaambia "pandeni niwasogeze".
Aiseee huwezi amini, kwenye kibebi woka changu waliingia wamama watano na askari wa usalama barabarani mmoja. Wamama wanne na yule askari walikaa nyuma. Halafu mama mmoja bonge kuliko wote alikaa mbele. Jumla watu sita, na mimi dereva tukawa saba. Aisee nilitamani nigeuke nyuma nione wale wamama wanne na yule askari walivokaa mpaka wakaenea kule nyuma 😂 😂 😂 .
Nikawasha indicator ya kulia (kuingia barabarani tena), nikakanyaga mafuta. Hapo nikawa nafikiria maneno ya Extrovert, joshua_ok na mng'ato wanasemaga eti "hizi babywoka hazina nguvu mlimani, tena ukiwa umepakiza watu wazima zikifika mlimani zinazima, au kutetemeka sijui nini bla bla". Nikasema leo ngoja nipime ukweli wa argument hiyo.
Kutoka pale njia panda kwenda utawala kuna kamlima kamechangamka halafu kana kona kona. Naonaga bajaji zikianza kupanda ule mlima zinaenda kama zinasindikiza bibi harusi. Lakin mie nikapanda huku nakanyaga kidogo kidogo gari inaenda vizuri tu. Hakuna cha gari kutetemeka, kuzimika wala kuishiwa nguvu. Nikafika pale Utawala yule askari akashuka akasema "asante kamanda". Wale wamama watano nikawaacha pale CONAS walivoshuka wakasema "asante sana baba, uwe unapita kila siku" wenzake wakacheka "heheheeee".
Nimejisikia faraja sana kuwapa watu msaada wa lift, hasa mida ile ya asubuhi "rush hours". Hatimae ndoto yangu imetimia kwa 50%. Magari mengi yalikua yanapita pale (tena ni wafanyakazi wa UDSM), kina mama wanapunga mkono kuomba lift hakuna anayesimama. Nasubiri shule zifunguliwe siku moja nipite kituoni niwabebe wanafunzi wa primary hata wawili tu niwasogeze hapo nitakua nimekamilisha "I wish" yangu kwa 100%.
Halafu kitu kingine nimegundua ukiwa unaendesha gari unapata heshima fulani hivi kutoka kwa watu barabarani. Bila kujali gari ni lako ama umeazima, bila kujali unaishi wapi au mfukoni una shingapi.
Sisemi gari gani lakin ni mojawapo kati ya haya matano (IST, VITZ, Passo, Honda Fit, Suzuki Swift)
Leo asubuhi sana kuna issue nilikua nawahi pale UDSM. Nilikua natokea Ubungo mataa, wakati nakunja pale kona ya njia panda ya Chuo (kuna kituo cha daladala na babaji nyingi wanapaki pale). Nikaona watu wengi wanapiga mkono kuomba msaada wa lift. Wengi wao walikua kinamama wanaofanya usafi na upishi katika cafeteria mbalimbali za UDSM.
Kutokana na kuwa wanafunzi wameanza likizo ndefu, daladala zinapita kwa kuotea sana pale. Kuna ile tunasema "I wish" kila mtu anakua nazo.
Mimi siku zote nimekua najisemea, "siku nikimiliki gari, nitakua nawapa lift kina mama, watoto wanafunzi wadogo wa primary na wazee hasa during rush hours au pakiwa na tabu ya usafiri". Basi mtu mzima nikaachia mafuta, nikawasha indicator ya kushoto, nikabonyeza breki pssssssssss... Nikasimama. Nikawaambia "pandeni niwasogeze".
Aiseee huwezi amini, kwenye kibebi woka changu waliingia wamama watano na askari wa usalama barabarani mmoja. Wamama wanne na yule askari walikaa nyuma. Halafu mama mmoja bonge kuliko wote alikaa mbele. Jumla watu sita, na mimi dereva tukawa saba. Aisee nilitamani nigeuke nyuma nione wale wamama wanne na yule askari walivokaa mpaka wakaenea kule nyuma 😂 😂 😂 .
Nikawasha indicator ya kulia (kuingia barabarani tena), nikakanyaga mafuta. Hapo nikawa nafikiria maneno ya Extrovert, joshua_ok na mng'ato wanasemaga eti "hizi babywoka hazina nguvu mlimani, tena ukiwa umepakiza watu wazima zikifika mlimani zinazima, au kutetemeka sijui nini bla bla". Nikasema leo ngoja nipime ukweli wa argument hiyo.
Kutoka pale njia panda kwenda utawala kuna kamlima kamechangamka halafu kana kona kona. Naonaga bajaji zikianza kupanda ule mlima zinaenda kama zinasindikiza bibi harusi. Lakin mie nikapanda huku nakanyaga kidogo kidogo gari inaenda vizuri tu. Hakuna cha gari kutetemeka, kuzimika wala kuishiwa nguvu. Nikafika pale Utawala yule askari akashuka akasema "asante kamanda". Wale wamama watano nikawaacha pale CONAS walivoshuka wakasema "asante sana baba, uwe unapita kila siku" wenzake wakacheka "heheheeee".
Nimejisikia faraja sana kuwapa watu msaada wa lift, hasa mida ile ya asubuhi "rush hours". Hatimae ndoto yangu imetimia kwa 50%. Magari mengi yalikua yanapita pale (tena ni wafanyakazi wa UDSM), kina mama wanapunga mkono kuomba lift hakuna anayesimama. Nasubiri shule zifunguliwe siku moja nipite kituoni niwabebe wanafunzi wa primary hata wawili tu niwasogeze hapo nitakua nimekamilisha "I wish" yangu kwa 100%.
Halafu kitu kingine nimegundua ukiwa unaendesha gari unapata heshima fulani hivi kutoka kwa watu barabarani. Bila kujali gari ni lako ama umeazima, bila kujali unaishi wapi au mfukoni una shingapi.