Profesa
JF-Expert Member
- Oct 28, 2010
- 905
- 624
Nipo na ndugu mmoja hapa ambaye ameajiriwa Airtel, anayonieleza sio ya sekta ya simu, hasa kampuni za simu za mkononi, wafanya kazi wana hali mbaya sana, aidha ni sisi kwa sisi tunanyanyasana au ni kampuni yenyewe imeanza kuwa na sera mbovu za kuwa support wafanya kazi wake kiuvivu uvivu huku wakijivunia faida kubwa kama tunavyojua... kwa uchache... mishahara imekuwa ikichelewa... vitendea kazi hafifu... unatumwa mkoani unaapakizwa basi na promotion materials in bulk (wakati hii ni kazi ya carriers) bila kupewa hela ya uhakika ya usafiri... Mikataba imekuwa haiko wazi tena ni ya utata utata hebu nijuzeni mlioko jikoni maana hili linashusha kile ambacho wengi tunaamini kuwa kampuni za simu ni sekta mojawapo inayoheshimika sasa ya ajira na kibiashara... Kama hili ni kweli itabidi tuliweke bayana kwa wateja maana hadhi ya kampuni ni muhimu sana kama mnataka niwe mteja wenu