Airport ZNZ & Dar Msalani 10 USD watalii kwa polisi (hongo au hamna kwenda chooni)

Zanzibar-Nyamwezi

JF-Expert Member
Jun 11, 2013
1,244
766
Wakuu hili jambo la Polisi lamba-lamba ovyo airport mbili ambazo mimi natumia karibu kila wiki Zanzibar na Daressalaam, Polisi wanaomba rushwa nje nje, yaani wananyoosha mkono kwa mtalii kama omba omba hivi.

La ajabu ambalo nimeshuhudia tukio la kwanza Daressalaam December 2012 mtalii kutoka Ulaya akilalamika, na bahati nzuri naelewa vizuri alichokuwa anahadisia kwa kundi la wenzake, yeye alikuwa anasubiri ndege ya transit kuelekea Zanzibar, Mama huyo alibanwa, akaomba msaada polisi, aonyeshwe choo, polisi kamkatisha kona mbili hivi halafu kamwomba Dola kumi ili amwonyeshe choo.
Mama huyo hakumpa alirudi tu, sio kuwa hana, ila hakupenda njia aliyotumia polisi huyo ya kuomba rushwa eti tu kwa sababu amebanwa.

Alidhani polisi vijibwa vyetu ni kama Maafsa wa Kwao ambao ndio kimbilio la Raia kwa kila kitu.
nimehadisia hapa Zanzibar, nikaambiwa hapa ndio mbaya zaidi kuliko Dar polisi omba omba airport.

NDUGU ZANGU AIRPORT NDIO PICHA YA KWANZA YETU SOTE KAMA WATANZANIA, TUPAMBANE NA KILA ANAEJARIBU KUTUCHAFULIA NYUSO ZETU MLANGONI.
 
Wakuu hili jambo la Polisi lamba-lamba ovyo airport mbili ambazo mimi natumia karibu kila wiki Zanzibar na Daressalaam, Polisi wanaomba rushwa nje nje, yaani wananyoosha mkono kwa mtalii kama omba omba hivi.

La ajabu ambalo nimeshuhudia tukio la kwanza Daressalaam December 2012 mtalii kutoka Ulaya akilalamika, na bahati nzuri naelewa vizuri alichokuwa anahadisia kwa kundi la wenzake, yeye alikuwa anasubiri ndege ya transit kuelekea Zanzibar, Mama huyo alibanwa, akaomba msaada polisi, aonyeshwe choo, polisi kamkatisha kona mbili hivi halafu kamwomba Dola kumi ili amwonyeshe choo.
Mama huyo hakumpa alirudi tu, sio kuwa hana, ila hakupenda njia aliyotumia polisi huyo ya kuomba rushwa eti tu kwa sababu amebanwa.

Alidhani polisi vijibwa vyetu ni kama Maafsa wa Kwao ambao ndio kimbilio la Raia kwa kila kitu.
nimehadisia hapa Zanzibar, nikaambiwa hapa ndio mbaya zaidi kuliko Dar polisi omba omba airport.

NDUGU ZANGU AIRPORT NDIO PICHA YA KWANZA YETU SOTE KAMA WATANZANIA, TUPAMBANE NA KILA ANAEJARIBU KUTUCHAFULIA NYUSO ZETU MLANGONI.

Hilo ni janga la taifa!!! Ni aibu sana Polisi kama kioo cha jamii pale Airport kugeuka ombaomba. Kama kuna viongozi waandamizi wa Polisi wanasoma taarifa hizi hapa JF wachukue hatua jamani kila mara ofisini tu wakati nchi inateketea hivi, tunapata hasira sana tunataka hata kutukana lakini tunaogopa BAN toka kwa MOD!!!
 
Nawasabahi waungwana, kwanza namshukuru mtoa uzi huu kwa kututaarifu, kwani uchungu wake umetugusa wote katika
hali hii ya kashfa ambayo tunaipakizia matope nchi yetu bila siye wenyewe kujitambua.
Hayo asemayo ni kweli. "Wakati huohuo waTanaznia tunatangaza kukribisha Utalii nchini " Sasa inakuwa Mmoja anajenga na mwengine anabomoa.... Hapo tutahitaji hatua za kisheria kuchukuliwa ili kuweza kulinda JINA la TAIFA kwa sababu ni Masilahi ya TAIFA ndiyo yanayochafuliwa na kipato cha Taifa huyayuka hewani. Endapo mtalii mmoja tu akitusema kwa ubaya ataweka taathira kwa watalii wengi (mouth talks) walokuwa karibu naye na wategemewa !! impact ya sifa yeyote ile ni kubwa. basi tubadilike kwa kulinda masilahi yetu na nchi kwa ujumla.
 
Sasa utawala wa nchi tunagawiana kiukoo unategemea nini? Mkuu wa polisi ni shemeji kuna kitu hapo kweli? Tutalamike tu kwani tuliyataka wenyewe. Hadi nchi imenuka mavi kabisaa tukiwa tunaona. Sasa imefikia kutuuwa kisha watanzania tumepelekea kuelewa. Huyu Kikwete ni afadhali asingalizaliwa kwani Tanzania ingelibakia maskini, lakini nchi yenye heshima na utu. Kwa sasa tumekosa vyote.
 
Back
Top Bottom