Airport yetu ya Dar inanuka uozo wa rushwa!

shamba la bibi hili!! hata box la condoms waliniomba rushwa!! laanakhum wala rushwa wote!
 
Nikiwa muathirika mkuu wa jambo hili limeniuma sana tena sana na sijui watanzania wangapi washafanyiwa hili jambo. Nikiwa miongoni wa wasafiri na kusubiri mizigo yetu pale sehemu ya kukusanyika mizigo nami nilikua na ka TV kangu nimekuja nacho kumbe sikua peke angu na kulikua na wazungu nao walikua na ma music system na vifaa vya electronic vyingine.

Baada ya kupakia kwenye kitoroli changu nikasimama nyuma ya wale wazungu hapo ndo wakaja watu wawili mmoja akajitambulisha kama TRA na mwengne kama ofisa usalama nikawauliza shida yao wakanijibu hii tv ukailipie ushuru nikamwambia sawa but na wale wazungu pia wakalipie ushuru music system zao yule jamaa wa TRA akaja juu wewe usituchagulie mtu wa kulipa ushuru nikamjibu mimi ni mhasibu na najua wajibu wa kulipa kodi so waite na wale walipe otherwise nitatafuta haki mbele ya safari akauchuna na kuondoka zake huku akinitazama kwa jicho la ushenzi. Nilipo muhadithia jamaa yangu mmoja ambae ni mhasibu pia akaniambia wale ni wababaishaji na sijui hata kama ethnic ya uhasibu wanaijua.

My take,
Serikali pamoja na watu wa idara ya mapato tupieni jicho airport maana kuna ushenzi wa hali ya juu. Na sitalifungia jicho hili suala nitahakikisha namfikishia kitilya alivalie njuga
Kwani huyo KITILA HAJUI? INAMAANA HAKUNA MTU WA SERIKALI ANAYEJUA MADUDU YA PALE AIRPORT? BELIEVE ME BROTHER HATA HUYO BWANA UNAEMTAJA ANANUFAIKA NA HAKO KA MCHEZO NDIO MAANA HAWATAFUTI SULUHU YA KUDUMU! NI WAJIBU WETU WATANZANIA KUTAFUTA SUSTAINABLE SOLUTION TO THESE VERY CHILDISH AND STRANGE INCONVINIENCES! VIONGOZI WETU TUMEWAPA MAGARI MAZURI; ULINZI MADHUBUTI NA MARUPURUPU MENGI TU; LAKINI HATA SUALA LA DK5 KUMALIZA UPUUZI WA PALE AIRPORT HAWAWEZI MPAKA AJE MWAKYEMBE AU MAGUFULI!
 
Pale pameoza!wananuka rushwa na wizi wa kwenye mizigo!mimi walikomba dola zangu 2500!nilishuka na Qatar ya Mchana kama sikosei ni QR544 A7-AHD...Nimemaliza kubeba mizgo na tolori,wakanisimamisha jamaa wawili...wakapekua sana passport yangu!mara kwanini unasafiri sana,mara wiki jana tu ulipita hapa...una kazi gani?nikawambia mi mfanyabiashara!wakanichukua na mizigo yangu..wakaenda kunipekua eti nimebeba unga...wakapekua mpaka kwenye boxer!aggrrrr nikafula sana...nikawambia sina unga mi nimetoka Doha kibiashara!kuja kutahamaki wamekwapua vidola vyangu,wakaiba simu na laptop!hawakunikuta hata na sigara...sikuwa hata ni unga maskini mie!ila wanawaogopa wazungu kisa lugha...pana wezi pale si Usalama wala custom!Unatamani ingekuwa inawezekana ukatue hata KIA upande bas uje Dar!JULIUS N.INTERNATIONAL AIRPORT NI WEZI...WANAOMBA MPAKA PAFYUMU,WACHAFU NA WATENDAJI WAKE WA SECURITY WAPELEKWE HATA ENGLISH COURSE!WANASHNDWA HATA KUWASILIANA NA WAGENI KISA LUGHA...HIVI VIONGOZ WETU HAWAENDI NJE WAKAJIFUNZE VIWANJA VYA WENZETU?INAUMA SANA SANA SANA SANA
 
Ule uwanja kuupa Jina la Mwalimu Nyerere ni aibu kubwa sana, ni bora wangeubadilisha jina na kuita Mkapa au Kikwete kwa jinsi ulivyojaa rushwa. Mwalimu alikuwa sio mlarushwa au mfujaji wa mali zetu. Uwanja wenyewe mchafu, vyoo vichafu, wafanyakazi walarushwa kama waajiriwa waliopangishwa na watanzania kule Magogoni. Hauna maana au faida yoyote kwa watanzania. Tena ukishuka pale ukiwa mtanzania ndio wanakuumiza sana kuliko mgeni, hii nchi imelaaniwa sana wenyewe kwa wenyewe hatupendani.
Ahsante mkuu kwa kunikoga moyo, yaani umenifurahisha sana!! tunahitaji system overhauling.
 
Mkuu. Sio kila mhasibu ni jambazi na fisadi mm binafsi nina audit firm yangu na sijawahi kumdhulumu mtu wala serikali yangu so na mm sipendi kudhulumiwa

Hakuna jambo la kushangaza hapa. Kama ufisadi unafanywa kuanzia ikulu, itakuwa ajabu airport? Huo ndiyo utamaduni uliowekwa na haka-kasirikali. SASA USIISHIE HAPO CHUKUA HATUA zaidi ya kuunganisha nguvu kukaondoa ka-sirikali madarakani... peopleeessss!!!
 
ethiopia ,air india, emirates, qatar lazima msachiwe hasa ukiwa kijana coz vijana wengi wanaitumia hii airpot kupisha unga na mizigo isiyolipiwa ushuru. NDIO HALI HALISI.
 
Hahahaha airpot kama stand ya mkoa ubungo. sasa utacheka ikiingia ethiopia air ndege nzima kama kuna mzungu basi ni mmoja. Utakuta abiria mmoja ana mizigo kama gunia 3 tena rumbesa . Harafu anabishana kulipa ushuru. Achana na vijana wa bwimbwi wa kumwaga. Yaani ni njaa + njaa = vituko
 
Na hao abiria vijana ukiuliza anakaa wapi utasikia magomeni mapipa, ilala ,kinondoni etc . Kanyoa kipara, katoboa hereni na macheni kibao . Sasa si lazima kuwe na sachi ya kutosha wandugu au.
 
Si kila anaepanda ethiopia ama air india ama qatar ni muuza unga hapana mfanya biashara anatafuta unafuu bt hili la kuwaacha wageni wakaja kusumbuliwa wazawa huo ni upumbavu na ujuha shame on dem
 
Mkuu Tanzania Air India haiji..ebu fanya uchunguzi
ethiopia ,air india, emirates, qatar lazima msachiwe hasa ukiwa kijana coz vijana wengi wanaitumia hii airpot kupisha unga na mizigo isiyolipiwa ushuru. NDIO HALI HALISI.
 
Kwani kutoka Magomeni na kunyoa kipara kuna nini?acha dhana potofu!ndo mana mnawaacha wazungu kisa Lugha inawashnda na wapo smart
Na hao abiria vijana ukiuliza anakaa wapi utasikia magomeni mapipa, ilala ,kinondoni etc . Kanyoa kipara, katoboa hereni na macheni kibao . Sasa si lazima kuwe na sachi ya kutosha wandugu au.
 
ethiopia ,air india, emirates, qatar lazima msachiwe hasa ukiwa kijana coz vijana wengi wanaitumia hii airpot kupisha unga na mizigo isiyolipiwa ushuru. NDIO HALI HALISI.

Wanashindwa kudhibiti unga na wauza unga mitaani wataweza Kikwete International Corruption Airport?
Wapo pale kwa ajili ya kunyanyasha Watanzania sio kuhudumia, Mijambazi inayoomba na inanuka vikwapa utafikiri wabeba magunia wa Kariakoo, rushwa yote wanayochukuwa lakini bado wamejikondea kama ndama wa Vasco, na wengine ukiwaona wanamitumbo mikubwa utafikri wanaumwa kwashakoo kwa ajili ya kula rushwa
 
Kwa kweli ule uwanja ni kero sana, na hawa wanaojiita Usalama wa Taifa na TRA pale wanazidisha kero kwa maswali yao. Siku baada ya kupita kwenye Ukaguzi wao, wakati naondoka Jamaa Mmoja akanisimamisha na kuniuliza nimebeba nini kwenye Begi langu? Nikamjibu nenda kamuulize yule dada (Mkaguzi) manake ametoka kunikagua sasa hivi, kisha nikaondoka. Wale ukiwaendekeza au ukionesha uoga lazima wakutoe mshiko..
 
Smartness ina matter dunia nzima. Kama hutaki basi. Unakuja na mizigo furushi kama landrover.receipt au invoice hutaki kutoa. ushuru unaleta longolongo. ABIRIA NDIO WANAKARIBISHA RUSHWA NA MLOLONGO MREFU
 
Hahahaha airpot kama stand ya mkoa ubungo. sasa utacheka ikiingia ethiopia air ndege nzima kama kuna mzungu basi ni mmoja. Utakuta abiria mmoja ana mizigo kama gunia 3 tena rumbesa . Harafu anabishana kulipa ushuru. Achana na vijana wa bwimbwi wa kumwaga. Yaani ni njaa + njaa = vituko

Kupe si kweli Ethiopian Airline mbona nimesafiri nayo juzi juzi tu wazungu walikuwa wengi tu ndani ya ndege. Tatizo uwanja wa ndege ni management mbona hata kwenye BA kuna watu wanakamatwa na unga?
 
ethiopia ,air india, emirates, qatar lazima msachiwe hasa ukiwa kijana coz vijana wengi wanaitumia hii airpot kupisha unga na mizigo isiyolipiwa ushuru. NDIO HALI HALISI.

tatizo si kusachiwa, tatizo ni kuibiwa na kuporwa pesa
 
basi angalau ule uwanja wangeukarabati.aah aibu tupu.wao ni rushwa na kuomba basi.inasikitisha kwa kweli,maybe mishahara yao midogo
 
Back
Top Bottom