Airport - Karamagi uso kwa uso na Zitto

Katika hatua nyingine, Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Kabwe Zitto, alikutana uso kwa uso na Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi na kusahau tofauti zao kwa muda.


'Mahasimu' hao walikutana jana uwanjani hapo na kusalimiana kwa kupeana mikono.Katika tukio la jana, Zitto alikutana na Karamagi uwanjani hapo alipokuwa akitokea nchini Kenya alikokwenda kuhudhuria kampeni za mgombea urais, Raila Odinga.


Karamagi alifika uwanjani hapo saa 8:00 mchana kwa ajili ya kumpokea Rais Jakaya Kikwete aliyewasili uwanjani hapo kutoka ziarani nchini Marekani.


Karamagi aliyekuwa na mawaziri wengine na waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari katika chumba cha watu mashuhuri (VIP), walipigwa na butwaa baada ya kumuona mbunge huyo akishuka ngazi akitokea katika sehemu ambayo wasafiri mashuhuri hutumia kupita.


Hali hiyo ilifanya karibu ukumbi mzima kukaa kimya kwa sekunde kadhaa kabla ya kuangua kicheko baada ya Zitto ambaye inasadikiwa alisafiri katika ndege moja na Rais Kikwete, kumshika mkono Waziri Karamagi huku waandishi wakichukua picha za tukio hilo. Kitendo hicho kilimshawishi Waziri Karamagi pia kuangua kicheko.


Hata hivyo, mbunge huyo alikaa katika eneo hilo muda mfupi na baadaye aliondoka uwanjani na kuacha maswali mengi yasiyo na majibu kwa viongozi hao waliotaka kujua alikokuwa ametokea na sababu za kufika wakati huo ambao rais aliwasili.


Tukio hilo la kusalimiana limetokea ikiwa ni mara ya kwanza kwa 'mahasimu' hao kukutana tangu Zitto asimamishwe kuhudhuria vikao vya Bunge hadi Januari, mwakani, baada ya kuwasilisha bungeni hoja binafsi kuhusu mkataba wa mradi wa mgodi wa dhahabu wa Buzwagi, wilayani Kahama uliosainiwa na waziri huyo jijini London, Uingereza.


Zitto aliwasilisha hoja hiyo akitaka kuundwa Kamati Teule kuchunguza mazingira ya utiaji saini mkataba huo.

http://www.mwananchi.co.tz/newsre.asp?id=2182

Mkuu Mwanakijiji cheki tena na source yako....naona mamboni tofauti apo.....


Hoja yangu imejibiwa, tufunge mjadala!
 
Thread Failed. why do we have to make a big deal out of every little thing ? jamani, mwanakijiji vipi tena wewe mkuu ? kama karamagi kamchunia zitto thats them, tunachotaka maendeleo, salamu zao hazina umuhimu kwenye taifa letu !



Thats JF for you

saa zingine wewe soma tuu maana ukistajaabu ya musa utashngaaa ya firauni
 
Ningelikuwa nzitto nisingempa mkono fisadi (joke),

Walipaswa kusalimiana kwani huo ndio utanzania ilaq kila mmoja akijua kuwa pindi akifanya madudu hakuna kulindana , nahisi kizazi cha wakina kingunge kuondoka muda sio mrefu .
 
Mwanakijiji naye kwa the dataz!!!!!!

Mwaka huu kuna kazi kweli JF.

Hivi lini tutaanza kujadili sera za vyama?
 
Mzee anaelekea kubaya!!! Unapomshambulia mtu/kiongozi beyond mambo yanayohusu maslahi ya taifa,,, ni ushabiki ambao hauna uzalendo ambao tuna-claim hapa!

Naanza kukumbuka watu waliokuwa wakereketwa/wafukukutwa/ngangari/ngunguri!!! Hoja zao zilikuwa hazitofautiani sana na ujumbe wa thread hii!!!


No wonder wakini kama Said Yakub siwasikii tena!!!

Jamani katika sisa vitu hivi ni muhimu sana, mnaweza kumbuka Al gore alipoteza umaarufu na pengine uchaguzi kwa kushangaa kwa sauti kwenye mic. Nyie mnashindwa kuelewa athari za waziri anaye mchunia kiongozi mwenzie aliyefichua uovu na kusema ni jambo dogo?

Mmeshindwa njia ya kumpinga MM mnaamua kumtegea. yeye kama raia mwingine ategemei waziri anaye act kama madada wa magomeni.

Huyo Said Yakubu kama naye alikuwa ana mawazo kama yako au ya kada au ya mtu wa pwani afadhali alivyojitoa labda amekwenda kuosha damu ya watanzania kwenye mikono yake
 
Kama kuna mtu alisoma maneno ya mwisho niliyoandika na muda niliyoopost? Utaona kuwa nilipoposti it was about few minutes tangu tukio hilo litokee na kabla Rais hajawasili. Sasa kama details za baadaye hazikuwa sahihi mniwie radhi lakini si kusudio langu kuupotosha umma, I report as I get the news... na there is always room for mistakes and corrections..... so you have to learn to live with it.. ambao mnatarajia kuwa "mwanakijiji will always be right" mnaweka standard ambayo hakuna mwanadamu anayeweza kuitimiza.
 
(Tanzania Daima)

IKIONEKANA ni mwendelezo wa kukwepa kujibu tuhuma, maswali na ukosoaji dhidi ya serikali kutoka kwa waandishi wa habari, jana, Rais Jakaya Kikwete, alionekana dhahiri kukwepa kuzungumza na waandishi wa habari, waliojitokeza katika mapokezi katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu J.K. Nyerere, Dar es Salaam.

Rais Kikwete ambaye amekuwa hana kawaida ya kukataa kuzungumza na waandishi wa habari mara anaporejea kutoka safari za nje ya nchi, baada ya kuwasili uwanjani hapo jana, alionekana kusalimiana na viongozi mbalimbali wa chama na serikali waliofika kumpokea.

Hali hiyo ilionekana kuwakatisha tamaa waandishi wa habari waliofika mapema uwanjani hapo wakiwa na shauku ya kupata ufafanuzi juu ya ziara yake sanjari na masuala mbalimbali yanayoendelea nchini hivi sasa.

Wakati Rais Kikwete akikwepa kuzungumza na waandishi wa habari nchini, ameonekana kukubali kuzungumza na vyombo vya habari, yakiwamo magazeti ya nje ya nchi.

Rais Kikwete amerejea nchini huku akikutana na matukio kadhaa ya mawaziri wake kuzomewa na wananchi wakati wakiwa katika ziara za kuelezea ubora wa bajeti mikoani, ambayo ilisomwa bungeni na Waziri wa Fedha, Zakia Meghji, miezi kadhaa iliyopita.

Mlolongo wa matukio hayo, pamoja na shinikizo kutoka kwa mabalozi wa nchi za nje, viongozi wa dini, wanaharakati na wananchi wanaotaka serikali ijisafishe dhidi ya tuhuma za ufisadi na zile za Benki Kuu ya Tanzania (BoT), unaonekana kumtesa Rais Kikwete.

Jana, rais baada ya kusalimiana na mawaziri na watendaji wengine wa ngazi za juu serikalini, alitoka nje ya chumba cha watu mashuhuri (VIP) na kusalimiana na makada wa CCM na wananchi wengine kabla ya kuingia katika gari na kuondoka na msafara wake.

Kabla ya kuwasili uwanjani hapo, umati wa watu wakiwamo makada wa CCM, walijitokeza wakiwa wamevalia sare za CCM huku wakiimba nyimbo za kuwakejeli wapinzani.

Mapokezi hayo yalitekwa na wafuasi wa CCM walioanza kuingia uwanjani hapo kwa mabasi ya abiria huku wakiwa na mabango yenye ujumbe wa kumsifu rais.

Baadhi ya mabango hayo yalikuwa na ujumbe unaosomeka: ‘Hongera Mheshimiwa… kwa kutangaza kuwapata wawekezaji,’ sisi ni CCM tawi la……, ‘Karibu Mwenyekiti… tuko pamoja na wewe’, huku wakisaliana kwa salamu za kichama.

Ujumbe na mabango hayo kwa ujumla, yalionekana kuwakera baadhi ya wananchi wa kawaida waliofika uwanjani hapo kumlaki rais.

Baada ya kushuka kwenye ndege, rais alilakiwa na Waziri Mkuu, Edward Lowassa, Waziri wa Fedha, Zakia Meghji, Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi, Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko, Basil Mramba, Spika Samuel Sitta na viongozi wengine wa chama na serikali.

Baada ya rais kuingi VIP, baadhi ya wasaidizi wake walisikika wakiwaambia waandishi waliokuwa wamemtangulia, kuwa hawakuwa na taarifa kama rais angekutana na waandishi wa habari.

Kwa mazingira hayo, waandishi wa habari walitoka nje baada ya kuelezwa kwamba baada ya muda rais atatoka nje kuwasalimia wananchi waliofika uwanjani hapo kumlaki.

Hata hivyo, baada ya kutoka nje, waandishi walikuwa na wakati mgumu wa kupata nafasi ya kumuuliza maswali, huku wasaidizi wake wakionekana kutotoa nafasi hiyo hadi alipopanda gari na kuondoka uwanjani hapo.

Katika hatua nyingine, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto (CHADEMA), jana aligongana ana kwa ana na Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi.

Mbunge huyo, aliyesimamishwa kuhudhuria vikao vya Bunge kwa miezi sita baada ya kudaiwa kulidanganya Bunge kusema uongo kuhusu kusainiwa kwa mkataba wa Buzwagi, aligeuka kuwa kivutio katika mapokezi hayo, baada ya kugongana ana kwa ana na Karamagi, aliyesaini mkataba huo nchini Uingereza.

Zitto alisimamishwa baada ya kutoa hoja ya kutaka kuundwa kwa kamati teule ya Bunge kuchunguza mazingira yaliyofanya mkataba huo kusainiwa London, Uingereza, Februari mwaka huu huku kukiwa na tamko la rais la kusitisha kusainiwa mikataba mipya.

Katika tamko hilo la Desemba mwaka juzi, Rais Kikwete alitaka kusitishwa kusainiwa kwa mikataba mipya hadi mikataba iliyopo itakapopitiwa upya.

Baada ya kukutana jana, Zitto alionekana kumchangamkia Karamagi aliyekuwa na Waziri Meghji, kwa kusalimiana nao na kisha kuondoka eneo hilo.
Zitto, alikuwa anarejea nchini akitokea Kenya alikokuwa amealikwa kwenda kuhudhuria uzinduzi wa kampeni za Chama cha Orange Democratic Movement cha Raila Odinga, ambako alikaa kwa siku tatu.

Rais Kikwete alikuwa ziarani nchini Marekani, ambako pamoja na mambo mengine, alihudhuria Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.

Katika ziara hiyo aliyoianza Septemba 15, Kikwete amefanya mambo mengi katika nyanja za siasa, uwekezaji, utalii, madini, michezo, biashara, elimu na utamaduni.
 
Zitto na Karamagi uso kwa uso

2007-10-08 17:27:12
Na Mwandishi Wetu, Jijini


Ama kweli siasa ni mchezo wa ajabu! Nani angejua kwamba mahasimu wawili ambao wanapelekana puta hivi sasa, Mheshimiwa Zitto Kabwe na Waziri wa Nishati na Madini, Mheshimiwa Nazir Karamagi, wangechekeana na kupeana mikono kama mtu na mdogo wake!

Lakini hivi ndivyo ilivyokuwa jana baada ya wawili hao kukumbana uso kwa uso kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere.

Inaelezwa kuwa mara baada ya Mhe. Zitto kutua uwanjani hapo akitokea nchini Kenya alikokuwa amekwenda kushuhudia uzinduzi wa kampeni za chama cha Orange cha Raila Odinga, alikwenda moja eneo wanaofikia watu maarufu.

Hata hivyo bila kutarajia, aliwakuta viongozi kadhaa akiwemo Waziri Karamagi kwenye ukumbi huo ambao pia inasemekana walishtuka kumuona.

Hali hiyo ilisababisha baadhi ya viongozi wa Serikali waliokuwa wamefika katika uwanja huo kila mmoja kusubiri kwa hamu kuona nini kitatokea baada ya `marafiki? hao kukumbana.

Habari zaidi zinasema Mhe. Zitto alikwenda kumsalimu Waziri Karamagi aliyekuwa kimya,hali iliyowafanya wawili hao kucheka na baadaye viongozi wengine nao kuungana nao.
Waziri Karamagi pamoja na viongozi wenzake, walifika uwanjani hapo kumpokea Rais Jakaya Kikwete wakati Mhe. Kabwe alikuwa anatokea nchini Kenya na akapanda ndege moja na JK.

Hiyo ni mara ya kwanza tangu mbunge huyo aliyesimamishwa kuhudhuria vikao vya Bunge hadi mwakani Januari kukumbana ana kwa ana na Waziri Karamagi.

Zali kati ya wawili hao liliibuka baada ya mbunge huyo kuibuka hoja bungeni iliyomtuhumu Waziri huyo kusaini mkataba wa madini mjini London, Uingereza katika mazingira ambayo yanaashiria rushwa.


SOURCE: Alasiri

My Take:

Katika ripoti zote zinazofuata zinaonesha kuwa ni Zitto aliyechukua initiative ya kumsalimia Karamagi na kulikuwa na ka aina fulani ka awkwardness .. so, I'm sticking to my original story!
 
Zitto na Karamagi uso kwa uso

2007-10-08 17:27:12
Na Mwandishi Wetu, Jijini


Ama kweli siasa ni mchezo wa ajabu! Nani angejua kwamba mahasimu wawili ambao wanapelekana puta hivi sasa, Mheshimiwa Zitto Kabwe na Waziri wa Nishati na Madini, Mheshimiwa Nazir Karamagi, wangechekeana na kupeana mikono kama mtu na mdogo wake!

Lakini hivi ndivyo ilivyokuwa jana baada ya wawili hao kukumbana uso kwa uso kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere.

Inaelezwa kuwa mara baada ya Mhe. Zitto kutua uwanjani hapo akitokea nchini Kenya alikokuwa amekwenda kushuhudia uzinduzi wa kampeni za chama cha Orange cha Raila Odinga, alikwenda moja eneo wanaofikia watu maarufu.

Hata hivyo bila kutarajia, aliwakuta viongozi kadhaa akiwemo Waziri Karamagi kwenye ukumbi huo ambao pia inasemekana walishtuka kumuona.

Hali hiyo ilisababisha baadhi ya viongozi wa Serikali waliokuwa wamefika katika uwanja huo kila mmoja kusubiri kwa hamu kuona nini kitatokea baada ya `marafiki? hao kukumbana.

Habari zaidi zinasema Mhe. Zitto alikwenda kumsalimu Waziri Karamagi aliyekuwa kimya,hali iliyowafanya wawili hao kucheka na baadaye viongozi wengine nao kuungana nao.
Waziri Karamagi pamoja na viongozi wenzake, walifika uwanjani hapo kumpokea Rais Jakaya Kikwete wakati Mhe. Kabwe alikuwa anatokea nchini Kenya na akapanda ndege moja na JK.

Hiyo ni mara ya kwanza tangu mbunge huyo aliyesimamishwa kuhudhuria vikao vya Bunge hadi mwakani Januari kukumbana ana kwa ana na Waziri Karamagi.

Zali kati ya wawili hao liliibuka baada ya mbunge huyo kuibuka hoja bungeni iliyomtuhumu Waziri huyo kusaini mkataba wa madini mjini London, Uingereza katika mazingira ambayo yanaashiria rushwa.


SOURCE: Alasiri

My Take:

Katika ripoti zote zinazofuata zinaonesha kuwa ni Zitto aliyechukua initiative ya kumsalimia Karamagi na kulikuwa na ka aina fulani ka awkwardness .. so, I'm sticking to my original story!


Mwanakijiji,

Tafadhali usije hata siku moja ukatumia gazeti la Alasiri kwenye utetezi wako, unaweza kuumbuka bure.

Hao Alasiri wapo kufurahisha watu baada ya kuchoka na kazi.
 
siyo hilo tu nimefuatilia original source na kulinganisha na ilivyoripotiwa na vyombo mbalimbali. Kumbuka nilipoweka news alert hakukuwa na chombo chochote kilichoripoti wakati huo..
 
Heshima ya JF ipo palepale,na hakuna anayetegemea mawazo ya mtu hapa,wewe Kada Mpinzania naona una chuki binafsi na Mwanakijiji.Hali ya hewa ya JF bado haijabadirika kama unavyodai,ila imebadirika kwa kuogopwa na mafisadi,kutoa mawazo makini,kuelimisha jamii,sasa wewe sijui unaposema hali imebadirika unamaanisha nini?Sidhani kama tutafika endapo tutakalia umbea badala ya kuongelea masuala ya maendeleo.

sawa nina chuki binafsi na mwanakijiji, that is in your way !
 
Kada Mpinzani, kwa jinsi Mkjj alivyoiweka hapa, huwezi kutumia maneno uyasemayo... Inaonekana una KINYONGO naye. Yeye ndiye wa kwanza kuweka kwamba ZK alikutana uso kwa uso na hao viongozi, sasa swala la kumchunia na kutomchunia lisiwe sababu ya kuanza kubadili mwelekeo... Kwa wanaoona hii si issue ya kujadiliwa hawaelewi nini maana ya HABARI... NAWAPONGEZA MWANANCHI KWA KULIONA HILO japo nadhani picha ya Kamaramagi na ZItto ingekua ni habari nzuri ya kuuza kwa wasomaji, lakini watu walibanwa kama Mtanzania walivyopewa "AGIZO toka JUU" wakaiweka picha ukurasa wa ndani wakati wao walitaka kuiweka ukurasa wa mbele. Kwa mkjj kuweka hapa alivunja ukimya na ndipo mjadala ukaanza na habari zaidi zitakuja kuhusiana na suala hilo. Kwa hiyo kwa wenye habari zaidi wazilete si kuanza kupondana. Habari huvunja habari nyingine

sawa nina kinyongo na Mwanakijiji !
 
heheee, i wonder kama wangesalimia if that would make any difference ! labda jamaa wote (zitto, karamagi) ni freemansons hivyo walipeana ishara zao wenyewe waliokuwepo pale ( mwanakijiji hukuwepo ) labda hawakuelewa !

..salamu zina maana zaidi ya moja!

..inaweza ikawa kebehi,kujigonga,kujipendekeza,ustaarabu,utongozaji,kujionyesha,kulaghai,kuibia,n.k

..deal ni kujua mtu kakusalimia kwa nia gani?shari au kheri?
 
..salamu zina maana zaidi ya moja!

..inaweza ikawa kebehi,kujigonga,kujipendekeza,ustaarabu,utongozaji,kujionyesha,kulaghai,kuibia,n.k

..deal ni kujua mtu kakusalimia kwa nia gani?shari au kheri?

ndio hapo niliposema salamu zao hazina maslahi kwa taifa letu ! thats personal !
 
hivi muungwana kila akirudi toka safari zake ni lazima baraza lake waje kumpokea? maana nimeshaona zaidi ya mara moja...sizimii kabisa hii tabia ya kupoteza muda na kutujazia foleni.
 
asipopokewa na kundi zima la serikali kuanzia Makamu, Waziri Mkuu, n.k atajuaje kuwa yeye ni Rais?
 
hivi muungwana kila akirudi toka safari zake ni lazima baraza lake waje kumpokea? maana nimeshaona zaidi ya mara moja...sizimii kabisa hii tabia ya kupoteza muda na kutujazia foleni.

..babako akitoka safari[tuseme unamtegemea]hutaenda kumpokea?

..ni suala la jadi na tamaduni,zaidi ya kupoteza muda!

..kwanza bora wakapoteze muda,badala ya kuutumia kutuibia!
 
Back
Top Bottom