Aina za matakwa ya wanawake

AbuuMaryam

JF-Expert Member
Dec 26, 2015
2,536
4,513
Kabla ya Ndoa kuna aina mbili:-
1. ANAYETAKA TU ILE SHEREHE IONEKANE NA IJULIKANE NA YEYE KAOLEWA.(Aina hii ni ya hatari), hawa ndio ndoa zao hazizidi mwaka zinakuwa zimevunjia, kwa sababu lengo la msingi limeshatimia, so whats waiting next then?

2. WANAYOITAKA ZAIDI HIYO NDOA.(afadhali ya hawa wana nia na hiyo ndoa), wako tayari hata bila sherehe hata kimya kimya mradi ajistiri apate heshima yake kuwa na nyumba yake. Atleast hawa huheshimu ndoa zao.

Sasa katika kundi hili la pili, ndani yake wapo wa aina mbili, ambao ni;-
a) WANAOITAKA ZAIDI NDOA NA MATOKEO YAKE. Hawa huipenda zaidi ndoa yao na kile kitakachotokana na ndoa zaidi ni mtoto, huwapenda na kuwajali sana watoto wao kiasi kwamba hatojali sana hata kama akiachwa lakini haina shida...ana mtoto.

b) ANAITAKA NDOA NA MWENYE NDOA. Kundi hili ni adimu sana, si rahisi katika kumi umpate hata mmoja...labda katika 100 umpate mmoja...hawa huitaka ndoa na Mume zaidi hupendwa...yeye mume kwake ni bora zaidi kuliko kitu chochote kile..na hawa ndio hata kama ana mtoto/watoto kwake mume first anapokuwepo.


SWALI:
KATIKA HAO WOTE WEWE MDADA UNAJIWEKA KUNDI GANI...?


NA JE KATIKA HAO MAKUNDI HAYO NI YUPI ATAIFURAHIA ZAIDI NDOA YAKE.
 
kazi ipo sikuhizi ni vurugu tupu yani ndani ya ndoa ni mateke na vichwa vya haja ila haya mambo kunawakati unaweza yawaza ukaona bora mtu akawa na maisha yake hasa ka ukikutana na namba 1
 
Na hao.ndio wengi. Wanataka ndoa maonyesho.
Na utawajua tu .. maana wengi utasikia harusi yangu nataka kile nataka hichi nataka sijui nn..
Mambo kibaao

Ukiona hiz dalili bail out mapema.

Wengine ni wale wa kutaka mtoto. Yaani yeye shida yake mtoto. Akishampata mapenz yanaisha.
Hawa nao utawajua kwa story zao.. utawaona tu.
Ukimpata mwanamke wa kundi la kwanza ni hatari sana kuliko hatari yenyewe.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukimpata mwanamke wa kundi la kwanza ni hatari sana kuliko hatari yenyewe.
Hawa wa instagram wote wapo kundi namba moja wenyewe wanasema wanataka wachafue insta tu basi na kuishi fake life ukitaka kuwapima we ukiingia kwenye gari utakuta busy kujipiga picha za ndani ya gari jua sio mwanamke huyo
 
Back
Top Bottom