G Sam
JF-Expert Member
- Apr 20, 2013
- 11,555
- 35,874
Hili ndilo jambo ambalo pengine ni aina ya mambo yanayonifanya niwaze sana kuhusu kifo.
Kuna watu wakati wa kufa ni anakumbana na aina fulani sijui tuseme ni mateso? Nimewahi kushuhudia vifo mbalimbali mfano wakati nikiwa mdogo yupo kijana mmoja kwanza aliumwa sana (nadhani ilikuwa ni UKIMWI) siku ya kufa Nakumbuka kuanzia saa moja usiku ilikuwa ni mwendo mara nishushe kutoka kitandani, mara nipeleke nje, mara niletee kitu fulani! Huyu jamaa alisumbua sana hadi inafika saa saba usiku ndipo anakata roho na wakati wote huo tulikuwa naye bize akitushughulisha hili na lile. Nakumbuka pia wakati akikata roho alijirusha rusha sana na kunyoosha shingo. Midomo nayo kuachana, macho kufunguka kupita kipimo n.k... Lakini historia ya huyu mtu haikuwa mbaya na hata huo ugonjwa nadhani aliupatia gerezani ambapo alikuwa akipelekwa mara kwa mara kutokana na akili zake kutokuwa sawa (ni kama alikuwa anapelekwa kule kupumzishwa tu) maisha yake yote hakuwahi kuwa na akili timamu.
Mwingine nilishuhudia wakati akifa alishuka kutoka kitandani na akainama palepale akafa (alibaki hivyohivyo akiwa ameinama)
Aidha yupo niliyeshuhudia huyu ilikuwa ni kimyakimya tu hakuna sauti wala mguno. Alikuwa amekaa kwenye kiti akipiga story ghafla akakata palepale bila bughudha yoyote!
Mwingine (huyu alikuwa bibi mmoja) Yeye wakati anakata roho alitumia takriban masaa kumi na moja akitaja jina la Mungu (alikuwa akisema nani kama Mungu? Kwa hayo masaa hadi anakata roho!
Sasa nasikia wapo wengine hutoa choo... Na yupo mzee mmoja aliwahi kuniambia kuwa wengi hasa wanaume hutoa mpaka manii wakati wakikata roho (hii nini maana yake? Inasababishwa na nini? )
Hapa nadhani kina mshana jr na wengine wanaweza kunisaidia na pengine wanaweza kunipa mtazamo tofauti!
Kuna watu wakati wa kufa ni anakumbana na aina fulani sijui tuseme ni mateso? Nimewahi kushuhudia vifo mbalimbali mfano wakati nikiwa mdogo yupo kijana mmoja kwanza aliumwa sana (nadhani ilikuwa ni UKIMWI) siku ya kufa Nakumbuka kuanzia saa moja usiku ilikuwa ni mwendo mara nishushe kutoka kitandani, mara nipeleke nje, mara niletee kitu fulani! Huyu jamaa alisumbua sana hadi inafika saa saba usiku ndipo anakata roho na wakati wote huo tulikuwa naye bize akitushughulisha hili na lile. Nakumbuka pia wakati akikata roho alijirusha rusha sana na kunyoosha shingo. Midomo nayo kuachana, macho kufunguka kupita kipimo n.k... Lakini historia ya huyu mtu haikuwa mbaya na hata huo ugonjwa nadhani aliupatia gerezani ambapo alikuwa akipelekwa mara kwa mara kutokana na akili zake kutokuwa sawa (ni kama alikuwa anapelekwa kule kupumzishwa tu) maisha yake yote hakuwahi kuwa na akili timamu.
Mwingine nilishuhudia wakati akifa alishuka kutoka kitandani na akainama palepale akafa (alibaki hivyohivyo akiwa ameinama)
Aidha yupo niliyeshuhudia huyu ilikuwa ni kimyakimya tu hakuna sauti wala mguno. Alikuwa amekaa kwenye kiti akipiga story ghafla akakata palepale bila bughudha yoyote!
Mwingine (huyu alikuwa bibi mmoja) Yeye wakati anakata roho alitumia takriban masaa kumi na moja akitaja jina la Mungu (alikuwa akisema nani kama Mungu? Kwa hayo masaa hadi anakata roho!
Sasa nasikia wapo wengine hutoa choo... Na yupo mzee mmoja aliwahi kuniambia kuwa wengi hasa wanaume hutoa mpaka manii wakati wakikata roho (hii nini maana yake? Inasababishwa na nini? )
Hapa nadhani kina mshana jr na wengine wanaweza kunisaidia na pengine wanaweza kunipa mtazamo tofauti!