Aida Khenan: Kama sikususia Uchaguzi siwezi kususia matokeo, CHADEMA iliniteua nikashinde na siyo kushiriki Uchaguzi

mwanamwana

JF-Expert Member
Aug 1, 2011
1,075
4,111
Mimi sijahama CHADEMA na wala sitegemei kuhama, mimi ni Mbunge mteule kwa hiyo nitawatumikia Wananchi kwa imani ambayo waliniamini, labda chama changu kitakavyoamua kama itakuwa vinginevyo basi itafahamika.

"Niliahidi kutokusaliti chama changu na kwa maana hiyo siwezi kuwasaliti wananchi walionipa heshima, utaratibu unaoendelea kwa chama changu cha CHADEMA wanaweza kuendelea nao kwa sababu sheria inawaruhusu.

Lakini kwenye jimbo langu pamoja na wananchi wangu na viongozi, tumeona hakuna sababu ya mimi kugomea kuapishwa kwa sababu chama kiliniamini nigombee na naamini kiliniteua nikashinde na siyo kushiriki uchaguzi.

Ni vigumu sana kurudi kwa wananchi kuwaambia nasusia matokeo, kama sikususia uchaguzi siwezi kususia matokeo, lakini maeneo ambayo wanafikiri kuna dosari waendelee kufuata utaratibu wa kisheria na haki itatendeka.
 
Huyu nae ni wa kuhurumia tu! Ipo siku atakuja juta maana miaka 5 si mingi. Magu si mtu na hana rafiki bali anakutumia pale tu anapokuhitaji.

Awaulize Mbatia na Lipumba .

Aendelee na ubunge wake na afanye yote lakini kamwe asinyee kambi.
 
Huyu mama awe makini na kila neno lake, naona amekuwa nyota wa mchezo kila siku kuhojiwa!
 
Mbunge si muwakilishi wa wananchi tu.

Ni muwakilishi wa wananchi kwa tiketi ya chama.

Hivyo, leo CHADEMA kama chama wakiamua kususia bunge, na huyu Mbunge akang'ang'ania kwenda bungeni, na CHADEMA wakamvua uanachama, kisheria atakosa uwezo wa kuwakilisha hao wananchi wake.

Not that we follow the law so much in Tanzania.

Hivyo, amalize tofauti zake na wenzake wa CHADEMA ndani ya chama.
 
Kwa akili yako unajidanganya ulishinda? Wewe ulipewa kwa sababu kees aliharibu utashinda aje hukuwa na mawakala
 
Mama hamia CCM Kama unataka ubunge. CHADEMA hakiitaji mwakilishi. Unga juhudi mkono. Ili mkaendelee na vikao vya CCM dodoma badala ya bunge
Mlimteua wa nini kama hankutaka aingie bungeni?

Kwanza ubunge kapata kwa gharama na juhudi zake binafsi, kumbuka hakuna mgombea ubunge aliyesaidiwa pesa na makao makuu, wote waliambiwa wajitegemee katika kampeni.

Bunge limlinde dhidi ya udikteta na ubinafsi wa viongozi wa CHADEMA.

Kuna mahali CHADEMA waliweka hoja mufilisi kuwa ni mpenzi wa mbunge mmoja wa CCM, sasa kwani hilo ni kosa? Watu wa vyama tofauti hawaruhusiwi kuwa na mahusiano ya kimapenzi? Mbona Jesca Kishoa na Kafulila wana mahusiano au Zitto na yule mtoto wa kiongozi wa CCM ( Amina) ni wapenzi hadi kuzaa mtoto? Kwa nini iwe nongwa kwa mbunge huyo wa CHADEMA?
 
Mlimteua wa nini kama hankutaka aingie bungeni?

Kwanza ubunge kapata kwa gharama na juhudi zake binafsi, kumbuka hakuna mgombea ubunge aliyesaidiwa pesa na makao makuu, wote waliambiwa wajitegemee katika kampeni...
Wapinzani wametuchelewesha sana.maendeleo haya chama
 
Huyu nae ni wa kuhurumia tu! Ipo siku atakuja juta maana miaka 5 si mingi. Magu si mtu na hana rafiki bali anakutumia pale tu anapokuhitaji.

Awaulize Mbatia na Lipumba .

Aendelee na ubunge wake na afanye yote lakini kamwe asinyee kambi.
No, she's right. Aligombea ili ashinde, na ameshinda, kwanini akatae ushindi? Na ametoa ushauri mzuri kuwa chama kifuate utaratibu wa kudai haki katika yale maeneo yenye dosari. Zifunguliwe kesi za uchaguzi kwa kutumia ushahidi uliopo. Wakifungua kesi majimbo yote, na zikathibitishwa mahakamani, itasaidia pia kama uthibitisho wa dosari kwenye uchaguzi wa rais japo hauhojiwi mahakamani.
 
Huyu nae ni wa kuhurumia tu! Ipo siku atakuja juta maana miaka 5 si mingi. Magu si mtu na hana rafiki bali anakutumia pale tu anapokuhitaji.

Awaulize Mbatia na Lipumba .

Aendelee na ubunge wake na afanye yote lakini kamwe asinyee kambi.
Acha ujinga ww Kama ungekua ww ungekubali garama aloweka kwenye uchaguzi utazilipa ww wakati wengine hata wanakopa kwenye ma benk
 
No, she's right. Aligombea ili ashinde, na ameshinda, kwanini akatae ushindi? Na ametoa ushauri mzuri kuwa chama kifuate utaratibu wa kudai haki katika yale maeneo yenye dosari. Zifunguliwe kesi za uchaguzi kwa kutumia ushahidi uliopo. Wakifungua kesi majimbo yote, na zikathibitishwa mahakamani, itasaidia pia kama uthibitisho wa dosari kwenye uchaguzi wa rais japo hauhojiwi mahakamani.
Hizo ndio akili za maCCM.
Ngoja nikupe shule hapa.
Hakuna mgombea aliyegombea ili kushindwa. Hivyo hoja ya kugombea ili ushinde haina mantiki hapa.
Pili kama yeye aligombea na kushinda haina maana kuwa uchaguzi katika jimbo lake ulikuwa huru na haki.

Tatu, Mgombea ni mali ya chama, ni chama ndio kinakupa hiyo nafasi ya kugombea (kumbuka kuna wanachama wengi wa CHADEMA walitaka kupewa hiyo nafasi lakini wakanyimwa ili huyo mmoja apewe kugombea), sasa chama kimesema hakiyatambui matokeo ya uchaguzi, mgombea anapata wapi sababu ya kusema mimi nawasikiliza kwanza wananchi walionichagua na sio chama kilichonipitisha?

Kwa Tanzania hakuna mbunge wa wananchi, wapo wabunge wa vyama na wabunge wa kuteuliwa na rais.
 
Huyo mama sio mzima kichwani.
CHADEMA walishatoa msimamo kuwa hawayatambui matokeo yote ya uchaguzi uliopita, sasa huyo mama anapaswa kutulia kama anajua nini maana ya chama na yeye kuwa mwanachama wa hicho chama.

Asitafute kick za kipumbavu kwa blah blah za uongo na kweli kuwa anawasikiliza wananchi wake.

Kama hakubaliani na uamuzi wa CHADEMA ni vyema akajivua uanachama wa CHADEMA na kuhamia kule anakotaka kwenda.
 
Huyu nae ni wa kuhurumia tu! Ipo siku atakuja juta maana miaka 5 si mingi. Magu si mtu na hana rafiki bali anakutumia pale tu anapokuhitaji.

Awaulize Mbatia na Lipumba .

Aendelee na ubunge wake na afanye yote lakini kamwe asinyee kambi.
Kagombee na wewe uone ilivyovigumu kupata ubunge!! Wewe upoupo tuu mara uko na Lowassa kwa sasa upoupo tu kama popo!
 
Huyo mama sio mzima kichwani.
CHADEMA walishatoa msimamo kuwa hawayatambui matokeo yote ya uchaguzi uliopita, sasa huyo mama anapaswa kutulia kama anajua nini maana ya chama na yeye kuwa mwanachama wa hicho chama...
Yupo Dodoma anasubiri kuapa ili akawatumikie wananchi wa Nkasi.
 
Back
Top Bottom