Aida Khenan: Chama kimeniteua nikashinde sio kushiriki uchaguzi

Replica

JF-Expert Member
Aug 28, 2017
1,441
7,780
Leo mbunge pekee wa kuchaguliwa kupitia chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kupitia jimbo la Nkasi Kaskazini amefanya mahojiano na mwandishi wa idhaa ya Kiswahili ya DW, Deo Makomba na mazungumzo yao yalikuwa kama ifuatavyo.

MWANDISHI: Unajisikia vipi hasa kuwa mmoja wa wabunge walioweza kushinda katika moja ya chama cha upinzani?

AIDA KHENAN: Moja, ninajisikia furaha kuwa mbunge wa kuchaguliwa kwenye jimbo langu ambalo ni kwa mara ya kwanza kupata mbunge mwanamke lakini mbunge wa kwanza wa upinzani kwenye mkoa wetu wa Rukwa. Lakini ninajisikia vibaya pia kuwepo peke yangu ndani ya Bunge kwa sababu nilikuwa mbunge wa viti maalum, nilikuwa na wabunge waliokuwa wamenitangulia na wabunge wengine ambao niliendelea kujifunza kutoka kwao na nilitamani niendelee kujifunza kutoka kwao.

MWANDISHI (DW): Uchaguzi haukuwa huru na haki, upande wako umeuonaje?

AIDA KHENAN: Upande wa jimbo langu nimetangazwa, kwenye maeneo mengine imekuwa tofauti, kwa kuwa chama kimeamua kwenda mahakama, kiendelee na huo mchakato. Haki ilitendeka au kutotendeka hiyo tafsiri itaenda kutolewa na mahakama.
 
Sasa mnataka asemeje kuna ma mtu yana roho mbaya sana, anayeona kaibiwa aende mahakamani huko bhana, mama kafight sana mpaka katoboa na ndo walivyoelekezwa kwenye chama chao na ameshinda alafu aanze kuingilia mambo ya wengine. Yaan yeye atoe tathmin ya uchaguzi kwenye Jimbo la Mbowe au la Sugu duuh hii Kali aisee.
 
Mahakama niijuayo ama nyingine. Mimi binafsi nayaamini maneno yake kwa asilimia 25. Pekee mashaka makubwa ni kuwa ni mpango mahususi wa kuhalalisha haramu, ama kujaribu kuigiza haki ilikuwepo na ilifanyika. Hata ni kisikiliza vizuri lafudhi si mzawa wa eneo la ushindi.Kama nakosea wajuzi wa mambo msaada tafadhali.Kwani Tanzania imekuwa ya maigizo zaidi kuliko uhalisia.
 
Huyu ameshaunga mkono juhudi ni suala la muda tu.
Mtaani pagumu jamani, muacheni mama akapige pesa za bwelele bungeni.

Wengi wenu humu hamjui mshahara wa mbunge ni million 14 kwa mwezi nje ya posho za kusinzia kwenye kiti, mkopo wa shangingi na pesa ya mafuta kila mwezi.

Dr Slaa alipoteuliwa kugombea Urais na Chadema alijuwa wazi hawezi kutangazwa mshindi, hivyo aliwapa Chadema condition kwamba analiachia jimbo la karatu lakini adiposhinda awe analipwa mshahara wa kibunge kwenye nafasi yake ya ukatibu mkuu.

Je Chadema kama chama kimempa offer gani huyu mama asamehe ubunge ili aunge mkono msimamo wa chama?

Na mkae mkijuwa huyu mama anajuwa vyema maslahi ya mbunge hass wa jimbo kwa sababu bunge lililopita alikuwa mbunge wa viti maalum.

Tuache mihemko turudi kwenye reality, January si mbali watoto wanataka school fees, acheni jamani, humu hakuna wa kuisamehe millioni 14 kwa mwezi mara miaka mitano plus mafao ya mwisho wa ubunge.

Acheni utani.
 
Mtaani pagumu jamani, muacheni mama akapige pesa za bwelele bungeni.

Wengi wenu humu hamjui mshahara wa mbunge ni million 14 kwa mwezi nje ya posho za kusinzia kwenye kiti, mkopo wa shangingi na pesa ya mafuta kila mwezi.

Dr Slaa alipoteuliwa kugombea Urais na Chadema alijuwa wazi hawezi kutangazwa mshindi, hivyo aliwapa Chadema condition kwamba analiachia jimbo la karatu lakini adiposhinda awe analipwa mshahara wa kibunge kwenye nafasi yake ya ukatibu mkuu.

Je Chadema kama chama kimempa offer gani huyu mama asamehe ubunge ili aunge mkono msimamo wa chama?

Na mkae mkijuwa huyu mama anajuwa vyema maslahi ya mbunge hass wa jimbo kwa sababu bunge lililopita alikuwa mbunge wa viti maalum.

Tuache mihemko turudi kwenye reality, January si mbali watoto wanataka school fees, acheni jamani, humu hakuna wa kuisamehe millioni 14 kwa mwezi mara miaka mitano plus mafao ya mwisho wa ubunge.

Acheni utani.

Umenena vyema kabisa. Hajafikia level ya kuutaka ubunge ili kulinda interest zake za kibiashara. Huyu amepata ubunge ili kujikwamua kiuchumi
 
Huyu mbunge mama kichwani yuko vizuri na anajua sheria mtu huwezi ita mwizi hadi mahakama ithibitishe.Yeye hajaibiwa anayeona kaibiwa aende mahakamani .Na kajibu kisheria kabisa kuwa uchaguzi kama ulikuwa haki au siyo mahakama ndio itasema sio porojo za vijiweni za Chadema.Ana akili huyu mama
 
Back
Top Bottom