IKUNGURU IJIRU CHUKU
JF-Expert Member
- Feb 27, 2021
- 484
- 541
Karne ya 21 bado unaamini maendeleo ni imani pasipo kufanya kazi kwa bidii na maarifa na kuwa na nidhamu ya pesa na muda.
Aibu yako! Matokeo ya kutafasiri maendeleo kama imani utaishia kuchinja albino, kuchanjwa chale makalioni, kulala makaburini, kuvaa hirizi kiunoni, kujisaidia haja kubwa kwenye sufuria la kupikia wageni, kuzini na vikongwe, kulala chini ya kitanda na wakati una kitanda kizuri, kunywa mkojo wa mbwa kila unapopata kiu na wakati Mungu kakupa maji safi bure, kuwafanya watoto wako mazezeta na wakati wewe wazazi wako walikulea vizuri, kuzaa na vichaa na wakati una mke mzuri na kila aina ya uchafu kisa, eti upate utajiri.
Aibu yako! Acha kuchekesha wagonjwa, maendeleo hayaji kwa bahati nasibu, ingekuwa ni hivyo basi kila mtu angekuwa tajiri Tanzania.
Karne ya 21 bado watawala wetu mnaamini umaskini utaondoka kwa semina elekezi. Unajua haya nayo ni maajabu! Afisa wa serikali na usomi wako wote unasafiri kwa gari na dereva wa serikali kuwahi semina elekezi pale Dar katika hoteli ya kifahari kumsikiliza mtaalamu kutoka Marekali na Ulaya Magharibi akupe mbinu za kupambana na umaskini. Mtaalamu mwenyewe kaufahamu umaskini wetu kupitia vitabu.
Ajabu sana! Aliyesema ignorance doesn’t kill but it makes you sweat a lot hajakosea. Njia sahihi ya kupambana na umaskini ni kwa kumtumia expert wa umaskni mwenyewe ambaye ni maskini alisema Hernando de Soto mwandishi wa, “The Mistery of Capital.”
Aibu yako! Matokeo ya kutafasiri maendeleo kama imani utaishia kuchinja albino, kuchanjwa chale makalioni, kulala makaburini, kuvaa hirizi kiunoni, kujisaidia haja kubwa kwenye sufuria la kupikia wageni, kuzini na vikongwe, kulala chini ya kitanda na wakati una kitanda kizuri, kunywa mkojo wa mbwa kila unapopata kiu na wakati Mungu kakupa maji safi bure, kuwafanya watoto wako mazezeta na wakati wewe wazazi wako walikulea vizuri, kuzaa na vichaa na wakati una mke mzuri na kila aina ya uchafu kisa, eti upate utajiri.
Aibu yako! Acha kuchekesha wagonjwa, maendeleo hayaji kwa bahati nasibu, ingekuwa ni hivyo basi kila mtu angekuwa tajiri Tanzania.
Karne ya 21 bado watawala wetu mnaamini umaskini utaondoka kwa semina elekezi. Unajua haya nayo ni maajabu! Afisa wa serikali na usomi wako wote unasafiri kwa gari na dereva wa serikali kuwahi semina elekezi pale Dar katika hoteli ya kifahari kumsikiliza mtaalamu kutoka Marekali na Ulaya Magharibi akupe mbinu za kupambana na umaskini. Mtaalamu mwenyewe kaufahamu umaskini wetu kupitia vitabu.
Ajabu sana! Aliyesema ignorance doesn’t kill but it makes you sweat a lot hajakosea. Njia sahihi ya kupambana na umaskini ni kwa kumtumia expert wa umaskni mwenyewe ambaye ni maskini alisema Hernando de Soto mwandishi wa, “The Mistery of Capital.”