Aibu ya polisi na nchi: Kudai rushwa kwa wageni

Mkulima wa Kuku

JF-Expert Member
Jan 13, 2011
1,270
533
Leo asubuhi jamaa yangu alikuwa amekuja kuchukua gari yake akielekea Zimbabwe. Alipofika kwenye kituo kimoja km 20-30 hivi kabla hajafika Tunduma mpakani askari wa Tanzania wakamsimamisha na kumtuhumu kuwa yeye ni polisi amekuja kufanya upelelezi kwa nchi na kuwa hawatamuachia mpaka awape pesa. Akawa hakubaliani na jambo hilo akaonyesha vitambulisho vyake na pasport yake inayosema yeye ni Mchungaji lakini wakamng'ang'ania kwa saa moja mpaka akawapa 10,000/= ndipo walipomuachia.

Nimewasiliana naye akasema akifika Zimbabwe atafungua jalada ubalozi wa Tanzania kwa ajili ya jambo hilo.
Hii ni aibu kwa Mwema, Rais na nchi kwa ujumla kudai fedha ndogondogo za aibu.

Naomba kuwasilisha.
 
Mimi wala sijaona ajabu yoyote humo maana viongozi wetu ndio hupokea mamilioni ya fedha kwa jina letu kutoka kwa wageni na kuzitia ndani kifisadi, sasa unafikiria polisi tu wataacha tabia hiyo ilioshamiri kote nchini????????
 
ukiwa unasafiri mchana we jiandae na rushwa ndogo ndogo ... yaani uwe na sh 2000 nyingi kwani kukamatwa kwa visingizio ni suala la kawaida
 
Huyo jamaa kweli mgeni...angewapa 2,000/= inawatosha na mbona wangemwachia saa nyingi.next akija kama hataki usumbufu mwambie achenchi buku2 nyingi za kutoa njiani!
 
Hizi njaa nyingine hizi... yaani hao polisi wanahatarisha ajira zao kwa ajili ya buku kumi tu!
 
Mimi wala sijaona ajabu yoyote humo maana viongozi wetu ndio hupokea mamilioni ya fedha kwa jina letu kutoka kwa wageni na kuzitia ndani kifisadi, sasa unafikiria polisi tu wataacha tabia hiyo ilioshamiri kote nchini????????
hapo ndg yangu umenena! Badala kugombana na kusemea hao wakubwa wanaochukua madola ya rushwa mnaangalia hawa askari wetu wanaochukua elfu 2 ilhali wanafanya kazi kubwa inaonekana! Suppose wakigoma 2hrs si 2tachinjana na kubakana?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom