Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 233
Yule kamanda wa polisi mkereketwa Na 1 wa CCM, Suleman Kova, afanye weledi katika kazi yake kwa kuutangazia umma ile kamati yake ya kipolisi ya kuchunguza sakata la kutekwa na kupigwa kwa Dr Ulimboka imefikia hatua gani?
Iwapo aliona ni weledi kwake kuutangazia umma, tena kwa mbwembwe kubwa kwamba ameunda kamati ya kuchunguza sakata hilo, awe jasiri tena na mbwembwe kwa kutuambia amefikia hatua gani, amehoji watu wangapi nk nk.
Vidokezo vyangu vinaonyesha kamati hiyo haijamhoji hata mtu mmoja! Haijamhoji hata yule Dr Deo Michael aliyokuwa na Dr Ulimboka wakati yule Rama (aka Abeid) na mabaunsa wake walipomteka Ulimboka.
Jameni, tuseme kile cha kweli kabisa na cha haki, hii si aibu kubwa kabisa katika jeshi letu la polisi katika kukosa weledi katika kazi zake hasa kutetea haki na maisha ya watu?
Mtu pekee aliyehojiwa ni yule kichaa mmoja aliyedai 'kutubu' kwamba ndiye alihusika na baadaye yeye mwenyewe kukiri kwamba huwa ana tabia ya kusema hovyo.
Iwapo aliona ni weledi kwake kuutangazia umma, tena kwa mbwembwe kubwa kwamba ameunda kamati ya kuchunguza sakata hilo, awe jasiri tena na mbwembwe kwa kutuambia amefikia hatua gani, amehoji watu wangapi nk nk.
Vidokezo vyangu vinaonyesha kamati hiyo haijamhoji hata mtu mmoja! Haijamhoji hata yule Dr Deo Michael aliyokuwa na Dr Ulimboka wakati yule Rama (aka Abeid) na mabaunsa wake walipomteka Ulimboka.
Jameni, tuseme kile cha kweli kabisa na cha haki, hii si aibu kubwa kabisa katika jeshi letu la polisi katika kukosa weledi katika kazi zake hasa kutetea haki na maisha ya watu?
Mtu pekee aliyehojiwa ni yule kichaa mmoja aliyedai 'kutubu' kwamba ndiye alihusika na baadaye yeye mwenyewe kukiri kwamba huwa ana tabia ya kusema hovyo.