Aibu nyingine hiyoooo!

The Invincible

JF-Expert Member
May 6, 2006
6,003
3,269
Hivi kweli Tanzania haina mzalendo yeyote mwenye sifa za kuwa mshauri wa viwanda mpaka tupate kutoka Japan? Au ndio kuomba fedha kwa njia mbadala? Nasikia kichefuchefu kwa hii tabia ya ombaomba. Vichwa vyote vya hapa JF kwa mfano, pasingekosekana walau watano wenye sifa hiyo.

Hii habari hapa chini nimeitoa Tanzania Daima.

Tanzania yapata mshauri wa viwanda toka Japan

na Tamali Vullu


SERIKALI ya Japan imeipatia Tanzania mtaalam mshauri wa masuala ya viwanda, ili kusaidia kushauri kuhusiana na jitihada za kuongeza kazi ya kuanzisha na kuendeleza viwanda nchini.

Taarifa iliyotolewa na Ikulu jana, ilieleza kuwa mshauri huyo, Yoshiyasu Mizuno, aliwasili nchini mwanzoni mwa mwaka huu na leo atakutana na Rais Jakaya Kikwete kwa mazungumzo na kupeana mikakati ya jinsi ya kuendeleza viwanda nchini.

Mizuno ambaye alianza kazi Februari 4, mwaka huu, atakuwa nchini kwa makubaliano ya miaka miwili.

Taarifa hiyo kwa vyombo vya habari inaeleza kuwa, tangu kuwasili nchini, Mizuno amekuwa akifanya kazi chini ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Masoko, lakini mipango ya kudumu ni kwa mtaalamu huyo kufanya kazi katika Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, ambayo imeanzishwa upya, baada ya mabadiliko ya hivi karibuni ya muundo wa serikali.

“Mizuno amekuja nchini kutokana na maombi yaliyotolewa na Mheshimiwa Rais Jakaya Kikwete kwa Serikali ya Japan wakati alipotembelea nchi hiyo mwishoni mwa 2006.

“Rais alitoa ombi hilo kwa kutilia maanani uzoefu mkubwa wa Japan katika maendeleo ya viwanda, na alitaka mtaalam mshauri huyo kuja kusaidiana na wataalam wa ndani katika kuboresha eneo la maendeleo ya viwanda,” ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.

Jukumu la msingi la mtaalamu huyo ni kuishauri serikali kitaalam katika kuendeleza viwanda nchini kulingana na malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo.

Taarifa hiyo inaeleza ushauri huo unalenga kuiwezesha sekta ya viwanda kukua na kuwa chachu ya maendeleo, na kuwa miongoni mwa sekta zinazochangia kwa kiasi kikubwa katika kukuza uchumi na kuondoa umasikini.

Mtaalam mshauri huyo anatarajiwa pia kutoa ushauri wa jinsi nchi nyingine zilivyoweza kutumia sekta ya viwanda kama moja ya mihimili ya kukuza uchumi.

Pia serikali inatagemea kuwa mtaalam mshauri huyo atachangia katika maandalizi ya mkakati unganishi na mpango madhubuti ambao utabainisha maeneo ya kipaumbele katika sekta ya viwanda yatakayoleta matokeo ya haraka katika muda mfupi, wa kati na ya muda mrefu.

Aidha, mtaalamu huyo anatarajia pia kusaidia katika mikakati ya kuendeleza maeneo maalum ya uzalishaji wa bidhaa za kuuzwa nje, yaani Export Processing Zones (EPZ).

Mkakati huo pia utasaidia katika kuibua miradi katika maeneo mbalimbali ya kipaumbele, hususan viwanda vya mbolea kwa maendeleo ya kilimo na maeneo maalum ya viwanda na biashara.

Source:http://www.freemedia.co.tz/daima/2008/3/5/habari7.php
 
Hata mimi nilikuwa najiuliza , hivi hatuwezi kuona importance ya kuwekeza kwenye viwanda mpaka Mjapan atueleze.
Nyerere alivyo wekeza kwenye Viwanda alipata ushauri wa Wajapan?
Vitu vingine ni kutumia tu akili zetu za kuzaliwa, sema baada ya kuanzisha then unaweza kuomba msaada wa kuongeza tija na mbinu zingine za biashara.
 
Lawama lazima zielekezwe panapostahili. Hapa wa kulaumiwa ni Kinara wetu ambaye alikwenda Japan kuomba wataalamu na Norway vile vile. Yeye anaamini kabisa kuwa Tanzania hatuna wataalamu. Sasa huyu atalipwa na serikali ya Japan au tutamlipa sisi kwa mshahara wa TX?
 
Afadhali wangemleta mshauri kutoka Vietnam ambao kimsingi wanategemea sana uzalishaji mdogo mdogo na tunaweza kujifunza kutoka kwao. Tatizo la mshauri kutoka Japan inaweza kuwa sawa na Mzee Small kumnong'oneza sikioni ngongoti.
 
SERIKALI ya Japan imeipatia Tanzania mtaalam mshauri wa masuala ya viwanda, ili kusaidia kushauri kuhusiana na jitihada za kuongeza kazi ya kuanzisha na kuendeleza viwanda nchini.

Serikali imeipatia?sio kwamba serikali iliiomba kupatiwa Mtaalam.M,ie sioni ubaya kama Serikali ikipatiwa Mtaalam ili aweze kusaidia maendeo ya Viwanda.Tumekuwa na viwanda miaka wa kadha ila vimeshindwa kustahimili soko hivy ni bora kujifunza kutoka kuliko bora.

Tuache kuoinga kila kitu na kuna mambo mengine ni mema kwa ajaili ya Maendeleo.
 
Serikali imeipatia?sio kwamba serikali iliiomba kupatiwa Mtaalam.M,ie sioni ubaya kama Serikali ikipatiwa Mtaala ili aweze kusaidia maendeo ya Viwanda.Tumekuwa na viwanda miaka wa kadha ila vimeshindwa kustahimili soko hivy ni bora kujifunza kutoka kuliko bora.

Tuache kuoinga kila kitu na kuna mambo mengine ni mema kwa ajaili ya Maendeleo.


gembe unapatiwa kitu ukiwa unakihitaji na ukipatiwa ukiwa hukihitaji unasema asante sana .Bado wanaweza kusema asante na kuwaeleza kwamba wataalam wa kilimo tunao .Hizo ni kujaza job creation ambazo Serikali ya Japan iliwaahidi wananchi wake sisi tunachekelea msaada kumbe kaja kuziba nafasi za wataalam wetu hapa nyumbani.
 
Serikali imeipatia?sio kwamba serikali iliiomba kupatiwa Mtaalam.M,ie sioni ubaya kama Serikali ikipatiwa Mtaalam ili aweze kusaidia maendeo ya Viwanda.Tumekuwa na viwanda miaka wa kadha ila vimeshindwa kustahimili soko hivy ni bora kujifunza kutoka kuliko bora.

Tuache kuoinga kila kitu na kuna mambo mengine ni mema kwa ajaili ya Maendeleo.

Gembe soma habari yote uelewe. Tabia ya ombaomba hii ilaaniwe. Wataalamu wa kizalendo wapo wa kufanya hiyo shughuli. JK aliahidi ajira milioni kwa mwaka.
 
Gembe soma habari yote uelewe. Tabia ya ombaomba hii ilaaniwe. Wataalamu wa kizalendo wapo wa kufanya hiyo shughuli. JK aliahidi ajira milioni kwa mwaka.
Je hao wataal unawafahamu?kama wapo mbona viwanda vimekufa?
 
..hili siyo jambo la ajabu hata kidogo. ukisaidiwa utaalamu basi umepewa ndoana na ujuzi wa kuvua, ukisaidiwa fedha umepewa samaki.

..kukabiliana na uhaba wa waalimu wa sekondari, nashauri serikali iagize waalimu wa sayansi na hisabati toka india.
 
Je hao wataal unawafahamu?kama wapo mbona viwanda vimekufa?

Viwanda vimekufa Tanzania si kwa sababu ya kukosa wataalamu. Tatizo kubwa ni wanasiasa wanaoingilia maamuzi ya kitaalamu. Kukiwa na nidhamu na uwajibikaji wa wanasiasa, wataalamu wetu wanaweza kufanya wonders.

Kuwafahamu wataalamu? JK angetangaza hiyo nafasi halafu tuone kama hakuna m-bongo hata mmoja mwenye sifa.
 
..hili siyo jambo la ajabu hata kidogo. ukisaidiwa utaalamu basi umepewa ndoana na ujuzi wa kuvua, ukisaidiwa fedha umepewa samaki.

..kukabiliana na uhaba wa waalimu wa sekondari, nashauri serikali iagize waalimu wa sayansi na hisabati toka india.

Ur right in many ways.....
 
Mheshimiwa mbunge wa Monduli bwana Lowasa alikwenda Asia kutafuta wataalam wa kutengeneza mvua! na sijui hio deal imefikia wapi.

Sasa anakuja mtaalam wa viwanda!

Je, anakuja kuelimisha namna ya kusimamia viwanda visife na vitoe bidhaa bora zitazouzika nje au anakuja kuelekeza namna ya kujenga viwanda vipya vya kisasa na vya kuzalosha bidhaa zipi?

Haya yote tutayajua baadae.

Siasa za kudanganyana hazina nafasi katika dunia ya leo. Mbona wataalamu wa kitanzania hawapelekwi kufunza watu wa nchi zilizoendelea na wala haitangazwi?

Lakini tuna wataalam na wahadhiri mbalimbali katika nchi zilizoendelea kama Marekani na Uingereza tena wanafundisha vyuo maarufu tu!

Ni lazima tujiulize ni kwanini waliondoka na kwanini tunalwtewa mtaalamu ambae anakuja kulipwa fwedha zetu za kigeni ambazo zingesadia akaunti hio.

Ni lazima kuna jambo kuhusu ujio wa mtu huyu nalo ni kuzidi kupata hasara katika fesha za kigeni maana mtu huyu ni lazima alipwe dola kama si Yen.
 
Kwa kutekeleza uzalendo wangu na mimi nimetafuta mtaalam huku anieleze Tanzania tutaendelea vipi???

Mtaalam anasema:::::

Matatizo Tanzania ni mengi sana, ila kwa kuanzia ni lazima efforts ziwekwe sehemu ambayo itagusa asilimia kubwa ya watu na kuform base ya uchumi.

Kwa kuwa asilimia 80 ya watanzania inategemea kilimo duni, simple solution ni::::

1)Kuuza VX zote za serikali ~~ 1000 VXs na kuagiza Matractor na kuyauza kwa mikopo kwenye wilaya zote

2) Kusimamisha semina na safari zote za wafanyakazi wa serikali kwa miaka miwili na kutumia pesa hizo kuagiza mbegu bora na mbolea na kuuza kwa mkopo kwa wakulima wilayani kote nchini.


ahaaha hamna cha mtaalam wala nini ni kutumia common sense tu.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom