Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 116,476
- 215,319
Mh Ally Kipendaroho ni miongoni mwa Wenyeviti wa serikali za mitaa waliopita bila kupingwa , kwenye uchaguzi uliosimamiwa kikamilifu na aliyekuwa Waziri wa Tamisemi Mtukufu Jaffo mwaka 2019 kutokea kijiji cha Torori , kata ya Chang'ombe , Wilayani Temeke.
Ni siku kadhaa sasa zimepita kwa Kipendaroho kuwa selo ya Polisi Chang'ombe kwa TUHUMA ZA KUVUNJA MAGODOWN , Upelelezi juu ya jambo hili ungali unaendelea.
Kijiji cha Torori ni miongoni mwa vijiji vichache sana vilivyobarikiwa kuwa na uwekezaji mkubwa wa viwanda , hivyo kuwa na Maghala mengi ya kuhifadhia bidhaa, huku kikizungukwa na familia nyingi duni zinazozalisha vijana wengi vibaka , wezi na walevi kupindukia.