Aibu kubwa! Msomi unakosaje kazi ya kufanya nchi hii yenye kila aina ya rasilimali?

Waje Mang'ura hapa Tuwafundishe kazi.... Vijana tunalima mpunga kama hatuna akili nzuri.
Tatizo hao waliomaliza digiriii wako sharo sana dah.. Acha waishi kwa mashemeji tu
 
Kuhusu masoko huo nao ni uvivu kwa sababu kuna zaidi ya Watanzania million 23 kwenye mtandao wa intaneti

Je mnatumia mtandao kutafutia wanawake na kuchat tu?
 
Anabwabwaja anafikiri Kilimo ni KAZI rahisi.Kilimo cha kisasa kinahitaji mtaji,ujuzi na maarifa, Elimu ya ugani nk.Anasema wazee wetu walitusomesha kwa Kilimo chenye tija ipo,unalima heka moja unapata junia kumi za mahindi badala ya junia zaidi ya hamsini.
Kama kilimo kingekuwa kinalipa,basi mikoa ya Kanda ya ziwa,nyanda za juu kusini ingeongoza kwa kipato kimkoa na mchango kwenye pato la Taifa,lakini unajua mkoa unaoongoza?ni Dar es salaam,mkoa ambao hauna shughuri kubwa za kilimo lakini unachangia asilimia 80 ya pato la Taifa!!
Kwa kila shilingi 100 inayoingizwa kwenye mfuko wa Taifa,asilimia 80 inatoka Dar!!hiyo mikoa inayolima ipo wapi??
Hoja zako kwamba vijana wakiomaliza vyuo waende mikoani,wakamate ardhi(ambayo ipo bwelele)walime,zimekaa kinadhalia tu na ni story za kwenye makaratasi hazina uhusiano na Hari halisi iliyopo kwenye mazingira yao.
Huwezi kutoka hapa ukaenda Katavi,ukachukua ardhi,ukaanza kulima mahindi,ukavuna!na ukapiga pesa ndeefu!?
Mfuko wa mbolea unauzwa 100000Tsh,gunia la mahindi linauzwa 20000Tsh!
 
Umuhimu wa kusoma ni kuongeza maarifa ili utatue changamoto za maisha.
kama umesoma ili upate kazi na bado una changamoto ya uchumi basi jua hauna akili na kweli hakuna umuhimu wa kusoma.
Baeleze mazee, maana kuna watu wanatoa maoni kana kwamba kusoma =kazi.
 
Hii ndio shida, mfumo wa elimu na mfumo wa ajira havina mawasliano

Unampeleka mtoto kukaa darasani miaka 17 halafu akitoka huko hamna kazi.... anaishia kuja kumwomba msaada yule ambae hakukaa darasani kabisaaa na kuanza kujifunza kwake kulima na kufuga🙄🙄
Upuuzi mtupu huu yani inakatisha tamaa
 
Anabwabwaja anafikiri Kilimo ni KAZI rahisi.Kilimo cha kisasa kinahitaji mtaji,ujuzi na maarifa, Elimu ya ugani nk.Anasema wazee wetu walitusomesha kwa Kilimo chenye tija ipo,unalima heka moja unapata junia kumi za mahindi badala ya junia zaidi ya hamsini.
Wasomi hamtaki kilimo. Kuweni wakweli msijifiche kwenye changamoto. Kuthihitisha hilo ndiyo maana hata wahitimu wa SUA hatuwaoni mashambani wako kwa masheji zao wanafua boksa wakisubiria kazi.

Kusema kwamba hukufundishwa kilimo ndiyo maana hulimi ni uwongo wa shetani kabisa. Kuna wahitimu wanafanya umachinga, bodaboda, na udalali. Nani aliwafundisha?
 
Ukiwa na nia inawezekana kabisa. Omba fedha toka kwa hao wanaokulisha na kukuvisha miaka yote hii ambayo unasubiria qjira.

Ama uza hicho kifaa kinachokuwezesha kuingia humu jf. Pia save hiyo hela ya bando utapata mtaji wa kilimo. Kilimo hwkihitaji mtaji mkubwa ndiyo maana hata bibi ywngu ni mkulima
Wewe jamaa nilifikiria una akili kumbe choko tu! Hivi nani ambaye ana hela za kukupa ukajaribu kilimo? Huyo mwenyewe aliekusomesha ameunga unga mpaka ukamaliza chuo nae amepata ahueni apumue sasa!

We unafikiri ukiuza smartphone kwa laki 2 tu hio laki 2 utakodi eneo na kununua dawa na petrol ya kumwagilia kwa kipindi chote hicho? Maana mazao ya muda mfupi ni miezi 3-5! Shamba heka nzima utasafishia bila vibarua!

Unaropoka kama vile hujawahi kulima kabisa mwehu wewe! Kilimo ni pesa! Kulima maharage tu acre 2 i wasted almost 2.5M na hio ni kwa uangalizi wa karibu na still nilipigwa usinga nikatoa gunia 8 instead ya 15 ambazo nili expect! Uzito nilipata kama 1.1 tonnes

Bei ya soko niliisubiria ikafika pazuri nikauza harage nikapiga 3.3M faida kama 800K ila haikuwa rahisi! By the time nilikua na kipato cha uhakika yani ila kwa hali ya sasa siwezi thubutu maana shamba litanishinda kuhudumia.
 
We unafikiri ukiuza smartphone kwa laki 2 tu hio laki 2 utakodi eneo na kununua dawa na petrol ya kumwagilia kwa kipindi chote hicho? Maana mazao ya muda mfupi ni miezi 3-5! Shamba heka nzima utasafishia bila vibarua!

Unaropoka kama vile hujawahi kulima kabisa mwehu wewe! Kilimo ni pesa! Kulima maharage tu acre 2 i wasted almost 2.5m na hio ni kwa uangalizi wa karibu na still nilipigwa usinga nikatoa gunia 8 instead ya 15 ambazo nili expect!
Mwanzo mgumu mkuu mkuu. Unapoanza tumia nguvu zako zaidi kama mtaji namba moja, lima, palilia na kuvuna mwenyewe. Wewe ulitumia hela nyingi kwasabb ulilima kwa remote (maagizo).

Pambana mwenyewe kwa miaka miwili upate mtaji wako halafu kidogo kidogo anza kujiondoa kwenye ushiriki wako wa moja kwa moja
 
Mwanzo mgumu mkuu mkuu. Unapoanza tumia nguvu zako zaidi kama mtaji namba moja, lima, palilia na kuvuna mwenyewe. Wewe ulitumia hela nyingi kwasabb ulilima kwa remote (maagizo).

Pambana mwenyewe kwa miaka miwili upate mtaji wako halafu kidogo kidogo anza kujiondoa kwenye ushiriki wako wa moja kwa moja
Nilienda mwenyewe daily, Kama ushapasikia mahali panaitwa Kahe!

Kilimo cha kimaskini huwezi pata mavuno ya maana nakwambia! Utalima heka nzima upate gunia 4! Mbaya zaidi uwe umelima mahindi yani 😂 gunia elfu 20 times 4 ni 80K huku gharama umetumia laki 4!
 
Hivi wewe ambaye unajiita umesoma halafu inalalamika kuwa huna kazi, unafahamu kwamba unajidhalilisha?

Acha wakose kazi vijana wa Ulaya na Marekani huko lkn siyo hapa Tanzania. Ardhi yenye rutuba isiyohitaji mbolea imejaa tele kwann usijiajiri kwenye kilimo?

Ardhi ya bure ipo tele katika mikoa ya Tabora, Katavi, Tanga, Ruvuma, n.k.

Kwani lazima ukae mjini? Mbona watanzania zaidi ya 80% wamejiajiri ktk kilimo tena wengi wao hawana madigrii kama ninyi lkn maisha yanasonga na ni watulivu wala hawapigi kelel za kukosa ajira.

Wengi wenu mmesomeshwa na wazazi wenu ambao ni wakulima wasiokuwa na elimu. Hawajawahi kuajiriwa na yeyote maisha yao yote.

Mmerogwa na nani ninyi mnaoenda shule? Kama hizi shule na vyuo mnavyoenda ndiyo vinawapeni huu ujinga mm nashauri zifutwe.

Kuna vijana chungu nzima walioishia darasa la saba wanaendeleza maisha kwa kilimo na shughuli nyingine hatusikii wakililia ajira. Wewe msomi umesoma halafu unalia. Usingesoma je? Jinga kabisa!

View attachment 1974112
Kwani we mwenzetu umesoma mpaka wapi? Maana hapa sioni kitu chochote cha msaada kwa hao vijana.Vipi huu ni mchambo ama ni kitu gani? Kingine hiyo ardhi unayosema ni kuwa inatolewa bure au vipi? Kama inatolewa bure unaweza wasaidia wapi inapatikana wakalime au kwa sababu we umezaliwa ukakuta mababu zako wana mashamba ukahisi kila mtu anayo hiyo fursa.

Kingine kuna tatizo gani mtu kuishi mjini? kama ndio kwao unataka aende wapi sasa.Mwisho kabisa achana na maneno ya kisiasa hayana msaada kwa vijana hao unaowasimanga.Unasema sijui asilimia kadhaa inafanya kilimo,Je hicho kilimo chenu kimekufikisheni wapi kama taifa?Kwahiyo unataka mtu apate mafunzo ya minimun 14 years then awe exposed kwenye hicho kilimo cha jembe na nyundo?Yes,they need to engage in production but not these stupid things done in your country.
 
Wasomi hamtaki kilimo. Kuweni wakweli msijifiche kwenye changamoto. Kuthihitisha hilo ndiyo maana hata wahitimu wa SUA hatuwaoni mashambani wako kwa masheji zao wanafua boksa wakisubiria kazi.

Kusema kwamba hukufundishwa kilimo ndiyo maana hulimi ni uwongo wa shetani kabisa. Kuna wahitimu wanafanya umachinga, bodaboda, na udalali. Nani aliwafundisha?
Acre kukodi ni 150K mpaka 200K kulingana na location yake na umbali toka mtoni.

Kilimo cha sasa hulimi na mkono! Trekta kukusafishia ni 50K-80K per acre!

Madawa nayo yanaweza kutafuna almost 150K kwa wastani pamoja na vifaa vya kukodi vile kwa msimu mzima!

Petrol pump na mpira lazma ukodishe.

Kupanda lazma ulipe watu.

Kipindi cha palizi lazma ulipe watu.

Kuvuna lazma ulipe watu.

Hizo zote ni gharama hamna power ilanda au hawafu mwenye nguvu wa kulima heka 1 au 2 peke yako! Hela lazma itumike ili ulime kwa ufasaha!

Hapo sijagusa gharama za usafiri kufata madawa, wewe kusavaivu shamba lazma ule na unywe maji ikibidi uende hospitalini.

Nani wakukupa hizo hela atleast 3M unaweza lima kitu cha maana kidogo!
 
Mwaka 2007 kuna kitabu nilisoma na nikaambiwa ili ufanikiwe unahitaji MTAJI, kitabu kikasema tena namna RAHISI KABISA ya kupata mtaji ni kwa kutumia ARDHI

Na nikaambiwa utajiri (maana ndiyo mnapenda kuita ndiyo mafanikio) unapatikana popote iwe ni mjini au kijijini

Mpaka leo bado nakubaliana na kitabu hiki na ni kweli kwa asilimia 100.
Everybody needs a little somethn for them to be independent! Nobody just grew up and became independent! ~ Tafakari za Genius Tupac Shakur atleast uta gain kitu mzee! Amna mtu alianza akatoboa tu bila support hakunaaa!!!


 
Back
Top Bottom