pascaldaudi
JF-Expert Member
- Mar 25, 2009
- 534
- 96
Dk Bilal asema kusomesha bure ni ndoto za mchana Send to a friend Thursday, 07 October 2010 08:12 0diggsdigg
Salim Mohamed na Raisa Said, Tanga
MGOMBEA mwenza wa urais kwa tiketi ya CCM, Dk Mohamed Bilal amewataka wananchi wa Mkoa wa Tanga kuwapuuza wapinzani kwa wanasema kwamba wakiingia madarakani wataoa huduma ya elimu na afya bure kwa kuwa mpango huo ni sawa na ndoto za mchana.
Dk Bilal aliyasema hayo jana katika mkutano wa kampeni wa chama chake uliofanyika katika uwanja wa Tangamano pamoja na mambo mengine alisema wananchi wa Tanga wakiwapeleka madarakani wataiboresha huduma ya usafiri wa Reli.
'Ndugu zangu wa Tanga kila siku nawasikia wapinzani wanakuja kwenu kuwaomba kura na kuwaahidi eti elimu na afya itakuwa bure hayo si ya kweli wameishiwa sera ndio maana kila siku wanasema hayo hayo," alisema Dk Bilal.
Dk Bilal alisema watajenga viwanda ili kuumarisha uchumi wa Taifa na kuwapa ajira vijana na bidhaa hizi zitasafirishwa kwenda nje ya nchi kupitia bandari ya Tanga na serikali itaongeza mapato yake na kutekeleza ahadi zake.
Alisema CCM imetekeleza ilani yake ya uchaguzi tangu uchaguzi wa kwanza wa mwaka 1995 na kuweza kufikia asilimia 98 na bado asilimia 2 tu ili iweze kufikia malengo yake na kuwataka wananchi wa mkoa huo kuwapa kura nyingi siku ya uchaguzi.
Alisema chama cha CCM kina uzoefu wa kuiongoza nchi na kudai kuwa ndio maana wanaomba tena wachaguliwe.
Source mwananchi (Dk Bilal asema kusomesha bure ni ndoto za mchana)
Salim Mohamed na Raisa Said, Tanga
MGOMBEA mwenza wa urais kwa tiketi ya CCM, Dk Mohamed Bilal amewataka wananchi wa Mkoa wa Tanga kuwapuuza wapinzani kwa wanasema kwamba wakiingia madarakani wataoa huduma ya elimu na afya bure kwa kuwa mpango huo ni sawa na ndoto za mchana.
Dk Bilal aliyasema hayo jana katika mkutano wa kampeni wa chama chake uliofanyika katika uwanja wa Tangamano pamoja na mambo mengine alisema wananchi wa Tanga wakiwapeleka madarakani wataiboresha huduma ya usafiri wa Reli.
'Ndugu zangu wa Tanga kila siku nawasikia wapinzani wanakuja kwenu kuwaomba kura na kuwaahidi eti elimu na afya itakuwa bure hayo si ya kweli wameishiwa sera ndio maana kila siku wanasema hayo hayo," alisema Dk Bilal.
Dk Bilal alisema watajenga viwanda ili kuumarisha uchumi wa Taifa na kuwapa ajira vijana na bidhaa hizi zitasafirishwa kwenda nje ya nchi kupitia bandari ya Tanga na serikali itaongeza mapato yake na kutekeleza ahadi zake.
Alisema CCM imetekeleza ilani yake ya uchaguzi tangu uchaguzi wa kwanza wa mwaka 1995 na kuweza kufikia asilimia 98 na bado asilimia 2 tu ili iweze kufikia malengo yake na kuwataka wananchi wa mkoa huo kuwapa kura nyingi siku ya uchaguzi.
Alisema chama cha CCM kina uzoefu wa kuiongoza nchi na kudai kuwa ndio maana wanaomba tena wachaguliwe.
Source mwananchi (Dk Bilal asema kusomesha bure ni ndoto za mchana)