Ahsanteni wakazi wa Dar es Salaam kwa kuupokea mradi wa Mabasi yaendayo Haraka (UDA-RT)

Lizaboni

JF-Expert Member
Feb 21, 2013
33,894
20,372
Wadau, amani iwe kwenu.

Hakika haikuwa lelemama kwa mradi wa Mabasi yaendayo Haraka kuanza kazi. Zipo changamoto za msingi ambazo zilijitokeza ambazo kwa hakika zilihitaji ufumbuzi wa lazima. Moja ya changamoto hizo ni suala zima la gharama za nauli ambapo awali nauli iliyokuwa imetangazwa haikuwa rafiki kwa wana Dar es Salaam. Nimpongeze Waziri Mkuu kwa kulisimamia hilo na kwa hakika wana Dar es Salaam wana kila sababu ya kumshukuru.

Pamoja na zile changamoto za msingi, mradi huo ulikuwa na figisu figisu nyingi huku vijana wa UKAWA wakijipanga kwa zamu kuhakikisha kuwa wanaweka mitandaoni kila aina ya uzushi wakilenga kuupinga mradi huo. Miongoni mwa uzushi huo ni pamoja na aina ya mabasi yaliyoagizwa kwamba hayana milango ya kutosha na milango yake haijakaa sawa kwa madai kuwa milango ipo juu mno. Kwamba mabasi hayo hayana ubora wowote na hayafai. Kwamba kuna harufu ya ufisadi kwenye mradi huo.

Wengine walikuja na hekaya kwamba mradi huo ni mali binafsi ya familia ya Jakaya. Wengine wakaja na hekaye eti muda unaotumika kwa magari hayo hauendani na dhana kuwa ni mabasi yaendayo Haraka.

Muda sasa umepita na changamoto za msingi zimepatiwa ufumbuzi. Hata wale ndugu zangu waliokuwa wanaukebehi mradi huo wameacha kuanzisha mijadala ya kipuuzi. Kwa ujumla wameukubali na wanakubaliana na Mzee Mwinyi kuwa Mabasi hayo ni URODA.

Niwaombe sana ndugu zangu wa UKAWA ambao mnapinga kila kitu. Kwamba, wakati ndio huamua siku zote. Kelele zenu na majungu yenu huwa yanafika wakati yanashindwa kufanya kazi. Oneni sasa mnavyoumbuka. Mradi huooooo unafanya kazi na una manufaa makubwa kwa wana Dar es Salaam.

Lazima tuheshimiane.
 
hivi huyu lizaboni yupo, sijamsikia kipindi kirefu, nilihisi kaukwaa ukuu wa wilaya
 
Kazi ni kazi aisee. Ila Lizaboni utakua unaifurahia sana kazi yako. Unapepewa na kiyoyozi, Una internet access unaperuzi social networks ukiifanya kazi ya kuitetea CCM na Serikali pamoja na kuwaponda wapinzani wake. Uzuri wa Kazi ni kuipenda kazi yako. Well done mkuu
 
Kazi ni kazi aisee. Ila Lizaboni utakua unaifurahia sana kazi yako. Unapepewa na kiyoyozi, Una internet access unaperuzi social networks ukiifanya kazi ya kuitetea CCM na Serikali pamoja na kuwaponda wapinzani wake. Uzuri wa Kazi ni kuipenda kazi yako. Well done mkuu
Safi sana Mkuu. Unajua kuna wengine wanadharau sana kazi za watu. Hizo Buku saba wanazozidharau wao wanazitafuta. Hapa Kazi Tu
 
Kazi ni kazi aisee. Ila Lizaboni utakua unaifurahia sana kazi yako. Unapepewa na kiyoyozi, Una internet access unaperuzi social networks ukiifanya kazi ya kuitetea CCM na Serikali pamoja na kuwaponda wapinzani wake. Uzuri wa Kazi ni kuipenda kazi yako. Well done mkuu
Safi sana Mkuu. Unajua kuna wengine wanadharau sana kazi za watu. Hizo Buku saba wanazozidharau wao wanazitafuta. Hapa Kazi Tu
 
mako.jpg
 
Yaan dada lizaboni uko vizur.......leo hujaleta uzi wa kumuattack mtu personaly ...hongera sanaa...vip kagame uliyekuwa unampinga naona kapewa shavu na mfalme ,sijui una maoni gan....nasikia mheshimiwa sasa anaendesha nchi kwa kutumia mawazo yake......
 
watanzania tupende vya kwetu mradi ni mzuri wote tuwe mabalozi wema wa kuusimamia vizuri, serikali imejitahidi kuleta mradi huu watu wanafika sehemu wanayoenda kwa kutumia hayo mabasi, hongera serikali kwa mradi huu mzuri
 
watanzania tupende vya kwetu mradi ni mzuri wote tuwe mabalozi wema wa kuusimamia vizuri, serikali imejitahidi kuleta mradi huu watu wanafika sehemu wanayoenda kwa kutumia hayo mabasi, hongera serikali kwa mradi huu mzuri
Nakubaliana na wewe Mkuu. Hakika mradi ni mzuri na manufaa yake yanaonekana
 
watanzania tupende vya kwetu mradi ni mzuri wote tuwe mabalozi wema wa kuusimamia vizuri, serikali imejitahidi kuleta mradi huu watu wanafika sehemu
wanayoenda kwa kutumia hayo mabasi,
hongera serikali kwa mradi huu mzuri[/
QUOTE]


Chanzo cha watanzania kuuchukia huu mradi ni kutokana na kuwa na makandokando mengi na familia za viongozi fulani serikalini kujimilikisha hisa za mwananchi kinyemela ndii maana bado hatuna imani kabisa na wanufaika wa huu mradi.
 
Tumekusikia. Halafu Lizaboni ,kwanini huwa ni mzushi sana unapozungumzia mtu binafsi? Mfano,umezusha jana tu humu kumhusu Wilfred Lwakatare. Nani anakulinda humu na uzushi wako? Kwa maslahi ya nani?
Analindwa na kina Maxence Melo mkuu we huoni sisi wanachama wa kawaida ukianzisha uzi wowote ukimgusa fisiem yeyote unafutwa haraka sana lakini huyu jamaa yao chochote atakachokizusha inakua hewala mkusanya nauli. Jf ifike mahala iache double standards.

Najua mods wataifuta comment hii kama kawaida yao.

Adumu mkusanya nauli.
 
Back
Top Bottom