Invisible
Robot
- Feb 11, 2006
- 9,076
- 7,835
Ilikuwa ni safari ya kifo cha uhuru wa habari Tanzania lakini sasa uhuru umerejea. Ni ushindi wa wana JF (wasomaji na waliojisajili) wote.
Naomba kutoeleza chochote zaidi lakini nipeleke shukrani zangu za kipekee kwa wana habari wote: Magazeti ya HabariLeo, Mtanzania, ThisDay, Kulikoni, Tanzania Daima n.k. Pia blog mbalimbali ambazo nimezipitia ikiwa ni pamoja na KLH News, Michuzi, eThinkTank na wengine wengi. Ukweli ni kuwa bila ninyi kuliweka wazi suala hili basi tulikuwa kwenye wakati mgumu sana.
Aidha niwashukuru watu binafsi ikiwa ni pamoja na Mwanakijiji, Mhariri wa ThisDay, Zitto Kabwe, John Mnyika, Tundu Lissu, Wakili Armao, Mchumba wangu (namhakikishia ndoa ipo tu July), Mbaraka, W. Malecela, Andrew, Abdallah, na watanzania wote ambao kwa namna moja ama nyingine walihakikisha wanapiga simu kwa DCI Manumba na kwingineko kuhakikisha wanaweka wazi kazi inayofanywa na JF.
Mwisho nawashukuru wenzetu William Mushi na Yona Fares Maro kwa jitihada zao.
Wana JF, tulikubali kuwa na collective responsibility kwa ajili yenu tukiamini nanyi hamtotutupa katika hali hiyo. Tulilazimika kubeba kila aina ya lawama kwa ajili yenu. Vitisho kwetu vimeendelea kuongezeka na usalama wetu unazidi kuwa mdogo. Tuombeane uzima tu.
Niseme kuwa tukubaliane kwamba Tanzania ni yetu sote na watu wachache wanaotaka kuzimika kwa harakati za kuisafisha wasipewe nafasi. Pia wanachama hapa tuache kabisa kuandika habari zisizo na uthibitisho ama zenye dhamira ya kulichafua taifa ambazo chanzo chake kina utata ama hakuna kabisa. Zitapelekea wakati mwingine watu kama FD ama Mnyika nao kukamatwa. Huenda nao wakakubali wao kuwa Invisible.
Kisha nadhani kuna watu wana wasiwasi kuwa kuna kitakachofutwa, sijaona kilichofutwa zaidi ya kuona vilivyohamishwa. Hiyo inamaanisha kuwa kila kitu kipo kama kilivyokuwa. Shukrani kwa moderators.
Namshukuru Invisible kwa kuniruhusu kutumia nickname yake kuweza kuwasilisha maoni haya kwa sasa na kuomba ushirikiano naye pindi mambo kama haya yanapotokea.
Sina mengi ya kuandika zaidi ya kusema "Ahsante watanzania, pamoja tutafika mbali".
Nitaendelea kuwawekea nafasi za kazi kadiri ninavyozipata.
Mac
Naomba kutoeleza chochote zaidi lakini nipeleke shukrani zangu za kipekee kwa wana habari wote: Magazeti ya HabariLeo, Mtanzania, ThisDay, Kulikoni, Tanzania Daima n.k. Pia blog mbalimbali ambazo nimezipitia ikiwa ni pamoja na KLH News, Michuzi, eThinkTank na wengine wengi. Ukweli ni kuwa bila ninyi kuliweka wazi suala hili basi tulikuwa kwenye wakati mgumu sana.
Aidha niwashukuru watu binafsi ikiwa ni pamoja na Mwanakijiji, Mhariri wa ThisDay, Zitto Kabwe, John Mnyika, Tundu Lissu, Wakili Armao, Mchumba wangu (namhakikishia ndoa ipo tu July), Mbaraka, W. Malecela, Andrew, Abdallah, na watanzania wote ambao kwa namna moja ama nyingine walihakikisha wanapiga simu kwa DCI Manumba na kwingineko kuhakikisha wanaweka wazi kazi inayofanywa na JF.
Mwisho nawashukuru wenzetu William Mushi na Yona Fares Maro kwa jitihada zao.
Wana JF, tulikubali kuwa na collective responsibility kwa ajili yenu tukiamini nanyi hamtotutupa katika hali hiyo. Tulilazimika kubeba kila aina ya lawama kwa ajili yenu. Vitisho kwetu vimeendelea kuongezeka na usalama wetu unazidi kuwa mdogo. Tuombeane uzima tu.
Niseme kuwa tukubaliane kwamba Tanzania ni yetu sote na watu wachache wanaotaka kuzimika kwa harakati za kuisafisha wasipewe nafasi. Pia wanachama hapa tuache kabisa kuandika habari zisizo na uthibitisho ama zenye dhamira ya kulichafua taifa ambazo chanzo chake kina utata ama hakuna kabisa. Zitapelekea wakati mwingine watu kama FD ama Mnyika nao kukamatwa. Huenda nao wakakubali wao kuwa Invisible.
Kisha nadhani kuna watu wana wasiwasi kuwa kuna kitakachofutwa, sijaona kilichofutwa zaidi ya kuona vilivyohamishwa. Hiyo inamaanisha kuwa kila kitu kipo kama kilivyokuwa. Shukrani kwa moderators.
Namshukuru Invisible kwa kuniruhusu kutumia nickname yake kuweza kuwasilisha maoni haya kwa sasa na kuomba ushirikiano naye pindi mambo kama haya yanapotokea.
Sina mengi ya kuandika zaidi ya kusema "Ahsante watanzania, pamoja tutafika mbali".
Nitaendelea kuwawekea nafasi za kazi kadiri ninavyozipata.
Mac