Ahsante; Neno dogo lenye nguvu ya kuleta mabadiliko kiroho na kimwili

Da'Vinci

JF-Expert Member
Dec 1, 2016
35,675
106,781
THE POWER OF BEING THANKSFULL
downloads.jpg

Habarii..

Katika maisha yangu ya kila siku hua nayaweka mbele maneno haya matatu ambayo ni Pole, samahani na Ahsante. Leo nitazungumzia neno Ahsante, ni neno dogo lakini lililojaa Nguvu kubwa sana kiroho..upande wangu hajalishi nimepewa nini lazima nitoe shukrani kwa kile nilichofanyiwa na hua naona neno ahsante pekee halitoshi. Hata kama nimekula kwa mama ntilie lazima niseme ahsante tena nitoe na vyombo. Ifuatayo Ni mifano ya ukweli ya faida niliyopata kwa kupenda kutoa shukrani kwa kile nilichopatiwa au kukiona kikanifurahisha.

  • Kukutana na mwandishi wa vitabu Dar es Salaam
Mwanzoni mwa mwaka 2018 nilikutana na muuza viitabu mitaa ya makumbusho akiuza vitabu nikawa naangalia vitabu alivyonavyo, niliona kitabu kimoja cha ujasiliamali na Mottivation basi tu nikakipenda kilikua kinauzwa elfu 6000. Kwanguu ni hela kubwa mno ila nilijidhiki nikatoa senti yangu ya mwisho nikakinunua. Nilikisoma choooote ndani ya siku moja nilikipenda ujumbe wake pia kilikua na mahadhi ya kidini. Baada ya kukisoma nilichukua E-mail yake iliyokua kwenye kitabu nikamtumia ujumbe wa kumshukuru kwa elimu aliyoitoa, alifurahi sana akaniomba namba yangu nikampatia akanipigia..Alishangaa sana kusikia mtu aliyekua anaongea nae sio aliyemtegemea maana vijana wa kipindi hiki ni ngumu kujisomea vitabu tena atoe hela yake anunue kitabu ambacho sio cha ubuyu/mapenzi/hadithi nk. Tuliongea meengi mno akanikaribisha kanisani kwao mabibo. Akanipa access ya kupata vitabu buure kutoka kwa ma-agent wake popote pale nilipo Tanzania. Kumpatia tu taarifa kua niko mkoa upi yeye ananielekeza wapi niende.



  • Nilivyokutana na Mwalimu wa Lugha ya Kihispania
Nikiwa katika harakati ya kufahamu lugha ya kihispania nilikua natafuta tutorial video YouTube kasha nazipakua, katika tafuta yangu nilikutana na mwalimu mmoja anaitwa Dr.Danny Evans nikapenda anavyofundisha nikapakua video zake nyiiingi nikawa namfuata hatua kwa hatua. Hatimae nami nikaanza kuwa mzoefu wa kuandika na kuongea Spanishi. Nilipoona nimefika hatua ya kuridhisha nikatafuta E-mail yake nimtumie ujumbe bahati mbaya sikumpata nikatafutisha Google hadi nikapata account yake ya Facebook….tuliwasiliana akafurahi kuona nina passion ya kufahamu lugha mbalimbali, alinishauri vingii na kunipatia video nyiingi na vitabu niweze kufahamu zaidi lugha ya kihispaniola. Tulibadirishana namba tunawasiliana mpaka leo na ni rafiiki

Biblia inatuambia nini………….??????

Kwakutumia mifano na mafundisho ya kibiblia hebu tuangalie jinsi mtu mmoja alivyopata neema ya wokovu kwa kusema tu ahsante, alimshukuru Yesu baada ya kumtibu magonjwa aliyokua nayo

Luka 17:13-19

“………Alipokua aaingia katika kijiji kimoja, watu kumi wnye ukoma walikutana nae wakasimama kwa mbali, wakapaza sauti yao wakisema Yesu mwalimu tuonee huruma! Alipowaona akawambia nendeni mkajionyeshi kwa makuhani, basi ikawa walipokua wanakwenda wakatakasika na kupona ukoma wao, mmoja wao alirudi na akamtukuza Mungu kwa sauti kubwa. Akajitupa chini mbele ya miguu ya Yesu huku akimshukuru, huyo alikua msamaria. Hapo yesu akasema Je , si watu kumi walitakaswa? Wale tisa wako wapi? Hakupatikana mwingine aliyerudi kumtukuza Mungu? Kisha akamwambia huyo mtu Simama nenda zako imani yako imekuponya.”

Wakuu kama tulivyoona hapo kwenye andiko yaani kati ya watu 10 waliopokea uponyaji ni mmoja tu aliyerudi kumshukuru yesu na kusema ahsante, hii ni ajabu! Mtu umepokea uatakaso lakini unashindwa kushukuru kwa neema hiyo.

Hata katika maisha ya kawaida watu wanafanyiwa mema lakini wanasahau kutoa shukrani tena wanaweza hata kulipa mabaya badala ya shukrani, mfano unalala usiku mzima hujui kinachoendelea pembeni yako! Mungu anakulinda usiku mzima na kukufikisha asubuhi salama lakini ukiamka tu unaamka kama mbuzi cha kwanza unafungua simu kuchungulia JF na mitandao ya kijamii mingine unasahau hata kumwambia Ahsante Mungu kwa kuniamsha salama. Unajiikia vibaya ukimpatia mtu msaada hafu asikushukuru, si ndio? Bas hivyo mdivyo ilivyo hata kwa Mungu! Anfurhi kuona watoto wake wanamshukuru….Imagine ulikua hufahamu kitu Fulani unafungua JF unakuta hiko kitu/mada unaisoma unavutiwa nayo unashindwa kumshukuru kwa kukuelimisha lakini hata kama huto mshukuru mpongeze tu au like post yake itamfanya atabasamu.

Kama mlivyooa hapo juu ni neno la shukrani tu ndio lilimfanya mkoma Yule apate neemaya utakaso! Ngugu yangu mm nawewe ni nani mpaka tushindwe kusema neno ahsante??? Haigharimu kitu kusema ahsante… kwanini usimshukuru Mtu aliyekusaidia jambo,Mungu aliyekulinda siku nzima?

“Sema ahsante kwa Yule aliyekufanyia jambo linalokufurahisha usiposema atakata tama kufanya lile linalokufurahisha”

Imeandikwa na:-

~Da’Vinci

JF Expert Member
Tchao
 
THE POWER OF BEING THANKSFULL
View attachment 999162
Habarii..

Katika maisha yangu ya kila siku hua nayaweka mbele maneno haya matatu ambayo ni Pole, samahani na Ahsante. Leo nitazungumzia neno Ahsante, ni neno dogo lakini lililojaa Nguvu kubwa sana kiroho..upande wangu hajalishi nimepewa nini lazima nitoe shukrani kwa kile nilichofanyiwa na hua naona neno ahsante pekee halitoshi. Hata kama nimekula kwa mama ntilie lazima niseme ahsante tena nitoe na vyombo. Ifuatayo Ni mifano ya ukweli ya faida niliyopata kwa kupenda kutoa shukrani kwa kile nilichopatiwa au kukiona kikanifurahisha.

  • Kukutana na mwandishi wa vitabu Dar es Salaam
Mwanzoni mwa mwaka 2018 nilikutana na muuza viitabu mitaa ya makumbusho akiuza vitabu nikawa naangalia vitabu alivyonavyo, niliona kitabu kimoja cha ujasiliamali na Mottivation basi tu nikakipenda kilikua kinauzwa elfu 6000. Kwanguu ni hela kubwa mno ila nilijidhiki nikatoa senti yangu ya mwisho nikakinunua. Nilikisoma choooote ndani ya siku moja nilikipenda ujumbe wake pia kilikua na mahadhi ya kidini. Baada ya kukisoma nilichukua E-mail yake iliyokua kwenye kitabu nikamtumia ujumbe wa kumshukuru kwa elimu aliyoitoa, alifurahi sana akaniomba namba yangu nikampatia akanipigia..Alishangaa sana kusikia mtu aliyekua anaongea nae sio aliyemtegemea maana vijana wa kipindi hiki ni ngumu kujisomea vitabu tena atoe hela yake anunue kitabu ambacho sio cha ubuyu/mapenzi/hadithi nk. Tuliongea meengi mno akanikaribisha kanisani kwao mabibo. Akanipa access ya kupata vitabu buure kutoka kwa ma-agent wake popote pale nilipo Tanzania. Kumpatia tu taarifa kua niko mkoa upi yeye ananielekeza wapi niende.



  • Nilivyokutana na Mwalimu wa Lugha ya Kihispania
Nikiwa katika harakati ya kufahamu lugha ya kihispania nilikua natafuta tutorial video YouTube kasha nazipakua, katika tafuta yangu nilikutana na mwalimu mmoja anaitwa Dr.Danny Evans nikapenda anavyofundisha nikapakua video zake nyiiingi nikawa namfuata hatua kwa hatua. Hatimae nami nikaanza kuwa mzoefu wa kuandika na kuongea Spanishi. Nilipoona nimefika hatua ya kuridhisha nikatafuta E-mail yake nimtumie ujumbe bahati mbaya sikumpata nikatafutisha Google hadi nikapata account yake ya Facebook….tuliwasiliana akafurahi kuona nina passion ya kufahamu lugha mbalimbali, alinishauri vingii na kunipatia video nyiingi na vitabu niweze kufahamu zaidi lugha ya kihispaniola. Tulibadirishana namba tunawasiliana mpaka leo na ni rafiiki yangu.

Kwa upande wa mifano kutoka kwangu naoamba niishie hapa ila kushukuru kumenikutanisha pia na msanii mmoja toka south Africa anaitwa Sho madjozi, just napenda nyimbo yake moja aliyoimba kwa Kiswahili akafurahi.

Biblia inatuambia nini………….??????

Kwakutumia mifano na mafundisho ya kibiblia hebu tuangalie jinsi mtu mmoja alivyopata neema ya wokovu kwa kusema tu ahsante, alimshukuru Yesu baada ya kumtibu magonjwa aliyokua nayo

Luka 17:13-19

“………Alipokua aaingia katika kijiji kimoja, watu kumi wnye ukoma walikutana nae wakasimama kwa mbali, wakapaza sauti yao wakisema Yesu mwalimu tuonee huruma! Alipowaona akawambia nendeni mkajionyeshi kwa makuhani, basi ikawa walipokua wanakwenda wakatakasika na kupona ukoma wao, mmoja wao alirudi na akamtukuza Mungu kwa sauti kubwa. Akajitupa chini mbele ya miguu ya Yesu huku akimshukuru, huyo alikua msamaria. Hapo yesu akasema Je , si watu kumi walitakaswa? Wale tisa wako wapi? Hakupatikana mwingine aliyerudi kumtukuza Mungu? Kisha akamwambia huyo mtu Simama nenda zako imani yako imekuponya.”

Wakuu kama tulivyoona hapo kwenye andiko yaani kati ya watu 10 waliopokea uponyaji ni mmoja tu aliyerudi kumshukuru yesu na kusema ahsante, hii ni ajabu! Mtu umepokea uatakaso lakini unashindwa kushukuru kwa neema hiyo.

Hata katika maisha ya kawaida watu wanafanyiwa mema lakini wanasahau kutoa shukrani tena wanaweza hata kulipa mabaya badala ya shukrani, mfano unalala usiku mzima hujui kinachoendelea pembeni yako! Mungu anakulinda usiku mzima na kukufikisha asubuhi salama lakini ukiamka tu unaamka kama mbuzi cha kwanza unafungua simu kuchungulia JF na mitandao ya kijamii mingine unasahau hata kumwambia Ahsante Mungu kwa kuniamsha salama. Unajiikia vibaya ukimpatia mtu msaada hafu asikushukuru, si ndio? Bas hivyo mdivyo ilivyo hata kwa Mungu! Anfurhi kuona watoto wake wanamshukuru….Imagine ulikua hufahamu kitu Fulani unafungua JF unakuta hiko kitu/mada unaisoma unavutiwa nayo unashindwa kumshukuru kwa kukuelimisha lakini hata kama huto mshukuru mpongeze tu au like post yake itamfanya atabasamu.

Kama mlivyooa hapo juu ni neno la shukrani tu ndio lilimfanya mkoma Yule apate neemaya utakaso! Ngugu yangu mm nawewe ni nani mpaka tushindwe kusema neno ahsante??? Haigharimu kitu kusema ahsante… kwanini usimshukuru Mtu aliyekusaidia jambo,Mungu aliyekulinda siku nzima?

“Sema ahsante kwa Yule aliyekufanyia jambo linalokufurahisha usiposema atakata tama kufanya lile linalokufurahisha”

Imeandikwa na:-

~Da’Vinci

JF Expert Member
Tchao
Asante sana mkuu kwa ukumbusho huu! Mungu akubariki sana!
 
Back
Top Bottom