Ahsante Mungu kwa kunipa nafasi ya kuchangia damu ya ukombozi wa taifa langu!

Leo, moyo wangu umejaa furaha kubwa baada ya kuchangia tone la damu yangu katika bakuli la sadaka ya damu ya ukombozi wa taifa hili, likitanguliwa na ukombozi wa Arumeru mashariki!

Nikiwa katika mkakati wa tafuta kura, piga kura na linda kura-mkakati ambao umetuzalia matunda mema na kutoa ujumbe kwa taifa zima kile alichosema Dr. Lwaitama wa UDSM katika makala yake iliyobeba kichwa cha habari "CCM sells by date can not be extended" ilikuwa ni katika gazeti la The Citizen katika forum yake ya thinking critically! Nimejikuta nikishangilia matokeo hayo nikiwa katika chumba maalum cha kuhifadhia wahalifu maarufu kama sero kwa zaidi ya masaa 16 hivi mjini Arusha nikiwa na wenzangu 59 kwa pamoja tukifanya watu 60 baada ya afande mmoja kututangazia rasmi kuwa CDM imetangazwa mshindi Arumeru Mash, na kusababisha kelele za kushangilia zikisikika kutoka kila chumba cha mahabusu!

Ni baada ya kutimuliwa katika eneo la kutangazia kura nikipita uchochoro fulani hivi nikilenga kutokea leganga, mara nikajikuta niko katika geti la Gateway lodge, Mungu wangu wee sikujua kama CCM walikuwa wakiishi hapo tangu kampeni zianze na kikosi maalum kiitwacho green guard wakiwa wakitusubiri hapo mithiri ya simba mwenye njaa aonapo kitoweo pengine ni kutekeleza amri waliyopewa na wakuu wao huku wakiwa na mapanga, shoka, viboko, fimbo na silaha za kila aina niliona kama mafuta ya petrol (sina uhakika) maana hata hivyo haikutumika, walituteka nakutupiga mapanga na kila walichojisikia na kisha wakatusachi na kuchukua kila walichoona kinawafaa!

Baada ya kuridhika wakawapigia polisi wakaja kutuchukua! Mambo kadha wa kadha yalikuwa dhahiri katika tukio hilo

1. Polisi watakuwa wanawafahamu watu hao maana hawakuchukua hatua yoyote ya kutaka japo waondoke na mmojawao ili akatoe ushahidi/maelezo ya uhalifu tulioufanya pamoja na kwamba waliwakuta hapo! Hivyo napata nafasi ya kuhisi walifanya kazi kwa ushirika!

2.Wale watu walitumwa na CCM kulingana na kauli walizokuwa wakitoa kama, ninyi ndio mnajiita people people kitu gani, mmesoma shule za CCM halafu mnatuambia people hapa!

Shukurani
Napenda kutoa shukrani zangu za dhani kwa waheshimiwa viongozi wa CHADEMA kwa kutuhangaikia mpaka hivi sasa napata fursa ya kuandika thread hii nikiwa nyumbani baada ya kukandwa majeraha na kuwaona tena familia yangu ikiwa ni baada ya kushinda mauti yaliyotuvamia masaa takribani 18 yaliyopita. Tulimuona mhe. Mbowe usiku ule pale USA akihangaika na baadae tukahamishiwa mjini napo tumemuona Dr. Slaa na makamanda wengine waliofanikiwa sisi kupata dhamana!

Pia namshukuru Mungu mweza yote aliyenipa fursa hii ya kutoa mchango wa damu ya ukombozi huku akitunza nafasi ya uhai wetu ili kunipa nafasi tena ya kushuhudia. Uhimidiwe Mungu wangu!

Free at last! free at last! thank you God Almighty I am free at last!

Pole sana na kama shairi la Kiingereza la Amando Guebuza linavyosema:

Frontline where manhood and consciousness is tested;
The only place to declare names immortal;
Trust me brother my shoulder will be next to yours



I like it when it is bitter
because out of bitterness comes joy and victory

Mshairi mwingine niliyemsahau sehemu ya shairi lake lasema:

My blood yet more your blood shall irrigate our victory;
 
Leo, moyo wangu umejaa furaha kubwa baada ya kuchangia tone la damu yangu katika bakuli la sadaka ya damu ya ukombozi wa taifa hili, likitanguliwa na ukombozi wa Arumeru mashariki!

Nikiwa katika mkakati wa tafuta kura, piga kura na linda kura-mkakati ambao umetuzalia matunda mema na kutoa ujumbe kwa taifa zima kile alichosema Dr. Lwaitama wa UDSM katika makala yake iliyobeba kichwa cha habari "CCM sells by date can not be extended" ilikuwa ni katika gazeti la The Citizen katika forum yake ya thinking critically! Nimejikuta nikishangilia matokeo hayo nikiwa katika chumba maalum cha kuhifadhia wahalifu maarufu kama sero kwa zaidi ya masaa 16 hivi mjini Arusha nikiwa na wenzangu 59 kwa pamoja tukifanya watu 60 baada ya afande mmoja kututangazia rasmi kuwa CDM imetangazwa mshindi Arumeru Mash, na kusababisha kelele za kushangilia zikisikika kutoka kila chumba cha mahabusu!

Ni baada ya kutimuliwa katika eneo la kutangazia kura nikipita uchochoro fulani hivi nikilenga kutokea leganga, mara nikajikuta niko katika geti la Gateway lodge, Mungu wangu wee sikujua kama CCM walikuwa wakiishi hapo tangu kampeni zianze na kikosi maalum kiitwacho green guard wakiwa wakitusubiri hapo mithiri ya simba mwenye njaa aonapo kitoweo pengine ni kutekeleza amri waliyopewa na wakuu wao huku wakiwa na mapanga, shoka, viboko, fimbo na silaha za kila aina niliona kama mafuta ya petrol (sina uhakika) maana hata hivyo haikutumika, walituteka nakutupiga mapanga na kila walichojisikia na kisha wakatusachi na kuchukua kila walichoona kinawafaa!

Baada ya kuridhika wakawapigia polisi wakaja kutuchukua! Mambo kadha wa kadha yalikuwa dhahiri katika tukio hilo

1. Polisi watakuwa wanawafahamu watu hao maana hawakuchukua hatua yoyote ya kutaka japo waondoke na mmojawao ili akatoe ushahidi/maelezo ya uhalifu tulioufanya pamoja na kwamba waliwakuta hapo! Hivyo napata nafasi ya kuhisi walifanya kazi kwa ushirika!

2.Wale watu walitumwa na CCM kulingana na kauli walizokuwa wakitoa kama, ninyi ndio mnajiita people people kitu gani, mmesoma shule za CCM halafu mnatuambia people hapa!

Shukurani
Napenda kutoa shukrani zangu za dhani kwa waheshimiwa viongozi wa CHADEMA kwa kutuhangaikia mpaka hivi sasa napata fursa ya kuandika thread hii nikiwa nyumbani baada ya kukandwa majeraha na kuwaona tena familia yangu ikiwa ni baada ya kushinda mauti yaliyotuvamia masaa takribani 18 yaliyopita. Tulimuona mhe. Mbowe usiku ule pale USA akihangaika na baadae tukahamishiwa mjini napo tumemuona Dr. Slaa na makamanda wengine waliofanikiwa sisi kupata dhamana!

Pia namshukuru Mungu mweza yote aliyenipa fursa hii ya kutoa mchango wa damu ya ukombozi huku akitunza nafasi ya uhai wetu ili kunipa nafasi tena ya kushuhudia. Uhimidiwe Mungu wangu!

Free at last! free at last! thank you God Almighty I am free at last!

Hii story umetunga au ni kweli mkuu?

Embu nihakikishie kama ni kweli nikuoneee huruma..

Nashawishika kusema kwa mambo ya kijasusi chadema na CCM hakuna kuchekana..inawezekana wote mmekutana..lol
 
Pole sana ndugu Nkunya ukijuwa ya kuwa ukombozi wa wengi huletwa na watu wachache.Wengi bado wamekamatwa na minyororo ya utumwa wa woga
 
"tel my people that I love them and that they must continue the struggle. My blood will nourish the tree that will bear the fruits of freedom. Aluta Continua'' haya yalikuwa ni maneno ya Comrade Solomon Mahlangu, mpigania ukombozi shupavu wa Afrika ya kusini. maneno haya aliyasema tarehe 5 Aprili 1979, siku moja kabla ya kunyongwa na utawala dhalimu na wa kibaguzi wa Afrika ya kusini. mateso na hata vilema waliyoyapata Ndg zetu Arumeru yanatupa moja muhimu sana katika historia ya nchi yetu ya kwamba bado nchi haijapata uhuru kamili na kwamba SAFARI YA UKOMBOZI ndo imeanza. Lakini niwahakikishie ndg zangu kwamba UKOMBOZI KAMILI utatimia muda si mrefu. Salam ziwaendee mawakala wa mwabanyenye na wale wote wanaoshiriki katka harakati za kutaka kukwamisha vuguvugu la mabadiliko ya kwamba taa mpya ya ukombozi inakaribia kufika ktk kilele cha mlima Kilimanjaro.
poleni sana makamanda tamati ya udhalimu inakaribia. haki itaishinda dhuluma, nuru itakishinda kiza, upendo utaishinda chuki, hekima itaushida ujuha wa mafisadi, heshima itatamalaki dhidi ya dharau, utii kwa umma utakishinda kiburi na majigambo ya kifisadi. na Tanzania mpya itakuwa imezaliwa. Aluta Continua
 
Back
Top Bottom