Ahmed Rajab sikubaliani na wewe katika hili!

thatha

JF-Expert Member
Apr 29, 2011
15,340
1,566
Nimemsikia Ahmed Rajab leo asubuhi akihojiwa na Waziri Hamsini wa BBC. Akijibu swali juu ya mwaliko wa Kikwete toka kwa Obama kuhudhuria mkutano wa G8, mchambuzi Ahmed Rajab kasema kaalikwa kwa vile nchi yetu TZ inaongoza kwa kuuza ardhi kwa wageni(wawekezaji wa kimataifa). Nakiri Ahmed Rajab ni mchambuzi na mwandishi mzuri na mimi ni msomaji mzuri wa makala zake katika gazeti la kila wiki la Raia Mwema. Nimemsikia mara kadhaa akichambua juu ya hali ya mambo katika mashariki ya kati, lazima nikiri nimeelimika sana juu ya hali ya mambo ilivyo mashariki ya kati kupitia chambuzi zake katika BBC.

Pamoja na hayo yote nilianza kutilia shaka dhamiri yake katika kuhabarisha umma pale alipoandika katika Raia Mwema historia ya mapinduzi ya Zanzibar ya 1964. Katika mfululizo wa makala zake kuhusu mapinduzi hayo Ahmed Rajab alijitahidi sana lakini bila mafanikio kuponda umuhimu(significance) wa ushiriki wa Field Marshal John Okello katka mapinduzi hayo matukufu. Ahmed Rajab alijaribu kuonyesha kuwa John Okello alidandia tu kilele cha mapinduzi lakini si mtu aliyeshiriki kikamilifu katika kuyaandaa na kuyatekeleza kama dunia nzima inavyojAhmed Rajabua. Katika kilele cha uongo wake aliandika kuwa siku chache baada ya mapinduzi, Mzee Aboud Jumbe siku moja alimuona John Okello katika kambi ya Welezo ,akiwa na bastola kiunoni kama ilivyokuwa kawaida yake, na kuuliza huyu ni nani. Mwandishi mahiri na mkongwe nchini Joseph Mihangwa alishindwa kuvumilia ghiliba hizi za mwandishi mwenzake Ahmed Rajab na kumjibu kikamilifu kwa kutoa maelezo ya kina juu ya nafasi ya John Okello katika mapinduzi ya Zanzibar.

Tukija katika uchambuzi wake wa leo kuhusu JK kualikwa na Obama napata shaka sana kuamini maneno ya Ahmed Rajab. Mchambuzi Ahmed Rajab atufanyie hisani wasomaji wake kwa kutoa takwimu za ekari za ardhi ambazo zimeuzwa kwa wageni kipindi cha JK. hili ni muhimu ili kulinda imani ya baadhi ya wapenzi wa makala na chambuzi zake.
 
Unajua umekwisha muhukumu kwenye kichwa chako kwamba ni mtu asiyeelezea mambo kwa ukweli.Wasi wasi wangu hata akikupa maelezo unayoyataka hadithi itakuwa ni ile ile ya kumpinga
 
Nimemsikia Ahmed Rajab leo asubuhi akihojiwa na Waziri Hamsini wa BBC. Akijibu swali juu ya mwaliko wa Kikwete toka kwa Obama kuhudhuria mkutano wa G8, mchambuzi Ahmed Rajab kasema kaalikwa kwa vile nchi yetu TZ inaongoza kwa kuuza ardhi kwa wageni(wawekezaji wa kimataifa). Nakiri Ahmed Rajab ni mchambuzi na mwandishi mzuri na mimi ni msomaji mzuri wa makala zake katika gazeti la kila wiki la Raia Mwema. Nimemsikia mara kadhaa akichambua juu ya hali ya mambo katika mashariki ya kati, lazima nikiri nimeelimika sana juu ya hali ya mambo ilivyo mashariki ya kati kupitia chambuzi zake katika BBC.

Pamoja na hayo yote nilianza kutilia shaka dhamiri yake katika kuhabarisha umma pale alipoandika katika Raia Mwema historia ya mapinduzi ya Zanzibar ya 1964. Katika mfululizo wa makala zake kuhusu mapinduzi hayo Ahmed Rajab alijitahidi sana lakini bila mafanikio kuponda umuhimu(significance) wa ushiriki wa Field Marshal John Okello katka mapinduzi hayo matukufu. Ahmed Rajab alijaribu kuonyesha kuwa John Okello alidandia tu kilele cha mapinduzi lakini si mtu aliyeshiriki kikamilifu katika kuyaandaa na kuyatekeleza kama dunia nzima inavyojAhmed Rajabua. Katika kilele cha uongo wake aliandika kuwa siku chache baada ya mapinduzi, Mzee Aboud Jumbe siku moja alimuona John Okello katika kambi ya Welezo ,akiwa na bastola kiunoni kama ilivyokuwa kawaida yake, na kuuliza huyu ni nani. Mwandishi mahiri na mkongwe nchini Joseph Mihangwa alishindwa kuvumilia ghiliba hizi za mwandishi mwenzake Ahmed Rajab na kumjibu kikamilifu kwa kutoa maelezo ya kina juu ya nafasi ya John Okello katika mapinduzi ya Zanzibar.

Tukija katika uchambuzi wake wa leo kuhusu JK kualikwa na Obama napata shaka sana kuamini maneno ya Ahmed Rajab. Mchambuzi Ahmed Rajab atufanyie hisani wasomaji wake kwa kutoa takwimu za ekari za ardhi ambazo zimeuzwa kwa wageni kipindi cha JK. hili ni muhimu ili kulinda imani ya baadhi ya wapenzi wa makala na chambuzi zake.

Mkuu nakubaliana na wewe 100%, nadhani huyu mpemba mwenzio kaamua kutupotosha wadanganyika.
 
Mimi nina shaka shaka sana na nia za ujumbe kwenye maadishi yake mengi. Kusema kweli sio mpenzi kabisa wa articles zake kwa sababu mara nyingi anakuwa kama afanya biashara ya kuwamba ngoz...anajaribu sana kuvutia kwake!
 
Amesahau Zanzibar walipoiuza Mombasa kwa Wakenya? Wamevunja rikodi kwa kuuza mji mzima na vitongoji vyake.
 
Nimemsikia Ahmed Rajab leo asubuhi akihojiwa na Waziri Hamsini wa BBC. Akijibu swali juu ya mwaliko wa Kikwete toka kwa Obama kuhudhuria mkutano wa G8, mchambuzi Ahmed Rajab kasema kaalikwa kwa vile nchi yetu TZ inaongoza kwa kuuza ardhi kwa wageni(wawekezaji wa kimataifa). Nakiri Ahmed Rajab ni mchambuzi na mwandishi mzuri na mimi ni msomaji mzuri wa makala zake katika gazeti la kila wiki la Raia Mwema. Nimemsikia mara kadhaa akichambua juu ya hali ya mambo katika mashariki ya kati, lazima nikiri nimeelimika sana juu ya hali ya mambo ilivyo mashariki ya kati kupitia chambuzi zake katika BBC.

Pamoja na hayo yote nilianza kutilia shaka dhamiri yake katika kuhabarisha umma pale alipoandika katika Raia Mwema historia ya mapinduzi ya Zanzibar ya 1964. Katika mfululizo wa makala zake kuhusu mapinduzi hayo Ahmed Rajab alijitahidi sana lakini bila mafanikio kuponda umuhimu(significance) wa ushiriki wa Field Marshal John Okello katka mapinduzi hayo matukufu. Ahmed Rajab alijaribu kuonyesha kuwa John Okello alidandia tu kilele cha mapinduzi lakini si mtu aliyeshiriki kikamilifu katika kuyaandaa na kuyatekeleza kama dunia nzima inavyojAhmed Rajabua. Katika kilele cha uongo wake aliandika kuwa siku chache baada ya mapinduzi, Mzee Aboud Jumbe siku moja alimuona John Okello katika kambi ya Welezo ,akiwa na bastola kiunoni kama ilivyokuwa kawaida yake, na kuuliza huyu ni nani. Mwandishi mahiri na mkongwe nchini Joseph Mihangwa alishindwa kuvumilia ghiliba hizi za mwandishi mwenzake Ahmed Rajab na kumjibu kikamilifu kwa kutoa maelezo ya kina juu ya nafasi ya John Okello katika mapinduzi ya Zanzibar.

Tukija katika uchambuzi wake wa leo kuhusu JK kualikwa na Obama napata shaka sana kuamini maneno ya Ahmed Rajab. Mchambuzi Ahmed Rajab atufanyie hisani wasomaji wake kwa kutoa takwimu za ekari za ardhi ambazo zimeuzwa kwa wageni kipindi cha JK. hili ni muhimu ili kulinda imani ya baadhi ya wapenzi wa makala na chambuzi zake.
Ahmed rajab ni mchambuzi ninaemuheshimu sana na huwa haumi umi maneno kama wewe.....

nikuulize....niwekee sababu za JK kwenda G8.....very concreate reasons...usiniambie ati kaalikwa na Obama....weka sababu za msingi
 
Sasa mtoa mada hukubaliani nae wapi???kwenye suala la muungano au kwenye suala la mapinduzi?????

Hata mimi sikubaliani na madai ya Rajabu lakini vilevile sikualiani na Aya ya Pili ya Mtoa mada manake naona kama haina uhusiano! Sana sana ninachokiona ni dhamira ya mtoa mada kuanza kujenga taswira kwama Ahmed Rajabu si mtu wa kumwamini linapokuja suala la uchamuzi wa baadhi ya mambo! Hapa, amewakosea wasomaji kwavile baadhi watakuwa tayari wameshaathiriwa na aya hiyo ya pili ya mtoa mada ambayo tayari imeshatoa negative perception abt Rajabu!
 
Hata mimi sikubaliani na madai ya Rajabu lakini vilevile sikualiani na Aya ya Pili ya Mtoa mada manake naona kama haina uhusiano! Sana sana ninachokiona ni dhamira ya mtoa mada kuanza kujenga taswira kwama Ahmed Rajabu si mtu wa kumwamini linapokuja suala la uchamuzi wa baadhi ya mambo! Hapa, amewakosea wasomaji kwavile baadhi watakuwa tayari wameshaathiriwa na aya hiyo ya pili ya mtoa mada ambayo tayari imeshatoa negative perception abt Rajabu!

madai ya leo asbuhi au ya MAPINDUZI????
 
..hebu tuweke kando views za Ahmed Rajabu kuhusu muungano.

..ukweli ni kwamba Tanzania na Ethiopia ziko ktk harakati kubwa sana za kuuza mapande ya ardhi kwa wawekezaji wa nje ili walime mazao kwa ajili ya ku-export. kuna mwanachama mwenzetu wa JF alilete article inayozungumzia suala hilo.

..Ahmed Rajabu hajakosea ktk madai yake.
 
Huyu Jamaa anachuki Binafsi na huyo Rajabu, njia sahihi ya kuonyesha upotoshaji wa Rajabu ni kwa mtoa mada kufanya hili kifuatacho.
1. Kuweka hapa sababu rasmi za mualiko wa Jakaya
2. Kuweka ushahidi kwamba sio kweli kwamba Tanzania inauza Ardhi Mapande kwa Mapande kwa wageni hasa wamarekani.

Ama sivyo naona Rajabu anataka kushambuliwa bila sababu za msingi.
 
Ni kweli Tanganyika inauza ardhi yake suala hili halina ubishi kabisa.
 
Nimemsikia Ahmed Rajab leo asubuhi akihojiwa na Waziri Hamsini wa BBC. Akijibu swali juu ya mwaliko wa Kikwete toka kwa Obama kuhudhuria mkutano wa G8, mchambuzi Ahmed Rajab kasema kaalikwa kwa vile nchi yetu TZ inaongoza kwa kuuza ardhi kwa wageni(wawekezaji wa kimataifa). Nakiri Ahmed Rajab ni mchambuzi na mwandishi mzuri na mimi ni msomaji mzuri wa makala zake katika gazeti la kila wiki la Raia Mwema. Nimemsikia mara kadhaa akichambua juu ya hali ya mambo katika mashariki ya kati, lazima nikiri nimeelimika sana juu ya hali ya mambo ilivyo mashariki ya kati kupitia chambuzi zake katika BBC.

Pamoja na hayo yote nilianza kutilia shaka dhamiri yake katika kuhabarisha umma pale alipoandika katika Raia Mwema historia ya mapinduzi ya Zanzibar ya 1964. Katika mfululizo wa makala zake kuhusu mapinduzi hayo Ahmed Rajab alijitahidi sana lakini bila mafanikio kuponda umuhimu(significance) wa ushiriki wa Field Marshal John Okello katka mapinduzi hayo matukufu. Ahmed Rajab alijaribu kuonyesha kuwa John Okello alidandia tu kilele cha mapinduzi lakini si mtu aliyeshiriki kikamilifu katika kuyaandaa na kuyatekeleza kama dunia nzima inavyojAhmed Rajabua. Katika kilele cha uongo wake aliandika kuwa siku chache baada ya mapinduzi, Mzee Aboud Jumbe siku moja alimuona John Okello katika kambi ya Welezo ,akiwa na bastola kiunoni kama ilivyokuwa kawaida yake, na kuuliza huyu ni nani. Mwandishi mahiri na mkongwe nchini Joseph Mihangwa alishindwa kuvumilia ghiliba hizi za mwandishi mwenzake Ahmed Rajab na kumjibu kikamilifu kwa kutoa maelezo ya kina juu ya nafasi ya John Okello katika mapinduzi ya Zanzibar.

Tukija katika uchambuzi wake wa leo kuhusu JK kualikwa na Obama napata shaka sana kuamini maneno ya Ahmed Rajab. Mchambuzi Ahmed Rajab atufanyie hisani wasomaji wake kwa kutoa takwimu za ekari za ardhi ambazo zimeuzwa kwa wageni kipindi cha JK. hili ni muhimu ili kulinda imani ya baadhi ya wapenzi wa makala na chambuzi zake.

sio kwamba wanauziwa ni kwamba wanapewa ardhi bure, mfano kule Rukwa wamarekani kupitia kampuni ya Agrisol wamepewa maelfu ya hekari kwa gharama ya tshs.200 (two hudred shillings) kwa hekari
 
Back
Top Bottom