AHMED RAJAB: Je, Sheikh Abeid Karume naye akitaka kurejesha usultani?

Bwana Ahmed Rajab, kwanini usipendekezee tu kuvunjwa muungano? mkataba wa nini tena, tusije koseana kwenye vipengere vya huo mkataba then tukaanza kupelekana mahakani tena, mi nafikiri kama unayo hoja juu ya muungano, washawishi tu wazanzibar wenzio muuvunje tu huu muungano na kila moja awe na chake, simple as that, kumsingizia JK Nyerere kwamba hata katika vyama vingi alikataa muungano usijadiriwe hiyo ni uongo, kwa muislam kama wewe kuongea uongo ni jambo baya sana, nadhani utakapo kwenda kupiga Rakaa leo kumbuka kumwomba msamaha muumba wako kwamba umemsingizia mtu, nakumbuka vizuri sana tena hata hotuba za mwalim bado ninazo, alilikemea kundi lile la G 55 juu ya hoja yao ya muungano, point yake ilikuwa hivi, "nyie ni wabunge wa CCM, mnaitumikia katiba ya CCM pia, kama mngekuwa wabunge wa vyama vya upinzani sina tatizo na hilo lakini sio nyie watu wa CCM ambao hata chama chenu kinaamini hivyo juu ya muundo wa muungano" sasa mkuu unaposema hata katika mfumo wa vyma vingi eti Nyerere alikataa watu wasijadiri muungano hiyo sio kweli, huo ni uongo na kama unaweza kutetea kitu hata kudanganya ndipo ninapodhani kuwa huenda una ajenda nyingine ya siri, halafu eti nasikia wewe huishi Zanzibar wala huku Tanganyika, hivi ni kweli?

katika hadidu rejea za tume ya mabadiliko ya katiba haziruhusu kutoa maoni ya kuvunja muungano that's y tunatoa maoni ya muungano wa mkataba ambao unakaribia kuwa sawa na kuvunja.
 

BARAZANI KWA AHMED RAJAB
.......dhana ya kwamba upinzani dhidi ya muundo wa sasa wa Muungano ulianza jana au kwamba umekuwa ukichochewa na mtu fulani au kikundi fulani chenye ‘ajenda ya siri.'
......hivyo tangu siku ya mwanzo ya kuzaliwa kwake ni wachache Zanzibar waliousherehekea kwa moyo mkunjufu. Wengi walikuwa na dukuduku na waliingiwa na wahasha lakini hawakuwa na la kufanya
Ahmed anaposema wachache au wengi hana takwimu za kuonyesha. Hii ni dhana yake binafsi.
Mimi nikisema wengi walishangilia na wachache walikataa nitakuwa sahihi kama yeye.
Kwakuwa amesema wengi walikataa halafu akasema hawakuwa na la kufanya, hapo anajichanganya kwasababu wengi walikuwa na uwezo wa kumwambia Karume hapana.
Hakuna ushahidi wa wengi kupinga jambo hilo aliouweka wazi. Ni maneno yake.

Kikundi kinachopinga muungano ni kile kinachoongozwa na washirazi na wale wenye unasaba na sultan.
Ndiyo maana Karume anatajwa kama Mnyasa, Mwinyi Mdengereko n.k. Akina Ramadhani Mapuri wakitoa maoni yao tofauti wanashambuliwa.
Pia jiulize kama Wazanzibar hawana vikundi kwanini Pemba iombe kujitenga.
Wajumbe kadhaa wa BLW la awali wameniambia kwamba lau suala hilo lingejadiliwa...wajumbe wa Baraza wangepewa wangeliupinga muundo huo wa Muungano.
Hawasemi kwamba wangelipinga kuwapo kwa aina ya umoja au shirikisho baina ya Tanganyika na Zanzibar, Tukumbuke kwamba wakati huo Baraza la Mapinduzi ndilo lililokuwa na majukumu ya utungaji wa sheria za Jamhuri ya Watu wa Zanzibar.
Kwa vile walikuwa na mamlaka ya kutunga sheria hakuna mahali panapoonyesha kuwa jaribio hilo lilifanyika. Kinyume chake wajumbe wengi walikubali nafasi za uteuzi katika serikali ya muungano akiwemo Hassan N.Moyo.
Huwezi kukataa kitu unachokitumikia. Ahmed aonyeshe mjumbe mmoja tu ambaye aligoma kutumikia serikali ya muungano kwasababu ya kupinga muungano
Wenye kuhoji kwambA kuupinga muundo wa Muungano wana ajenda ya siri ya kurejesha usultani wanajikanganya.
Sheikh Abeid Karume alikuwa na ajenda gani ya siri alipokuwa akiupiga vijembe Muungano katika siku za mwisho za uhai wake. Wakati huo alikuwa amekwishatanabahi kwamba muundo wa Muungano kama ulivyo haukuwa na manufaa kwa nchi yake. Ndiyo maana akatamka kwamba ‘Muungano ni kama koti likikubana unalivua'
Kuna ushahidi gani kuonyesha wazi kuwa Karume alishaona muungano hauna faida zaidi ya masimulizi? Mwanzo umesema wajumbe wengi walipinga muungano, huoni hiyo ilikuwa nafasi nzuri ya wajumbe hao na Karume kuvunja muungano.
Alitamka muungano ni koti na alishaona linambana nini kilimzuia yeye kuwatumia wajumbe'wengi' wa baraza la mapinduzi waliopinga muungano kuuvunja
Wakati mwingine siku moja tu kabla hajaiaga dunia alimwambia Bwana Salim Rashid, katibu mkuu wa kwanza wa Baraza la Mapinduzi, kwamba Muungano ni kama matoto ya treni na Zanzibar inashikilia shoka ambalo karibu italitumia kuukata mnyororo....Tanganyika ingekwenda upande wake na Zanzibar ingekwenda upande wake
Kitu gani kilimshinda yeye hata pale alipokuwa na shoka kukata mnyororo tena akiungwa mkono na wajumbe wa baraza la mapinduzi walio 'wengi'. Je Karume aliondoka na shoka kiasi cha kutokuwa na jingine hadi miaka 48 imepita. Hadi hapa Ahmed anaonyesha kuwa Zanzibar pamoja na Karume hawakutaka muungano.
Redio Zanzibar walikuwa na ajenda gani na ya kumrejesha sultani gani Zanzibar.
Ninakukumbusha kwamba upinzani dhidi ya Muungano haukuanza jana wala leo....upinzani huo ulijikita pia ndani ya duru za waliokuwa wakihodhi madaraka Visiwani Zanzibar baada ya Mapinduzi ya mwaka 1964
Ajenda ya kumrudisha Sultan haikuwa wazi hadi siku za karibuni ambapo wanasultan kama Ahmed wamejitokeza wazi wazi na maandiko kudai ushirazi na umiliki wa Zanzibar. Imejitokeza wazi pale akina Jusa waliposimama na kumlaani Karume kwa Mapinduzi. Siku za karibuni kumekuwa na kususia mapinduzi hadi kuyaita ya Nyerere, na pia kuamsha hisia kwamba Zanzibar ilikuwa bora kabla ya 1964. Yote haya yamepelelea wazanzibar wengine kuita 'mapinduzi daima' Chimbuko la kauli ni kupinga njama za kundi la Wanasultan kuirudisha nchi chini ya minyororo ya Sultan.

Endapo upinzani ulijikita ndani ya waliohodhi madaraka na wajumbe wa baraza la mapinduzi, kwanini hawakumuunga mkono Jumbe alipojaribu kuinasua Zanzibar.
Kinyume chake waliohodhi madaraka kama Seif walimsaliti kwa kuvujisha habari zake.
Kwanini akina Nassor Moyo, Thabiti Kombo, Natepe, Mwakanjuki n.k walikubali kukaa katika kamati na vikao vilivyomuondoa Jumbe. Kwanini Ali Hassan ambaye ni mjumbe wa baraza la mwazo alikubali kuchukua nafasi ya Jumbe
Kwa mfano, Sheikh Aboud Jumbe kupokonywa wadhifa wake wa kuwa Rais wa Zanzibar mnamo mwaka 1984 Aling'olewa madarakani kwa nazaa na Chama cha Mapinduzi (CCM) na wala si na Baraza la Mapinduzi kama ilivyotakiwa na Katiba ya Zanzibar
Endapo ni hivyo, je CCM ilimuondoa bila ushiriki wa wazanzibar? Wakati huo Seif alikuwepo, Mwinyi, Thabiti Kombo n.k. Walikaa katika vikao na Nyerere kama CCM na kumuondoa Jumbe. Ahmed amesahau kuwa Seif alishiriki vizuri sana katika hili.

Asichosema Ahmed ni kuwa mjumbe madhubuti Thabiti Kombo Jecha ndiye alimpendekeza Ali Hassan.
Ali Hassan alikuwa ni mjumbe wa baraza la mapinduzi.Hapo tu unaona kuwa wajumbe wa kutosha walikubali kuondoka kwa Jumbe na sijui kama kungekuwa na matokeo tofauti ndani ya baraza la mapinduzi
......kila walipopata fursa ya kutoa maoni yao juu ya Muungano, mfano, wakati wa Tume za Nyalali na Kisanga Wazanzibari wengi walipendelea pawepo na mfumo wa serikali tatu katika Muungano.Waliamini kwamba mfumo huo ungeirejeshea Zanzibar mamlaka yake yaliohamishiwa Bara
Huko nyuma amesema wazanzibar wengi hawakuta muungano, hapa anasema wengi walitaka kuwe na serikali tatu ili kurudisha mamlaka ya ZNZ. Anachofanya hapa ni kutumia neno 'wengi' pale anapodhani hoja yake inatakiwa kuungwa mkono, lakini kufanya hivyo anajichanganya. Endapo wengi walitaka serikali 3 ni lini tuliona juhudi za wao kumuunga mkono Jumbe kama tunavyoona UAMSHO sasa?
......katika vikao mbalimbali vya BLW tokea miaka ya 1980 suala la Muungano lilikuwa likiibuka mara kwa mara na kwamba Baraza hilo kila lilipopata fursa lilikata maamuzi yenye kutetea maslahi ya Zanzibar. Mifano ya hivi karibuni ni pamoja na yale maamuzi yanayohusika na masuala ya mafuta na gesi asilia
Kama wameweza kutetea masilahi kama mafuta na gesi kwa kutumia BLW ni kitu gani kinalishanda baraza hilo lenye nguvu kuamua kujitoa katika muungano.Ni lini kuliwahi kuwa na muswada wa kupendekeza aina ya muungano au kuuvunja
........kwani Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alisema kwamba vyama vipya vya kisiasa vinaweza kujadili masuala yote lakini visiuguse Muungano
Ningeshangaa kama Ahmed angemaliza makala bila ya kueleza chuki zake dhidi ya Nyerere. Kama mwandishi anayejulikana zanzibar kuwa msomi, Ahmed alitakiwa amnukuu mwalimu alisema hayo maneno lini, wapi na katika mazungumzo yaliyo husu nini.

Kutuletea maneno bila source ni uandishi wa kibubusa sana.
Ameulizwa pia lini na wapi Karume alisema muungano ni koti.
Mwandishi makini na anayetumia kalamu kwa busara kuchukua maneno ya mitaani na kuyashadidia kuwa ni kweli tena katika vyombo vya habari. Huu ni uandishi uliokusudia kupindisha ukweli kwa kujaza uongo
.......Sasa hali imebadilika na ndiyo maana Wazanzibari wanaosema kuwa wanataka pawepo Muungano wa Tanganyika na Zanzibar utaojengeka juu ya msingi wa Mkataba na si Katiba.
Ahmed hajaeleza huu muungano tulio nao upo kundi gani kiasi cha kudai mkataba. Lakini fikiria kuwa huyu ndiye aliyewahi kusema wazanzibar hawakutaka muungano. Katika makala zake za mwaka jana Ahmed aliorodhesha mambo ya mkataba wa muungano. Mara zote amekuwa akisema mambo yaliyokubaliwa yamekiukwa hadi kufikia 32. Sasa anasema wazanzibar wanataka mkataba! huu ni uzuzu uliotamalaki.
Wanataka mkataba upi wakati muungano uliopo ni wa mkataba wa mambo anayosema 11!
Huko nyuma amesema wazanzibar hawataki muungano, sasa anasema wanataka mkataba.
Huyu mwandishi wa kiwango fulani,maana huwezi kutapika na kurudi kula matapishi yale yale.
Ahmed hajui anataka kusema nini au kuwashawishi wazanzibar wadai nini
Katika Muungano wa aina hiyo kila nchi itakuwa na mamlaka kamili ya utawala wa mambo ya ndani ya nchi yake pamoja na shughuli za kigeni au za kimataifa. Mfumo huo ni bora zaidi kushinda ule wa serikali tatu ambao wengi wanauona kuwa umepitwa na wakati na uliokwishakataliwa na Serikali za Jamhuri ya Muungano ya Tanzania.
Ahmed anasema kila nchi iwe na mamlaka kamili ya ndani na ya nje. Hapo hapo anasema kuwe na mkataba,mnaona jinsi huyu mtu anvyoyumba.
Ukiwa una mamlaka ya ndani na nje kamili hakuna kitu kitachounganisha Tanganyika na Zanzibar tena. Kwa maneno mengine muungano ufe. Na kama ni hiyo kwanini asiseme wazi. Na kwanini asiseme mkataba utahusu mambo gani ambayo hayamo katika mamlaka kamili ya ndani na nje.

Ahmed mwaka huu mwezi wa sita ameandika kuhusu serikali 3. Miezi miwili mawazo yake yamepitwa na wakati.
Ukweli ni kuwa amesoma habari za JF kuwa Tanganyika ikirudi hakuna kubebana, pasu pasu.
Ukiweka sheria ya ardhi kulinda watu wako upande wa pili utaweka yao. Gharama ni sawa sawa.
Ahmed na kundi lake wakagundua kuwa wamewatia mkenge wazanzibar na sasa anarudi na upuuzi wa kuwasingizia wazanzibar kuwa hawataki serikali 3 kwa kupitwa na wakati bila kujua bado wanaimba nyimbo potofu alizowafundisha.
Kadhalika, kuna uwezekano mkubwa kwamba muundo wa aina hiyo utaweza kuzivutia nchi nyingine katika kanda ya Afrika ya Mashariki na ya Kati kujiunga na Muungano wetu na hivyo kuimarisha kidhati Umoja wa Kiafrika
Ahmed hajui kuwa kuna SADC, EAC, COMESA ambazo hazitegemei kuona zanzibar inataka nini. Kama ni hivyo hatuna sababu ya kuwa na mkataba wa Tanganyika na Zanzibar tu, twende EAC kama nchi kamili kila moja na huko tuunganishe nguvu tuwe na mkataba wa EAC.
Muungano wa aina hiyo utakuwa imara.....Zanzibar daima imekuwa na dukukudu..... Historia ...Wazanzibari.....wameonewa katika mahusiano kati ya nchi yao na Tanganyika.
Mwandishi huyu amesahau kuwa yeye anataka zanzibar huru yenye mamlaka kamili. Na kama anataka mkataba ni wazi huo si muungano tena. Kwanini ZNZ iwe na manung'uniko, kwanini wasijitoe kwenda kuungana na nchi nyingine? Why Tanganyika!

Ameshindwa kuonyesha nchi moja tu yenye muungano wa mkataba. Ameshasahu hoja yake kuwa wajumbe wa baraza la mapinduzi hawakutaka muungano, na wazanzibar wengi hawaupendi muungano.
Wakati huo huo analalama kuwa wanonewa huku akinyanyua akipiga kifua kuwa baraza la wawakilishi linatetea masilahi ya wazanzibar. Wameshindwa nini kutetea masilahi hadi kuonewa
Kama kweli tunataka bara la Afrika liungane kiuchumi, kisiasa na kijamii ...nchi zinazoungana ziungane kila moja ikiwa na mamlaka kamili ya kujiamulia mambo yenye kuhusika na maslahi yake
Huwezi kuwa na mamlaka kamili ukawa na muungano. Nchi za ulaya zilipoungana kuwa EU bado kila nchi ili sacrifice baadhi ya thamani zake.

Kwa ubinafsi na uchoyo wa Zanzibar hilo halitawezekana kwani hulka ya mzanzibar ni kutaka atendewe si yeye amtendee mtu. Imeshindikana katika muungano huu ambapo zanzibar si mshiriki bali 'social welfare' sembuse huo anaofikiri upo.

Hapa Ahmed anaungana na Maalim kama kwenye kundi lao kuleta hoja ya kipuuzi ya muungano wa EU baada ya hoja za mwazo kugonga mwamba.
Zanzibar inaweza kuungana na Comoro, Kenya au Mauritius kwa mkataba wanaotaka wawo. Kwanini wameng'ang'ania Tanganyika.Huu upuuzi wa kuungana au kuwa na mkataba wa kubebana Tanganyika haitaki
.
Muungano aina hiyo utafana endapo tu utakuwa ni wa hiyari na si wa kulazimishwa na ikiwa utaipa kila nchi iliyomo ndani yake haki ya kuwa na kauli sawa na uhuru wa kujiamulia yaliyo yake bila ya kuyadhuru maslahi ya nchi nyingine zilizo ndani ya Muungano huo.
Msomi huyu wa Unguja anaendeleza nyimbo za mkataba wa EU. Hizi ni njama za kuingiza upuuzi wa mkataba wa EU zinazopangwa na kikundi hiki cha sultan kikiongozwa na maalimu seif na Ahmed. Huwezi ukaonewa halafu ukataka mkataba.

Hitimisho: Kwa Watanganyika ni wazi sasa kuwa Zanzibar inaihitaji Tanganyika na Tanganyika haihitaji Zanzibar kwa lolote lile. Hoja za serikali 3, mkataba na sasa EU ni kutapa tapa kwa Zanzibar kwa kuelewa kuwa nje ya muungano Zanzibar itakuwepo lakini katika maumivu makali sana hasa kwa watu wa chini.

Kwa vile Zanzibar haina mchango wa aina yoyote kwa maisha ya Mtanganyika, kuendelea na mkataba au vinginevyo kama inavyodaiwa na kundi hili la wachochezi ni kutaka kumbebesha Mtanganyika mzigo.
Kwa miaka 48 tumebeba zigo hili bila shukrani na haionekani kama kuna njia mbadala ya kuwaridhisha hawa ndugu zetu.

Tanganyika, hatuna cha kupoteza. Kwanini tusiwaombe ndugu zetu wafunge mabegi yao tu warejee kwenye utawala wa Kisultani ambao ni bora kuliko sasa. Ahmed, acha kuwahadaa wazanzibar kwa maandiko wasioweza kuyatafsiri.

Ujanja wako mwisho chumbe, baada ya hapo njoo bara ukiwa na hoja za mkataba wa nini na kuhusu nini, kama huna kuwaimbisha wazanzibar! Tanganyika huna usomi zaidi ya ubabaishaji na matumizi ya maneno. Huna solution zaidi ya kuwachochea wazanzibar na siku si nyingi watavuka bahari wakilia huku wewe ukiwa Uingereza.

Wanatapa tapa sasa, hamkani si shwari. Hawana hoja za mkataba. Tunasema hivi hatuwahitaji kwasababu hakuna lolote ndani ya serikali 3, Mkataba, EU, Mkataba wa Uswiss, Muungano wa Vanuata na Haiti n.k. ambao utamsadia Mtanganyika.
Tanganyika haiihitaji Zanzibar hata kidogo. Kwanini msitafute mshiriki mwingine mnataka kubaki na maumivu ya miaka 48.


LET ZANZIBAR GO!









 
Nguruvi3,

..wa-ZNZ wanaogopa kutoka ktk muungano.

..wanajua wakiwa nje ya muungano watakufa na njaa.

..juzi Wachina wamewapa mkopo wa sh bil 14.8.

..linganisha na bil 32 alizopewa Dr.Bilali toka bajeti ya Tanganyika kwa ajili ya maendeleo ya ZNZ.
 
Last edited by a moderator:
Nicholas, Mwanakijiji, Nguruvi3 , jokakuu na Jasusi.

Siku zote kwa mtu makini na msomi mwenye kuelimika anajibu hoja kwa kutoa hoja. Kwa maana kuwa kunakuwa na ushindanishaji wa hoja kwa hoja na sio dharau wala kejeli.

Msomi yoyote aliyeelimika anapoanza kutoa lugha za mkato na kejeli pasi na kujikita kutoa hoja basi huyo anaitwa MUF'LIS kwa maana amefirisika sio tu kiakili bali hata kimawazo.

Sasa ushauri wangu kwenu wote jaribuni kwa kadri ya uwezo wenu kujibu hoja zake ambazo kwangu mimi naziona ni madh'buti sana na amezipangilia kwa mpangirio na mtiririko mzuri sana na hazina hata chembe ya shaka ndanimwe.

Alichobainisha Ahmed Rajab ni uhalisia na ukweli mtupu. Na kama kwa waandishi mahiri na waliobobea kama Ahali yangu Ahmed (nimezoea kumuita Tuyuri wa kingazija) ametoa suluhisho lake ambalo nyie wote ndio mnapingana nalo kwa maneno ya kejeli.

Sasa kwa kuwadarsisha kidogo. Mtu makini anatakiwa kusoma hoja zote za mwandishi nutufa kwa nutufa na kuelewa na kujua ametumia mtindo gani katika kujenga hoja zake. Hapo kwenye suluhisho ni sehemu ya mwisho sana katika kufikia tamati.

Kumbukeni kuwa kila mwenye kupinga Muungano wenu basi anasababu zake za msingi zinazomfikisha hapo na vile vile kila mwenye kuutetea muungano basi ana sababu zake za kumfikisha katika maamuzi hayo. lakin ikumbukwe kuna wale wasio na hoja ambao siku zote ni bandera kufuata upepo na wamekuwa washabiki pasi na kuwa na hoja kama mlivyo nyie.

Nawashauri kwa mara nyingine jikiteni katika kujenga hoja ili kuungana/ kupingana na hoja za mwandishi. Kwani muungano wenu ni wa nchi mbili huru na kila upande una fursa sawa ya kuujenga/ kuuvunja. sasa msiwe mwanyonge kiasi cha kusema basi wao wajitoe kwani nasi tumewachoka. Kumbukeni hata nyie mnayo nafasi ya kuwafurusha kama mumewachoka.na sio kubakia kusema LET THEM GO

Fungukeni kiakili na acheni woga. Kwani siku zote ukweli udumu daima

Barubaru, kama unafikiri ana hoja naomba unisaidie kujibu swali hili: Kama kila nchi itakuwa na mamlaka kamili ya kuendesha mambo yake ya ndani na ya nje mtakuja kuungana kwenye mambo gani na kwanini? Maana lengo la muungano wa nchi zozote zile ni kusurrender sovereignty - iwe yote (total) au kwa sehemu (partially).
 
katika hadidu rejea za tume ya mabadiliko ya katiba haziruhusu kutoa maoni ya kuvunja muungano that's y tunatoa maoni ya muungano wa mkataba ambao unakaribia kuwa sawa na kuvunja.

njia ya kutoa maoni ni kudai serikali moja... mtauvunja!
 
katika hadidu rejea za tume ya mabadiliko ya katiba haziruhusu kutoa maoni ya kuvunja muungano that's y tunatoa maoni ya muungano wa mkataba ambao unakaribia kuwa sawa na kuvunja.
Ahmed Rajab anachosema ni kuwa muungano uwepo. Msome vizuri sana maana mimi nafuatilia siku nyingi uchochezi na hoja zake dhaiifu sana.

Kwanza aliasisi serikali 3 hizo zimegonga mwamba. Sasa anasema mkataba ili hali alishawahi kusema kuna mkataba wa mambo 11. Siri ya hiki anachokisema ni kuwa kuwepo mkataba utakaotoa unafuu kwa wzanzibar.

Anafahamu kuwa hawana soko la ajira wala biashara, ardhi n.k. na kwa namna yoyote ile Zanzibar itaitegemea Tanganyika itake isitake. Ndivyo jiografia na mazingira ya kisosholojia yalivyo (nature). Hutasikia znz ilitaka serikali 3 au mkataba na Kenya au Comoro

Hili la mkataba ni la ajabu sana maana haweki hadharani mambo ya mkataba. Siku zote anaweka 'maonevu' ya wazanzibar hasemi mazuri yatokanayo. Kuna siri gani ya mkataba isiyowekwa hadharani?

Halafu wakati anataka mkataba anataka pia uhuru kamili wa mambo ya ndani na nje. Huwezi ukawa na vitu hivyo viwili ukawa na mkataba. Mkataba siyo maandishi au kuruhusu wazanzibar wajazane bara na kutumia rasilimali.

Mkataba ni mahusiano maalumu kwa maandiko yenye tija kwa pande husika. Zanzibar haihitaji mkataba inataka social welfare!Social welfare ndio kitu anachokificha Ahmed. Anajua hadi sasa wanapata social welfare nzuri tu

Ahmed anajua kabisa kuwa muungano ni kimbilio la Wazanzibar. Hakuna nchi nyingine duniani iliyobeba wazanzibar kama Tanzania bara. Na hakuna nchi nyingine itakayotoa zaka kwa zanzibar kama Tanganyika.

Ukweli usio na dhihaka ni kuwa zanzibar ni kula kulala. Ulinzi bure, usalama bure, elimu bure, umeme bure, bilioni 32 zisizo na kazi ofisi ya Bilal, Sumatra bure, nafasi za elimu za upendeleo, gharama za viongozi wastaafu akiwemo Seif buree, nafasi za ajira Tanganyika bwerere hata kilaza atapewa kwa jina la uzanzibar n.k. Wajitoe waende wapi!!

Tulieni wazanzibar hamna nyimbo katika muungano! pigeni kelele mkapambane na dhiki ya maisha!
Mlijaribu passport mkaufyata, this time imekula kwenu.
Hatuwahitaji kwasababu hamtusaidii lolote.

LET ZNZ GO!
 
Mkuu, huyu jamaa ni member JF. Ukisoma makala hii anajaribu kujibu tuhuma zilizotolewa zikihoji ushiriki wake katika kuwadanganya wazanzibar akishirikiana na maalimu Seif.

Mara ya pili amekana serikali 3 baada ya kupashwa kuwa Tanganyika ikirudi kila mtu na lake.
Sasa ameshupalia mkataba.

Ni mwandishi wa kiwango cha chini sana. Kawatia wenzake mkenge wa nyimbo ya tatu,tatu halafu kawarudi.
Anawaimbisha tena mkataba, mkataba.

Mambo magumu hawana pa kushika, kuondoka hawataki wanataka kubaki mguu nje mguu ndani.
Subiri tume ziingie Mijini na kwenye majiji wataambiwa wazi

LET ZNZ GO!
hivi ahmed rajab ni muandishi wa kiwango cha chini? unadanganya umma ni muandishi tunayejivunia sisi wazanzibar katika dunia ya habari! kumbuka hata dunia inaziamini makala na habari zake! udogo wake katika tasnia ya habari iko wapi?
 
hivi ahmed rajab ni muandishi wa kiwango cha chini? unadanganya umma ni muandishi tunayejivunia sisi wazanzibar katika dunia ya habari! kumbuka hata dunia inaziamini makala na habari zake! udogo wake katika tasnia ya habari iko wapi?
OK! tunachosema hapa ni kuwa hoja zake kuhusu muungano ni dhaiifu sana.
Si unaona anavyowadanganya kila siku! Kawaimbisha serikali 3 kashindwa kuzitetea amechomoa. Sasa anawaimbisha mkataba hawezi kuutetea mnaitika tu. Anataka muungano, hataki muungano! Hawaelezi ukweli hata siku moja.

Hajawaambia mnafaidikaje na muungano, anawajaza uchochezi na ututusa wa kuona muungano ni shetani.
Mwandishi anatakiwa aweke habari katika mizania kuonyesha sehemu zote kwa uhalisia.
Muulizeni awaambie ukweli maana siku ukweli ukifika atarudi uingereza aliko Sultan na kuwaacha mkisaga vumbi.
Kuandika ni suala moja, kujua unaandika nini ni suala jingine.

Kwa viwango vya ZNZ he is good! kiwango hicho mwisho chumbe
 
Nguruvi3,

..umekuwa kama bondia vile.

..yaani ukiona mpinzani wako kapata nundu basi na wewe ndiyo unapiga hapo hapo.

..tatizo la Ahmed Rajab ni kutokusema ukweli.

..Sovereignity na muungano ni sawa na mafuta na maji, haviwezi kuwa pamoja.

..labda kinachowafaa hawa ni kuwa na MOU na siyo mkataba.

..MOU huwa iko loose-loose yaani unatekeleza maagizo kulingana na matakwa na uwezo wako.

..kwa msingi huo napendekeza "muungano wa MOU."
 
Last edited by a moderator:
OK! tunachosema hapa ni kuwa hoja zake kuhusu muungano ni dhaiifu sana.
Si unaona anavyowadanganya kila siku! Kawaimbisha serikali 3 kashindwa kuzitetea amechomoa. Sasa anawaimbisha mkataba hawezi kuutetea mnaitika tu. Anataka muungano, hataki muungano! Hawaelezi ukweli hata siku moja.

Hajawaambia mnafaidikaje na muungano, anawajaza uchochezi na ututusa wa kuona muungano ni shetani.
Mwandishi anatakiwa aweke habari katika mizania kuonyesha sehemu zote kwa uhalisia.
Muulizeni awaambie ukweli maana siku ukweli ukifika atarudi uingereza aliko Sultan na kuwaacha mkisaga vumbi.
Kuandika ni suala moja, kujua unaandika nini ni suala jingine.

Kwa viwango vya ZNZ he is good! kiwango hicho mwisho chumbe

Nguruvi3,

Unajua siku zote ni rahisi sana kupinga hoja zinazotolewa na mwandishi wa makala yoyote. LAKIN NI VIGUMU SANA KUANDIKA MAKALA YA KUPINGA HOJA ZILIZOPO MEZANI. Kwani katika kaanun za kiandishi unapopingana na hoja unatakiwa kutoa hoja zako ambazo mwenyewe unaamini kuwa ni nzito na kuwaacha wasomaji wengine waamue.

Sasa kwa hapa wewe mwenyewe msomaji, mpingaji na mwamuzi pasi na kutuwekea hoja zako unazodai ni math'buti na sio tu kusema hoja za Ahmad ni dhwaifu.

Kiungwana tuwekee basi hizo hoja zako unazodai ni nzito ili tushindanishe na hizi za Ahali yenye Ahmad Rajab.

 
Barubaru, kama unafikiri ana hoja naomba unisaidie kujibu swali hili: Kama kila nchi itakuwa na mamlaka kamili ya kuendesha mambo yake ya ndani na ya nje mtakuja kuungana kwenye mambo gani na kwanini? Maana lengo la muungano wa nchi zozote zile ni kusurrender sovereignty - iwe yote (total) au kwa sehemu (partially).
.

Mwanakijiji,

Naona suala lako mbona limeshajijibu lenyewe. Kumbuka kuwa Muungano wowote ni kitu cha hiari cha pande au nchi zaidi ya moja kuungana iwe kwa mkataba kama ilivyo Znz na Tanganyika au Kuungana Kisharia. Ukichukulia muungano wenu wa Tanzania , utaona wazi mlikubaliana kuungana katika baadhi ya mambo tu na mengine yaliyobaki kila nchi inakuwa na madaraka nayo. sasa kumbuka kuwa mnaweza hata kukubaliana jambo moja tu na mkashirikiana na mengine kila mtu akajifanyika mwenyewe. Huo wote ni muungano.

Na kama hamtaweza kukubaliana katika mkataba wenu kuungana katika baadhi ya mambo basi mtabaki kama majirani kama ilivyo Kenya, Uganda au nchi nyingine yoyote jirani.

Sasa wasi wasi mliokuwa nao watu wa Tanganyika ndio unaotia khofu. Kwani mumekuwa dhaifu sana katika kudai maslahi ya nchi yenu kiasi cha kupelekea kujiona kama nyie ni wadogo sana katika maamuzi ya muungano huo au muna nafasi ndogo katika kudai haki zenu katika muungano kwa kauli zenu LET THEM GO na sio LET ME GO.

Kwa mtu makini siku zote kama umechoshwa na karaha unajiengua na sio kumwambia partners wako jiondoeni kama wewe huusiki katika kujiondoa.

Nawashauri lazima muwe na uwezo mkubwa wa maamuzi na kujiona mna nafasi sawa na Znz katika maamuzi ya huo muungano wenu. Hivyo kama mnaona mnadhurumiwa na kunyanyasika mnahaki kamili ya kushawishi wenzenu wa Tanganyika na wote kwa sauti moja mkapaza sauti ya kutaka kujitoa kama wanavyyofanya waZnz.

Kumbukeni nyie ndio wenye nyenzo zote za kuulinda na kuutetea huo mvungano wenu.Kwani mambo yote ya muungano mumeyakumbatia kwani mlikubali na nia moja kuuwa utaifa na jina la nchi yenu na kujivika joho na jina la muungano wenu.

Kumbukeni Mola siku zote hawezi kuwa na waoga. jitazameni.

 
Batu baru,
Hoja za Ahmed ni dhaifu sana kwasababu hazisimami kwa miguu.
Ni dhaifu kwasababu tumeivunja ile hoja yake ya serikali 3 kwa kuonyesha wazi Tanganyika ikirudi nini kitatokea.
Ni kutokana na kusoma makala hizo ndipo akaja na hoja ya kuwa serikali 3 imepitwa na wakati, bila kumbu kumbu kuwa miezi si zaidi ya miwili amekuwa anashadidia hoja hiyo. Hakujua anaweka nini mezani

Ni dhaifu kwasababu huwezi kuwaambi watu mkataba! bila kuonyesha mkataba wa nini.
Ni dhaifu kwasababu ni Ahmed huyo huyo aliyewahi sema kuwa mambo ya mkataba ni 11 na yameongezwa hadi 32 kwahiyo huo ulikuwa ukiukaji wa mkataba.
Sasa anaposema hivyo anarudi tena kuomba kuwa na muungano wa mkataba kwani nuu uliopo ni wa nini.

Nikuonyeshe udhaifu wa hali ya juu wa ndugu yangu Ahmed. Lini na wapi amewahi kuwaambia WZNZ
1.Manufaa au faida za muungano kabla hajawaambia hasara. Haiwezekani huu muungano usiwe na zuri hata moja. Nadhani hata akili yako inakataa hili jambo. Na kama muungano hauna zuri au jema kwanini tuwe na mkataba?

2. Nionyeshe wapi na lini Ahmed amewahi kutaja jambo moja tu la mkataba.
Sasa sisi Watanganyika tuna akili huwezi kutuambia 'simama twende' tuatakuuliza wapi, kufanya nini na kwanini kabla hatujaondoa mguu.Udhaifu wa Ahmed upande wa unguja asituletee huku kwasababu sisi tuna vichwa na tunavitumia.

Hadi atakapotaja jambo moja tu la mkataba ndipo tutaweza kumsikiliza, vinginevyo mktaba mwisho chumbe!
Tanganyika tuna uwezo mkubwa wa kutumia vichwa kufikiri na si kuimba.

Hapo ndipo udhaifu wa Ahmed unapokuja, kwamba ni mchochezi na mnafiki, huwezi kuwa na muungano mbaya usio na jema ili hali 350,000 wanaishi kwa muungano hu huo.
In fact huyu si dhaifu tu ni mnafiki mkubwa.
 
Barubaru,

..nakumbuka ktk moja ya post zako hapa JF uliandika kwamba Tanganyika na Zanzibar zimeungana "kimkataba" na siyo "kikatiba."

..sasa anapoibuka Mzanzibari mwenzako na kupendekeza "muungano wa mkataba" huoni kwamba analeta ubabaishaji??

..mimi nadhani wakati umefika kwa wa-Zanzibari wawe wazi ktk kile wanachokitaka, na pia kile wasichokitaka.

..ingependeza kama mngeweza kutueleza ktk huo mkataba mpya kati ya Tanganyika na Zanzibar mnataka mambo gani yawepo humo.

Jokakuu.

Kumbuka kuwa Muungano wenu ni wa Mkataba. Hilo halina ubishi.

Vile vile kila mtu ana mawazo yake binafsi kutokana na maono yake kuhusu huomuungano. Sio tu kwa WaZnz bali pia hata kwa Watanganyika. Kinachotakiwa nohoja mfikie muafaka na maamuzi sahihi. Pasitokee mtu kujiona ni superior kuliko mwingina katika kutoa mawazo hayo. Zishindanishwe hoja.

lakin la Mwishomimi siMznz wala Mtanzania. Mimi ni Mu Oman. huo ndio utaifa wangu na Avatar yangu imebainisha wazi na vazi langu la Taifa ninalolipenda na kuvaa kila siku nikiwa kazini na katika sharehe mbalimbali na hata muda wangu wa kawaida.

Vipi na nyie vazi lenu la Taifa limefikia wapi?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom