Ahadi za Rais Zinavyowatesa Mawaziri kwenye Bunge la Bajeti Nani wa Kulaumiwa?

Kingcobra

JF-Expert Member
Jan 28, 2011
1,000
309
Wakuu,

Kwa muda mrefu sasa, wabunge wengi wanapochangia hoja za mawaziri wanaowasilisha bajeti zao bungeni wamekuwa wakiwalaumu mawaziri kwa kutotekeleza ahadi za serikali kwenye majimbo yao. Wengine hutia uzito wa hoja zao kwa kukumbusha kwamba baadhi ya ahadi alitoa mkuu wa nchi kwa maana ya rais Dr. Jakaya Kikwete na wanawashangaa mawaziri kwa kukaidi kutekeleza ahadi za kiongozi mkuu wa nchi.

Ninachojiuliza ni je, hivi wa kulaumiwa ni nani, ni mawaziri au rais mwenyewe anayeahidi na kusahau palepale yaani baada ya hapo hafuatilii tena utekelezaji wake? Kama wa kumlaumu ni waziri, je, rais kabla ya kuahidi kuwa anawasiliana na mawaziri wake kabla ili ajiridhishe na uwezekano wa kutekelezaji anachokusudia kuahidi? Kama sivyo, kwa nini lawama zielekezwe kwa waziri na siyo rais mwenyewe. Tafadhali wataalam mtujuze hapa.
 
Kwa taarifa yako bado anaendelea kuahidi. Juzi alikuwa Mbeya ameahidi tena. Tehe tehe tehe eeeee!!!
 
Kweli JK ni kiboko anasema atatimiza ahadi zake zote zile 78 plus,sidhani kama ataweza hata nusu yake,anajisifia kwa hili zoezi la dar (ambalo msingi wake ni mwaka 2002) ,daraja kigamboni (bado ndoto) mradi wa maji mbeya (pesa ya wafadhili) mpango wa siku nyingi...na kiwanja ndege Songwe!hakuasisi yeye!!
JK amesahau viwanja vya ndege Tanzania nzima ameahidi kuviweka hadhi kimataifa hadi cha Mugumu....zile meli(anadai zinaunganishwa)...bado ndege ..hapo sitaki kwenda kwenye afya,shule,barabara na maji.....
 
Hakuna mawasiliano hapo kati ya Rais na mawaziri. Ni kama Sumatra na mamlaka ya hali ya hewa. Tumegundua kwa gharama kubwa ya uhai wa watu.
 
Kukubali uwaziri ni kukubali kumsaidia Rais kutekeleza ahadi anazotoa kwa wananchi. Kama mtu hataki "kuteseka" na ahadi za Rais asikubali uwaziri. Kuna msemo unasema "ukipenda boga,..."
 
Back
Top Bottom