Ahadi za Dkt. Philip Mpango ni pigo kwa Mafisadi

Kijogoodi

JF-Expert Member
Mar 29, 2021
1,363
2,372
Habari,

Akilihutubia bunge kwa mara mwisho mara baada ya kuteuliwa kuwa makamu wa Rais, Dr Philip Mpango ameahidi kuwa miradi yote iliyoachwa na hayati Rais Magufuli lazima ikamilishwe. Dr Mpango ameitaja miradi ya SGR, Bwawa la Nyerere, Maji ,Afya etc kuwa kukamilika kwa miradi hiyo ndiyo njia pekee ya kumuenzi kipenzi cha watanzania Dr. Magufuli, hivyo anaenda kutumia nguvu na uadilifu wote kuhakikisha miradi hiyo inakamilika.

My take:
Ahadi hii ya Dr Mpango ni pigo kubwa kwa mafisadi kwani kama ilivyokuwa 2015 kwa JPM, sasa hivi tena Chadema wako bize kumsifia, kumfundisha na kumpa maelekezo mbalimbali Rais Samia bila kujua kuwa huyo ni Rais anayetokana na CCM na anatekeleza ilani ya CCM.

Godbless Lema, Tundu Lisu hawazungumzii kabisa maendeleo ya Chadema wao ni bize kumpangia cha kufanya Rais Samia, hivyo kukamilika na kuzinduliwa kwa miradi hiyo itakuwa ni aibu kubwa sana kwa Chadema na mafisadi wote wasioitakia mema nchi yetu.

 
Ahadi za mwanasiasa
promises-e1443541498873.png
 
Wanazi wa ufipa wanashangilia wasichokijua. Uteuzi wa Dr. Mpango kuwa Makamu wa Rais maana yake ni kukamilisha ndoto ya MAGUFULI (RIP).
NB: Dr. Mpango aliibuliwa na Magufuli, tena kwa kuteuliwa na kuwa mbunge hatimaye akamteua kuwa waziri wa wizara nyeti kabisa ya Fedha kwa imani kubwa sana. Huyu ndiye mwendeleza maono ya MAGUFULI.
 
Ana ahidi kwani yeye ndie Raisi? So vikikamilika atakuwa amekamirisha Mpango au Mama Samia? aache ubazazi Kazi ni ya Mama now yeye ni Msaidizi tu aache Sifa.. Asiwe kama Anold Shwarzternegger Baada ya kuchaguliwa kuwa Govana wa Jimbo la Calfornia alijua ndio keshakuwa Raisi wa United States of America.
 
Hivi sisiem wamerogwa tukishangilia akifanya mambo mazuri yenye tija kwa taifa shida iki wapi? Taifa sio la sisiem na raisi ni wa nchi sio wa lumumba hata hio ilan ya ccm ikikamilishwa ndio vizuri zaidi kma kuna mazuri kwakua wanufaika n watnzania sisi kupiga kelele ni kuleta chachu na motivation kwa viongozi na kuwakosoa na kuwakumbusha. Acheni ushamba hatutakaa kimya kamwe kwakua hakuna mwenye hati miliki ya hii nchi.
 
Wanazi wa ufipa wanashangilia wasichokijua. Uteuzi wa Dr. Mpango kuwa Makamu wa Rais maana yake ni kukamilisha ndoto ya MAGUFULI (RIP).
NB: Dr. Mpango aliibuliwa na Magufuli, tena kwa kuteuliwa na kuwa mbunge hatimaye akamteua kuwa waziri wa wizara nyeti kabisa ya Fedha kwa imani kubwa sana. Huyu ndiye mwendeleza maono ya MAGUFULI.
Usiongelee usichokijua! Philip Mpango aliibuliwa na Jakaya Kikwete akiwa ameondoka kufanya kazi World Bank, akawa mshauri binafsi ya uchumi wa Kikwete

Sent from my VFD 301 using JamiiForums mobile app
 
Hivi sisiem wamerogwa tukishangilia akifanya mambo mazuri yenye tija kwa taifa shida iki wapi? Taifa sio la sisiem na raisi ni wa nchi sio wa lumumba hata hio ilan ya ccm ikikamilishwa ndio vizuri zaidi kma kuna mazuri kwakua wanufaika n watnzania sisi kupiga kelele ni kuleta chachu na motivation kwa viongozi na kuwakosoa na kuwakumbusha. Acheni ushamba hatutakaa kimya kamwe kwakua hakuna mwenye hati miliki ya hii nchi.
Mwambie Lisu afanye kazi za umakamu mwenyekiti wa chadema
 
Back
Top Bottom