Ahadi kumi (10) za mwana TANU na Tanzania yetu ya sasa

Mkuu genekai hebu mwache ZeMarcopolo niongee naye. Kwa bahati nzuri nina bundle zangu za kutosha leo na muda wa kubishana naye ZeMarcopolo ninao.





Context ya Kipindi cha Mtei ipo kama ifuatavyo. Wasomi walikuwa wachache kweli. Nyerere na Mtei wakiwapo katika kundi hili la wasomi wachache. Nyerere alikuwa mmoja katika Watanganyika wenye vipaji vya uongozi wakati huo. Lakini hakuwa peke yake mwenye kipaji.

Maelezo yako yenye mapungufu ni pamoja na haya: Kwamba Mtei aliona utawala wa mkoloni unavumilika. Haya ndiyo unayoyasema wewe ZeMarcopolo. Na kwamba kila pale taifa lilipomuhitaji alilitelekeza. Hali ya uchumi ilivyoyumba kutokana na vita ya Uganda akalitelekeza taifa tena.

Maelezo yako wewe ZeMarcopolo yanatuambia wasomaji wako kwamba hujui historia, hujui dhana ya ushindi katika vita hutegemea falsafa zipi.

Hakuna Mtanganyika aliyekubali kuwa ukoloni ulikuwa unavumilika. Wewe ZeMarcopolo huna ushahidi popote kuonesha kuwa Mtanganyika mmoja kwa jina la Edwin Mtei alitaka ukoloni uendelee. Kama unao ushahidi huo uweke hapa. Tukio la Mtei kufanya kazi katika Shirikia la Kimataifa haliwezi kuwa kigezo cha kuvumilia ukoloni kwa kuwa Shirika alilofanya kazi nalo malengo yake hayakuwa kuendeleza ukoloni. Malengo yake yalikuwa kusaidia kujenga mfumo wa kiuchumi ulio bora zaidi katika dunia. Na upo ushahidi kuwa malengo ya shirika hilo yanafanikiwa katika kila nchi inayofuata mfumo huu ambao umejitofautisha na mifumo mingine ambayo imekufa, ama imeshindwa kushindana vizuri na huo mfumo.

Tunamsifu Mwalimu Nyerere kwa mazuri aliyoyafanya. Tunafukia mabaya kwa sababu si akili nzuri kukuza madhaifu ya mtu mwenye mengi mazuri. Wewe unanilazimisha kujadili mabaya ya Nyerere ili nikuoneshe kuwa "withdrawal" katika eneo la utawala uambao unashindwa kukubaliana nao katika kila kitu si kukimbia vita. Withdrawal inawezekana kabisa ikawa tactical; ni sahihi kabisa mtu kuondoka eneo la mabishano ampatie mbishani wake nafasi ya kushindwa, ili wazo lake lipate nafasi ya pili na kuthibisha alikuwa na wazo bora zaidi.

Edwin Mtei ni mzalendo aliyekuwa na wazo zuri ambalo ndo hilo tunalitekeleza sasa. Pengine yeye binafsi atakuwa na maelezo tofauti na haya kuelezea sababu zake za kutoweka katika vipindi unavyovieleza, lakini ninachojua ni kwamba alifanya vizuri kumwacha Nyerere kutekeleza wazo lake ambalo halikuwa likikubalika na Mtei kwa asilimia zote, hadi pale lilipofikia kuonesha halikuwa wazo sahihi kwa asilimia 100.

Angalizo ni maneno haya: Tactical Withdrawal, na hii inaruhusiwa katika mazingira ya mabishano.

Kumbe wewe ndiye usiyejua historia. Hujui kuwa Edwin Mtei alikuwa mtumishi mtiifu wa serikali ya mkoloni.

Hujui kuwa Edwin Mtei alikataa kusaidia kazi za kuendeleza TANU. Na wala hujui kuwa machief wengi hawakuipenda TANU.

Kukubali serikali ya mkoloni sio lazima asimame jukwaani na kusema "jamani mimi naivumilia serikali ya mkoloni", kitendo cha yeye kutokushiriki shughuli yoyote ya kuondoa ukoloni na kuitumikia serikali ya mkoloni kwa utiifu ni kuikubali tosha.

HAKUNA jambo alilofanya Mzee Edwin Mtei kwa kujitolea. Kila alichokifanya alilipwa mshahara mnnono. Huo si uzalendo, ni kutafuta ajira tu kama jinsi mtanzania anavyoweza kwenda leo Afrika Kusini kutafuta kazi haimaanishi anaipenda Afrika Kusini.

Swala la Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kuwa na mapungufu yake haliwezi kuwa sababu tosha ya Mzee Mtei kulitelekeza Taifa. Inamaana Mzee Mtei alivumilia mapungufu ya Mwalimu mpaka siku nchi ilipopatwa na ugumu wa uchumi uliotokana na vita ndio akashindwa kuvumilia! Mtei alilitelekeza taifa, hakutaka elimu yake ilinufaishe taifa. Mzee Mtei ni mbinafsi wa kupindukia na historia ya maisha yake inadhihirisha hilo.

Ndio maana nawatahadharisha vijana kuwa chadema haijaanzishwa na mtu mwema kwa taifa na HAWEZI kuwa na malengo mema kwa taifa. Vijana msikubali kulaghaika...
 
Ikumbukwe pia kuwa Mzee Ediwn Mtei mwanzilishi wa chadema alikataa kushirikia katika harakati za TANU za kutafuta Uhuru wa Tanganyika. Alikuwa mtumishi mtiifu wa serikali ya wakoloni na aliona kupigania uhuru ni kuharibu utawala unaompa mshahara kila mwezi.

Kwahiyo kiufupi ni kwamba mwanzilishi wa chadema mzee Mtei aliona ahadi hizo za TANU hazina manufaa.

Je ukoloni haukuwa na faida/jema lolote? Ni nini tofauti ya kaburu mweusi na kaburu mweupe?

CCM mna wema/faida gani mliyoitenda nchi hii mpaka sasa? Mmeiharibu nchi kuliko Mwingereza na Mjerumani combined. shame on you, shame on ccm
 
Je ukoloni haukuwa na faida/jema lolote? Ni nini tofauti ya kaburu mweusi na kaburu mweupe?

CCM mna wema/faida gani mliyoitenda nchi hii mpaka sasa? Mmeiharibu nchi kuliko Mwingereza na Mjerumani combined. shame on you, shame on ccm

Mawazo yanafanana na ya Mzee Mtei kwa kuwa yeye aliona ukoloni una faida kwa sababu alipatiwa nyumba ya kuishi na mshahara mzuri. Lakini mnapaswa kufahamu kuwa heshima yako kama binadamu ina thamani kubwa kuliko nyumba na mshahara.

Ukoloni haukuwa na faida YOTOTE. Umeturudisha nyuma na ungeendelea kuturudisha nyuma sana iwapo mawazo kama ya Mtei yanesikilizwa.

Sasa hivi wananchi wanaamua wenyewe nani awe kiongozi wao. Kwa mfano wewe umeona CCM haifai, lakini mamilioni ya watanzania wameona inafaa na kuichagua. Kila miaka mitano tunaulizana tena nani anafaa. Hilo halipo kwenye serikali ya kikoloni.

Mfano mwingine unaposema shame on CCM. Hiyo ni faida ya kuwa katika nchi huru. Una utashi wa kuona kuwa CCM haifai, ungekuwa chini ya mkoloni usingefikiria hata hivyo. Ndio maana kauli yako ya shame on CCm inapendwa na wapenda nchi kwa sababu CCM iliruhusu mfumo wa vyama vingi ili watu kama wewe wajisikie huru zaidi katika nchi yao. Kwahiyo kauli yako hiyo ni matunda ya maamuzi ya CCM ambayo imeweza kuwepo kwa sababu nchi iko huru.
 
Watu wengine bana, badala ya kujadili uzi uliowekwa hapa kuhusu ahadi za TANU na kama CCM iliyozirithi inaziamini na kuzitekeleza, watu wanajadili mtu....Mtei. You people discuss IDEAS not individuals.

Binafsi naamini tungetekeleza kwa vitendo ahadi no 5 peke yake kwa asilimia hamsini tu, tungekuwa hatushikiki. Hii ni kwa wote bila kujali itikadi zetu.
 
Watu wengine bana, badala ya kujadili uzi uliowekwa hapa kuhusu ahadi za TANU na kama CCM iliyozirithi inaziamini na kuzitekeleza, watu wanajadili mtu....Mtei. You people discuss IDEAS not individuals.

Binafsi naamini tungetekeleza kwa vitendo ahadi no 5 peke yake kwa asilimia hamsini tu, tungekuwa hatushikiki. Hii ni kwa wote bila kujali itikadi zetu.

Mkuu.
Umenena kweli! Kuna watu humu jukwaani kazi yao ni kukwepesha mada kwa maslahi binafsi ili kile kilichopo kisijadiliwe, usipo kuwa makini ukidondookea kwenye mtego wao unajikuta mada nzima haina maana tena.

Wadau rudini kwenye mada iliyoko hewani.
 
Watu wengine bana, badala ya kujadili uzi uliowekwa hapa kuhusu ahadi za TANU na kama CCM iliyozirithi inaziamini na kuzitekeleza, watu wanajadili mtu....Mtei. You people discuss IDEAS not individuals.

Binafsi naamini tungetekeleza kwa vitendo ahadi no 5 peke yake kwa asilimia hamsini tu, tungekuwa hatushikiki. Hii ni kwa wote bila kujali itikadi zetu.
 
Mkuu.
Umenena kweli! Kuna watu humu jukwaani kazi yao ni kukwepesha mada kwa maslahi binafsi ili kile kilichopo kisijadiliwe, usipo kuwa makini ukidondookea kwenye mtego wao unajikuta mada nzima haina maana tena.

Wadau rudini kwenye mada iliyoko hewani.

Mkuu Mtoi, tuwasamehe hawa watu kwakuwa hawajui wanachotenda. Na ndiyo wanaoturudisha nyuma kifikra na kimaendeleo
 
Kumbe wewe ndiye usiyejua historia. Hujui kuwa Edwin Mtei alikuwa mtumishi mtiifu wa serikali ya mkoloni.

Hujui kuwa Edwin Mtei alikataa kusaidia kazi za kuendeleza TANU. Na wala hujui kuwa machief wengi hawakuipenda TANU.

Kukubali serikali ya mkoloni sio lazima asimame jukwaani na kusema "jamani mimi naivumilia serikali ya mkoloni", kitendo cha yeye kutokushiriki shughuli yoyote ya kuondoa ukoloni na kuitumikia serikali ya mkoloni kwa utiifu ni kuikubali tosha.

HAKUNA jambo alilofanya Mzee Edwin Mtei kwa kujitolea. Kila alichokifanya alilipwa mshahara mnnono. Huo si uzalendo, ni kutafuta ajira tu kama jinsi mtanzania anavyoweza kwenda leo Afrika Kusini kutafuta kazi haimaanishi anaipenda Afrika Kusini.

Swala la Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kuwa na mapungufu yake haliwezi kuwa sababu tosha ya Mzee Mtei kulitelekeza Taifa. Inamaana Mzee Mtei alivumilia mapungufu ya Mwalimu mpaka siku nchi ilipopatwa na ugumu wa uchumi uliotokana na vita ndio akashindwa kuvumilia! Mtei alilitelekeza taifa, hakutaka elimu yake ilinufaishe taifa. Mzee Mtei ni mbinafsi wa kupindukia na historia ya maisha yake inadhihirisha hilo.

Ndio maana nawatahadharisha vijana kuwa chadema haijaanzishwa na mtu mwema kwa taifa na HAWEZI kuwa na malengo mema kwa taifa. Vijana msikubali kulaghaika...


Ukiongea sana lazima utajichanganya tu!

Ushahidi huu hapa. Wewe ZeMarcopolo umeongea mno humu JF leo umeanza kujichanganya mwenyewe. Hoja yangu umeanza kuifanya ya kwako. Mtei hakuwapenda wakoloni. Na wewe mwenyewe unakubali Edwin Mtei hakuwapenda wakoloni. Soma haya maneno yako mwenyewe: ni kutafuta ajira tu kama jinsi mtanzania anavyoweza kwenda leo Afrika Kusini kutafuta kazi haimaanishi anaipenda Afrika Kusini. Unaona sasa...kumbe Mtei alipokwenda kufanya kazi nje ya nchi alikwenda kufuata ajira tu.

Jamani ee, kumbe huyu ZeMarcopolo kuna siku na yeye anajuaga point iko wapi! Kuhusu kufanya kazi yenye mshahara mnono, sioni ubaya wa mtu yeyote kufanya kazi yenye ujira mzuri. Utakuwa mpumbavu kushabikia sera inayotaka ufanye kazi yenye mshahara mdogo hadi unashindwa kusomesha watoto. Tufanye wewe ZeMarcopolo unaona ni kitu cha fahari saaaana, na uzalendo saaaana, unaposikia Katibu Mkuu Kiongozi aliyeitwa Apiyo anaishi Gongo la Mboto kwenye Nyumba mbovu ambayo alishindwa kuimaliza kwa sababu alikubaliana saaana na Nyerere? We unaona hiyo ni akili sana ee?

Kwa hiyo kipimo chako cha uzalendo wewe ZeMarcopolo ni hizi taarifa unaposikia Mkuu wa Majeshi mstaafu akiitwa Gen. Sarakikya anapewa Pensheni ya dola 25 kwa mwezi. Huo ndo uzalendo eti? Kajipange vizuri urudi kubishana na mimi
 
Ukiongea sana lazima utajichanganya tu!

Ushahidi huu hapa. Wewe ZeMarcopolo umeongea mno humu JF leo umeanza kujichanganya mwenyewe. Hoja yangu umeanza kuifanya ya kwako. Mtei hakuwapenda wakoloni. Na wewe mwenyewe unakubali Edwin Mtei hakuwapenda wakoloni. Soma haya maneno yako mwenyewe: ni kutafuta ajira tu kama jinsi mtanzania anavyoweza kwenda leo Afrika Kusini kutafuta kazi haimaanishi anaipenda Afrika Kusini. Unaona sasa...kumbe Mtei alipokwenda kufanya kazi nje ya nchi alikwenda kufuata ajira tu.

Jamani ee, kumbe huyu ZeMarcopolo kuna siku na yeye anajuaga point iko wapi! Kuhusu kufanya kazi yenye mshahara mnono, sioni ubaya wa mtu yeyote kufanya kazi yenye ujira mzuri. Utakuwa mpumbavu kushabikia sera inayotaka ufanye kazi yenye mshahara mdogo hadi unashindwa kusomesha watoto. Tufanye wewe ZeMarcopolo unaona ni kitu cha fahari saaaana, na uzalendo saaaana, unaposikia Katibu Mkuu Kiongozi aliyeitwa Apiyo anaishi Gongo la Mboto kwenye Nyumba mbovu ambayo alishindwa kuimaliza kwa sababu alikubaliana saaana na Nyerere? We unaona hiyo ni akili sana ee?

Kwa hiyo kipimo chako cha uzalendo wewe ZeMarcopolo ni hizi taarifa unaposikia Mkuu wa Majeshi mstaafu akiitwa Gen. Sarakikya anapewa Pensheni ya dola 25 kwa mwezi. Huo ndo uzalendo eti? Kajipange vizuri urudi kubishana na mimi

Umeshindwa kuelewa kuwa kuhusu ajira sizungumzii kazi za nje ya nchi. Nasema Mtei hajajitolea kujenga nchi ila aliajiriwa na serikali ya Tanzania kama jinsi ambavyo angeweza kuajiriwa sehemu nyingine duniani. Je, una kitu chochote unachojua Mtei kaisaidia taifa zaidi ya yeye kuajiriwa na kulipwa mshahara mnono?

Hakuna mtu anayeunga mkono watu kulipwa pesa ndogo lakini kulitekeleza taifa baada ya uchumi kulegezwa na vita vya Uganda ni kitendo kibaya sana alichofanya Mtei. Mtei hakuwahi kulisaidia taifa na sasa anawalaghai vijana kupitia chama chake cha chadema ili ajinufaishe zaidi.

Kama una ushahidi wa jambo lolote ambalo Mtei amelisaidia taifa lilete tujadili.
 
Umeshindwa kuelewa kuwa kuhusu ajira sizungumzii kazi za nje ya nchi. Nasema Mtei hajajitolea kujenga nchi ila aliajiriwa na serikali ya Tanzania kama jinsi ambavyo angeweza kuajiriwa sehemu nyingine duniani. Je, una kitu chochote unachojua Mtei kaisaidia taifa zaidi ya yeye kuajiriwa na kulipwa mshahara mnono?

Najua Mtei ametunza siri nyingi sana za taifa hili. Hakuna uzalendo mkubwa kushinda hulka hiyo. Wewe niambie ukosefu wa uzalendo katika maisha ya Mtanzania huyu anaoujua.
 
CHADEMA ni chama cha MABEPALI hakina MALENGO mazuri na nchi hii, kama watu wanbisha waajaribu kuionja sumu hii waone matumbo yatakavyovimba.
 
Najua Mtei ametunza siri nyingi sana za taifa hili. Hakuna uzalendo mkubwa kushinda hulka hiyo. Wewe niambie ukosefu wa uzalendo katika maisha ya Mtanzania huyu anaoujua.

Mtu yeyote aliyefanya kazi katika nafasi kubwa kama Gavana na Waziri lazima anakuwa na siri. Na ni AIBU kwa mtu aliyekuwa kijana msomi katika kipindi ambacho nchi inapigania uhuru kusema kuwa mchango wake yeye ni kutunza siri!!!
Kwa lugha nyepesi mchango wa Mtei ni SIFURI. Yeye amechuma zaidi kutoka kwenye nchi kama muajiriwa tu na hakuwa tayari kujitolea pale hali ilipohitaji.

Aliona harakati za kupigania Uhuru kuwa ni kero kwa ajira yake akiwa kama mtumishi wa serikali ya mkoloni mwingereza.

Mtei ameshindwa hata na baadhi waingereza waliojitolea kumsaidia mwalimu kuorganise nchi baada ya uhuru.

Huyo ndio muasisi wa chadema na hivi karibuni amekuwa akitoa kauli za kutia AIBU zaidi mpaka chama chake kinajitenga na kauli hizo.
 
Mkuu Highlander, Mtei hasafishiki na kadiri unavyozidi kuyatetea maovu yake ndivyo unavyozidi kumuumbua.

Mtei ni msaliti kama ilivyo CHADEMA yake.
 
Last edited by a moderator:
CHADEMA ni chama cha MABEPALI hakina MALENGO mazuri na nchi hii, kama watu wanbisha waajaribu kuionja sumu hii waone matumbo yatakavyovimba.

Niupofu au ni kuvaa viatu visivyo tosha! Angalia kwa makini mada inaelezea nini!

Mmeona hamna pa kutokea?!
 
Mtu yeyote aliyefanya kazi katika nafasi kubwa kama Gavana na Waziri lazima anakuwa na siri. Na ni AIBU kwa mtu aliyekuwa kijana msomi katika kipindi ambacho nchi inapigania uhuru kusema kuwa mchango wake yeye ni kutunza siri!!!
Kwa lugha nyepesi mchango wa Mtei ni SIFURI. Yeye amechuma zaidi kutoka kwenye nchi kama muajiriwa tu na hakuwa tayari kujitolea pale hali ilipohitaji.

Aliona harakati za kupigania Uhuru kuwa ni kero kwa ajira yake akiwa kama mtumishi wa serikali ya mkoloni mwingereza.

Mtei ameshindwa hata na baadhi waingereza waliojitolea kumsaidia mwalimu kuorganise nchi baada ya uhuru.

Huyo ndio muasisi wa chadema na hivi karibuni amekuwa akitoa kauli za kutia AIBU zaidi mpaka chama chake kinajitenga na kauli hizo.

Tatizo lako wewe ZeMarcopolo ni hulka yako ya kurahisisha mambo kwa uchambuzi wa lugha nyepesi. Jifunze kutofautisha mijadala ya vijiwe vya gahwa na mijadala inayohusu mustakabali wa maendeleo ya taifa kubwa kama Tanzania. Hii nchi haiwezi kupelekwa mbele kwa fikra nyepesi kama hizi za lugha nyepesi za kina ZeMarcopolo. Jifunze kufikiri kwa kina.

Jina Edwin Mtei ni jina la mtu wa Kimataifa. Mtu anayeitazama Tanzania katika context ya kuiweka nchi yetu katika uchumi wa Kimataifa. Na hilo haliwezi kuelezeka kwa lugha nyepesi nyepesi kama za kwako.

WanaCCM wenzio wanamjua vizuri Edwin Mtei; ndio maana wameendelea kumpa nafasi kuwashauri katika Bodi ya Kahawa ya Taifa, pamoja na kuwa muasisi wa chama cha siasa shindani, lakini pia pamoja na kuwa na umri mkubwa sana. Kawaulize wanaCCM wanzio wanaendelea kuona nini kizuri katika maisha ya Mtanzania huyu kuendelea kutumia akili yake. Kajipange vizuri urudi kubishana na mimi.
 
Tatizo lako wewe ZeMarcopolo ni hulka yako ya kurahisisha mambo kwa uchambuzi wa lugha nyepesi. Jifunze kutofautisha mijadala ya vijiwe vya gahwa na mijadala inayohusu mustakabali wa maendeleo ya taifa kubwa kama Tanzania. Hii nchi haiwezi kupelekwa mbele kwa fikra nyepesi kama hizi za lugha nyepesi za kina ZeMarcopolo. Jifunze kufikiri kwa kina.

Jina Edwin Mtei ni jina la mtu wa Kimataifa. Mtu anayeitazama Tanzania katika context ya kuiweka nchi yetu katika uchumi wa Kimataifa. Na hilo haliwezi kuelezeka kwa lugha nyepesi nyepesi kama za kwako.

WanaCCM wenzio wanamjua vizuri Edwin Mtei; ndio maana wameendelea kumpa nafasi kuwashauri katika Bodi ya Kahawa ya Taifa, pamoja na kuwa muasisi wa chama cha siasa shindani, lakini pia pamoja na kuwa na umri mkubwa sana. Kawaulize wanaCCM wanzio wanaendelea kuona nini kizuri katika maisha ya Mtanzania huyu kuendelea kutumia akili yake. Kajipange vizuri urudi kubishana na mimi.


Tatizo lako unachanganya mambo.

Ukisoma vizuri utaelewa ninayoandika.

Hakuna sehemu niliposema Mtei sio mtaalam mzuri. Nimesema again and again na ninarudia kwamba Mtei ni MSOMI na ni mtaalam mzuri wa kiwanbgo cha kimataifa.

Ninachomlaumu Mtei ni kuwa mchoyo wa kuutumia utaalamu wake kwa maslahi ya taifa. Yeye kila alilofanya alitaka alipwe pesa kama yuko sokoni. Hakutofautisha kuitumikia Tanganyika/Tanzania na kuitumikia Afrika Kusini kwake yeye mshiko mbele.

Tabia yake hii ya kutanguliza pesa mbele ndio ilimfanya akatae kushiriki shughuli za TANU kwa sababu shughuli za TANU zilikuwa za kujitolea. Vilevile uchumi wa nchi ulivyoyumba Mwalimu aliomba watumishi wote wa umma na wananchi kiujumla "wafunge mikanda". Mtei akaona kufanya kazi serikali haina faida. Akalitelekeza taifa.

Mtei alikuwa kijana msomi kipindi ambacho wasomi walikuwa wanahitajika sana lakini yeye usomi wake alihakikisha unamfaa yeye tu. Hakuna kazi aliyofanya ya kujitolea/ Tulimlipa pesa stahiki kwa kila anachofanya. Yaani hakuna tofauti na kama tungemwajiri mtaalamu toka Burundi.

Ngoja nikupe mfano rahisi: Chukulia wewe unafanya harusi Mdogo wako ambaye ni mtaalam wa mapambo anakuja kupamba. Unamlipa pesa halisi ya wapambaji wanavyolipwa. Halafu mdogo wako huyo hatoi mchango mwingine wowote na anajitamba kuwa amekusaidia kwenye harusi. Je, mdogo wako huyo anakuwa amekusaidia au wewe ndio umemsaidia? Tanzania ni kama kaka mwenye harusi na Mtei ndio mpambaji ambaye hajatoa mchango wowote zaidi ya kupamba na kulipwa pesa stahiki.
 
Je ukoloni haukuwa na faida/jema lolote? Ni nini tofauti ya kaburu mweusi na kaburu mweupe?

CCM mna wema/faida gani mliyoitenda nchi hii mpaka sasa? Mmeiharibu nchi kuliko Mwingereza na Mjerumani combined. shame on you, shame on ccm
Wewe nawe bora tu bora unyamaze kama hujui historia ya Tanganyika/Tanzania. Huu uharo wako ni afadhari ukaumwage kwenye kikao cha BAVICHA ambako ndiko watakuelewa kwa kuwa kwao TRASH WORDS is a wise words.
 
Tatizo lako unachanganya mambo.

Ukisoma vizuri utaelewa ninayoandika.

Hakuna sehemu niliposema Mtei sio mtaalam mzuri. Nimesema again and again na ninarudia kwamba Mtei ni MSOMI na ni mtaalam mzuri wa kiwanbgo cha kimataifa.

Ninachomlaumu Mtei ni kuwa mchoyo wa kuutumia utaalamu wake kwa maslahi ya taifa. Yeye kila alilofanya alitaka alipwe pesa kama yuko sokoni. Hakutofautisha kuitumikia Tanganyika/Tanzania na kuitumikia Afrika Kusini kwake yeye mshiko mbele.

Tabia yake hii ya kutanguliza pesa mbele ndio ilimfanya akatae kushiriki shughuli za TANU kwa sababu shughuli za TANU zilikuwa za kujitolea. Vilevile uchumi wa nchi ulivyoyumba Mwalimu aliomba watumishi wote wa umma na wananchi kiujumla "wafunge mikanda". Mtei akaona kufanya kazi serikali haina faida. Akalitelekeza taifa.

Mtei alikuwa kijana msomi kipindi ambacho wasomi walikuwa wanahitajika sana lakini yeye usomi wake alihakikisha unamfaa yeye tu. Hakuna kazi aliyofanya ya kujitolea/ Tulimlipa pesa stahiki kwa kila anachofanya. Yaani hakuna tofauti na kama tungemwajiri mtaalamu toka Burundi.

Mungu wangu eee...bado unaendelea kujichanganya. Wasomi mchango wao huo ni wa mawazo. Siku hizi wanaita consultancy. Michango ya aina hii huwezi kuonesha rundo la kazi kama fundi seremala anavyoweza kuonesha rundo la maranda ujue kafanya kazi. Mtei hana rundo la Maranda kuonesha kafanya lipi. Lakini pamoja na kazi yake kuwa ya kitaalam, bado naweza kukuonesha kitu kafanya.

Hii kauli uliyoibandika hapa ni ya uongo: Kwamba "usomi wake alihakikisha unamfaa yeye tu." Design ya mfumo wa kodi mpya kafanya mtei na kamati yake wakati wa Mwinyi. Matunda yake tunayaona. Kwenye bodi ya Kahawa ameweka mawazo mazuri mengi kuboresha zao hili, likiwapo la matumizi ya miche ya kisasa, ambapo mawazo na mitizamo mingine anafundisha watu kwa matendo badala ya maneno au maandiko. Mtei analo shamba la kahawa la mfano watu wakajifunze kwake kwa matendo.

Wewe ZeMarcopolo hujui kitu kuhusu Mtei.

Chadema kilipoanza 1992/93 Mtei alikusanya Watanzania wenzake kutoka karibu kona zote za Tanzania kuanzisha chama pale Kisutu. Ni mtu aliyekubalika na Watanzania wenzake wa wakati huo, akaweka mchango wa mawazo uliokubalika kikazaliwa chama makini. Nimetaja mchango wake katika Tume ya kubadili mfumo wetu wa kodi kuleta huu tunaoutumia sasa, nimetaja mchango wake katika bodi ya Kahawa hadi siku za hivi karibuni (sijui kama bado yupo humo wiki hii) na uasisi wake wa chama makini; lengo langu ni kufuta fikra zako potofu kuwa elimu yake imemsaidi yeye binafsi. Elimu yake imelisaidia taifa letu. Wasomi hufanya kazi ya kushauri. Kazi ya kushauri ameifanya vizuri katika maisha yake kwa faida ya Watanzania wote.

Kajipange vizuri urudi kubishana na mimi.
 
Mkuu Mtoi, tuwasamehe hawa watu kwakuwa hawajui wanachotenda. Na ndiyo wanaoturudisha nyuma kifikra na kimaendeleo
Bandiko lako halina mantiki yoyote zaidi ya EMPTY RHETORIC. Watu wasiojua watakurudishaje nyuma wewe mwenye uelewe kama siyo kuwa na wewe huna uelewa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom