BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,005
Aggreko yakwepa kodi 10bn/-
Gloria Tesha
Daily News; Saturday,December 06, 2008 @00:02
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imezuia kwa kuweka makufuli katika lango la kampuni ya kufua umeme ya Aggreko Dar es Salaam jana, baada ya kuwapo taarifa inahamisha kinyemela mitambo yake na kuipeleka nje ya nchi, kwa lengo la kukwepa kulipa deni la Sh bilioni 10 inalodaiwa na mamlaka hiyo.
Kwa mujibu wa taarifa zilizolifikia gazeti hili kutoka chanzo cha habari ndani ya TRA juzi na jana, zilidai kuwa Aggreko inadaiwa Sh 10,117,558,321 ikiwa ni deni la kodi ya miaka mitatu ya uzalishaji umeme nchini. TRA ilithibitisha Aggreko kudaiwa deni ingawa hawakuwa tayari kusema ni kiasi gani, kwa kuwa ni mkataba wa siri kati yake kampuni hiyo ambayo wanaitambua kama mlipakodi wao.
Tangu wameingia hapa nchini hawa wawekezaji ambao waliitwa kutokana na dharura iliyolikumba taifa kipindi cha nyuma, hawajawahi kulipa kodi, na tumefanya nao mikutano bila mafanikio, tumewaletea taarifa za maandishi, hawajaonyesha kujibu, kilisema chanzo chetu cha habari.
Katika eneo la tukio jana, tafrani ilizuka wakati maofisa wa TRA pamoja na wa Kampuni ya Majembe Auction Mart, walipofika wakiwa katika magari ya kawaida na kuwaamuru walinzi wafungue mlango mkuu wa kuingia ilipo mitambo hiyo.
Kutokuelewana kulianza pale walipogundua kuwa ni maofisa wa TRA na wanahitaji Mkuu wa eneo ili waamuru wafanyakazi wake watoke ndani, kwani mtambo huo unafungwa hadi deni hilo litakapolipwa; ndipo walinzi walipotaka kuwatoa kwa nguvu maofisa na wanahabari, jambo lililozua zogo bila mafanikio ya kuwaondoa.
Mpelelezi Msaidizi wa TRA aliyekuwa eneo la tukio, Kalist Lyimo aliwaambia waandishi wa habari kuwa TRA imekuwa ikiidai Aggreko deni kubwa (bila kutaja kiasi) la miaka mitatu kuanzia mwaka 2006 na hatua ya kufunga ofisi za mtambo huo ni kuzuia mtambo wowote kutoka nje ya hapo mpaka deni lilipwe.
Alisema hatua hiyo imefanyika baada muda wa kulipa fedha hiyo waliokubaliana katika mkataba kumalizika tangu Novemba 26, mwaka huu na pia baada ya kupata taarifa kwamba baadhi ya mitambo inahamishwa kinyemela usiku kwenda nje ya nchi (hakutaja sehemu).
Aidha, Msimamizi Mkuu wa Uendeshaji wa kampuni ya Aggreko Kituo cha Ubungo Maziwa, Dar es Salaam, Shaughen Tyreman alipotakiwa kutoa ufafanuzi kuhusu deni hilo, aligoma kusema kwa kisingizio kuwa si msemaji, ila alikiri mitambo inafunguliwa tayari kusafirishwa kwenda Dubai.
Juhudi za waandishi katika eneo la tukio zilifanikiwa kusoma waraka wa agizo lililoitaka Aggreko ikubali deni na kuondoka katika mtambo huo likionyesha kampuni hiyo inadaiwa Sh bilioni 10.11. Sina neno la kusema kuhusu suala hilo, ondokeni ondokeni eneo hili ni la hatari kwenu tafadhali, mimi si msemaji, hapa tunafungua mitambo tunaipeleka Dubai, ni hatari kwenu, ondokeni , alisikika akimaka msimamizi kuyo.
Baadhi ya wafanyakazi wa kampuni hiyo walikumbwa na mshangao na kushindwa kuendelea kufungua mitambo hiyo na walipoulizwa, walisema hawakuwa na taarifa zozote za ujio wa TRA na wanachofahamu ni kwamba Aggreko imekuwa ikiwalipa mishahara yao bila matatizo na wanastaajabu kama kweli deni hilo wanadaiwa au wapo wakubwa wanaohusika.
Akizungumza na wanahabari ofisini kwake, msemaji wa TRA ambaye pia ni Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Walipa Kodi, Protas Mmanda alithibitisha mamlaka hiyo kuchukua hatua hiyo baada ya muda wa kulipa deni kupita. Muda ulishapita wa wao kulipa tangu Novemba mwaka huu na wanataka kuondoka, lakini bado tunamdai kodi, tulishawapa taarifa mara mbili hii ya tatu, lakini hawajachukua hatua yoyote, alisema Mmanda.
Hata hivyo, alisema wanaifahamu Aggreko kama mlipa kodi wao na kama alishindwa kulikuwa na hatua ambazo alipaswa kuchukua kama vile kupeleka malalamiko kwa Kamishna endapo aliona deni hawezi kulipa ili utaratibu mwingine ufanyike, lakini siyo kuanza kufungua mitambo na kuondoka. Meneja Mawasiliano wa Tanesco, Badra Masoud aliliambia gazeti hili jana kuhusu tukio hilo kuwa shirika hilo lilikwishamaliza mkataba na kampuni hiyo na kwamba halihusiki kwa namna yoyote na deni hilo.
Aidha, wakazi wa Ubungo Maziwa, waliokuja eneo la tukio kushuhudia zoezi hilo waliieleza HabariLeo kwa nyakati tofauti kuwa wanashuhudia mitambo ikihamishwa usiku kwa magari makubwa, lakini walikuwa hawajui kinachoendelea. Aggreko ni miongoni mwa kampuni zilizoingia nchini mwaka juzi kutokana na tatizo la umeme lililoikumba taifa na kutakiwa kufua umeme wa dharura wa megawati 40. Hata hivyo, serikali ilishasitisha mkataba wa kuzalisha umeme huo wa dharura kupitia Shirika la Umeme la Tanesco tangu Novemba mwaka huu.
Gloria Tesha
Daily News; Saturday,December 06, 2008 @00:02
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imezuia kwa kuweka makufuli katika lango la kampuni ya kufua umeme ya Aggreko Dar es Salaam jana, baada ya kuwapo taarifa inahamisha kinyemela mitambo yake na kuipeleka nje ya nchi, kwa lengo la kukwepa kulipa deni la Sh bilioni 10 inalodaiwa na mamlaka hiyo.
Kwa mujibu wa taarifa zilizolifikia gazeti hili kutoka chanzo cha habari ndani ya TRA juzi na jana, zilidai kuwa Aggreko inadaiwa Sh 10,117,558,321 ikiwa ni deni la kodi ya miaka mitatu ya uzalishaji umeme nchini. TRA ilithibitisha Aggreko kudaiwa deni ingawa hawakuwa tayari kusema ni kiasi gani, kwa kuwa ni mkataba wa siri kati yake kampuni hiyo ambayo wanaitambua kama mlipakodi wao.
Tangu wameingia hapa nchini hawa wawekezaji ambao waliitwa kutokana na dharura iliyolikumba taifa kipindi cha nyuma, hawajawahi kulipa kodi, na tumefanya nao mikutano bila mafanikio, tumewaletea taarifa za maandishi, hawajaonyesha kujibu, kilisema chanzo chetu cha habari.
Katika eneo la tukio jana, tafrani ilizuka wakati maofisa wa TRA pamoja na wa Kampuni ya Majembe Auction Mart, walipofika wakiwa katika magari ya kawaida na kuwaamuru walinzi wafungue mlango mkuu wa kuingia ilipo mitambo hiyo.
Kutokuelewana kulianza pale walipogundua kuwa ni maofisa wa TRA na wanahitaji Mkuu wa eneo ili waamuru wafanyakazi wake watoke ndani, kwani mtambo huo unafungwa hadi deni hilo litakapolipwa; ndipo walinzi walipotaka kuwatoa kwa nguvu maofisa na wanahabari, jambo lililozua zogo bila mafanikio ya kuwaondoa.
Mpelelezi Msaidizi wa TRA aliyekuwa eneo la tukio, Kalist Lyimo aliwaambia waandishi wa habari kuwa TRA imekuwa ikiidai Aggreko deni kubwa (bila kutaja kiasi) la miaka mitatu kuanzia mwaka 2006 na hatua ya kufunga ofisi za mtambo huo ni kuzuia mtambo wowote kutoka nje ya hapo mpaka deni lilipwe.
Alisema hatua hiyo imefanyika baada muda wa kulipa fedha hiyo waliokubaliana katika mkataba kumalizika tangu Novemba 26, mwaka huu na pia baada ya kupata taarifa kwamba baadhi ya mitambo inahamishwa kinyemela usiku kwenda nje ya nchi (hakutaja sehemu).
Aidha, Msimamizi Mkuu wa Uendeshaji wa kampuni ya Aggreko Kituo cha Ubungo Maziwa, Dar es Salaam, Shaughen Tyreman alipotakiwa kutoa ufafanuzi kuhusu deni hilo, aligoma kusema kwa kisingizio kuwa si msemaji, ila alikiri mitambo inafunguliwa tayari kusafirishwa kwenda Dubai.
Juhudi za waandishi katika eneo la tukio zilifanikiwa kusoma waraka wa agizo lililoitaka Aggreko ikubali deni na kuondoka katika mtambo huo likionyesha kampuni hiyo inadaiwa Sh bilioni 10.11. Sina neno la kusema kuhusu suala hilo, ondokeni ondokeni eneo hili ni la hatari kwenu tafadhali, mimi si msemaji, hapa tunafungua mitambo tunaipeleka Dubai, ni hatari kwenu, ondokeni , alisikika akimaka msimamizi kuyo.
Baadhi ya wafanyakazi wa kampuni hiyo walikumbwa na mshangao na kushindwa kuendelea kufungua mitambo hiyo na walipoulizwa, walisema hawakuwa na taarifa zozote za ujio wa TRA na wanachofahamu ni kwamba Aggreko imekuwa ikiwalipa mishahara yao bila matatizo na wanastaajabu kama kweli deni hilo wanadaiwa au wapo wakubwa wanaohusika.
Akizungumza na wanahabari ofisini kwake, msemaji wa TRA ambaye pia ni Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Walipa Kodi, Protas Mmanda alithibitisha mamlaka hiyo kuchukua hatua hiyo baada ya muda wa kulipa deni kupita. Muda ulishapita wa wao kulipa tangu Novemba mwaka huu na wanataka kuondoka, lakini bado tunamdai kodi, tulishawapa taarifa mara mbili hii ya tatu, lakini hawajachukua hatua yoyote, alisema Mmanda.
Hata hivyo, alisema wanaifahamu Aggreko kama mlipa kodi wao na kama alishindwa kulikuwa na hatua ambazo alipaswa kuchukua kama vile kupeleka malalamiko kwa Kamishna endapo aliona deni hawezi kulipa ili utaratibu mwingine ufanyike, lakini siyo kuanza kufungua mitambo na kuondoka. Meneja Mawasiliano wa Tanesco, Badra Masoud aliliambia gazeti hili jana kuhusu tukio hilo kuwa shirika hilo lilikwishamaliza mkataba na kampuni hiyo na kwamba halihusiki kwa namna yoyote na deni hilo.
Aidha, wakazi wa Ubungo Maziwa, waliokuja eneo la tukio kushuhudia zoezi hilo waliieleza HabariLeo kwa nyakati tofauti kuwa wanashuhudia mitambo ikihamishwa usiku kwa magari makubwa, lakini walikuwa hawajui kinachoendelea. Aggreko ni miongoni mwa kampuni zilizoingia nchini mwaka juzi kutokana na tatizo la umeme lililoikumba taifa na kutakiwa kufua umeme wa dharura wa megawati 40. Hata hivyo, serikali ilishasitisha mkataba wa kuzalisha umeme huo wa dharura kupitia Shirika la Umeme la Tanesco tangu Novemba mwaka huu.