Agenda za kidini Bungeni ..... Iko haja ya kuzizuia au zitengewe muda?

KipimaPembe

JF-Expert Member
Aug 5, 2007
1,285
696
Jamani kuna trend imeanza kujitokeza hivi karibuni kwa mambo ya kidini kuingia Bungeni. Sheria ya nchi inazuia kuanzishwa kwa vyama vya siasa vyenye mrengo wa kidini. Pamoja na kuwa wanasiasa wana dini, lakini kuifanya dini agenda ya kisiasa, ni sawa na kuanzisha chama chenye mrengo wa kidini.
  1. Je, iko haja ya spika kuzuia mijadara yenye mwelekeo wa kidini Bungeni au mijadara ya dini iwekewe muda wake kama ilivyo bajeti?
  2. Ikiwa wabunge wanaweza kujadili mambo yenye mrengo wa kidini bungeni, iko haja viruhusiwe vyama vya kisiasa vyenye mrengo wa kidini ili wakati wa uchaguzi tuwe tunajua kuwa huyu tukimchagua ataenda kutetea dini yetu?
  3. Iko haja ya kutoa nafasi za ubunge kwa dini zetu ili wenye utaalam wa masuala ya dini waende kuzisemea dini zao bungeni?
  4. Je bungeni ni mahali muafaka pa kutetea maslahi ya dini? Wabunge huo uwezo wamepewa na nani?
  5. Je iko haja wabunge wawe wanaleta na hoja za kidini wakati wa uchaguzi ili tujue kuwa bungeni wataenda kutetea maslahi ya dini zetu vile vile?
Nimeamua kuanzisha thread hii ili tujadiri hili tatizo la wabunge waliochaguliwa kwa hoja za kimaendeleo wanapoingia bungeni kuanza kudandia mambo ya dini ili tu kujipatia umaarufu.
 
Majibu ya Maswali haya yapo kwa CCM na kama ndio Amani wao ndio wanaweza kufanya taifa letu lianze machafuko?? Kuna haja ya kumtafuta Philip Mangula na aje aseme kama ni kweli aliweka suala la Mahakama ya kadhi kwenye Ilani ya CCM. Hakuna haja kila mtu ana dini zake na imani yake!! Hakuna haja mzee wangu. tukianza kufanya hivyo tunakwenda wapi?? Kuna watu wasio na Dini, Je wakisema hivyo na bwana Kakobe naye akapendekeza misimamo yake Mikali ndio ya kufuata itakuaje?? Hakuna haja ya kufanya hivyo. kama watu wanataka kufanya Dini waanze kuhubiri mitaani na kusema kuwa Dini ya nani ni nzuri au watu wafuate dini ya nani?
 
Spika aonyeshe leadership. Mimi naona kinachoendelea ni bunge kujalidi Ilani ya CCM. Mijadala kama hii ilitakiwa iwe within CCM. Bunge ingehushwa tu iwapo kungekuwa na mswaada unaohusiana na jambo hili.
 
Ikiwa CCM waliweka kwenye Ilani yao ya uchaguzi agenda ambayo ni ya kidini, hili si suala la kikatiba? Kwa nini CCM waje na ajenda ya kidini wakati wao si chama cha kidini? Je kwa kuweka suala hilo kwenye ilani ya uchaguzi CCM hawakuvunja katiba?
 
Majibu ya Maswali haya yapo kwa CCM na kama ndio Amani wao ndio wanaweza kufanya taifa letu lianze machafuko?? Kuna haja ya kumtafuta Philip Mangula na aje aseme kama ni kweli aliweka suala la Mahakama ya kadhi kwenye Ilani ya CCM. Hakuna haja kila mtu ana dini zake na imani yake!! Hakuna haja mzee wangu. tukianza kufanya hivyo tunakwenda wapi?? Kuna watu wasio na Dini, Je wakisema hivyo na bwana Kakobe naye akapendekeza misimamo yake Mikali ndio ya kufuata itakuaje?? Hakuna haja ya kufanya hivyo. kama watu wanataka kufanya Dini waanze kuhubiri mitaani na kusema kuwa Dini ya nani ni nzuri au watu wafuate dini ya nani?

Hapa Mangula unamuonea mkuu!
 
Ikiwa basi Bungeni kuna mabench ya wataalam kwa ajili ya kutoa ufafanuzi wa kitaalam inapotokea ufafanuzi unahitajika, mf mwanasheria mkuu wa serikali, mkemia mkuu, n.k. Basi serikali iweke na wataalam wa dini mbali mbali ambao watakuwa wakitoa ufafanuzi authoritative kuhusu dini mbali mbali bungeni. Vinginevyo Bunge halizitendei haki dini.
 
Lakini vile vile wabunge wanapola haki ya kuzizungumzia dini wakati hawana authority na hatuna ushahidi kuwa dini wanazozizungumzia zimewatuma kweli wazitetee bungeni.

Vinginevyo vyama vyenye ajenda za kidini basi vitamke kuwa pamoja na malengo yake mengine, dini vile vile ni sehemu ya sera zao. Vyama viruhusiwe kusema ni dini gani wanajiainisha nayo. Manake tunachagua vyama na wabunge, wakiisha ingia bungeni, dini zinaanza.
 
Hapa Mangula unamuonea mkuu!
Hapana JK aliwahi kusema kuwa yeye alikuwa hajui kama kuna suala la mahakama ya kadhi kwenye Ilani ya CCM mimi nasema hivyo kwasababu Ilani ilitayarishwa na CCM na pia MANGULA alikuwa Katibu mkuu wa CCM na yeye Jk alisema kuwa hicho waliweka Wakristo na sio yeye. Sasa Mimi nasema kuna haja ya kutafutwa MAngula aje aseme kama kweli yeye ndio aliyetoa shinikizo la Mahakama ya Kadhi liwe kwenye Ilani ya CCM. Hivyo wao nao Bila ya kujua hata wale wenzangu na mimi walichagua mtu ambaye anataka Mahakama ya kadhi. Waislamu wana haki ya kudai Mahakama ya kadhi. Kuna tetesi kuwa waliwahi hata kukaa vikao vya siri kule Dodoma kujua ni lini wataanzisha mahakama ya kadhi. CCM ndio wameyataka haya. Mimi nadiliki kusema kuwa CCM ndio cha cha Kidini cha sasa
 
CCM kwa hiyo wanaexploit dini kwa kuweka agenda ya kidini kwenye irani yao ya uchaguzi. Ofisi ya msajiri wa vyama vya siasa wamekaa kimya. Je vyama vingine ni haki vile vile kuleta agenda za kidini?

Nadhani hapa CCM waseme waliteleza au wakubali kuwa dini ni sera yao!!
 
Wakati ilipojitokeza hoja ya serikali ya Tanganyika ndani ya bunge mwalimu aliisambaratisha kwa kusema hii si sera ya CCM. Hoja ya OIC vile vile ilionekana ni uvunjaji wa katiba na si sera ya CCM.

Leo hii baada ya mwalimu, CCM wamepenyeza hoja za kidini ndani ya ilani yao ya uchaguzi. Hii inaonekana hoja hizi yaani kuingiza mahakama ya kadhi na kujiunga OIC ni sera ya CCM rasmi. Kwa nini? Kwa sababu tumeshaona CCM wakizipigia chapuo hoja hizi ndani na nje ya bunge.

Waziri membe alisema serikali inataka kujiunga na OIC. Kumbuka waziri alikuwa akitoa msimamo wa serikali ya CCM. Tena wabunge wa CCM wamekuwa wakizichomekea hoja hizi hapa na pale na hatujasikia uongozi wa CCM ukisimama na kusema hizi si sera ya chama hiki. Rais ambaye ni mwenyekiti wa CCM hajasema lolote kuhusu mambo haya mbali na kusema kuwa si yeye aliyeingiza mambo haya kwenye ilani ya uchaguzi.

Lakini CCM haijawahi kutoka mbele na kusema hoja hizi yaani kuingiza mambo ya ibada serikalini (mahakama ya kadhi - kwa waislam ni ibada) na kujiunga na OIC (ambayo ni jumuiya ya kidini) si sera yake. Maana yake ni kuwa hizi ni sera rasmi za CCM.

Sasa je la kujiuliza hizi ni sera za kidini au siyo? Naam, hizi sera ni za kidini moja kwa moja. Kwa CCM kuingiza mambo ya kidini kama moja ya sera zake rasmi ni kitendo blatantly cha kuvunja katiba. Kwa hiyo iko haja ya kuruhusu na vyama vingine kuingiza dini katika sera zao. Kwa maana hiyo hiyo badala ya kufanya CCM kuendesha siasa za dini kinyemela, viruhusiwe vyama vya kidini ili mambo haya yawe rasmi.
 
Last edited:
Jamani kuna trend imeanza kujitokeza hivi karibuni kwa mambo ya kidini kuingia Bungeni. Sheria ya nchi inazuia kuanzishwa kwa vyama vya siasa vyenye mrengo wa kidini. Pamoja na kuwa wanasiasa wana dini, lakini kuifanya dini agenda ya kisiasa, ni sawa na kuanzisha chama chenye mrengo wa kidini.
  1. Je, iko haja ya spika kuzuia mijadara yenye mwelekeo wa kidini Bungeni au mijadara ya dini iwekewe muda wake kama ilivyo bajeti?
  2. Ikiwa wabunge wanaweza kujadili mambo yenye mrengo wa kidini bungeni, iko haja viruhusiwe vyama vya kisiasa vyenye mrengo wa kidini ili wakati wa uchaguzi tuwe tunajua kuwa huyu tukimchagua ataenda kutetea dini yetu?
  3. Iko haja ya kutoa nafasi za ubunge kwa dini zetu ili wenye utaalam wa masuala ya dini waende kuzisemea dini zao bungeni?
  4. Je bungeni ni mahali muafaka pa kutetea maslahi ya dini? Wabunge huo uwezo wamepewa na nani?
  5. Je iko haja wabunge wawe wanaleta na hoja za kidini wakati wa uchaguzi ili tujue kuwa bungeni wataenda kutetea maslahi ya dini zetu vile vile?
Nimeamua kuanzisha thread hii ili tujadiri hili tatizo la wabunge waliochaguliwa kwa hoja za kimaendeleo wanapoingia bungeni kuanza kudandia mambo ya dini ili tu kujipatia umaarufu.


Kaazi kweli kweli. The statement you close with is unethical and malicious.
 
Back
Top Bottom