Afya ya mwanangu inateteleka kisa mke wangu maziwa yanatoka kwa shida!

Mlishe mkeo vyakula kama supu ya samaki, ndizi za mchuzi, nk ili mwili wake utengeneze maziwa ya kutosha, vilevile mkazanie anyonyeshe mara kwa mara maana Wasichana wengi wakizaa sikuhizi ni wazembe kunyonyesha wanabania matiti kisa wanadhania kufanya hivyo ndo hayataanguka.
Jaman naomben msaada! mwanangu ana wiki mbili ananyonya kwa shida kisa mke wangu mziwa hayatoki inavyotakiwa! ni nini sababu? na tufanyaje ili kutibu tatizo?
 
Acheni kuwapa watoto maziwa ya kopo, zile ni kemikali

Unawatoto wangapi?

Unafaham matatizo ya uzazi nakulea?

Umeshakumbana na tatizo la mama hatoi maziwa na mtoto anamiezi miwili au mitatu? Ulimpa nini?

Naomba Majibu tafadhali
 
Mpe uji wa pilipili manga hakika yatatoka,.


Nb:tatizo likizidi mpeleke hospital,.
Lishe ni muhimu sana, na pia akiwa anapata sato mchemsho ile fresh itamsaidia, ila kama shemeji yetu anapenda usasa, hiyo yote haitasaidia, mtafutie tu maziwa ya kopo umnusuru mtoto. Mother Confesssor nimeongezea tu kwako mkuu.
 
Lishe ni muhimu sana, na pia akiwa anapata sato mchemsho ile fresh itamsaidia, ila kama shemeji yetu anapenda usasa, hiyo yote haitasaidia, mtafutie tu maziwa ya kopo umnusuru mtoto. Mother Confesssor nimeongezea tu kwako mkuu.
Ondoa shaka mkuu...!!!
 
Kiukweli wanawake walio wengi hata ofisini nawaona wanajali sana muonekano wao wa nje bila kujua madhara ya kutokunyonyesha; kwanza ukimnyonyesha mtoto ni afya kwa kwako mama na kwa mtoto...mi ningekua waziri wa afya nigeweka sheria kwamba kila mwaamke ni lazima amnyonyeshe mtoto unless awe na tatizo la kiafya linalomzuia kunyonyesha

Tunawanyima watoto haki zao za msingi kwa kutaka uzuri usio na maana; mtu kama
Hataki maziwa yalale asizae basi; na hata asipizaa umri unavyosogea mwili unabadilik tu huwezi kuwa kijana forever

Kuna mmoja aliniambia hataki kuzaa kawaida anaogopa papuchi yake itakua kubwa

Na kweli alimwomba
Dokta amfanyie oparesheni...nilimshangaa na kumdharau sana

Ila na nyie wanaume angalieni sio kila mwanamke anafaa kuwa mke na sii kila mke anafaa kuwa mama; wengine hawapo tayari kubeba zile motherhood sacrifice...you sacrifice everything for the family

Being a mother needs so much sacrifices wakati mwingine unasahau hata fasheni zilizoingia maana unakua bize na watoto hata kutoka huwezi; unaamka wa kwanza kila siku na unalaa wa mwisho

comment yako imenifanya nikuone wa pekee sana,hawa wadada form four leavers Sana shida saba,yuko tayar mtoto afya itetereke kwa kutonyonya ipasavyo wakizingatia matiti yasilale,aiseee nilizama kwa CO nikiwa nimechafukwa nikaomba ruhusa nikaeleweka nikapata siku 21,pale home ilibid niwe taahira kidogo kueleweka,mbele ya mama mkwe nilipageuza pale home ni depo,nilipoeleweka kuwa Dogo nataka anyonye maziwa ya mama kwa gharama na hali yoyote nilishangaa maziwa yamekuwa mengi kwa mama bila kutumia dawa yoyote ile,hongera sana rafiki yangu,unajielewa ad nimekupenda asee
 
Back
Top Bottom