Alwaz
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 6,830
- 10,360
Leo Jumanne televisheni ya taifa ya Oman imetangaza kuwa Afya ya Mfalme wa nchi hiyo inaendelea kuimarika na kwamba hatua za matibabu zinaendelea kama kawaida.
Mheshimiwa Qaboos bin Said Albusaidy wiki mbili zilizopita alirudi kutoka kwenye matibabu nchini Ubelgiji alikokaa takriban wiki moja.Alipoondoka kwa ajili ya safari hiyo ya matibabu aliwaaga raia zake lakini aliporudi haikuelezwa zaidi kuhusiana na afya yake.
Kwenye misikiti ya nchi hiyo kumekuwa na hamasa kubwa ya wananchi kumuombea afya nzuri. Dua kama hizo zimefanyika maeneo mbali mbali ya Tanzania ikiwemo Dar es salaam na Zanzibar.
Mfalme Qaboos bin Said mwenye umri wa miaka 79 ni mshirika mkubwa wa nchi za Magharibi tangu pale alipompindua baba yake katika mapinduzi baridi mwaka 1970 kwa msaada wa Uiengereza.
Baada ya mapinduzi hayo ameiongoza nchi hiyo na kupata maendeleo makubwa ya kiuchumi kwa kutumia rasilimali ya mafuta.
Mfalme Qaboos bin Said inajulikana hana mke na wala hana watoto ambao wangeweza kuchukua nafasi yake kama mapishano ya kifalme ya nchi nyengine yanavyokuwa.
Kwa katiba ya nchi hiyo mfalme hamtaji mrithi wake hadharani kabla ya kifo chache na ni jukumu la baraza maalum la mpito kumchagua mtu wanayemuona anafaa kukalia kiti hicho. Lakini kama wakishindwa baada ya siku tatu utafunguliwa usia wa mfalme na kutajwa jina alilolichagua na ndiye atakayekuwa mfalme mpya.
Pamoja na uhusiano mkubwa wa kidugu kati ya Oman na Tanzania lakini mfalme huyo pamoja na kukalia kiti cha ufalme kwa muda mrefu sina kumbukumbu kwamba amewahi kutembelea nchi hiyo.
Mheshimiwa Qaboos bin Said Albusaidy wiki mbili zilizopita alirudi kutoka kwenye matibabu nchini Ubelgiji alikokaa takriban wiki moja.Alipoondoka kwa ajili ya safari hiyo ya matibabu aliwaaga raia zake lakini aliporudi haikuelezwa zaidi kuhusiana na afya yake.
Kwenye misikiti ya nchi hiyo kumekuwa na hamasa kubwa ya wananchi kumuombea afya nzuri. Dua kama hizo zimefanyika maeneo mbali mbali ya Tanzania ikiwemo Dar es salaam na Zanzibar.
Mfalme Qaboos bin Said mwenye umri wa miaka 79 ni mshirika mkubwa wa nchi za Magharibi tangu pale alipompindua baba yake katika mapinduzi baridi mwaka 1970 kwa msaada wa Uiengereza.
Baada ya mapinduzi hayo ameiongoza nchi hiyo na kupata maendeleo makubwa ya kiuchumi kwa kutumia rasilimali ya mafuta.
Mfalme Qaboos bin Said inajulikana hana mke na wala hana watoto ambao wangeweza kuchukua nafasi yake kama mapishano ya kifalme ya nchi nyengine yanavyokuwa.
Kwa katiba ya nchi hiyo mfalme hamtaji mrithi wake hadharani kabla ya kifo chache na ni jukumu la baraza maalum la mpito kumchagua mtu wanayemuona anafaa kukalia kiti hicho. Lakini kama wakishindwa baada ya siku tatu utafunguliwa usia wa mfalme na kutajwa jina alilolichagua na ndiye atakayekuwa mfalme mpya.
Pamoja na uhusiano mkubwa wa kidugu kati ya Oman na Tanzania lakini mfalme huyo pamoja na kukalia kiti cha ufalme kwa muda mrefu sina kumbukumbu kwamba amewahi kutembelea nchi hiyo.