Afungua kesi mahakama ya Mwanzo Ilala kudai talaka baada ya kunyimwa tendo la ndoa kwa miaka mitano

62 kwa 42, gape la miaka 20. Hapo dada anataka wagawane mali akaolewe na umri wake.

FUNZO: Wazee wenzangu tuoe umri wetu
Gap Mbona dogo tu hilo!!,Watu wanaoana kwa Magap ya miaka Thelathini au zaidi na wanaishi.Angalia Hayati Mugabe wa Zimbabwe na mkewe, Hayati Reginald Mengi na Mkewe Jackline Mengi.
 
HAPO KINACHOTAFTWA NI KUGAWANA MALI WALA SI TENDO LA NDOA!
Na ukichunguza sana unakuta huyo mwanamke ndo alianza kuchepuka mzee akaamua kutokumpa talaka kuhofia Mali,
Huenda mzee Mali kaona azihamishe taratibu kwa watoto!
Huyo mwanamke kagundua mchezo kaona aje na ombi la talaka kwa kukosa unyumba!

LAKINI LENGO NI MALI NA NYUMBA!
Kama watoto wa huyo mzee ni wakubwa wanajitambua;
Dawa ni kupita naye hivi huyo mwanamke mapema sana! Kosakosa aokote hata makopo potelea mbali
Aisee inawezekana.
 
Ndoa zimekuwa na utata kila kukicha, sasa mtu ana miaka 62 anataka kumuaacha kwa nini? Au ndio kutaka kugawana mali mapema?

Adela Ngogolo (42) amefungua kesi ya madai mahakama ya mwanzo Ilala akiomba kupewa talaka na mumewe, Alcado Mkondola (62) kwa madai kuwa ameshindwa kumpatiwa haki yake ya tendo la ndoa kwa miaka mitano. Adela na mumewe kwa pamoja wanaishi Tabata Kimanga jijini Dar es Salaam.

Kwa hisani ya Dar Mpya.
Sema kimeumanaaaa!!!!
 
Mtu menopause bado,kwanini asiwe na hamu?..ushafika miaka 42 ukaona hilo?
Kimsingi mwanamke anapokuwa na umri MKUBWA mahitaji HUWA makubwa pia ila wababa umri MKUBWA HUWA na mahitaji madogo.nikipata muda taleta somo Hilo hapa
Sasa si wangeachana kimya kimya kama walivyokutana ,mambo ya kwenda kuaibishana ya nini?
Huwenda jamaa kaombwa kuacha kimya kimya lakini hakutii vikao vya washenga,familia,mabaraza ya usuluhishi ikabidi Bimkubwa aende mahakamaniiiii.
 
Ushahidi mahakamani unakuwa ni nini kama mzee anadinda kwa kiasi si anashinda tu kesi?..

Huyu mwanamke anataka mali navyohisi
mzee namjua ni mstaafu wa shirika moja la usafirishaj af ni mtu wa feg sana kuna kipind aliugua tb mwanamke kakosa tu busara mzee afya ni mgogoro bint anataka tu mali asepe kwa dogodogo mzee kwa umri wake atakua kachoka ivo ni busara tu kutumika
 
Back
Top Bottom