Abu Ubaidah Commando
JF-Expert Member
- Sep 8, 2016
- 7,593
- 6,934
Ingelikua utajiri unaupata kwa kulialia, kulalamika na kutaka huruma basi Afrika, hususani hapa Bongo/Afrika ingeongoza kwa utajiri kuliko taifa/bara lolote duniani.
Point yangu ni hiii👇🏽
Kwa waliotazama mpira wa jana
Jana zimecheza timu 4
Al ahly tripoli na Orlando pirates
Berkane na Mazembe
Mpira ulimalizika,
Orlando ndani, tripoli nje kwa goli 3-2
Berkane ndani, Mazembe nje kwa goli 4-2
Nimefuatilia mitandaoni wadau wa michezo wakilalamikia ushindi wa Berkane dhidi ya mazembe, kwa mtu anaejua mpira hawezi kulialia na kulalamika eti Berkane wamebebwa, haingii akilini kwa mtu anaejua mpira akadai mazembe wameonewa.
Naamini asilimia 90 ama zaidi ya hiyo walikua wanatamani mazembe ashinde, na hao hao ndio wanalialia na kulalamika mara oh waarabu matapeli, figisu, fitina, refa amehongwa, mara oh ile sio red card, ile sio penalt, wengine wanawatukana waarabu kisa tu mazembe ametolewa.
Kama wamebebwa, je! Huyo mazembe alishindwaje kumfunga hizo goli 4 kwake!!! Badala yake akaishia na ushindi wa goli MOJA!!! mnadhani Berkane ni timu ndogo!!! Fuatilieni historia yake hapo nyuma ndio mtajua Berkane ni nani, Pesa pesa pesa ndio kila kitu.
Naamini kabisa ushindi wa jana kwa Berkane, lau ingelikua ndio mazembe ameshinda hizo goli 4, na mchezaji wa berkane amepata red card, na kupata penati msingekuja hapa kulialia na kulalamika wameonewa, labda wachache sana wanaoelewa na kutambua nini maana ya mpira.
Mechi ya Orlando na Tripoli sijaicheki, ila nimejaribu kupitia comments za wadau, tena ni wachache sana wakidai kuwa tripoli amenyimwa penati MBILI dhidi ya Orlando. Wadau hawa hawazidi 10, na sijaona kutukanwa kwa ORLANDO.
Lakinii, timu za wenzetu(NORTH AFRIKA) zikipata ushindi kelele nyingi sana, mara wanabebwa, marefa wanahongwa, hapo miaka ya nyuma walikua wanalalamika sana kuhusu ushindi wa Al ahly/Egypt eti kwakua RAIS WA CAF alikua ni mwarabu ndio maana, haya na sasa RAIS wa sasa tulienae ni Mwafrika na bado malalamishi yako pale pale.
Kwa wale mliotazama mechi ya Egypt na senegal mliona nini kilitokea ni wazi egypt alifanyiwa uhuni, mechi ya Algeria dhidi ya Cameroon ni wazi Algeria alifanyiwa uhuni, lakini huwezi kukuta wadau wakitukana na kulalamikia timu za waarabu zinaonewa, labda wachache sana sana. Sisapoti kutukana, kudhania n.k.
Kuweni wanaume bwana, wanaume wa shoka na tuacheni kulalamika na kujilizaliza, mpira haupo hivyo, wenzetu ndio maana wamefika mbali.
👇🏽
NO TO RACISM
(UBAGUZI WA RANGI BADO UNALITIKISA BARA LETU KULIKO JAMII/BARA LOLOTE HAPA DUNIANI) HUSUSANI HAPA KWETU BONGO, ILA WACHACHE WANAJITAMBUA👈🏾 WATU HAWA KWANGU NAWAPA KONGOLE.
Nawaombeni tuchangie kwa ustaarabu na sio kutukana, kukejeliana n.k.
Ahsanteni!
Point yangu ni hiii👇🏽
Kwa waliotazama mpira wa jana
Jana zimecheza timu 4
Al ahly tripoli na Orlando pirates
Berkane na Mazembe
Mpira ulimalizika,
Orlando ndani, tripoli nje kwa goli 3-2
Berkane ndani, Mazembe nje kwa goli 4-2
Nimefuatilia mitandaoni wadau wa michezo wakilalamikia ushindi wa Berkane dhidi ya mazembe, kwa mtu anaejua mpira hawezi kulialia na kulalamika eti Berkane wamebebwa, haingii akilini kwa mtu anaejua mpira akadai mazembe wameonewa.
Naamini asilimia 90 ama zaidi ya hiyo walikua wanatamani mazembe ashinde, na hao hao ndio wanalialia na kulalamika mara oh waarabu matapeli, figisu, fitina, refa amehongwa, mara oh ile sio red card, ile sio penalt, wengine wanawatukana waarabu kisa tu mazembe ametolewa.
Kama wamebebwa, je! Huyo mazembe alishindwaje kumfunga hizo goli 4 kwake!!! Badala yake akaishia na ushindi wa goli MOJA!!! mnadhani Berkane ni timu ndogo!!! Fuatilieni historia yake hapo nyuma ndio mtajua Berkane ni nani, Pesa pesa pesa ndio kila kitu.
Naamini kabisa ushindi wa jana kwa Berkane, lau ingelikua ndio mazembe ameshinda hizo goli 4, na mchezaji wa berkane amepata red card, na kupata penati msingekuja hapa kulialia na kulalamika wameonewa, labda wachache sana wanaoelewa na kutambua nini maana ya mpira.
Mechi ya Orlando na Tripoli sijaicheki, ila nimejaribu kupitia comments za wadau, tena ni wachache sana wakidai kuwa tripoli amenyimwa penati MBILI dhidi ya Orlando. Wadau hawa hawazidi 10, na sijaona kutukanwa kwa ORLANDO.
Lakinii, timu za wenzetu(NORTH AFRIKA) zikipata ushindi kelele nyingi sana, mara wanabebwa, marefa wanahongwa, hapo miaka ya nyuma walikua wanalalamika sana kuhusu ushindi wa Al ahly/Egypt eti kwakua RAIS WA CAF alikua ni mwarabu ndio maana, haya na sasa RAIS wa sasa tulienae ni Mwafrika na bado malalamishi yako pale pale.
Kwa wale mliotazama mechi ya Egypt na senegal mliona nini kilitokea ni wazi egypt alifanyiwa uhuni, mechi ya Algeria dhidi ya Cameroon ni wazi Algeria alifanyiwa uhuni, lakini huwezi kukuta wadau wakitukana na kulalamikia timu za waarabu zinaonewa, labda wachache sana sana. Sisapoti kutukana, kudhania n.k.
Kuweni wanaume bwana, wanaume wa shoka na tuacheni kulalamika na kujilizaliza, mpira haupo hivyo, wenzetu ndio maana wamefika mbali.
👇🏽
NO TO RACISM
(UBAGUZI WA RANGI BADO UNALITIKISA BARA LETU KULIKO JAMII/BARA LOLOTE HAPA DUNIANI) HUSUSANI HAPA KWETU BONGO, ILA WACHACHE WANAJITAMBUA👈🏾 WATU HAWA KWANGU NAWAPA KONGOLE.
Nawaombeni tuchangie kwa ustaarabu na sio kutukana, kukejeliana n.k.
Ahsanteni!