Aaron Arsenal
JF-Expert Member
- Jul 24, 2014
- 24,504
- 28,691
Mentality ni nini kwa Kiswahili? "Ni njia ya kufikiria ya mtu au kikundi."
Hivyo katika watu ambao tuna shida ya "mentality" ni watu Weusi na Waarabu. Jamii hizi kwa asilimi kubwa zinaishi kwa itikadi sana hasa ya dini. Jamii hizi daima zinarusha lawama zake kwa watu wa magharibi, kila tatizo au migogoro ya kiuchumi nk ni kulalamika tu. Nimeudhuria sana mijadala ya watu weusi na Waarabu kuhusu maisha ya kiujumla ila nimeona mzungu ndio ameshushiwa zigo la lawama.
Lakini ukifuatilia sana kwa makini utaona jamii yetu ya Weusi pamoja na Waarabu ni wabinafsi mno na wote wanasali sana lakini ni wachoyo sana. Wao ni kupokea tu na si kutoa. Nchi zetu za Afrika na za Kiarabu zinapokea sana fedha kutoka Ulaya na Marekani lakini ndio wa kwanza kuwalalamikia hao hao katika shida zao. Hebu tuone jambo hili.
Mnamo mwaka 2015, Amerika ilitoa zaidi ya dola bilioni 8 kusaidia nchi 47 za Kusini mwa Sahara; na USAID inaboresha kanda 27 za nchi za barani Afrika. Na toka 2015 mpaka 2019 misaada inaongezeka. Hapo sijataja nchi za Ulaya.
Na nchi za Kiarabu ndio zinaongoza kupokea misaada kutoka Marekani nchi kama Afghanstan, Jordan, Misri, Palestina, Iraq nk. Afghanistan inapokea $ 4,533.51 milioni katika misaada ya kigeni ya Amerika ambayo ni kama $ 148 kwa kila mtu.
Hiyo ni misaada tu bado mikopo, Afrika tumekopa sana kiasi nchi zingine zimeshafikia mstari mwekundu wa kukopa, hazikopesheki sasa. Ukiwaza hizo pesa zinaenda wapi utastajabu sana, ndizo utasikia eti ndio zimekuwa "EPA" yaani watu walikula na familia zao, na wanabeba kwa magunia na kujiita vigogo, halafu hilo deni anabebeshwa muuza Nyanya na muuza dagaa. Halafu utakuta watu fulani tena wanajiita wasomi wanatetea upuuzi huu na kutoa oyeee, na viongozi wa dini bila hiyana nao wanaunga mkono asasi ambazo zimefanya ufisadi huu.
Huo ni ubinafsi mkubwa na laana nzito, tusitegemee Mungu atazibariki nchi kama hizi, bila kubadilisha mentality tutaendelea kulalamika mpaka Yesu atakuja. Vijiweni na mabungeni utasikia mabeberu wanatunyonya, kwani walikushikia panga au bunduki na kukulazimisha kukopa kwao? au walikushinikiza kufanya mikataba ya hovyo ukiwa guest? na kama wanakukera mbona unapokea misaada kutoka kwao? kataa basi kama una njia mbadala.
Taifa halifanikiwi kwa kuwa na chama cha siasa chenye nguvu, au kuwa na jeshi bora lenye silaha kali ama kuwa na raisi bora kiasi cha watu kuomba aendelee kutawala kinyume cha katiba, bali taifa linafanikiwa kwa kuitamka HAKI NA KUITENDA. Biblia inasema hivi,
"Haki huinua taifa...[Mithali 14:34]."
Na usitegemee hata mara moja nchi itabarikiwa kwa kuonea maskini, maskini ambao nguvu ndio mtaji wao, unamwekea kodi kuu, kiasi cha kulia usiku na mchana. Mtaji wa laki moja unaliwa kwa kodi mpaka unateteketea, kodi zisizo zingatia utu na kumuinua mjasiliamali mdogo, halafu na hizo hizo pesa za kodi zinapelekwa kwenye siasa au kwenye mambo ya hovyo. Lazima mlaaniwe tu. Nabii Daniel alimwashauri hivi mfalme mkuu mwonevu wa maskini na mkanyaga haki,
"Kwa sababu hiyo, Ee mfalme, shauri langu lipate kibali kwako; ukaache dhambi zako kwa kutenda haki, ukaache maovu yako kwa kuwahurumia maskini; huenda ukapata kuzidishiwa siku zako za kukaa raha. [Dan 4:27]."
Mfalme huyo alipuuza ushauri huo wa Daniel, lakini matokeo yake alipinduliwa na raia wake. Ushauri huo mpaka sasa unawafaa viongozi wote, kiongozi muovu ambaye anakanyaga haki na kuonea maskini kwa kodi na kutwaa haki zao, uiletea nchi matatizo na laana. Pia ukionea wafanyakazi na kuwadhulumu stahiki zao, tambua unaleta mabalaa katika nchi. Biblia inasema,
Ole wake aijengaye nyumba yake kwa uovu! Na vyumba vyake kwa udhalimu! Atumiaye utumishi wa mwenzake bila ujira, Wala hampi mshahara wake; [Yeremia 22:13].
Huwezi kuijenga nchi kwa dhuluma ya haki za wafanyakazi na nchi hiyo ikafanikiwa. Pia kuwadhulumu wakulima haki zao za ukulima, ni kumuuzi Mungu, na Mungu analipa. Biblia inasema,
"Angalieni, ujira wa wakulima waliovuna mashamba yenu, ninyi mliouzuia kwa hila, unapiga kelele, na vilio vyao waliovuna vimeingia masikioni mwa Bwana wa majeshi. [Yakobo 5:4]."
Hizo dhuluma zote utazikuta Afrika ni mwendo wa ufisadi na kung'ang'ania madaraka, Mungu haziakiwi apandacho mtu ndicho atakachokivuna. Lawama hazitatupigisha hatua kamwe. Adam baada ya kutenda dhambi kwa kula tunda, alivyo hojiwa na Mungu, lawama zote alimtishwa mkewe kuwa ndio kamsababisha kula tunda. Kwa maana nyingine alimwambia Mungu usingenipa huyu mwanamke au nisingekuwa na huyu mwanamke nisingetenda dhambi.
Mungu halimhukumu ADAM bila kusikiliza hizo sababu za kijinga na kumpa adhabu ambayo mpaka leo tunapitia machungu ya uchaguzi wake. Ndivyo ilivyo Afrika, ikiulizwa kwanini huko kwenu kumejaa umaskini mkubwa na uonevu? inajibu ni kwa sababu ya MZUNGU [BEBERU]. Maovu yetu tunayaficha kwa uvuli wa neno Beberu/ mzungu. Mungu atahukumu Afrika kwa uchaguzi wao mbovu na si kwasababu ya udhuru wa BEBERU.
Tubadilishe mtazamo wa fikra.
Hivyo katika watu ambao tuna shida ya "mentality" ni watu Weusi na Waarabu. Jamii hizi kwa asilimi kubwa zinaishi kwa itikadi sana hasa ya dini. Jamii hizi daima zinarusha lawama zake kwa watu wa magharibi, kila tatizo au migogoro ya kiuchumi nk ni kulalamika tu. Nimeudhuria sana mijadala ya watu weusi na Waarabu kuhusu maisha ya kiujumla ila nimeona mzungu ndio ameshushiwa zigo la lawama.
Lakini ukifuatilia sana kwa makini utaona jamii yetu ya Weusi pamoja na Waarabu ni wabinafsi mno na wote wanasali sana lakini ni wachoyo sana. Wao ni kupokea tu na si kutoa. Nchi zetu za Afrika na za Kiarabu zinapokea sana fedha kutoka Ulaya na Marekani lakini ndio wa kwanza kuwalalamikia hao hao katika shida zao. Hebu tuone jambo hili.
Mnamo mwaka 2015, Amerika ilitoa zaidi ya dola bilioni 8 kusaidia nchi 47 za Kusini mwa Sahara; na USAID inaboresha kanda 27 za nchi za barani Afrika. Na toka 2015 mpaka 2019 misaada inaongezeka. Hapo sijataja nchi za Ulaya.
Na nchi za Kiarabu ndio zinaongoza kupokea misaada kutoka Marekani nchi kama Afghanstan, Jordan, Misri, Palestina, Iraq nk. Afghanistan inapokea $ 4,533.51 milioni katika misaada ya kigeni ya Amerika ambayo ni kama $ 148 kwa kila mtu.
Hiyo ni misaada tu bado mikopo, Afrika tumekopa sana kiasi nchi zingine zimeshafikia mstari mwekundu wa kukopa, hazikopesheki sasa. Ukiwaza hizo pesa zinaenda wapi utastajabu sana, ndizo utasikia eti ndio zimekuwa "EPA" yaani watu walikula na familia zao, na wanabeba kwa magunia na kujiita vigogo, halafu hilo deni anabebeshwa muuza Nyanya na muuza dagaa. Halafu utakuta watu fulani tena wanajiita wasomi wanatetea upuuzi huu na kutoa oyeee, na viongozi wa dini bila hiyana nao wanaunga mkono asasi ambazo zimefanya ufisadi huu.
Huo ni ubinafsi mkubwa na laana nzito, tusitegemee Mungu atazibariki nchi kama hizi, bila kubadilisha mentality tutaendelea kulalamika mpaka Yesu atakuja. Vijiweni na mabungeni utasikia mabeberu wanatunyonya, kwani walikushikia panga au bunduki na kukulazimisha kukopa kwao? au walikushinikiza kufanya mikataba ya hovyo ukiwa guest? na kama wanakukera mbona unapokea misaada kutoka kwao? kataa basi kama una njia mbadala.
Taifa halifanikiwi kwa kuwa na chama cha siasa chenye nguvu, au kuwa na jeshi bora lenye silaha kali ama kuwa na raisi bora kiasi cha watu kuomba aendelee kutawala kinyume cha katiba, bali taifa linafanikiwa kwa kuitamka HAKI NA KUITENDA. Biblia inasema hivi,
"Haki huinua taifa...[Mithali 14:34]."
Na usitegemee hata mara moja nchi itabarikiwa kwa kuonea maskini, maskini ambao nguvu ndio mtaji wao, unamwekea kodi kuu, kiasi cha kulia usiku na mchana. Mtaji wa laki moja unaliwa kwa kodi mpaka unateteketea, kodi zisizo zingatia utu na kumuinua mjasiliamali mdogo, halafu na hizo hizo pesa za kodi zinapelekwa kwenye siasa au kwenye mambo ya hovyo. Lazima mlaaniwe tu. Nabii Daniel alimwashauri hivi mfalme mkuu mwonevu wa maskini na mkanyaga haki,
"Kwa sababu hiyo, Ee mfalme, shauri langu lipate kibali kwako; ukaache dhambi zako kwa kutenda haki, ukaache maovu yako kwa kuwahurumia maskini; huenda ukapata kuzidishiwa siku zako za kukaa raha. [Dan 4:27]."
Mfalme huyo alipuuza ushauri huo wa Daniel, lakini matokeo yake alipinduliwa na raia wake. Ushauri huo mpaka sasa unawafaa viongozi wote, kiongozi muovu ambaye anakanyaga haki na kuonea maskini kwa kodi na kutwaa haki zao, uiletea nchi matatizo na laana. Pia ukionea wafanyakazi na kuwadhulumu stahiki zao, tambua unaleta mabalaa katika nchi. Biblia inasema,
Ole wake aijengaye nyumba yake kwa uovu! Na vyumba vyake kwa udhalimu! Atumiaye utumishi wa mwenzake bila ujira, Wala hampi mshahara wake; [Yeremia 22:13].
Huwezi kuijenga nchi kwa dhuluma ya haki za wafanyakazi na nchi hiyo ikafanikiwa. Pia kuwadhulumu wakulima haki zao za ukulima, ni kumuuzi Mungu, na Mungu analipa. Biblia inasema,
"Angalieni, ujira wa wakulima waliovuna mashamba yenu, ninyi mliouzuia kwa hila, unapiga kelele, na vilio vyao waliovuna vimeingia masikioni mwa Bwana wa majeshi. [Yakobo 5:4]."
Hizo dhuluma zote utazikuta Afrika ni mwendo wa ufisadi na kung'ang'ania madaraka, Mungu haziakiwi apandacho mtu ndicho atakachokivuna. Lawama hazitatupigisha hatua kamwe. Adam baada ya kutenda dhambi kwa kula tunda, alivyo hojiwa na Mungu, lawama zote alimtishwa mkewe kuwa ndio kamsababisha kula tunda. Kwa maana nyingine alimwambia Mungu usingenipa huyu mwanamke au nisingekuwa na huyu mwanamke nisingetenda dhambi.
Mungu halimhukumu ADAM bila kusikiliza hizo sababu za kijinga na kumpa adhabu ambayo mpaka leo tunapitia machungu ya uchaguzi wake. Ndivyo ilivyo Afrika, ikiulizwa kwanini huko kwenu kumejaa umaskini mkubwa na uonevu? inajibu ni kwa sababu ya MZUNGU [BEBERU]. Maovu yetu tunayaficha kwa uvuli wa neno Beberu/ mzungu. Mungu atahukumu Afrika kwa uchaguzi wao mbovu na si kwasababu ya udhuru wa BEBERU.
Tubadilishe mtazamo wa fikra.