Kingsmann
JF-Expert Member
- Oct 4, 2018
- 4,448
- 16,306
Mama wa mtoto katika shule ya awali ya Laerskool Schweizer-Reneke iliyopo katika jimbo la North West huko Afrika Kusini, amechukizwa vikali baada ya picha inayomuonesha mtoto wake wa kike na watoto wengine watatu wa Kiafrika wakiwa wamekaa peke yao mbali na watoto wengine wa kizungu kwenye darasa lao. Picha hiyo ambayo inasambaa kwa kasi mtandaoni, imesababisha hasira kubwa kwa raia wa nchi hiyo kutokana na kuwa na ishara ya ubaguzi wa rangi.
Picha hiyo ilitumwa kwenye kundi la WhatsApp la shule hiyo na mwalimu wa darasa. "Hii ilipaswa kuwa siku ya kufurahisha kwangu lakini sio,” amesema mzazi huyo. Mama huyo ambaye hakutajwa jina kulinda utambulisho wa mwanae, ameiambia tovuti ya TimesLIVE ya nchini humo kuwa siku ya kwanza katika darasa hilo ilianza vizuri.
Yeye na wazazi wengine waliwapeleka watoto wao na kuambiwa waondoke katika eneo la shule. Saa tatu asubuhi walitumiwa taarifa kutoka kwa mwalimu wa watoto hao kuhusu siku ilivyokwenda kupitia WhatsApp group. Picha hiyo ilionesha watoto 18 wa kizungu wakiwa darasani wamekaa dawati moja lililounganishwa katikati ya darasa, wakati watoto wanne wa Kiafrika wakiwa wamekaa kwenye dawati moja lililowekwa kwenye kona ya darasa hilo. "Nilichoona ni jumbe toka kwa wazazi wa kizungu wakisema asante asante kwenye WhatsApp group, lakini hakuna yeyote aliyesema kuhusu walivyotenganishwa,” alisema mzazi huyo.
Amesema baada ya kujadiliana na mzazi mwingine nje ya WhatsApp group, mzazi huyo aliwasiliana na mkuu wa shule kuuliza kuhusu ukaaji wa watoto hao darasani. TimesLIVE imedai mkuu huyo wa shule alisema hakuwa na taarifa za suala hilo. Wamedai kuwa wanasubiri jibu toka kwa shule hiyo.
Alipoulizwa kuhusu anavyojisikia kutokana na hali hiyo, mama huyo amesema ana matumaini kuwa mwanae mwenye umri wa miaka mitano bado ni mdogo kuweza kutambua kilichotokea.
"Lakini nimechukia,” alisema mama huyo aliyeahidi kuchukua hatua zaidi.
Source: Bongo5
Picha hiyo ilitumwa kwenye kundi la WhatsApp la shule hiyo na mwalimu wa darasa. "Hii ilipaswa kuwa siku ya kufurahisha kwangu lakini sio,” amesema mzazi huyo. Mama huyo ambaye hakutajwa jina kulinda utambulisho wa mwanae, ameiambia tovuti ya TimesLIVE ya nchini humo kuwa siku ya kwanza katika darasa hilo ilianza vizuri.
Yeye na wazazi wengine waliwapeleka watoto wao na kuambiwa waondoke katika eneo la shule. Saa tatu asubuhi walitumiwa taarifa kutoka kwa mwalimu wa watoto hao kuhusu siku ilivyokwenda kupitia WhatsApp group. Picha hiyo ilionesha watoto 18 wa kizungu wakiwa darasani wamekaa dawati moja lililounganishwa katikati ya darasa, wakati watoto wanne wa Kiafrika wakiwa wamekaa kwenye dawati moja lililowekwa kwenye kona ya darasa hilo. "Nilichoona ni jumbe toka kwa wazazi wa kizungu wakisema asante asante kwenye WhatsApp group, lakini hakuna yeyote aliyesema kuhusu walivyotenganishwa,” alisema mzazi huyo.
Amesema baada ya kujadiliana na mzazi mwingine nje ya WhatsApp group, mzazi huyo aliwasiliana na mkuu wa shule kuuliza kuhusu ukaaji wa watoto hao darasani. TimesLIVE imedai mkuu huyo wa shule alisema hakuwa na taarifa za suala hilo. Wamedai kuwa wanasubiri jibu toka kwa shule hiyo.
Alipoulizwa kuhusu anavyojisikia kutokana na hali hiyo, mama huyo amesema ana matumaini kuwa mwanae mwenye umri wa miaka mitano bado ni mdogo kuweza kutambua kilichotokea.
"Lakini nimechukia,” alisema mama huyo aliyeahidi kuchukua hatua zaidi.
Source: Bongo5