mkiluvya
JF-Expert Member
- May 23, 2019
- 802
- 725
sasa mkubwa ulitaka wawe upinzani kumbuka 1992 waliosema wanataka mageuzi walikuwa chini ya asilimia 20% ulitegemea kenge akamzaa bata pamoja na kwamba wote wanataga mayai ninafikiri wewe ni mmoja wa wapumbavu mnaotumiwa na mabeberuKuna nchi nyingi Afrika ambazo ukitafakari kwa makini, hata kama hazikuhusu utakuta zinakera sasa. Nyingi zimefikia kuwa na siasa za kipumbavu, uongozi wa kipumbavu na maamuzi ya kipumbavu. TRump kuna wakati aliziita hit hole countries - nchi za shimo la kinyesi. Nina uhakika alijua asemalo, hata kama na yeye ana matatizo yake yanayofanana na nchi hizo.
Ni wazi kwamb nchi hizo zinaekea kusiko kuzuri, lakini wengi wa watu wao hawalioni hilo. Wengi wanaburuzwa tu na kusukumwa kama mikokoteni, huko wakishangilia kila ujinga unaofanyika. Wengi wakifanya hivyo kwa uoga, kujipendekeza au kwa kuwa ni mbubumbu tu wa siasa.
Suala ni kwamba, raia katika nchi hizi watavumilia kuwa katika siasa za kipumbavu, uongozi wa kipumbavu na maamuzi ya kipumbavu. kwa muda gani? La ajabu ni kwamba wengi wa wananchi katika nchi hizi wanakuwa wananchama wa vyama tawala, na unajiuliza, hivi chama chako kikifanya siasa za kipumbavu, uongozi wa kipumbavu na maamuzi ya kipumbavu basi unakuwa sio upumbavu tena? Ni mtu taahira tu ndio anaweza kudhani upumbavu wa chamba chake au viongozi wa chama chake sio upumbavu kwa sababu unafanywa na chama chake!