Afrika ‘haiwezi kuhimili’ wimbi la pili la virusi vya corona

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,010
9,875
mwanamke
Nchi nyingi za Afrika zimelegeza masharti ya kukabiliana na kusambaa kwa virusi vya corona

Shirika la afya duniani (WHO) limeonya kuwa Afrika haiwezi kuhimili wimbi la pili la Covid-19, likisema kuwa litakuwa na athari kubwa hususan za kiuchumi.

Onyo hilo linatolewa wakati maambukizi yakiendelea kuongezeka katika nchi nyingi ambazo zililegeza sheria za kupambana na maambukizi hayo hivi karibuni.

WHO linasema virusi havitaweza kudhibitiwa kama Mataifa ya Afrika yataendelea kufungua shughuli zake bila kuweka tahadhari za kuzuia maambukizi ya virusi vya Corona.

Imeonya pia juu ya kurejea kwa vipindi vya amri za kutotoka nje ambazo inasema Afrika haiwezi kuvihimili.

Mkurugenzi wa WHO kanda ya Afrika, Matshidiso Moeti, pia amesema hatua zimewekwa kuhakikisha bara hilo linapata sehemu yake ya chanjo yoyote inayotengenezwa.

Afrika imeripoti zaidi ya visa milioni 1.6 vya virusi vya corona tangu mlipuko huo ulipoanza huku watu 39,000 wakifa kutokana na maradhi hayo.
 
Hata yaje mia, hamna kitakacho badilika hapa kwetu Afrika, tuko salama na Mungu anatupenda.

Huu ugonjwa WHO wanaukuza sana sijui nyuma kuna ajenda gani, halafu takwimu zao zimebase sana Africa.
Mwezi wa 5 afisa mmoja WHO Zimbabwe kwa mujibu wa data zao walizo zikusanya WHO kwamba mpaka mwaka kuisha zaidi ya waafrika 250 mil watakuwa wamevuta lakini ukiangalia tumebakisha miezi miwili still bado tunadunda.

Hata Ulaya tunaona wamechoka kukaa ndani, USA kuna maandamano kibao ya kupinga upaguzi wa rangi, juzi Lakers kashinda ubingwa wa NBA watu wamejimwaga barabarani, Bayern kachukua UEFA mashabiki wamejimwaga barabarani vilevile kwa mashabiki wa Arsenal bila kusahau mashabiki wa Liverpool tena hawa walipagawa kabisa na ubingwa EPL wakajimwaga barabarani, hawana barakoa wala sanitizer.

Huu ugonjwa hauishi leo wala kesho cha msingi watu wajifunze kuishi nao kama tunavyoishi na magonjwa mengine mfano Malaria,Homa ya Ini,HIV nk.
 
Mikwala ju ya mikwala, kila siku ni mikwara tu. Wali predict kwamba May na June could be worse in Africa, ndioo kwanza tukafungua na shule, sasa hvi watoto wapo zao class wanakula book with no problem. Kinga pelekeni walikoathirika sana, huku Africa sio mojawapo
 
Kwani ajenda yao ni nini hasa? Maana macho yao yote na huo ugonjwa ni kwa Africa tu, kama wametuchoka watutenge tu kila mtu abaki kwao,
Hii dunia ni yetu sote mambo ya kupangiana jinsi ya kuishi hatutaki
 
Hio tahadhari na sisi Tanzania ametuwekamo ? Maana huo uhayawani sis hautuhusu kabisa
 
View attachment 1601950Nchi nyingi za Afrika zimelegeza masharti ya kukabiliana na kusambaa kwa virusi vya corona

Shirika la afya duniani (WHO) limeonya kuwa Afrika haiwezikuhimili wimbi la pili la Covid-19, likisema kuwa litakuwa na athari kubwa hususan za kiuchumi.

Onyo hilo linatolewa wakati maambukizi yakiendelea kuongezeka katika nchi nyingi ambazo zililegeza sheria za kupambana na maambukizi hayo hivi karibuni.

WHO linasema virusi havitaweza kudhibitiwa kama Mataifa ya Afrika yataendelea kufungua shughuli zake bila kuweka tahadhari za kuzuia maambukizi ya virusi vya Corona.

Imeonya pia juu ya kurejea kwa vipindi vya amri za kutotoka nje ambazo inasema Afrika haiwezi kuvihimili.

Mkurugenzi wa WHO kanda ya Afrika, Matshidiso Moeti, pia amesema hatua zimewekwa kuhakikisha bara hilo linapata sehemu yake ya chanjo yoyote inayotengenezwa.

Afrika imeripoti zaidi ya visa milioni 1.6 vya virusi vya corona tangu mlipuko huo ulipoanza huku watu 39,000 wakifa kutokana na maradhi hayo.
Mungu yuko Afrika na bustan ya aden iko huku
 
Nimemuona Trump anapiga kampeni zake bila barakoa huku akiendelea kuzikebei! Nikajiuliza huyu si alikuwa mgonjwa wa corona huyu? Afrika amkeni wazungu nao ni wajinga, tukiamua tunawapita kabla ya 2050!
 
Nchi nyingi za Afrika zimelegeza masharti ya kukabiliana na kusambaa kwa virusi vya corona

Shirika la afya duniani (WHO) limeonya kuwa Afrika haiwezikuhimili wimbi la pili la Covid-19, likisema kuwa litakuwa na athari kubwa hususan za kiuchumi.
sijuui lini Corona (Covid-19) iliondoka Afrika
acheni ije tena km haikufyekelewa mbali na huyo mwenzake wa awali ambaye yupo
mafua hayajamtisha mwafrika
 
Back
Top Bottom